Hahah nimegundua wewe Mwoga, usijaribu kama hauna moyo, mimi binafsi sikurudia na sitarudua mchezo huoUnakaa kwenye kona kwa nje au kwa ndani, na nikiwaona halafu nikasepa inakuwaje kabla hawajarudi?
Acha tu hilo tukio mpk leo huwa hata sielewi kabisa yaani ilikuwaje ni Mungu tu ndio mwenye kujuaMkuu mwli ulipataje nguvu za kukimbia hvo
Kumbe rahisi tu, 😃.Hakuna asiye nervous katika hali kama hizo kinachohitajika ni courage tu katikati ya hofu mkuu.Sasa mwenye nyumba baadae aliwa mind au mlichuniana tu😃😃.Hahah nimegundua wewe Mwoga, usijaribu kama hauna moyo, mimi binafsi sikurudia na sitarudua mchezo huo
Nb: Unakaa kwenye kona nje ya nyumba.
Naomba nimuite ndugu Mshana Jr aweke neno. Haya mambo yapo kwa kuusema usemi, "lisemwalo lipo,kama halipo, litatokea."
Binafsi sijawahi shuhudia chochote kwa macho yangu ya nyama zaidi ya haya...
Wakati flani nilikaa maeneo ya bonde la mpunga, hapo wakazi wake wengi ni waswahili na mie maisha yangu ilikuwa kwenda kazini kurudi najifungia ndani.
Usiku mmoja nimelala chumbani kwangu nikastuka naona taswira kama ya kibibi kinaingia dirishani kwangu kwa njia za kimiujiza huku anapiga kelele. Nikaanza kusema kwa jina la Yesu tokaa (nililelewa kwenye familia za kilokole) kikapotea nikarudi kulala.
Siku ingine nimelala nastuka kabisa nasikia mtu amevuta nywele zangu za utosini kwa kuzikata na kucha ya kidole chake na baada ya hapo akatoweka sikuona mtu ila hali ya nywele kutoka kwenye utosi wangu niliisikia kabisa japo sikusikia maumivu na hapakubaki kipara nilikuwa na nywele ndefu.
Mara nyingine inanitokea usingizini napambana na nguvu za giza usingizini maana ya kwamba kama mashetani au kitu kinanikaba. Kisha sauti inaniambia kemea, sali nikianza kusali napata nguvu na kile kitu kinakimbia, baadae kinarudi tena nakemea naongeza nguvu nazidi kukemea halafu najiona nguvu za maombi zinaniongezeka ghafla nastuka kutoka usingizini najikuta naendelea kusali na inaweza kuchukua hata nusu saa nzima kama si lisaa ndo maombi yanakata, nikijaribu kuacha kusali nashindwa nakuwa sina utashi wa kunyamaza hadi hali ya kusali iishe..
Huwa najiuliza kama ni ndoto nilipostuka ilitakiwa ikate, sasa nastuka bado najikuta naendeleza kusali kwa kukemea, safari moja hadi nikainuka kitandani out of my will nikiwa nasali.
Sijajua kama hayo nayo ni matukio ya kutisha au vimbwanga ama laah...
Nachojua, ulimwengu wa roho upo na unapande mbili, nuru na giza. Si mtu wa dini sana ila...lisemwalo lipo kama halipo litatokea.
Si muamini wa mambo ya kishirikina na yafananayo ila kwa dini yangu ya kikristo niliyokulia natambua ulimwengu wa giza unamazagazaga kama hayo waliyoelezea memba wengine halo juu.
Mimi binafsi nakumbu miaka ya nyuma sana katika kijiji chetu walikuja waganga ambao wanaitwa lambalamba bs bwana hao kz yao kutoa uchawi kwa kila nyumba na kila mtaa sasa nilichokishuudia kwa macho yangu, palikuwa na kijana akawa anawazalau wale waganga Ebwana wakamgeuza mwanamke palepale,sasa ikawa mshikemshike kumpepua ndugu wakja yomi pale wanawaomba wamueke sawa waganga wakawa wanataka 300000 taslim ndugu awana wao wana 200000,Ndio kuwasaidia.Jamani uchawi upo,
Sent using Jamii Forums mobile app
Kaka mtoto wa mama mkubwa alienda kutandika kitanda baada ya kula usiku waende kulala.Pembeni ya nyumba yao kulikua na msufi mkuuuuuuuubwa ndio mti mkubwa zaidi pale kijijini.
Alipoenda kutandika hakurudi tena hadi saa linapita mtu hatoki ndani, kwenda kumtafuta hayupo! Walimuwinda nyumba nzima hawamuoni karibia masaa 3 nyumba yote hawaoni mtoto. Baadae walimuona chini ya meza ya kula (ndogo tu) kajikunyata hawesi kuongea. Wakampeleka kwa mganga usiku huo huo kafanyiwa dawa ndio akaanza kuongea kua kuna kitu kilimchukua kikampeleka ndani ya huo msufi.
Tumewangiwa utotoni kinoma noma..ilibidi mama ahamishe kitanda tulale chumbane mwake. Alikua akiwasha kibatali aone vizuri ndani anaona kiganja kinazima kibatali.
Wachawi waliniiba wakanitoa chumbani wanipeleka kunilaza chini ya mtungi..kwenye kona la nyumba. Walinipata asubuhi nikiwa nimesinzia nimefunikwa ushungi kama mtoto mchanga.
RIP kuna mbwa wetu alikua anapambana nao usiku wakamuuua
Sijawahi ona kiumbe Cha ajabu wala kuhisi sijui minyato ya kichawi au uchawi hapana kabisa!.. hii inanifanya hata niwe mgumu kuuamini huo ulimwengu! Japo nimekuwa muda mwengine mzururaji sometimes maeneo hatarishi ambayo wengine huogopa lkn binafsi hakuna la ajabu nililoliona!.. yanayonitokea ni matukio ya kawaida kabisa ila Kuna baadhi yanaleta utata ila sio utata wenye kunifanya niamini kuwa kuna walakini!!
Mfano kuna mahali palikuwa panasemekana kuwa huwa kuna sijui majini ama mizimu ila kuna miti ya miembe na mapera,siku moja nipo mi najamaa fulani ktk pitapita tukakuta mti wa mpera tukaanza kuchuma lkn sio kwa kupanda punde tukiwa tunachuma aliongezeka kijana mwengine Sasa utata baada ya kuondoka Yule kijana ndo tukaanza kujiuliza alitokea wapi!!
Maana kipindi anakuja hatukumuona! Si tulishangaa tu tupo watatu nae anachuma mapera lkn chengine alichotutatanisha ni ni maswali yake juu ya ule mpera na hata sikumbuki Kama alichuma hata!!
Swala la kutokumuona alivyokuja nililivunjilia mbali maana kibarabara tulikuwa bize kutafuta mapera wahuni[emoji23]
Na apotelea pote huko tukio lake halina mantiki..
Sijui nini kitakuja nifanya niamini haya mambo ila mi nachohisi kitu usipokiweka bayana nawe kukuzingua au kujionyesha mbele yako kina nafasi ndogo Sana ya kujionyesha..
Na mnaona hayo mambo na muone siku nikishuhudia huo ulozi kwa sababu ya kimantiki iliyoshiba nitakuja kusimulia humu.
Alikuja asubuhi akatutania nyie vijana ni (wajeshi sana) akimaanisha wakakamavu, baada ya wiki Tulipewa notice akidai anataka afanye ukarabati wa nyumba yake[emoji23]Kumbe rahisi tu, [emoji2].Hakuna asiye nervous katika hali kama hizo kinachohitajika ni courage tu katikati ya hofu mkuu.Sasa mwenye nyumba baadae aliwa mind au mlichuniana tu[emoji2][emoji2].
Dah aisee hii mbinu simple sana then unamjua mbaya wako...
😂😂😂 daah noma sana aisee,nimekaa hapa katika kona na stuli na jiwe naona bado,sijui wamenishtukia au sijakaa fresh,kuna mother ana shape wanasema ni mkali wa hizo mambo,akija kinyume nyume sirushi jiwe na enjoy tuAlikuja asubuhi akatutania nyie vijana ni (wajeshi sana) akimaanisha wakakamavu, baada ya wiki Tulipewa notice akidai anataka afanye ukarabati wa nyumba yake[emoji23]
Mzee mwenzangu TiticombNajua umekubali kuepusha ubishi lakini rohoni bado una amini ilikuwa nguvu za giza au mazingara ya kichawi au majini.
Siyo lazima niwe sahihi nadharia yangu, lakini nilikuwa najaribu kuelezea uwezekano wa hilo kutokea kisayansi ya baiolojia, maana sleep walking ni tatizo la kibaiolojia kwamba kuna sehemu ya ubongo wako iliyotakiwa kulala/kupumzika ilikuwa bado inaendelea kufanya kazi.
Ilitakiwa sehemu ya ubongo inayo husika kuwezesha viungo vyako kama limbs zisifanye kazi nayo ilale kama sehemu zingine za ubongo, ibakie sehemu ya ubongo ile ya kufanya kazi za msingi za upumuaji na kusukuma damu.
CC: Carleen njoo unikosoe baiolojia huku, mimi sikusoma kabisa Biology elimu ya upili au kokote zaidi ya shule ya msingi St. Kayumba.
katika vitu siamini in uchawi sijui majini labda mpaka nishuhudieMzee mwenzangu Titicomb
Sleep walking ipo na uchawi upo..! Kuna mambo mengi sana humu duniani, usibishane sana kwa kitu ambacho wenzio wamekishuhudia wewe hujashuhudia!!
Enwei, naamini uchawi upo ila sijawahi kumbana nao uso kwa uso..!
Una bahati ulikuwa bado mtoro huyo mrefu alokuwa anakufata nyuma huwa mshenzi sana sema haui ila huwa anasumbua balaaa. Hapendi kukimbiwa. Ukimkimbia imekula kwako, we akija jifanye humuoni ikiwezekana kaa chini ama lala chini ili apite. Ila komesha yake vua nguo zote utembee uchi ama vaa kwa mtindo huu.Dah imenikumbusha miaka ya 90s nikiwa Tabora wilaya moja hivi kijijini nikichukua elimu ya ya msingi shule yetu ilikuwa upande wa magharibi kuna makaburi halafu shule ina miti kibao ya mikaratusi,mikorosho mijohoro mizambarawe na miti fulani hivi inatoa ubani upepo ukipiga inavuma kama gari, dah nakumbuka hiyo siku niliamka kwenye kigheto changu pale home kama saa nane hivi mabalamwezi imekubali nje maana ilikuwa wiki ya mwalimu mmoja hivi kusimamia usafi na wechelewaji na ukichelewa unapata bakora za miguuni na lile baridi la kijijini balaa mwanaume mbalamwezi ile nikajua kumekucha nikanawa faster faster hata sikuwastua wazazi ambapo sio kawaida huwa lazima niwaamshe kwenye gheto lao mzee nikanyanyua ufagio mkononi na kidumu cha maji mbio kwenda kabla ya kufika shule kuna kipori flani lazima ukipite ndio ufike shule mwanaume sikujari japo njiani sikuona mtu yeyote hiyo haikunistua mie nilijona mshindi leo nawahi namba shule, aisee nimepita chini ya mikorosho na hiyo miti mingine bila kujari nahisi akili haikuwa yangu nakumbuka nafika shule nikakimbilia darasani nafika mlangoni nilichokishuhudia acha niliona moto mkubwa unawaka mule na kuna watu wamekaa kama wako kwenye kikao halafu wote wakaniangalia ila sura sikuziona hapi ndio akili ikarudi kwamba nimezingua niligeuka mbio kurudi home halafu ule upande wa makaburi nilishuhudia watu wakiwa na mguu mmoja wanaruka ruka kwa mstari mbio zangu nilikuwa nahisi kuna kitu nyuma kinanifata kugeuka nyuma niliona mtu mrefu sana kichwa hakionekani ila kavaa vazi refu linag'aa kama mbaramwezi ilivyokuwa inag'aa mwanaume niliongeza speed nilienda nikaingia na mlango mpk ndani yule jini sijui nini nilipokaribia nyumbani nilisikia msonyoo mmoja hatari sana wazazi wakaamka kufungua mlango kuja kunikuta sijitambui wakanichukua nikaenda kulala kwao asubuhi ndio kuwaelezea ni moja ya tukio ambalo huwa sipendi kabisa kulikumbuka maana baada ya hapo mpk leo kuna vitu huwa naviona ambavyo sio vya kawaida na niliwasumbua sana wazazi baada ya hapo . nimejaribu kufupisha ila kuna mambo mengi sana kwa ule usiku na miaka ile niliyashuhudia baada ya ilo tukio.
Watu wa aina yako yakiwakuta ndiyo mashuhuda wazuri sana..!!katika vitu siamini in uchawi sijui majini labda mpaka nishuhudie
au mods mnasemaje???
hata mimi nafikiri hivyo😊😊Watu wa aina yako yakiwakuta ndiyo mashuhuda wazuri sana..!!
Una bahati ulikuwa bado mtoro huyo mrefu alokuwa anakufata nyuma huwa mshenzi sana sema haui ila huwa anasumbua balaaa. Hapendi kukimbiwa. Ukimkimbia imekula kwako, we akija jifanye humuoni ikiwezekana kaa chini ama lala chini ili apite. Ila komesha yake vua nguo zote utembee uchi ama vaa kwa mtindo huu. Anzia chupi igeuze nje ndani halafu ivae mbele nyuma fanya hivo kwa nguo zote soks na viatu kulia kushoto. Halafu tembea kawaida tu hatakiona. Ungekuwa mtu mzima ungekimbia ukastuoia akili zinarudi upo kijijiji cha 8. Ndo ungejiuliza umefikaje huko
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimejaribu kila njia ya kukutana na haya mambo lakini wapi
Nikisikia huyu bibi mchawi au huyu mzee ni mshirikina mimi kazi yangu ni kuwauliza tu hivi mnapata faida gani kuroga?
Yote hiyo natafuta huo wanga
Sina woga labda ndio sababu nao wananipuuza
Nikaona isiwe shida nikawa naenda kukaa makaburini manane ya usiku maana nikuambiwa ndio mda wa wawangaji kuwanga
Napo sikuambulia kitu zaidi ya mara mbili jamaa kunikimbia huku wanapiga yowe [emoji23][emoji23]
Yaani mpaka haunted house nimeingia sana zaidi ya baadhi ya vyumba kuwa baridi la kufa mtu lakini hakuna kitu cha kunifanya nikimbie
Kuna kizee Fulani waliniambia huwa kanapaa usiku
Nikakauliza naomba lift
Kakasema ya wapi tena nikakaambia kwenye ungo kalisonyaa mpaka kanapotea [emoji23][emoji23]
Sent from my iPhone using Tapatalk
Una bahati ulikuwa bado mtoro huyo mrefu alokuwa anakufata nyuma huwa mshenzi sana sema haui ila huwa anasumbua balaaa. Hapendi kukimbiwa. Ukimkimbia imekula kwako, we akija jifanye humuoni ikiwezekana kaa chini ama lala chini ili apite. Ila komesha yake vua nguo zote utembee uchi ama vaa kwa mtindo huu. Anzia chupi igeuze nje ndani halafu ivae mbele nyuma fanya hivo kwa nguo zote soks na viatu kulia kushoto. Halafu tembea kawaida tu hatakiona. Ungekuwa mtu mzima ungekimbia ukastuoia akili zinarudi upo kijijiji cha 8. Ndo ungejiuliza umefikaje huko
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kwahiyo umeamua kuongea matusi ili niache? Siachi