NYARAKA: Katiba Inayopendekezwa Oktoba, 2014 (Tanzania's Proposed Constitution)

NYARAKA: Katiba Inayopendekezwa Oktoba, 2014 (Tanzania's Proposed Constitution)

Unafikiria kwa kutumia utumbo wewe, unabwabwaja tuu ili uingize siku.

Tangu lini utumbo ukatumika kufikiri? Kwahiyo ukawa ndo mnafikiri kwakutumia kichwa?

Kama ndiyo mbona mmepigwa -kumbo???
 
Nakshi ndio neno sahihi .ila bora katiba ya sasa kuliko hii rasimu
Kuweka haki za bongo flavor ndani ya katiba lakini ukutaa kuwawekea waislam utaratibu mzuri wa sheria ili wapate haki zao za ndoa urithi na malezi ya watoto kwa mujibu wa taratibu zao sioni uzuri wa hii rasimu ya chenge
Tayari tuna sheria ya copy right hivyo kuweka hili haki za bingo flavor kikatiba ni mbinu ya kuimbiwa bongo flavor wakati wa kampeni.
Kama ni katiba ya muungano siungi mkono neno kuulinda muungano. Kuna wakati ndani ya muungano mmoja wenu atasema ama sasa basi kwa sababu mbali mbali hivyo kujitoa lazima .katiba isilazimishe kuukosoa muungano ni dhambi ili ya kina farid yaendelee.
Katiba hii ni ya muungano wa nchi mbili lakini wazanzibar hawana ruhsa kuweza kuingoza nchii hii. Makamo wa rais imefanywa atoke znz maisha na sasa rias wa znz ndio makamo tena wa pili na makamo wa kwanza na waziri mkuu ni mtanganyika then unaweka kipengele kuwa hakuna kuusema muungano.
Lazima tungeweka utaratibu wa kupokezana urais huu muungano ni wa nchi mbili.
Kuna kifungu cha mikopo na mashirika hii ni pipi ya maneno huwezi kujiunga na WHO OIC UNESCO SADDC EAC Nk kama sio memba wa UN.
Hata FIFA hawataweza itabaki kuwemo kwenye kijarida cha Sita
Naipitia vizuri lakini hakuna uzurii wowote hasa kwa znz na ni kitanzi cha mwisho kwa visiwa hivyo kufutwa rasmi katika ramani ya dunia
 
Kama watu wenye uelewa wa namna hii wapo wengi hapa nchini,utawala bora utakuwa ni ndoto

Kwahiyo uelewa mzuri ni wenu kuhanikiza mnataka katiba mpya halafu mnakimbia mchakato??

Au uelewa mzuri ni Wa ukawa kushinikiza mambo ya kipuuzi yaingie kwenye katiba??
 
Kuainisha haki za makundi mbalimbali haitoshi, kuweka mfumo bora wa kikatiba wa kutekeleza haki hizo hiki ndicho kimekosekana katika katiba pendekezwa.
 
Kwa hiyo unakubaliana nami kuwa katiba hiyo sio mpya bali ni ile ile ya zamani iliyofanyiwa marekebisho? Kwa msingi huo basi Kikwete alikuwa na haja gani ya kuunda tume ya katiba wakati alijua wazi kuwa anahitaji marekebisho ya katiba na sio katiba mpya? Au tafsiri ya upya kwenu ni kubadili kava la nje? Au ndo namna ya kuwadanganya wananchi na hao wanaojiita bunge la katiba kuwa wameweka historia ya katiba mpya kumbe ukweli wameweka historia ya kurekebisha katiba ya zamani?

Huwezi ukawa na katiba mpya yenye mfumo ule ule. Kama mahitaji yaliopo hayahitaji mfumo kubadilika basi hakukuwa na haja ya katiba mpya. Kilichotakiwa ni maboresho tu ya katiba iliopo. Kazi ilotakiwa ifanywe la bunge la jamuhuri.

Binafsi sioni haja ya mapendekezo haya kupelekwa kwa wananchi maana hayakidhi vigezo vya upya wa katiba.

Kama Hakuna mabadiliko ya mfumo hakuna katiba mpya.

Wewe shukuru Mwenyezi Mungu tumepata katiba bila kumwaga damu ndio jambo la msingi wezetu kenya walimwaga damu tuwe makini na hao viongozi waroho wamadaraka
 
usisizungumzie ujumla imawalenga wakulima ,wafugaji wavuvi kivipi, achene kauli za jumla,kama umeweza kuongeza viti vya ubunge kutoka 75 mpaka 390,mwananchi ,mkulima,mvuvi amelindwaje,madaraka ya rais yameongezeka,mkulima kalindwaje,rais wa zanzibar automatically anakuwa kiongoz wa watanganyika,mkulima kalindwaje,mwananch hawezi kumuajibisha kiongozi aliyemchagua hapo mkulima,mvuvi,mfuagaji amelindwaje.acheni mahaba ya vyama
 
WanaJF

Natumaini wote ni wazima na mnaendelea kulitumikia taifa letu.

Tunaomba mwenye Nakala ya Katiba inayopendekezwa airushe humu mjengoni ili tuanze kazi ya kufanya mahusianisho na ile ya Mhe. sana Mzee wetu Jaji Sinde Warioba. Nitahukumu BMK baada ya kuisoma hiyo katiba ili niweze kuwa na "grounds" za kuitetea au kuikataa. Tafadhali wadau irusheni. Jana Nilishamwona Mhe. Lissu akiwa nayo Arusha. Kama vipi Katibu wa Bunge Kashilila airushe kwenye mtandao wa Bunge au warudishe na zile document za Warioba warushe maana wameshamaliza mission yao.
 
WanaJF

Natumaini wote ni wazima na mnaendelea kulitumikia taifa letu.

Tunaomba mwenye Nakala ya Katiba inayopendekezwa airushe humu mjengoni ili tuanze kazi ya kufanya mahusianisho na ile ya Mhe. sana Mzee wetu Jaji Sinde Warioba. Nitahukumu BMK baada ya kuisoma hiyo katiba ili niweze kuwa na "grounds" za kuitetea au kuikataa. Tafadhali wadau irusheni. Jana Nilishamwona Mhe. Lissu akiwa nayo Arusha. Kama vipi Katibu wa Bunge Kashilila airushe kwenye mtandao wa Bunge au warudishe na zile document za Warioba warushe maana wameshamaliza mission yao.

Umenena vyema mkuu, katiba inayopendekezwa ipo hapa.

Tovuti Rasmi ya Bunge Maalum la Katiba. |

Nenda sehemu ya matangazo utapata nakala uisome upate msingi wa hoja
 
Big_in hatujapata katiba mpya bado bali tunaletewa katiba ya 77 ilofanyiwa marekebisho.

Huwezi kuwa na nyumba ileile kisa umeipiga rangi ukaiita ni mpya. Wakati kila kilichomo ndani ni kile kile cha zamani.

Neno Mfumo lina maana kubwa sana na mara nyingi watanzania tuu waoga wa kubadili mifumo. Lakini hatuwezi kupiga hatua mbele bila mfumo kubadilika. Tulikuwa na mfumo wa chama kimoja ikafikia mahala ikawa hauwezi tena kukidhi haja za siasa tumelazimika kubadili mfumo na kuingia wa vyama vingi. Sasa mfumo wa katiba hii ya 77 umefika mwisho lazima ubadilike tu. Na kama watawala hawataki kuubadili kwa amani ni kweli utangarimu damu za watu na hiyo ndio gharama ya mabadiliko pindi yanapokuja na watawala wanazuia.

Waache watawala waendelee kufurahia mfumo wao ulopitwa na wakati. Ila wajue wazalendo wa kweli wa nchi hii tutaendelea kuhamasisha mabadiliko hadi yapatikane
 
Hii katiba ni nzuri ndio lakini huko juu kwenye viongozi ndio kuna tatizo! Wanataka kutumia njia hiyo kuwafunga macho wananchi wasione jinsi walivyojipendelea wao viongozi.
 
...Hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja, na ikifika wakati watanzania wote tukawa na mawazo yanayofanana basi tujue kwamba tunapaswa kujitazama upya. Kutofautiana kimtazamo ni jambo la kawaida na
...

CCM iliamua kuwa na msimamo mmoja - no discussion. Waliojaribu kwenda kinyume, walitishwa kimya kimya na mmoja tayari kafukuzwa kazi kimbwa huko Zanzibar. So, jitazameni upya.
 
Ina weza kuwa bora kuliko ya sasa ila si bola kwa mifumo tuliyo nayo sasa tusishangae kesho tukaanza marekebisho ya katiba kama ujui mwone kano mzuri wa katiba utaona ipo sawa lakini ina geps ambazo ni muhimi sana
 
Katiba ya kinafiki.Haina jipya la msingi.Hizo haki za wafugaji na wakulima ni hadaa tu.Tulitegemea katiba mpya ingefumua muundo wa uongozi ili kutatua kero sugu kama ufisadi, uwajibikaji , masuala ya muungano na muingiliano wa mihimili.
Katiba pendekezi imewabeba wenye mamlaka na kuwahadaa wananch wa kawaida.
 
KATIBA INAYOPENDEKEZWA NI BORA KULIKO YA SASA, HONGERA MH. RAISI, HONGERA WATANZANIA.

Katika historia ya uandishi wa katiba mpya duniani hakuna nchi yeyote ambayo iliwahi kuandika katiba mpya ikakidhi matakwa ya wananchi wote na taifa kwa 100%. Katiba si msaafu wala si biblia kwamba haiwezi kufanyiwa maboresho. Leo hii jambo ambalo tumeliona lina tija na manufaa kwa taifa na tukaliingiza kwenye katiba, kesho tutaliona halina tija na tutakubaliana kuliondoa au kuliboresha. Vilevile jambo ambalo leo tumeliona halina tija na kutoliingiza ndani ya katiba kesho tutaona umuhimu wake na tutakubaliana kuliingiza ndani ya katiba yetu.

Katiba inayopendekezwa imetambua haki za makundi mbalimbali kama vile wakulima, wafugaji, wafanyakazi, wasanii, vijana, wanawake na wengine. Pia katiba inayopendekezwa imetambua haki bunifu, mgombea, binafsi, maboresho katika muungano wetu sambamba na kuweka mfumo bora wa kusimamia rasirimali za taifa na kudhibiti mianya ya matumizi mabovu ya rasirimali. Kundi pekee ambalo linadhani halijatendewa haki katika katiba hii ni kundi la wanasiasa wachache ambao kwao tafsiri ya katiba bora ni ile inayokidhi maslahi yao ya kisiasa. Hili ni jambo ambalo watanzania hawana budi kulikataa.

Jambo la msingi ambalo kila mtanzania anapaswa kukubali ni kwamba katiba inayopendekezwa ni bora kuliko ile ya sasa. Wakati ambapo baadhi ya watu wakiipinga na kudai kwamba haiwezi kulivusha taifa letu, wapo watanzania tena asilimia kubwa ambao wanaiona katiba inayopendekezwa kuwa ni chombo madhubuti ambacho kitachochea maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja, na ikifika wakati watanzania wote tukawa na mawazo yanayofanana basi tujue kwamba tunapaswa kujitazama upya. Kutofautiana kimtazamo ni jambo la kawaida na
hiyo ndiyo afya ya demokrasia iache ichukue nafasi yake. Tupingane kwa hoja bila kuhatarisha amani ya taifa letu.

Hongera Mh. Raisi Dr. Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa uliyoifanya. Hili ni jambo la kihistoria ambalo halijawahi kutokea katika historia ya Taifa. Hii ni mara ya kwanza kwa Taifa letu kuandika katiba yake kwa kushirikisha wananchi wake. Yapo mataifa ambayo yaliwahi kuandika katiba zao kwa kutumia Bunge la katiba pekee, wapo waliogeuza Bunge la kawaida na kuwa Bunge la katiba. Kwa taifa letu, mchakato umekuwa wa kidemokrasia zaidi kiasi kwamba wapo wanazuoni, wanasiasa na mataifa mbalimbali ambao wameishangaa Tanzania kwa kuruhusu demokrasia kwa kiwango hiki. Kwa hakika Mh. Rais anastahili pongezi na daima watanzania tutakukumbuka na jina lako haliwezi kufutika katika fikra zao.

Mkuu naona wewe ni member mpya mpya hapa kwenye jamvi. Hapa Kwa kawaida huwa hatuwasifii watu kufanya kazi waliomba kutaka kuifanya. Huwa hatumsifii baba kwa kumnunulia mtoto wake viatu. Kwa hiyo ni vizuri ukijisemea mwenyewe usiwasemee watanzania wote, si wote tunajikomba.

Tukiachana na hilo, tukiangalia undani wa katika yenyewe, sina hakika kama kwenye JK ndiye aliyfanya kazi ya kuandika katiba hadi astahili pongezi. Hata kama kweli utamsifu JK kwa katiba hii, inawezekana hata JK mwenyewe atakuona mj!nga, mtu yoyote mwenye akili timamu hata siku moja hawezi kusema katika hii ni nzuri. Uziru wa asilimia 80 wa katiba unaweza kusifiwa kwa nchi kama Somalia au jamhuri yoyote ya ndizi, sio Tanzania.

Kwa ulichoandika naona kabisa hata katiba yenyewe hujasoma, na hata hujui katiba yenyewe ya mwaka 1977, hujui randama ya kwanza, ya pili, na hata hii iliyochakachuliwa.

Jisemee mwenyewe usitusemee wote.
 
KATIBA INAYOPENDEKEZWA NI BORA KULIKO YA SASA, HONGERA MH. RAISI, HONGERA WATANZANIA.

Katika historia ya uandishi wa katiba mpya duniani hakuna nchi yeyote ambayo iliwahi kuandika katiba mpya ikakidhi matakwa ya wananchi wote na taifa kwa 100%. Katiba si msaafu wala si biblia kwamba haiwezi kufanyiwa maboresho. Leo hii jambo ambalo tumeliona lina tija na manufaa kwa taifa na tukaliingiza kwenye katiba, kesho tutaliona halina tija na tutakubaliana kuliondoa au kuliboresha. Vilevile jambo ambalo leo tumeliona halina tija na kutoliingiza ndani ya katiba kesho tutaona umuhimu wake na tutakubaliana kuliingiza ndani ya katiba yetu.

Katiba inayopendekezwa imetambua haki za makundi mbalimbali kama vile wakulima, wafugaji, wafanyakazi, wasanii, vijana, wanawake na wengine. Pia katiba inayopendekezwa imetambua haki bunifu, mgombea, binafsi, maboresho katika muungano wetu sambamba na kuweka mfumo bora wa kusimamia rasirimali za taifa na kudhibiti mianya ya matumizi mabovu ya rasirimali. Kundi pekee ambalo linadhani halijatendewa haki katika katiba hii ni kundi la wanasiasa wachache ambao kwao tafsiri ya katiba bora ni ile inayokidhi maslahi yao ya kisiasa. Hili ni jambo ambalo watanzania hawana budi kulikataa.

Jambo la msingi ambalo kila mtanzania anapaswa kukubali ni kwamba katiba inayopendekezwa ni bora kuliko ile ya sasa. Wakati ambapo baadhi ya watu wakiipinga na kudai kwamba haiwezi kulivusha taifa letu, wapo watanzania tena asilimia kubwa ambao wanaiona katiba inayopendekezwa kuwa ni chombo madhubuti ambacho kitachochea maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja, na ikifika wakati watanzania wote tukawa na mawazo yanayofanana basi tujue kwamba tunapaswa kujitazama upya. Kutofautiana kimtazamo ni jambo la kawaida na
hiyo ndiyo afya ya demokrasia iache ichukue nafasi yake. Tupingane kwa hoja bila kuhatarisha amani ya taifa letu.

Hongera Mh. Raisi Dr. Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa uliyoifanya. Hili ni jambo la kihistoria ambalo halijawahi kutokea katika historia ya Taifa. Hii ni mara ya kwanza kwa Taifa letu kuandika katiba yake kwa kushirikisha wananchi wake. Yapo mataifa ambayo yaliwahi kuandika katiba zao kwa kutumia Bunge la katiba pekee, wapo waliogeuza Bunge la kawaida na kuwa Bunge la katiba. Kwa taifa letu, mchakato umekuwa wa kidemokrasia zaidi kiasi kwamba wapo wanazuoni, wanasiasa na mataifa mbalimbali ambao wameishangaa Tanzania kwa kuruhusu demokrasia kwa kiwango hiki. Kwa hakika Mh. Rais anastahili pongezi na daima watanzania tutakukumbuka na jina lako haliwezi kufutika katika fikra zao.

