NMB Tanzania Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri

nmb mmekuwa mkichelewesha cheque za mishahara zinazo kwenda benki nyingine kwa makusudi kitu ambacho ni usumbufu hasahasa mishahara
 
Mimi niliomba mkopo toka mwezi march mwanzoni mpaka leo sijapata kitu, ingawa nilipata offer letter ambayo ninatakiwa kupata pesa within 14 days ila huo muda umepitiliza bila ya majibu yoyote kutoka kwa wahusika?? je ni mimi ndo nina tatizo kama hilo au wenzangu mna experience gani?? kama loan officer anahitaji rushwa si awe wazi na siyo kwa kificho???
kila siku excuses!!!! till when ?? am tired of nmb bank!!!!!
 
hawa jamaa wamewachoka wateja wao. siku hizi hawajali kabisa.
 
NMB ni kero mnajijua mnawateja wengi kwann atm chache jana nimeshindwa kutoa hela ifakara na kwa nn songea hamfungui blanchi jingine mnaona raha gani kulundika watu pale
 
biharamulo network yenu inazingua hadi leo password ya kadi hamna kila siku njoo kesho n shda
 
Nmb kwanini mnapenda kuona watu wamepanga mstali mrefu kwenye bank zenu kusubiria huduma?aisee uwajibikaji kwenu mm naona ni sifuri na Bahati yenu mna matawi mpaka vijijini isingekuwa ivyo hakika crdb wangewapita kwa kasi ya ajabu
 

nmb ni benk kubwa sijui kwa nn mnashindwa kununua viti vya wateja kukaa? Mbona benk ndogo wameweza? Too boring.

Kingine dah vidada vya nmb vinaringa ndo ukute kabaki mwenyewe may be break time utakoma sijui wanatufanyia sisi wadada wenzao au na wanaume ndo ivo? Afu wakawaida sasa sijui kwa nn wanaringa wakati hela zetu ndo mishahara yao?
 
Me nawaombaga kazi kila.kukicha hamnipi sasa sijui mnaajili walio soma bible knowledge?maana basi bora nijue basi kuwa interview imenishinda sasa hata shortlist duu na degree ya marketing u mean hata customer care siwezii..mungu wangu endelea kubariki kazi za mikono yetu wana wa network query
 
Nmb kwanini mnapenda kuona watu wamepanga mstali mrefu kwenye bank zenu kusubiria huduma?aisee uwajibikaji kwenu mm naona ni sifuri na Bahati yenu mna matawi mpaka vijijini isingekuwa ivyo hakika crdb wangewapita kwa kasi ya ajabu

-foleni hapa na mbagala!(ndani branch na kwenye atm)
-atm zenyewe zipo chache kila branch halafu zipo very slow
-kwa nini msiingie kwenye huduma za visa na master card?mpo manual sana...na mkiingia tu kwenye visa/master card tunawakimbia wote
-poa customer service
 
Nataka kufanya payment ya online do you guys have visa ...? Plz PM me majibu cause naeza nisione hapa
 
nimefungua A/C ila sijapewa ATM Card,je naweza kuchua pesa? ikiwa tayari nina Account Number?
 
Huduma ni nzur. Ila rekebisheni baadhi ya ATM zinakuwana matatizo ya kutoa risiti bila pesa. Naukifuatilia utachukuwa takribani wiki ili kuipata pesa hiyo
 
Juzi nimedraw million 8....kabla cjapewa Pesa nimeulizwa maswali mia kidogo mpaka nikaisi Pesa nimeiba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…