Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Shukuru Mungu kama hujawahi kutana na hayo mambo,
Mambo hayo husababishwa na Kama kuna Ndugu wana michezo hiyo, Majirani au watu wanaokuzunguka maeneo unayoishi na husababishwa na Husda,michezo,mazoea
Hayo Mambo bwana mkubwa yapo sana sana tu, kama hayajakukuta utayadharau na kupuuza, Kuna muda unakutana na majaribu mpaka unajiuliza hivi kweli mm huwa nasali, kama nasali mbona bado siko imara huyu Mungu ninae miomba ni wa wapi,mbona wengine hawakumbani na hizi zahama..
Mfn: Sumbawanga unaweza sikia vitimbi vingi sana ila wewe ukapangiwa kazi huko ukaishi vzr na ukakataa kuhama kabisa, ila mwinhine anaweza pangiwa huko mwezi mmoja tu akakutana na vitimbi vya hatari haya mambo yanaendana na Ukoo sometimes
Naunga mkono kwa kiasi chake
mama angu bibi yake mzaa mama alikua mwanga mno Aliwatafuna watoto wa kwanza wa wajukuu zake wote wa kike na baadhi ya mama zangi wadogo hawajazaa mpaka leo.

Mama aliniambiaga kuwa chochote unachotaka kufanyiwa kishirikina lazima mchawi wa ukoo wenu akithibitishe. Kama hakithibitishi hufanyiwi kitu ( ni kama hukumu ya kunyongwa mpaka rais atie sahihi) akanipa mfano; Mkiwa ndani asubuhi mkiamka lazima nyumba muifungue wenyewe mtoke nje, mtu wa nje hawezi kufungua kuingia ndani. Kwahiyo hapo kwenye ukoo hapo nakubaliana huwenda ndio maana hatuoni mauza uza ila pia anakiukizaga mikoba ya bibi huyo kairithi nani [emoji3]
 
Share nasi mkuu baadhi ya mambo kama elimu
Dah imenikumbusha miaka ya 90s nikiwa Tabora wilaya moja hivi kijijini nikichukua elimu ya msingi shule yetu ilikuwa upande wa magharibi kuna makaburi halafu shule ina miti kibao ya mikaratusi,mikorosho mijohoro mizambarawe na miti fulani hivi inatoa ubani upepo ukipiga inavuma kama gari, dah nakumbuka hiyo siku niliamka kwenye kigheto changu pale home kama saa nane hivi mabalamwezi imekubali nje maana ilikuwa wiki ya mwalimu mmoja hivi kusimamia usafi na wechelewaji na ukichelewa unapata bakora za miguuni na lile baridi la kijijini balaa mwanaume mbalamwezi ile nikajua kumekucha nikanawa faster faster hata sikuwastua wazazi ambapo sio kawaida huwa lazima niwaamshe kwenye gheto lao mzee nikanyanyua ufagio mkononi na kidumu cha maji mbio kwenda kabla ya kufika shule kuna kipori flani lazima ukipite ndio ufike shule mwanaume sikujari japo njiani sikuona mtu yeyote hiyo haikunistua mie nilijona mshindi leo nawahi namba shule, aisee nimepita chini ya mikorosho na hiyo miti mingine bila kujari nahisi akili haikuwa yangu nakumbuka nafika shule nikakimbilia darasani nafika mlangoni nilichokishuhudia acha niliona moto mkubwa unawaka mule na kuna watu wamekaa kama wako kwenye kikao halafu wote wakaniangalia ila sura sikuziona hapo ndio akili ikarudi kwamba nimezingua niligeuka mbio kurudi home halafu ule upande wa makaburi nilishuhudia watu wakiwa na mguu mmoja wanaruka ruka kwa mstari mbio zangu nilikuwa nahisi kuna kitu nyuma kinanifata kugeuka nyuma niliona mtu mrefu sana kichwa hakionekani ila kavaa vazi refu linag'aa kama mbaramwezi ilivyokuwa inag'aa mwanaume niliongeza speed nilienda nikaingia na mlango mpk ndani yule jini sijui nini nilipokaribia nyumbani nilisikia msonyoo mmoja hatari sana wazazi wakaamka kufungua mlango kuja kunikuta sijitambui wakanichukua nikaenda kulala kwao asubuhi ndio kuwaelezea ni moja ya tukio ambalo huwa sipendi kabisa kulikumbuka maana baada ya hapo mpk leo kuna vitu huwa naviona ambavyo sio vya kawaida na niliwasumbua sana wazazi baada ya hapo . nimejaribu kufupisha ila kuna mambo mengi sana kwa ule usiku na miaka ile niliyashuhudia baada ya ilo tukio.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Jini kuchomoza baharini na kuelea hewani.

