NMB wagoma kurudisha hati ya nyumba, japo deni lao limeshalipwa lote

 NMB wagoma kurudisha hati ya nyumba, japo deni lao limeshalipwa lote

Status
Not open for further replies.
Lengo la benki wanakulazimisha ukope tena kwao hiyo tabia ni kawaida sanaa kwa benki za bongo, wanakopesha ili wakufilisi kwa kushindwa kulipa sasa hapo wakutegemea kama utamaliza, hati utapewa ila baada ya kuisotea .
Unakua kama unaomba msaada wakati ni hako yako
 
Unaweza kuta nyumba walishauza maana walijua hataweza toboa malipo! Hapo aandike barua kwa meneja wa benki au branch kuomba hati, kama asipopewa jibu zuri basi atafute wakili matata! Hapo ni kesi anafungua na kuomba fidia ya usumbufu!

Pia akishaandika barua asipopewa majibu mazuri anaweza peleka TAKUKURU wa eneo hilo then takukuru watamuita yeye pamoja na meneja wa benki atoe ufafanuzi!
Yote hayo ya kuandika barua ameshafanya imagine 5years kila siku wanasema utapigiwa simu
 
Juzi rafiki yangu alikuwa ananipa stori kuhusu mama yake. Alichukua mkopo NMB kama miaka 5 iliyopita, akaweka hati ya nyumba yake kama dhamana.

Uyo Mama kahangaika sana hadi akalipa deni lote, AJABU NMB SENGEREMA hawataki kumpa hati yake. Mbona kama nanusa mchezo mchafu? Inakuwaje benki kubwa hivi hawajahifadhi hati ya huyu mteja kwamba akimaliza mkopo wamrudishie mali yake?

Ziadi ya miaka 4 wanamzungusha mama wa watu amejaribu hata kutafuta watu anaojuana nao huko NMB ila nao hawasaidii kitu hebu anayeweza kufikisha taarifa, afikishe.

NMB tawi la SENGEREMA kuna mtu anataka kumpiga huyo Mama nyumba yake. Sio sawa
Lah!
Mwambie huo mama achunge namba sana.
Kumbukumbu zake zote zinazohusiana na mkopo na ulipaji wa mkopo awe nazo karibu sana. hao Benki wasije kuibuka na kutaka kunadi nyumba.
Lakini kwa maelezo yako, hujasema lolote Benki wanasemaje kuhusu mkopo huo. Wanamwambia mama nini kuhusu kurudishiwa hati yake. Wewe umesema "anazungushwa tu", anazungushwa vipi, na nani kwenye hiyo Benki. Ni nani hasa anashughulikia swala lake moja kwa moja. Kisha fika kwa meneja wa tawi? Kaambiwa nini, tueleze nasi tujue kabla hujatushirikisha katika kuwalaumu Benki.
 
Juzi rafiki yangu alikuwa ananipa stori kuhusu mama yake. Alichukua mkopo NMB kama miaka 5 iliyopita, akaweka hati ya nyumba yake kama dhamana.

Uyo Mama kahangaika sana hadi akalipa deni lote, AJABU NMB SENGEREMA hawataki kumpa hati yake. Mbona kama nanusa mchezo mchafu? Inakuwaje benki kubwa hivi hawajahifadhi hati ya huyu mteja kwamba akimaliza mkopo wamrudishie mali yake?

Ziadi ya miaka 4 wanamzungusha mama wa watu amejaribu hata kutafuta watu anaojuana nao huko NMB ila nao hawasaidii kitu hebu anayeweza kufikisha taarifa, afikishe.

NMB tawi la SENGEREMA kuna mtu anataka kumpiga huyo Mama nyumba yake. Sio sawa
Je ana kumbukumbu zote za malipo ya marejesho? Huo utakuwa uthibitisho kwamba alikopa benki
Hapo nimetumia akili za kuvukia barabara
 
Ndugu Zangu Majizi Yapo Hata Bank
Alipokopa Mkopo Alipewa Mkataba Unaoonyesha Pesa Na Makato Kila Mwezi Na Mwaka Wa Kumaliza. Kama Mleta Mada Huyo Mzee Wako Anao Anaweza Kukuonyesha
Warudishe Hati Hapa JF Hili Jambo Halitapita Kimya Tawi Husika Wafanye Hima
 
Mbona hapo NMB wamempa biashara nzuri ya kuwapiga fidia ya mamilioni? Hapo ni mahakamani straight kuvuna hela za bure. Sema NMB nao wanaangalia sura za kuwafanyia huo upuuzi.
 
Ungefuata taratibu ungewasiliana na bank husikia unaweza ukawa umekurupuka kuja mtandaoni kuleta lawama, ungemtafuta mkurugenzi mkuu kama unataka kusaidia
Yote hayo wameshafanya juzi tu hapa ameenda ameambiwa "nenda tutakupigia simu" hii ni mpaka lini yani mtu anasuburi kupigiwa simu kwa miaka 5 kweli?
 
Ndugu Zangu Majizi Yapo Hata Bank
Alipokopa Mkopo Alipewa Mkataba Unaoonyesha Pesa Na Makato Kila Mwezi Na Mwaka Wa Kumaliza. Kama Mleta Mada Huyo Mzee Wako Anao Anaweza Kukuonyesha
Warudishe Hati Hapa JF Hili Jambo Halitapita Kimya Tawi Husika Wafanye Hima
Amefata process zote na barua ya kuomba hati aliandika lakini kila akienda anaambiwa aondoke tu atapigiwa simu. NAOMBA TUSAIDIANE KUPATA HAKI YA HUYU MAMA
 
Lah!
Mwambie huo mama achunge namba sana.
Kumbukumbu zake zote zinazohusiana na mkopo na ulipaji wa mkopo awe nazo karibu sana. hao Benki wasije kuibuka na kutaka kunadi nyumba.
Lakini kwa maelezo yako, hujasema lolote Benki wanasemaje kuhusu mkopo huo. Wanamwambia mama nini kuhusu kurudishiwa hati yake. Wewe umesema "anazungushwa tu", anazungushwa vipi, na nani kwenye hiyo Benki. Ni nani hasa anashughulikia swala lake moja kwa moja. Kisha fika kwa meneja wa tawi? Kaambiwa nini, tueleze nasi tujue kabla hujatushirikisha katika kuwalaumu Benki.
Ipo hivi huwa anaenda Bank kufuatilia hati lakini akifika anaambiwa "NENDA TUTAKUPUGIA SIMU" KWA MIAKA 5 SASA na ameshaonana hadi na meneja wa Benk akampa kijana wa kufatilia huyo kijana na yeye kamwambia siku fulani urudi utakuta tayari, hiyo siku imefika amerudi anaambiwa "MAMA WEWE NENDA TU NITAKUPIGIA SIMU NITAITAFUTA" kwa hiyo akiendelea kusubiri kupigiwa simu si itachuka miaka 10 aiseee
 
Amefata process zote na barua ya kuomba hati aliandika lakini kila akienda anaambiwa aondoke tu atapigiwa simu. NAOMBA TUSAIDIANE KUPATA HAKI YA HUYU MAMA
Atapewa Na Endapo Wanangoja Kuuziana Wstaumbuka Sasa, Tanzania Shida Sana
Tawi Lao Lipo Hapo RoundAbout Sengerema
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom