NMB wagoma kurudisha hati ya nyumba, japo deni lao limeshalipwa lote

 NMB wagoma kurudisha hati ya nyumba, japo deni lao limeshalipwa lote

Status
Not open for further replies.
Nyinyi mnaomfahamu huyo mama na munao uelewa wa kutosha, msaidieni.
Kwanza kabisa, maneno ya mdomoni tu hayasaidii chochote. Inatakiwa pawepo na kitu, karatasi ya ushahidi kuwa hivyo alivyo ambiwa kwa miaka mitano ndivyo kweli.
Ni lazima aweke katika maandishi lawama zake zote tokea alipoanza kuzungushwa. Majina ya watu alioonana nao huko Benki anayo?
Ni lazima pawepo na ushahidi wa kimaandishi. Kama Benki hawajibu, hilo litakuwa tatizo lao, siyo lake.
Nyaraka za mkopo zipo, hakupewa mkopo kwa kutumia maneno ya mdomoni tu. Malipo kafanya, natumaini siyo kwa mdomo tu, bali stakabadhi zote anazo; na pengine hata barua ya Benki kuonyesha kwamba hadaiwi tena baada ya kulipa kila kitu, anayo.
Tahadhari: Asije kuwa analipa na pesa haiingizwi kwenye 'account' yake. Asije akashangaa mwisho wa siku anaambiwa mkopo bado haujalipwa.
Awahusishe na viongozi wa kijamii, kama hawezi kwa sasa kwenda mahalkamani.

Kwenda Benki na kupewa taarifa ya mdomo anapoteza tu muda wake.
Shukrani sana na ndio maana tumekuja huku ilo tupate mawazo mbalimbali tupate pa kuanzoa au hao NMB wakiona itakuwa sawa pia
 
Juzi rafiki yangu alikuwa ananipa stori kuhusu mama yake. Alichukua mkopo NMB kama miaka 5 iliyopita, akaweka hati ya nyumba yake kama dhamana.

Uyo Mama kahangaika sana hadi akalipa deni lote, AJABU NMB SENGEREMA hawataki kumpa hati yake. Mbona kama nanusa mchezo mchafu? Inakuwaje benki kubwa hivi hawajahifadhi hati ya huyu mteja kwamba akimaliza mkopo wamrudishie mali yake?

Ziadi ya miaka 4 wanamzungusha mama wa watu amejaribu hata kutafuta watu anaojuana nao huko NMB ila nao hawasaidii kitu hebu anayeweza kufikisha taarifa, afikishe.

NMB tawi la SENGEREMA kuna mtu anataka kumpiga huyo Mama nyumba yake. Sio sawa

Pia soma


Hivi ni kweli kuwa hao jamaa wanakata wateja shilingi 17,000/- kwa kila saving account ya kila mteja kwa kila mwezi ? 🙆‍♂️🤦‍♀️
 
Shukrani sana na ndio maana tumekuja huku ilo tupate mawazo mbalimbali tupate pa kuanzoa au hao NMB wakiona itakuwa sawa pia
Mkuu 'Nyabukika', nadhani tayari mmepata ushauri wa kutosha hapa kuweza kumsaidia huyo mama. 'THE BEEKEEPER' kaweka hata nanmba ya simu.

Mkifanikiwa hili usikose kurudi hapa JF kutoa mrejesho, maana mtandao huu unaweza kuwa na msaada kwa watu wanaoonewa kwa njia mbalimbali.
Acheni ujuaji wa kushauri vitu ambavyo hamvijui. TAKUKURU akafanye nini?

The best solution ni kumuona Wakili ambaye atamuandikia demand notice and an intention to sue au Kwa Kiswahili inaitwa HATI YA MADAI NA KUSUDIO LA KUSHTAKI.

WAKILI aipe Benki siku kadhaa (30 zinatosha) kuhakikisha kwamba wame-release Hati ya nyumba ya mteja wake, aombe na fidia ya usumbufu na gharama za huduma ya Wakili (Mimi hapo ningeomba 10 million) ili waki-bargain watoe hata 7 million.

Niliwahi kuwa na scenario kama hii Dodoma, Benki ilikuwa CRDB, niliwachapa demand notice ya siku 21 nikaomba na fidia ya million 7, ilivofika siku ya 9 Meneja wa Tawi akanipigia simu niende ofisini kwake nikiwa na mteja wangu. Kufika akaanza kuwa mpole, ooh unajua wateja wakikopa Huwa hati tunazipeleka Makao makuu ya benki Dsm
emoji28.png
emoji28.png


Baadaye wakabembeleza wakatoa mil 3 na kuahidi kui-release hati baada ya siku 3, tukasepa zetu na mteja wangu na kibunda chetu, baada ya siku 3 akarudishiwa hati yake.

Hao sio wa kuwachekea.
Mimi nimependa huu hapa.
Mwambieni mama asipoteze sana muda wake mwingi kwenda Benki. Miaka mitano kuzungushwa ni muda mrefu sana; sasa ni kuchukua hatua tu, basi.
THE BEEKEEPER kaweka namba ya simu, wasiliana naye kama anaweza kusaidia.
 
