Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

wakuu mie binafsi sijawahi kukutana na kisa kikubwa chakutisha kivile sema kunakimoja ambacho kilitokea ambacho kinanipa maswali mpaka iitwayo leo

ilikuwa ni kipindi flani wazee wangu wanapata huduma ya kiroho ka waumini wengine katika kanisa flani basi wakawa wanapata shuhuda mbalimbali toka kwa wenzao basi nao wakataka nao wapate baraka hizo za Mungu maana hakuna asiyezitaka ukizingatia nao walikuwa na shida zao. Basi wakaendelea kufanya taratibu zao ka kawaida ili wawezepata kibali chao cha kumshuhudia Mungu wao namie nikiwa ka mtu wa kando ka hayo mambo hayaniusu. Wakaendelea kupata maombi na kuhudhuria ibada basi siku moja kiongozi wao wa kiroho akawaahidi kufika nyumbani kwaajili ya kufanya maombi na kuombea nyumba na familia kwa ujumla

Day one alifika mida ya usiku ka mida ya saa mbili, ikiwa mama ndo alikuwepo akanialika namie kuweza kupata baraka na mengine ya kiroho, mchungaji akafanya maombo kiasi pamoja na wasaidizi wake baada ya muda akasema nitakuja sikunyingine kwaajili ya maombi tena. basi akaondoka. na mzazi akaondoka siku iliyofuatia mie ndo nikaachwa kwaajili ya kumpokea kiongozi huyo wa kiroho siku atakayokuja.

Siku iliyofuatia baada ya siku kadhaa ilikuwa ngumu kumpata kiongozi huyo wa kirohoo maana alikuwa anahudumia watu wengi na alikuwa busy na majukumu mengine ya Kanisa, nikafanya jitihada za kuwasiliana nae mara kwa mara basi akaniahidi one day atafika.

Hiyosiku aloyofika akafika salama maana alikuwa anatokea mbali kiasi na alifika mida ya usiku maana alitoka kutoa huduma sehemu nyingine basi akafanya maombi nikiwa nae na baadhi ya watu wengine baada ya hapo akaanza kumwaga maji ya baraka nyumba nzima na vyote vilivyokuwepo nyumbani hasa magari na nyumba zote na vyumba vyote, baada ya hapo akarudi tena akafanya maombi kiasi then akaniambia twende nje.

Tukazunguka kwenye eneo la nje akaanza kutafuta tafuta akaniambia ka naona kitu, nikamjibu sioni akatafuta tena na tena kwakutumia mwanga wa simu basi akaanza kusema 'lilikuwa linataka kukimbia tena na leo' basi akakiona kumbe ilikuwa kibuyu na kichupa vimefungwa pamoja na vinashanga na kitu ka irizi nyeusi na nyekundu, nilistaajabu sana. akanijuza kuwa ilikuwa inataka kukimbia na ndo maana siku ya kwanza alishindwa kuikamata. na hizo zana za kishirikina zilikuwepo sehemu nyeupe ambayo ni rahisi kuviona ila akaniambia vilikuwa ndani ya banda lililokuwepo karibu ila kwakuwa alimwaga maji yaliyobarikiwa kikashindwa kukimbia kikaishia hapo nje na akanijuza kwa macho ya kawaida huwezi ona

Mpaka leo najiuliza sana hivi ule ushirikina ulitoka wapi na uliwekwa pale nyumbani toka lini na unawezaje kukimbia pindi nguvu ya Mungu ijitokezapoooo? Mpaka leo lile tukio huwa nalikumbuka sana na vile kibuyu kilivyousisimua moyo wangu.
Pole sana, ni heri umeandika hapa ili ufahamu ukweli, hao watu ni matapeli tu, wanaotumia kivuli cha Mungu ili wawaangamize wengine..Jambo kama lako lilishanitokea na mimi zamani kidogo, lakini kabla ya hapo nilishawahi kuwasikia kwenye radio, lakini sikutilia maanani mpaka nilipokutana nao..