Nakumbuka ilikua ni usiku wa manane, nikiwa kwenye harakati za ushikirikina Uko sehem( sipendi kutaja jina). Nikiwa na mganga akiendelea kufanya mambo ya kishirikina baharini, Ambapo alisema anaita kiumbe( jini) hili anitimizie haja zangu . Kwa akili yangu nilijua tu ni danganya toto, hakuna lolote. Baada ya kama dakika 45 za yule mganga kufanya ushirikina wake. Ghafla akatokea mwanamke mrefu tofauti na urefu wetu wa kawaida wa binadamu alikua baharini anaelea tu, miguu haionekani kwa kweli nilikimbia, Bahati nzuri wale wasaidizi wa mganga wakanikamata kunizuia nisikimbie. Uzuri hakua anatisha wala nini, alikua tu ni mwanamke wa kawaida ingawa alikua na urefu usio na kawaida, na alikua kakasirika sana, alikua analalamika tunamuita sana tuna shida gani.....
malizia kwanza hii.
 
Nimeandika hapo na usingizi mwenyewe umekata maana hata chumba nilichopo nakiogopa ila mambo haya ni nguvu ya kishirikina na ninadhani ule ulikuwa ndio mwisho wangu ila Mungu mwenyewe alinipigania ila uchawi upo na unafanya kazi vizuri sana ile kitu ilikuwa planned na walioplan mmoja akiwa ni jirani yetu japo kwa umri sasa hivi ni mzee sana na wenzake walishatangulia mbele ya haki ila kiukweli mambo ni mengi mie ilikuwa ikifika usiku ujue raha sina maana najua kumekucha hakuna kulala moja ya tukio kuna siku pale home baada ya tukio hilo ilikuwa jmos asubuhi nikaambiwa nikateke maji mtoni nikazingua nikaendekeza kucheza kuja kustuka bi mkubwa ananiita huwezi nikakimbilia porini kwa kuogopa kuchapwa toka saa nne aasubuhi ajabu ni kuwa nilikuwa sijui polini nimeenda kutafuta nini na kumbuka tabora kunaoongoza kuwa na nyoka koboko basi mie ndio nikaenda huko zungunga sana jua la saa nane nipo huko nakula matunda pori tu nikawa nimesikia joto katika kuzunguka zunguka nilitokea sehemu kuna maji mengi kama ziwa na lile joto nililokuwa nalo nikasema ngoja nivue nguo nioge nikavua ila roho ikasita kuoga nikavaa nikaondoka nikajikuta sijui njia ya kunirudisha nyumbani na kigiza kinaingia Mungu saidia kuna mzee mmoja wa kijiji cha pili alikuwa anachunga ng'ombe akaniaona na anawajua pale home ndio kunirudisha nyumbani ajab mama hakunichapa na alikuwa ameshanitafuta kwa washikaji wangu wote hakunipata hivyo baada ya kuniona kwanza nimepauka nilipewa tu maji ya moto kuoga na kula nikashida nikaenda kulala sasa cha ajabu asubuhi ambayo ilikuwa j2 nikawasimulia sehemu nilipoona lile ziwa la maji ile sehemu hakuna historia ya kuwa ziwa la maji hata bwawa kuna miti ya Milumba na mitundu kwa wingi kama unaijua, wazee nao ikabidi waanze kuhangaika ndio mambo kutulia ila hii dunia ina mambo sana ukijiona mzima unalala vizuri unaamka salama hakuna wenge lolote mshukuru sana Mungu mie wazazi walikuwa watu wa dini sana walikuwa hawaamini uchawi ila waliamini
[/QUOTE]

We jamaa nikiangalia avatar yako naona kivuli, nikirudi kwenye muandiko wako najikuta nakuwazia "mambo ya ajabu ajabu". Mkuu huna mambo ya kiganga-ganga kweli??
 

We jamaa nikiangalia avatar yako naona kivuli, nikirudi kwenye muandiko wako najikuta nakuwazia "mambo ya ajabu ajabu". Mkuu huna mambo ya kiganga-ganga kweli??
[/QUOTE]
Hayo ni mawazo yako tu
 
We jamaa nikiangalia avatar yako naona kivuli, nikirudi kwenye muandiko wako najikuta nakuwazia "mambo ya ajabu ajabu". Mkuu huna mambo ya kiganga-ganga kweli??
Hayo ni mawazo yako tu
[/QUOTE]
Oya transpoter endelea kumwaga vitu.
 
Umenikumbusha two years ago nikiwa nimepanga maeneo flani hivi DSM ..nilikuwa naishi kwenye chumba na sebule maeneo hayo ..nikiwa na wapangaji wenzangu ila wengi walikuwa wanafunzi wa chuo...mama mwenye nyumba tulikuwa hatuishi nae ila alikuwa mtata mno na kwa taarifa za chinichini nilisikiaga alikuwa mfuasi mzuri wa mambo ya kishirikina...

nilikuwa naishi mwenyewe so muda mwingi nilikuwa nakuwa kazini ..mara nyingi home nakuwa jioni na muda wote nikiwa home mimi ni mtu wa kujifungia ndani na kuangalia movies ..

siku hiyo nimetoka job late hours nimechoka kinoma...nilifika home na kwenda kuoga nikarudi zangu nikawa nachat na michepuko yangu mwishowe kama kausingizi kakanipitia ghafla kuja sijui nini kilinistua usingizini mara papu nikaona mtu yupo kwa juu anaelea kwenye ungo ...najaribu kupiga kelele sauti haitoki ...kitu nilichoweza ni kuchukua simu yangu na kukirushia na kutimua nje mbio...

baada ya lile tukio nilihama ile nyumba ndani ya week mbili ...nilikopata pesa ya kodi wala sikumbuki niliitoa wapi..lakini tangu nimehama nile nyumba hususani ile apartment yangu mpaka leo imekosa mpangaji.

UCHAWI UPO NA NGUVU ZA GIZA ZIPO ..Jambo jema ni kumtemgemea Mungu tu.!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kuna binadamu wamepewa uwezo wa kung'amua vitu na kuna wengine katika ulimwengu wa kiroho ni vipofu wasioona kitu chochote. Macho yao yamefungwa. Sikumbuki vizuri ila katika biblia kuna mtume mmoja walizingirwa na maadui lakini hakuonesha wasi wasi wowote. msaidizi wake akamwambia sasa tunauwawa. Yeye akajibu ondoa wasiwasi tunaulinzi yule akashangaa ulinzi u wapi. Ndipo yule mtume akamfungua macho yule mtumishi akaona jeshi kubwa la malaika limewazunguka. Ndipo wasiwasi ukaondoka. wanaojua Biblia watasema ni nani. Nilitaka tu kukwambia haya mambo ni ktk roho. uwezi yaona mpaka uwe katika ulimwengu wa rohoni. Majini, Malaika uwezi waona kwa macho ya nyama. Kuna watu wanazaliwa wananguvu maalum za kiroho. Haya mambo yapo!
Sio Yesu kweli?
 
Mimi nitasimulia kisa kimoja tu, tena cha utotoni maana kiliniogopesha sana kwa umri ule wa miaka isiyofika hata kumi. Hiki ni kisa kati ya visa vingi vya nguvu za giza nilivyovishuhudia, na ninavyoendelea kuvishuhudia mpaka kesho. Mnivumilie na mnisamehe mdogo wenu maana nitaandika kurasa ndefu.

Picha linaanza pale marehemu mama(PKA mama yangu mzazi, na Mungu akurehemu kwa rehema zake) alipoolewa na baba yangu. Kwa miaka zaidi ya mitatu, mama hakuweza kukaa na ujauzito zaidi ya miezi mitatu, na badala yake mimba ziliharibika.
Mama aliisha kwa masimango, na kuonekana sawasawa na papai linalobeba corona badala ya vitamin! (Ni mchezo uliokuwa ukichezwa na majirani zetu, wenyej wa Kigoma, na Ukweleni hapo)....Lakini mama hakuchoka kuvumilia, na kumwomba Mungu.

Hatimaye mama akashika ujauzito wangu, haukutoka tena, na nikazaliwa pale MNH, na nikaitwa jina la "dawa ya Mungu", maisha yakaendelea kijijini kwetu Boko.

Katika makuzi yangu, utotoni wazazi wangu walikumbana na matukio na changamoto nyingi za kukatisha tamaa. Kuna wakati usiku mama alimka na akakuta sipo kitandani, ananitafuta kwa mda mrefu wakiwa na mzee, hatimaye wananikuta chini ya uvungu wa kitanda nalia, au wananikuta kwenye pembe ya nyumba, mama alikuwa akilia weee, hatimaye maisha yanaendelea. Ilifika mda nikiwa na umri wa mwaka na nusu, nililishwa nyama ya kisigino ya maiti, niliumwa sana kutikana na hili chupuchupu nilambe udongo, wazazi walipambana, Mungu akasaidia, nikatoka salama.

Balaa kwa macho yangu, lilikuwa hapa sasa. Nikiwa darasa la pili, miaka hiyo ya tisini nilitokewa na tukio la kwanza, mubashara ambalo lilinitisha sana maana hapa niliona kwa macho na akili zangu. Usiku nikiwa nimelala ghafla nywele nikahisi zinasisimuka, damu inaenda mbio, na mwili unachemka....ghafla nikashtuka na kuamka paaap! Uso kwa uso na mwanaume aliyeshika kitanda changu, miguuni mwangu nywele zake zinawaka moto mkubwa ila haziteketei, macho yake yanawaka moto kama mkaa wa moto, na mikucha mirefu.

Kulia kwangu, wanawake wanne wakiwa uchi kabisa, wamebeba vyungu kichwani vinawaka moto. Kushoto kwangu wanaume watatu wapo uchi nao wamebeba vyungu, nao vinawaka moto, na mtu mmoja wa kiume(jini) mrefu akikaribia kugusa paa, mweupe kwa rangi(mwarabu) amevaa miwani mweupe, kanzu ndefu, nyeupe mpaka chini, na alikuwa na ndefu ndefu kiasi.

Tukakaziana macho sana, nikawa nawageukia wote mithili nataka niamke niwarukie ila nahisi nazuiwa, nataka kupiga kelele sauti haitoki. Baada ya dakika kama 3 au 4, nikaanza kuuona ukuta kwenye pembe ya nyumba, mubashara unafunguka na wanaanza wanawake kutoka nje kinyumenyume, wakifuata wanaume, na yule jini anakuwa wa mwisho. Hatimaye ukuta unajifunga tena baap! Na hatimaye ndo sauti inatoka mamaaaaaaa........!!!

Mama na baba wanakuja, wananikuta nalia na nimeloa jasho mwili mzima. Hatimaye nawasimulia, mama analia sana, ananikumbatia, na anamlilia Mungu, ananichukua ananipeleka chumbani kwake kwenda kulala nao chumbani kwao. Mama akaniambia watoto ni malaika, huona majini na wachawi ila ukikua hutowaona. Ila haikuwa hivyo mimi mpaka kesho hawa washenzi hawakatishi anga zangu.

Asubuhi ikafika, nikajiandaa kwenda zangu shule, na mama akaniambia kwa sasa hali ilipofikia itabidi niwe nalala na mbwa chumbani kwangu, yaani mbwa anafungwa kwenye mguu wa kitanda changu. Hii ilinisaidia ila hawa washenzi walimuua mbwa wetu(PKA Jeck) ni mbwa aliyepambana sana na hawa washenzi, ila usiku mmoja alipiga kelele kushtuka damu zinamtoka puani na mdomoni ndo ukawa mwisho wake Jeck wangu.

Hili ni tukio mojawapo kati ya matukio mengi niliyokumbana, na ninayokumbana nayo. Ila kama ukilala unaamka tu flesh bila kuona haya mavitu, muombe Mungu akujalie hivyo hivyo. Haya mavitu yanatisha sana.
Asanteni, na poleni kwa kuwachosha!

Sent using Jamii Forums mobile app
Elezea ilikuaje
Mzee anasimulia Zamani za Kale, Kipindi katoka akumuoa Mama yangu alitoka Kupata Kilaji Kidogo kwenye Kasenta Ketu hako ( Mji wetu) around 1960s.

Sasa ile anarudi home, yaani Kufika Junction ambapo kupafikia Nyumbani ni Kama Mita 200, akakutana na huyo Jamaa Mrefu. Mshua alikuwa anakula Fegi, anakwambia Fegi Ikadondoka Palepale, ile Kukimbia, aisee anakuta Karibia Kunapambazuka ndiyo akili inamrejea yupo takribani 25Kms toka home. Ndiyo akaanza Kujikongoja Kureje home karibia Kumepambazuka tayari.
 
Mungu aliumba vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. Na kwa Bahati nzuri akaweka kizuizi kwa kupitia uwezo wake wa kiungu hili tusiweze kushuhudia viumbe hivyo ambavyo havionekani kwa macho yetu ya kibinadamu isipokua kwa utaalamu flani wa mambo ya kiroho.

Viumbe hivyo vikiwemo , Malaika, Majini , Wachawi pamoja na viumbe vingine vya kutisha sana, ikiwemo wanyama wa ajabu wenye ukubwa wenye kutetemesha na kuogofya kwa wanadamu wa kawaida.

Danieli 7:4 “Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.”

Danieli 8:3 “Ndipo nikainua macho yangu nikaona, na tazama, mbele ya mto alisimama kondoo mume, mwenye pembe mbili; na pembe zile mbili zilikuwa ndefu; lakini moja ilikuwa ndefu kuliko ya pili, na ile iliyokuwa ndefu zaidi ilizuka mwisho.”

Danieli 8:5 “Nami nilipokuwa nikifikiri, tazama, beberu akatoka upande wa magharibi, juu ya uso wa dunia nzima, bila kuigusa nchi; na beberu yule alikuwa na pembe mashuhuri kati ya macho yake.”

Danieli 7:6 “Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.”

Wengi tukisoma Habari kama hizi za kuona simba mwenye vichwa vinne na miguu kama ya binadamu, beberu mwenye pembe kumi, nyoka mwenye vichwa saba na wanyama wengine wa kutisha, tunajipa moyo na kusema hiyo ni lugha tu ya biblia/ lugha ya picha hakuna viumbe kama hivyo. Ila ukweli ni kuwa viumbe hivyo vipo na vinaishi kwenye ulimwengu mwingine tofauti na huu wetu unaonekana. Na kuna binadamu wenzetu wameshashuhudia kabisa kwa macho yao.

Tuachane na hayo na turudi kwenye maada yetu ya leo . Tuzungumzie kuhusu mikasa ya kutisha ambayo tumewahi kukutana nayo kwenye ulimwengu huu ambayo kwa namna moja au nyingine vimekuacha midomo wazi na kukufanya uwe traumatized.

Ngoja nianze na mikasa / mambo ya kutisha niliyowahi kukutana nayo hapa duniani ambayo mpaka sasa hivi bado najiuliza kama ni viini macho au ni kweli , lakini ukweli unabaki kuwa ni kweli .

1. Jini kuchomoza baharini na kuelea hewani.

Nakumbuka ilikua ni usiku wa manane, nikiwa kwenye harakati za ushikirikina Uko sehem( sipendi kutaja jina). Nikiwa na mganga akiendelea kufanya mambo ya kishirikina baharini, Ambapo alisema anaita kiumbe( jini) hili anitimizie haja zangu . Kwa akili yangu nilijua tu ni danganya toto, hakuna lolote. Baada ya kama dakika 45 za yule mganga kufanya ushirikina wake. Ghafla akatokea mwanamke mrefu tofauti na urefu wetu wa kawaida wa binadamu alikua baharini anaelea tu, miguu haionekani kwa kweli nilikimbia, Bahati nzuri wale wasaidizi wa mganga wakanikamata kunizuia nisikimbie. Uzuri hakua anatisha wala nini, alikua tu ni mwanamke wa kawaida ingawa alikua na urefu usio na kawaida, na alikua kakasirika sana, alikua analalamika tunamuita sana tuna shida gani.....

2. Niliwahi kushuhudia kwa macho yangu , binadamu akiwa nusu mtu , nusu simba, Ana sura ya kutisha sana , mbaya mfano hakuna, ilibaki kidogo tu nizimie.

3. Binadamu mfupi kama stuli, Ana ndevu nyingi mpaka chini na alikua na mguu mmoja tu , na macho yake yanawaka moto.

4. Mzimu wa mtu maarufu ambaye alikufa miaka mingi iliyopita.

Hii ndo mikasa ya kutisha niliyowahi kukutana nayo hapa duniani, ambayo kiukweli mpaka leo inanipa shida sana, na ilichukua miaka kadhaa mpaka kuweza kukubali hii hali mpaka kufikia kuzoea kidogo. Ila hapa duniani kuna viumbe vya ajabu mno, na kama ukitaka kuviona unaweza.

View attachment 1430585



Sent from my iPhone using JamiiForums
Ufyongo wote huu umeuona peke yako.
 
Mzee anasimulia Zamani za Kale, Kipindi katoka akumuoa Mama yangu alitoka Kupata Kilaji Kidogo kwenye Kasenta Ketu hako ( Mji wetu) around 1960s.
Sasa ile anarudi home, yaani Kufika Junction ambapo kupafikia Nyumbani ni Kama Mita 200, akakutana na huyo Jamaa Mrefu. Mshua alikuwa anakula Fegi, anakwambia Fegi Ikadondoka Palepale, ile Kukimbia, aisee anakuta Karibia Kunapambazuka ndiyo akili inamrejea yupo takribani 25Kms toka home. Ndiyo akaanza Kujikongoja Kureje home karibia Kumepambazuka tayari.
Na ww unakula fegi.?[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ilikuwa mwaka 2004 Mzee wetu alihamishiwa kikazi mkoa fulani kanda ya ziwa, ikabidi familia yote tuhamie huko..
Kutokana na uchache wa nyumba za serikali akapangisha nyumba mtaani.

Mzee akapata safari ya kikazi kwa muda, Maza nae akawa chuo mkoa mwingine.. Nikabakia mimi na brother.
Mambo yakaanza, siku ya kwanza tukasikia madirisha ya nyumba yanafunguliwa na upepo mkali unaingia ndani ilikuwa saa nne usiku, tukatoka na mapanga kutafuta mwizi hakuonekana.

Siku ya pili mlango ukafunguliwa na kiumbe kilichoingia kikawa kinafanya shughuli zote tunazofanya mchana mf. Kuwasha radio na kubadili station, kufagia, kufungua fridge nk.

Tulihangaika ikawa kila siku mziki unanza saa mbili usiku, tukawa hatulali.. Akaja mshikaji wake broo akamwambia tukae nje usiku kwenye pembe ya nyumba tutawaona wanaotusumbua.

Tukajipanga tukaenda kukaa, baada kama ya dakika arobani alipita mtu wa kwanza anakimbia kinyume nyume mwendo wake sijapata kuona, baada ya muda akarudi akiwa na mwenzake wakiwa na mwendo wa kawaida tukawatambua kumbe ni baba mwenye nyumba na jirani yetu.

Jambo la kutisha waliamua kutuadhibu baada ya kutugundua tumewaona.. Hivyo tulipigwa ganzi karibia masaa matatu hamna kusogea wala kuongea hata kujikuna. Wao wakaendelea na mambo yao.
Duh pole mkuu vp walivyoawaachia hamkuwafata na mapanga asubuhi huku mkitema povu?
 
wakuu mie binafsi sijawahi kukutana na kisa kikubwa chakutisha kivile sema kunakimoja ambacho kilitokea ambacho kinanipa maswali mpaka iitwayo leo

ilikuwa ni kipindi flani wazee wangu wanapata huduma ya kiroho ka waumini wengine katika kanisa flani basi wakawa wanapata shuhuda mbalimbali toka kwa wenzao basi nao wakataka nao wapate baraka hizo za Mungu maana hakuna asiyezitaka ukizingatia nao walikuwa na shida zao. Basi wakaendelea kufanya taratibu zao ka kawaida ili wawezepata kibali chao cha kumshuhudia Mungu wao namie nikiwa ka mtu wa kando ka hayo mambo hayaniusu. Wakaendelea kupata maombi na kuhudhuria ibada basi siku moja kiongozi wao wa kiroho akawaahidi kufika nyumbani kwaajili ya kufanya maombi na kuombea nyumba na familia kwa ujumla

Day one alifika mida ya usiku ka mida ya saa mbili, ikiwa mama ndo alikuwepo akanialika namie kuweza kupata baraka na mengine ya kiroho, mchungaji akafanya maombo kiasi pamoja na wasaidizi wake baada ya muda akasema nitakuja sikunyingine kwaajili ya maombi tena. basi akaondoka. na mzazi akaondoka siku iliyofuatia mie ndo nikaachwa kwaajili ya kumpokea kiongozi huyo wa kiroho siku atakayokuja.

Siku iliyofuatia baada ya siku kadhaa ilikuwa ngumu kumpata kiongozi huyo wa kirohoo maana alikuwa anahudumia watu wengi na alikuwa busy na majukumu mengine ya Kanisa, nikafanya jitihada za kuwasiliana nae mara kwa mara basi akaniahidi one day atafika.

Hiyosiku aloyofika akafika salama maana alikuwa anatokea mbali kiasi na alifika mida ya usiku maana alitoka kutoa huduma sehemu nyingine basi akafanya maombi nikiwa nae na baadhi ya watu wengine baada ya hapo akaanza kumwaga maji ya baraka nyumba nzima na vyote vilivyokuwepo nyumbani hasa magari na nyumba zote na vyumba vyote, baada ya hapo akarudi tena akafanya maombi kiasi then akaniambia twende nje.

Tukazunguka kwenye eneo la nje akaanza kutafuta tafuta akaniambia ka naona kitu, nikamjibu sioni akatafuta tena na tena kwakutumia mwanga wa simu basi akaanza kusema 'lilikuwa linataka kukimbia tena na leo' basi akakiona kumbe ilikuwa kibuyu na kichupa vimefungwa pamoja na vinashanga na kitu ka irizi nyeusi na nyekundu, nilistaajabu sana. akanijuza kuwa ilikuwa inataka kukimbia na ndo maana siku ya kwanza alishindwa kuikamata. na hizo zana za kishirikina zilikuwepo sehemu nyeupe ambayo ni rahisi kuviona ila akaniambia vilikuwa ndani ya banda lililokuwepo karibu ila kwakuwa alimwaga maji yaliyobarikiwa kikashindwa kukimbia kikaishia hapo nje na akanijuza kwa macho ya kawaida huwezi ona

Mpaka leo najiuliza sana hivi ule ushirikina ulitoka wapi na uliwekwa pale nyumbani toka lini na unawezaje kukimbia pindi nguvu ya Mungu ijitokezapoooo? Mpaka leo lile tukio huwa nalikumbuka sana na vile kibuyu kilivyousisimua moyo wangu.
 
Sijawahi ona kiumbe Cha ajabu wala kuhisi sijui minyato ya kichawi au uchawi hapana kabisa!.. hii inanifanya hata niwe mgumu kuuamini huo ulimwengu! Japo nimekuwa muda mwengine mzururaji sometimes maeneo hatarishi ambayo wengine huogopa lkn binafsi hakuna la ajabu nililoliona!.. yanayonitokea ni matukio ya kawaida kabisa ila Kuna baadhi yanaleta utata ila sio utata wenye kunifanya niamini kuwa kuna walakini!!

Mfano kuna mahali palikuwa panasemekana kuwa huwa kuna sijui majini ama mizimu ila kuna miti ya miembe na mapera,siku moja nipo mi najamaa fulani ktk pitapita tukakuta mti wa mpera tukaanza kuchuma lkn sio kwa kupanda punde tukiwa tunachuma aliongezeka kijana mwengine Sasa utata baada ya kuondoka Yule kijana ndo tukaanza kujiuliza alitokea wapi!!
Maana kipindi anakuja hatukumuona! Si tulishangaa tu tupo watatu nae anachuma mapera lkn chengine alichotutatanisha ni ni maswali yake juu ya ule mpera na hata sikumbuki Kama alichuma hata!!
Swala la kutokumuona alivyokuja nililivunjilia mbali maana kibarabara tulikuwa bize kutafuta mapera wahuni😂
Na apotelea pote huko tukio lake halina mantiki..
Sijui nini kitakuja nifanya niamini haya mambo ila mi nachohisi kitu usipokiweka bayana nawe kukuzingua au kujionyesha mbele yako kina nafasi ndogo Sana ya kujionyesha..

Na mnaona hayo mambo na muone siku nikishuhudia huo ulozi kwa sababu ya kimantiki iliyoshiba nitakuja kusimulia humu.
Huna Nyota inayowaka! hii yako imezima kabisa! tunachotaka wachawi ni mwili wenye bahati njema za kuzaliwa! tuna uwezo wa kuwajua! tunajua Ma-Rais, Wafanya biashara! Viongozink , wengine hazitoki wengine zinatoka kabisa!

Ndo pale unaona mtoto hapendi shule, wakati alianza vizuri, Ugonjwa, kufukuzwa kazi, ulevi nk, Mzazi akilegea tu zina chukuliwa mapema utotoni.
 
Huna Nyota inayowaka! hii yako imezima kabisa! tunachotaka wachawi ni mwili wenye bahati njema za kuzaliwa! tuna uwezo wa kuwajua! tunajua Ma-Rais, Wafanya biashara! Viongozink , wengine hazitoki wengine zinatoka kabisa!

Ndo pale unaona mtoto hapendi shule, wakati alianza vizuri, Ugonjwa, kufukuzwa kazi, ulevi nk, Mzazi akilegea tu zina chukuliwa mapema utotoni.
Kaeni na minyota yenu
 
Back
Top Bottom