Ubora wake ni upi zaidi ya ile ya 1977??katiba inayopendekezwa ina zile zile ibara zinazompa nguvu raisi na kua kama Mungu mtu akati ni mwajiriwa wetu ambazo ibara hizo hizo Mwl Nyerere aliwahu kiri kuwa kwa katiba hiyo angeweza kua dictator..
Pia kuelezea siasa ni haki ya kila mtu na sio kundi dogo kama unavoelezea wewe kila mtu ana haki ya kugommbea nafasi yoyote na kumchagua mtu anayetaka..
pia kumbuka hizo haki unazotaja hapo juu ni haki za binadamu ambazo zipo kwenye Universal declaration of human rights ambapo Tanzania nao wamesaini
Na ukisoma kuhusu Human rights unaambiwa they are not created by constitution rather,they are only recognized by constitution ikiwa ni kwamba thet are inborn rights..mtu anazipata pale tu anapozaliwa na sio kua anapewa na katiba na hiyo inadhihirisha na mfano mmoja mdogo tu wa kesi ya Mtikila kuhusu mgombea binafsi..
Alishinda kesi alipoappeal kwenye mahakama ya Africa na although katiba ya Tanzania ilikua hairuhusu mgombea binafsi lakini alishinda kutokana na concept kua human rights are inborn rights..

Pia kingine unachokiongelea kuhusu sijui kila nyanja imeguswa ni hivi wasanii,wakulima na wavuvi wote wamewekwa kwenye sura ya pili ya katiba inayopendekezwa ambapo hyo sura inaitwa directive principles of state policy ambapo pia sura kama hiyo ipo kwenye katiba ya India ambayo India nayo wameitoa kwenye katiba ya Ireland
Disadvantage ya kitu kuwepo kwenye hiyo sura ni kua chochote kilicho pale ni unenforceable kwenye mahakama yoyote na mahakama haina nguvu kutoa hukumu kuhusu chochote kinachohusu hiyo sura na hilo limejidhihirisha kutoka ibara ya 20(2) ya katiba inayopendekezwa...so yoote hayo kama serikali,haitatekeleza hamna ktu chochote wananchi tunachoweza fanya ila tutabaki kuyaona hayo kama ni yard stick kupima ufanisi wa serikali ili kama wameshndwa kuyatekeleza tuwavote out kitu ambacho kwa Tz ni uongo
Pia hizo haki unazoongelea zmewekewa limitation sana na kuzierrode mfano haki ya elimu imetolewa lwa elimu ya msingi tu..

Na mwisho watanzania tupende kusoma na sio kuhadidhia kwana hata Biblia imesema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa
soma upate maarifa..
 
ukiona mtu anasifia uchafu basi hujui kwao wote wana asili ya uchafu mtu mwenye akili timamu hawezi kuisifia huu upuuzi wa ccm kutuletea rasimu ya ccm halafu unasema katiba mpya iliyopendekezwa hii aibu kwa serikali ya ccm kuwadanganya wananchi wake hatuwezi kuvumilia huu upuuzi wa ccm tena lazima tujiandae kupambana
 
Mkuu naona wewe ni member mpya mpya hapa kwenye jamvi. Hapa Kwa kawaida huwa hatuwasifii watu kufanya kazi waliomba kutaka kuifanya. Huwa hatumsifii baba kwa kumnunulia mtoto wake viatu. Kwa hiyo ni vizuri ukijisemea mwenyewe usiwasemee watanzania wote, si wote tunajikomba.

Tukiachana na hilo, tukiangalia undani wa katika yenyewe, sina hakika kama kwenye JK ndiye aliyfanya kazi ya kuandika katiba hadi astahili pongezi. Hata kama kweli utamsifu JK kwa katiba hii, inawezekana hata JK mwenyewe atakuona mj!nga, mtu yoyote mwenye akili timamu hata siku moja hawezi kusema katika hii ni nzuri. Uziru wa asilimia 80 wa katiba unaweza kusifiwa kwa nchi kama Somalia au jamhuri yoyote ya ndizi, sio Tanzania.

Kwa ulichoandika naona kabisa hata katiba yenyewe hujasoma, na hata hujui katiba yenyewe ya mwaka 1977, hujui randama ya kwanza, ya pili, na hata hii iliyochakachuliwa.

Jisemee mwenyewe usitusemee wote.

Word....watu kabla ya kuongea wanapaswa kusoma kwanza na sio kusoma tu pia kusoma na kuelewa..
 
Back
Top Bottom