Mazingira yao ni hayo hayo, watakuja day one, wataondoka, kisha watarudi, mara ya pili au hata ya tatu, lakini safari hii wakiwa na vihirizi vyao walivyojiundia wenyewe, na ni lazima waje usiku..sasa wanachofanya ni kuvirusha, aidha nje,au ndani wakati wanapoingia au wanapojifanya wanafanya maombi wakati wewe umefumba macho, lakini kwa siri..Wakishamaliza, wanajifanya wameingia katika rohoni, kisha baadaye wanakwambia nimeona kitu, wanakuambia tuondoke twende..wanaelekea maeneo yale yale yaliyotupa hizo takataka zao, kisha wanajifanya wanatafuta tafuta..

Baadaye wanaona, ndio hapo wanakwambia walikuwa wanataka kukimbia wakaacha hirizi zao..sasa kama wewe ni yule wa kuombewa ombewa tu, bila kujitathimini Imani yako na Mungu wako ipo wapi, watakuzomba na maji haraka sana...

Mimi nilikuwa na watu wengine nao walikuwa wameshaogopa, kumbuka saa hiyo ni usiku wa saa 4 au 5 hivi..Lakini nilivyoona vile nikamweka chini siku subiri muda, nikamuhubiria, nikamwambia hapa umekutana na nuru, na ukijaribu kupambana na Nuru utakuwa kipofu..akaogopa, nikataka kumfukuza, watu wakasema tumwache tu asubiri asubuhi aondoke, ilipofika asubuhi aliondoka kwa aibu ya ajabu, mpaka leo hii sijui yule mtu alipotelea wapi, sijamwona tena..

Hivyo kwa ufupi jua hakuna uchawi wowote hapo,..Usiogope, ila na wewe pia, au mwingine yeyote anayesoma uzi huu, simama katika Imani yako. Mwamini Mungu. Soma Neno..Kwasababu hizi ni nyakati za mwisho. Manabii wengi wa uongo wapo duniani, na watawadanganya wengi..
 
Huna Nyota inayowaka! hii yako imezima kabisa! tunachotaka wachawi ni mwili wenye bahati njema za kuzaliwa! tuna uwezo wa kuwajua! tunajua Ma-Rais, Wafanya biashara! Viongozink , wengine hazitoki wengine zinatoka kabisa!

Ndo pale unaona mtoto hapendi shule, wakati alianza vizuri, Ugonjwa, kufukuzwa kazi, ulevi nk, Mzazi akilegea tu zina chukuliwa mapema utotoni.
[emoji33]Mh! Hata mi nahisi hawa mafala watakuwa walichukua yangu , waliponinyoa nywele usiku
Maana kuna mambo unaset fresh ikifikia wakat wa kuanza mabalaa yanatokea
Mchawi sio m2 mzur kabisa
 
Mwaka 2006 ilitokea binamu yangu akafariki, kipindi hicho tulikuwa tunaishi Bunju na bunju ilikuwa haijawa kama ilivyo sasa hivi yani kulikuwa hakujaendelea.

Kabla ya kufariki alianza kuugua akawa hana nguvu sasa alikuwa ana tabia akitoka kazini wakati anapanda ngazi kwenda chumba chake kwasababu nyumba ilikuwa ni ghorofa chumba chake kilikuwa floor ya juu, akipanda ngazi kama nne anachoka anakaa kwenye ngazi ana guna Mmmh.

Sasa wakati anafariki alikuwa kasafiri kaenda kuhuduhira harusi ya ndugu yake akiwa hhuko mkoa akazidiwa akakimbizwa bugando akafia Bugando. Tulipigiwa simu kuwa kafariki na mazishi yalikuwa hukohuko Mwanza hivyo tulipaswa kuondoka kesho yake kwenda huko. Sasa ajabu kesho yake kabla hatujaondoka, tulianza kumhisi akiwa humo ndani na muda mwingine unasikia akiita au akipanda ngazi na kuguna kama alivyokuwa anafanyaga.
Tukaenda kwenye mazishi tukazika na kurudi.

Hali ikaendelea hasa ile ya kusikia anapanda ngazi na kuguna. Ikawa tukienda kazini ndani anabaki dada wa kazi nyumba anaiogopa anaikimbia anaenda kukaa kwa majirani mpaka tukirudi.

Ikafika kipindi watu tukawa hatulali kila mtu anateseka kwa style yake. Nyumba ikawa siyo nyumba ile yani ikifika muda wa kurudi nyumbani kutoka kazini unatamani ulale huko huko.
Nakumbuka alikuja mchungaji flani akaiomba ile nyumba ndipo visanga vikaisha. Kwa sasa hiyo nyumba iligeuzwa shule.