Kwahiyo bank watakuja kukiri kwamba hawajairudisha pamoja na kuwa wamelipwa? Mi ninachojua nimesharudishiwa, nani atapinga?
Mbona hueleweki?
Unamaana Benki ing'ang'ane kuwa walishamrudishia huyo mama hati yake?
Ingekuwa hivyo si wangekuwa walishamtoa njiani tayari kwa madai walisharudisha hati?
Hati inapotolewa Benki kupata mkopo kuna nyaraka zinazowekwa sahihi. Nina hakika pia inaporudishwa baada ya kumaliza deni kutakuwepo na makabidhiano kwa nyaraka. Sasa labda useme Benki waghushi sahihi ya huyo mama. Hili litakuwa swala tofauti kabisa na haya yanayojadiliwa.
 
Shukrani sana na ndio maana tumekuja huku ilo tupate mawazo mbalimbali tupate pa kuanzoa au hao NMB wakiona itakuwa sawa pia
Huyo mama ana barua ya kumaliza mkopo, maana wengine husema wamelipa deni lote kumbe kuna interest zimeongezeka, ikiwa kamaliza na alishawahia kuandika barua ya kuomba hati , basi achukue hiyo barua aandike barua ya malalamiko kwenda BoT akiomba apewe hati yake na benki wanavyomsumbua awacopy na Benki kwenye hiyo barua , apeleke barua customer protection desk(kama sijakosea) . Akifikisha hapo BoT watawaandikia barua tu NMB ambayo responce yake ni kati ya siku 7 au 14 , kama kweli alimaliza atapewa hati yake. Maana huko BoT ukichelewa kujibu tu fine bank inapigwa . Ikifail huko sasa ndio aende kwa wakili maana najua hii njia ya pili inagharama
 
Acheni ujuaji wa kushauri vitu ambavyo hamvijui. TAKUKURU akafanye nini?

The best solution ni kumuona Wakili ambaye atamuandikia demand notice and an intention to sue au Kwa Kiswahili inaitwa HATI YA MADAI NA KUSUDIO LA KUSHTAKI.

WAKILI aipe Benki siku kadhaa (30 zinatosha) kuhakikisha kwamba wame-release Hati ya nyumba ya mteja wake, aombe na fidia ya usumbufu na gharama za huduma ya Wakili (Mimi hapo ningeomba 10 million) ili waki-bargain watoe hata 7 million.

Niliwahi kuwa na scenario kama hii Dodoma, Benki ilikuwa CRDB, niliwachapa demand notice ya siku 21 nikaomba na fidia ya million 7, ilivofika siku ya 9 Meneja wa Tawi akanipigia simu niende ofisini kwake nikiwa na mteja wangu. Kufika akaanza kuwa mpole, ooh unajua wateja wakikopa Huwa hati tunazipeleka Makao makuu ya benki Dsm [emoji28][emoji28]

Baadaye wakabembeleza wakatoa mil 3 na kuahidi kui-release hati baada ya siku 3, tukasepa zetu na mteja wangu na kibunda chetu, baada ya siku 3 akarudishiwa hati yake.

Hao sio wa kuwachekea.
Wewe ndo mjuaji sasa, Hakuna wakili anakupa demand notice ya siku 21, kisheria ni siku 90. Na Takukuru anaenda kudai kwamba anatengenezewa mazingira ya rushwa kabla hajachukua hatua zaidi. Kama mkopo kamaliza, kwanini wanamcheleweshea hati yake..?
Unaleta personal feelings kwenye kazi ambazo tunazifanya kila siku na watu wanasaidika. Hii njia ya wakili kuna gharama ndo maana tunamshauri apite PCCB kwanza then baada ya hapo kuna hatua za kufuata kama kuiandikia BOT au kwenda moja kwa moja mahakamani. Hii ya kupitia BOT ina pro na cons zake ambazo sina tu muda wa kuanza kukuelezea hapa.
 
Juzi rafiki yangu alikuwa ananipa stori kuhusu mama yake. Alichukua mkopo NMB kama miaka 5 iliyopita, akaweka hati ya nyumba yake kama dhamana.

Uyo Mama kahangaika sana hadi akalipa deni lote, AJABU NMB SENGEREMA hawataki kumpa hati yake. Mbona kama nanusa mchezo mchafu? Inakuwaje benki kubwa hivi hawajahifadhi hati ya huyu mteja kwamba akimaliza mkopo wamrudishie mali yake?

Ziadi ya miaka 4 wanamzungusha mama wa watu amejaribu hata kutafuta watu anaojuana nao huko NMB ila nao hawasaidii kitu hebu anayeweza kufikisha taarifa, afikishe.

NMB tawi la SENGEREMA kuna mtu anataka kumpiga huyo Mama nyumba yake. Sio sawa

Pia soma
Naomba msaada wa wakili mzuri aliyepo Sengerema, Mwanza atakayeweza kusaidia hili suala la NMB kugoma kutoa hati ya mteja wao kwa miaka mitano
Watakua wameikopea tena
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom