Pole sanaa mkuu kwa changamoto, ni hali ya kawaida kukutana na hali hiyo ukiwa mwajiriwa, pia hata kwenye mahusiano n.k
Lakini kabla ya kulaumu, fanya utafiti wakina kujua sababu zinazokufanya ukumbane na changamoto hiyo, Pia angalie wafanyakazi wenzako wanavyoishi then relate mahusiano yao na Boss wako. Hii itakusaidia kujua boss wako ni mtu wa aina gani,anapenda kipi/hapendi kipi, anapenda/hapendi watu wa aina fulani.
Pia kumbuka hakuna boss anaependa aonekane kuwa chini ya wafanyakazi wake, kama umemzidi elimu,akili,muonekano(smart) au kama unakubalika sanaa na wafanyakazi wako kuliko yeye atatafuta sababu ya kukushusha hadhi yako. NB: sio wote wana roho hiyo ya kuchukia wafanyakazi,pia Wapo maboss wanaopenda wafanyakazi wanaokuwa smart kwenye kazi (Kuna kabila/jamii huwa wanatabia hiyo.. wakipanda cheo lazima mtaona chamoto, ni nature yao kwahiyo ishi nao kwa akili)
Lakini kunasababu zinazoweza kusababisha boss kukuchukia:
●Kutotimiza wajibu wako. Hakuna boss anayependa kuwa na mfanyakazi ambaye hatimizi wajibu wake, Yaani kilakitu lazima uambiwe,ukumbushwe kila kitu unakuwa wa mwisho. Kama una hiyo tabia acha mara moja.
●Kuwa na uwezo mdogo wa kujenga hoja. Fahamu deeply taaluma yako, pata ujuzi mpya kila siku, ikitokea kuna tatizo ofisini usikae kimya toa msaada wa mawazo ya kuimarisha ofisi.
●Kuto jali muda. Hakuna kitu muhimu kwenye taasisi yoyote kama muda, Jali muda wa kuingia kazini na kutoka, muda wa kuanza kazi na kumaliza, Jali muda mkihaidiana mfano kikao,kutoa repoti,n.k
●Kutoshirikiana na wafanyakazi wenzako. Kuna muda wa kazi, na muda wa kupumzika, hivyo kuwa social, zungumza na wenzako usijitenge sanaa, na usiwazoee sanaa.
●Acha mazoea na boss wako kwenye mambo ya kipuuzi, hapa kuna kuna seheme tofauti kama kwenye media,whatsapp the way unavyochat na watu wanakuchukulia boya tu, so yanakushusha hadhi, acha upuuzi.
●Usiwe mropokaji wa ovyo ovyo, Yaani Chochote unacho zungumza kiwe na manufaa,Kama wenzako wanajadili upuuzi usitoe maoni stay cool,Sometimes to be silent is better
●Epuka kutoa siri za maisha yako kwa kila mtu, watu wasijue kilakitu ulichonacho, au unachokipitia au tabia zako nje ya kazi. Kama unapiga gambe sanaa punguza.
●Kuwa Ruler 📏 kama YES iwe YES, NO iwe NO. Usiwe mtu wa kuyumbishwa tu na watu, Watu wajue unamsimamo. Hata boss akijua una msimamo ata kuheshimu, hawezi kuja kichwakichwa.
Maisha hayana njia moja, sio lazima njia uliyonayo ndiyo utakayo tokea.
● Mwisho : Usiache imani ya Mungu wako. Kwenye ofisi zetu za kibongo kuna mambo mengi sana kama ushirikina,waenda kwa waganga kukupiga tukio n.k (Hii wanaita kukupaka mavi ,kama kuna mtu kakufanyia hilo, hapo hutoboi hadi utafukuzwa kazi) namna ya kutoka fuata kanunu za kiimani, asubuhi kabla ya job Pray, ukiwa kazini Pray, ukitoka Pray, eneo la kazi Pray, Pray daily. Then urudi utupe mrejesho.
Asante