Kuna mengi nimeyashuhudia ila dunia ina mambo nyie acheni.
 
...yaani umeniongelea mimi mkuu
...sasa sijui tufanyeje ?
[emoji33]Mh! Hata mi nahisi hawa mafala watakuwa walichukua yangu , waliponinyoa nywele usiku
Maana kuna mambo unaset fresh ikifikia wakat wa kuanza mabalaa yanatokea
Mchawi sio m2 mzur kabisa
 
...yaani umeniongelea mimi mkuu
...sasa sijui tufanyeje ?
Mkuu acha tu, mi ningefanikiwa kumtambua nabii WA kweli kwenye dunia ya sasa ningeenda huko akaniponye
Maana wengi ni matapeli
 
Nakumbuka kuna mwaka tulienda kufanya sampling mkoa fulani, kutoka mjini hadi huko kiijijini ni mbali mno na barabara zenyewe ziko hovyo.

Baada ya sampling tukaanza safari ya kurudi mjini, njiani kuna mzee mmoja akatuomba lift tukamwambia mzee gari imejaa akasema sawa,

Basi baada ya kama km 2 gari likaharibika tukachokonoa chokonoa yule mzee akatukuta na akatupita, gari lika faa tuakanza safari, tukampita yule mzee tena ila baadaye likaharibika tena, yule mzee akatupita tena.

Basi mchezo ukawa ule ule mwisho tukaona itakuwa huyu mzee ndo anatuchezea, tukaona ngoja tumpe lift tu, alivyotukuta tena tunachokonoa chokoa tukamwambia mzee, subiri turekebishe tukupe lift mzee akakubari.

Gari lilivyo faa halikuhabirika tena hadi tunafika mjini.
 
Nakumbuka kuna mwaka tulienda kufanya sampling mkoa fulani, kutoka mjini hadi huko kiijijini ni mbali mno na barabara zenyewe ziko hovyo.

Baada ya sampling tukaanza safari ya kurudi mjini, njiani kuna mzee mmoja akatuomba lift tukamwambia mzee gari imejaa akasema sawa,

Basi baada ya kama km 2 gari likaharibika tukachokonoa chokonoa yule mzee akatukuta na akatupita, gari lika faa tuakanza safari, tukampita yule mzee tena ila baadaye likaharibika tena, yule mzee akatupita tena.

Basi mchezo ukawa ule ule mwisho tukaona itakuwa huyu mzee ndo anatuchezea, tukaona ngoja tumpe lift tu, alivyotukuta tena tunachokonoa chokoa tukamwambia mzee, subiri turekebishe tukupe lift mzee akakubari.

Gari lilivyo faa halikuhabirika tena hadi tunafika mjini.
Duh ni hatari mkuu
 
Mwaka 2006 ilitokea binamu yangu akafariki, kipindi hicho tulikuwa tunaishi Bunju na bunju ilikuwa haijawa kama ilivyo sasa hivi yani kulikuwa hakujaendelea.
Kabla ya kufariki alianza kuugua akawa hana nguvu sasa alikuwa ana tabia akitoka kazini wakati anapanda ngazi kwenda chumba chake kwasababu nyumba ilikuwa ni ghorofa chumba chake kilikuwa floor ya juu, akipanda ngazi kama nne anachoka anakaa kwenye ngazi ana guna Mmmh.
Sasa wakati anafariki alikuwa kasafiri kaenda kuhuduhira harusi ya ndugu yake akiwa hhuko mkoa akazidiwa akakimbizwa bugando akafia Bugando. Tulipigiwa simu kuwa kafariki na mazishi yalikuwa hukohuko Mwanza hivyo tulipaswa kuondoka kesho yake kwenda huko. Sasa ajabu kesho yake kabla hatujaondoka, tulianza kumhisi akiwa humo ndani na muda mwingine unasikia akiita au akipanda ngazi na kuguna kama alivyokuwa anafanyaga.
Tukaenda kwenye mazishi tukazika na kurudi. Hali ikaendelea hasa ile ya kusikia anapanda ngazi na kuguna. Ikawa tukienda kazini ndani anabaki dada wa kazi nyumba anaiogopa anaikimbia anaenda kukaa kwa majirani mpaka tukirudi.
Ikafika kipindi watu tukawa hatulali kila mtu anateseka kwa style yake. Nyumba ikawa siyo nyumba ile yani ikifika muda wa kurudi nyumbani kutoka kazini unatamani ulale huko huko.
Nakumbuka alikuja mchungaji flani akaiomba ile nyumba ndipo visanga vikaisha. Kwa sasa hiyo nyumba iligeuzwa shule.
Kuna mengi nimeyashuhudia ila dunia ina mambo nyie acheni.
Mmh...aliyemviza yupo karibu yenu kabisa..
 
Nakumbuka kuna mwaka tulienda kufanya sampling mkoa fulani, kutoka mjini hadi huko kiijijini ni mbali mno na barabara zenyewe ziko hovyo.

Baada ya sampling tukaanza safari ya kurudi mjini, njiani kuna mzee mmoja akatuomba lift tukamwambia mzee gari imejaa akasema sawa,

Basi baada ya kama km 2 gari likaharibika tukachokonoa chokonoa yule mzee akatukuta na akatupita, gari lika faa tuakanza safari, tukampita yule mzee tena ila baadaye likaharibika tena, yule mzee akatupita tena.

Basi mchezo ukawa ule ule mwisho tukaona itakuwa huyu mzee ndo anatuchezea, tukaona ngoja tumpe lift tu, alivyotukuta tena tunachokonoa chokoa tukamwambia mzee, subiri turekebishe tukupe lift mzee akakubari.

Gari lilivyo faa halikuhabirika tena hadi tunafika mjini.


Mzee alitisha sana huyo😄
 
Pol
Dah imenikumbusha miaka ya 90s nikiwa Tabora wilaya moja hivi kijijini nikichukua elimu ya msingi shule yetu ilikuwa upande wa magharibi kuna makaburi halafu shule ina miti kibao ya mikaratusi,mikorosho mijohoro mizambarawe na miti fulani hivi inatoa ubani upepo ukipiga inavuma kama gari,

Dah nakumbuka hiyo siku niliamka kwenye kigheto changu pale home kama saa nane hivi mabalamwezi imekubali nje maana ilikuwa wiki ya mwalimu mmoja hivi kusimamia usafi na wechelewaji na ukichelewa unapata bakora za miguuni na lile baridi la kijijini balaa mwanaume mbalamwezi ile nikajua kumekucha nikanawa faster faster hata sikuwastua wazazi ambapo sio kawaida huwa lazima niwaamshe kwenye gheto lao mzee nikanyanyua ufagio mkononi na kidumu cha maji mbio kwenda kabla ya kufika shule kuna kipori fulani lazima ukipite ndio ufike shule mwanaume sikujari japo njiani sikuona mtu yeyote hiyo haikunistua mie nilijona mshindi leo nawahi namba shule,

aisee nimepita chini ya mikorosho na hiyo miti mingine bila kujari nahisi akili haikuwa yangu nakumbuka nafika shule nikakimbilia darasani nafika mlangoni nilichokishuhudia acha niliona moto mkubwa unawaka mule na kuna watu wamekaa kama wako kwenye kikao halafu wote wakaniangalia ila sura sikuziona hapo ndio akili ikarudi kwamba nimezingua niligeuka mbio kurudi home halafu ule upande wa makaburi nilishuhudia watu wakiwa na mguu mmoja wanaruka ruka kwa mstari mbio zangu nilikuwa nahisi kuna kitu nyuma kinanifata kugeuka nyuma niliona mtu mrefu sana kichwa hakionekani ila kavaa vazi refu linag'aa kama mbaramwezi ilivyokuwa inag'aa mwanaume niliongeza speed nilienda nikaingia na mlango mpk ndani yule jini sijui nini nilipokaribia nyumbani nilisikia msonyoo mmoja hatari sana wazazi wakaamka kufungua mlango kuja kunikuta sijitambui wakanichukua nikaenda kulala kwao asubuhi ndio kuwaelezea ni moja ya tukio ambalo huwa sipendi kabisa kulikumbuka maana baada ya hapo mpk leo kuna vitu huwa naviona ambavyo sio vya kawaida na niliwasumbua sana wazazi baada ya hapo . nimejaribu kufupisha ila kuna mambo mengi sana kwa ule usiku na miaka ile niliyashuhudia baada ya ilo tukio.
 
Back
Top Bottom