NYARAKA: Katiba Inayopendekezwa Oktoba, 2014 (Tanzania's Proposed Constitution)

NYARAKA: Katiba Inayopendekezwa Oktoba, 2014 (Tanzania's Proposed Constitution)


Nawashukuruni sana Mungu awabariki wakubwa. Ngoja sasa nijifungie nisome taratibu ili nikipiga kura nijue napigia nini.
 
KATIBA INAYOPENDEKEZWA NI BORA KULIKO YA SASA, HONGERA MH. RAISI, HONGERA WATANZANIA.

Katika historia ya uandishi wa katiba mpya duniani hakuna nchi yeyote ambayo iliwahi kuandika katiba mpya ikakidhi matakwa ya wananchi wote na taifa kwa 100%. Katiba si msaafu wala si biblia kwamba haiwezi kufanyiwa maboresho. Leo hii jambo ambalo tumeliona lina tija na manufaa kwa taifa na tukaliingiza kwenye katiba, kesho tutaliona halina tija na tutakubaliana kuliondoa au kuliboresha. Vilevile jambo ambalo leo tumeliona halina tija na kutoliingiza ndani ya katiba kesho tutaona umuhimu wake na tutakubaliana kuliingiza ndani ya katiba yetu.

Katiba inayopendekezwa imetambua haki za makundi mbalimbali kama vile wakulima, wafugaji, wafanyakazi, wasanii, vijana, wanawake na wengine. Pia katiba inayopendekezwa imetambua haki bunifu, mgombea, binafsi, maboresho katika muungano wetu sambamba na kuweka mfumo bora wa kusimamia rasirimali za taifa na kudhibiti mianya ya matumizi mabovu ya rasirimali. Kundi pekee ambalo linadhani halijatendewa haki katika katiba hii ni kundi la wanasiasa wachache ambao kwao tafsiri ya katiba bora ni ile inayokidhi maslahi yao ya kisiasa. Hili ni jambo ambalo watanzania hawana budi kulikataa.

Jambo la msingi ambalo kila mtanzania anapaswa kukubali ni kwamba katiba inayopendekezwa ni bora kuliko ile ya sasa. Wakati ambapo baadhi ya watu wakiipinga na kudai kwamba haiwezi kulivusha taifa letu, wapo watanzania tena asilimia kubwa ambao wanaiona katiba inayopendekezwa kuwa ni chombo madhubuti ambacho kitachochea maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja, na ikifika wakati watanzania wote tukawa na mawazo yanayofanana basi tujue kwamba tunapaswa kujitazama upya. Kutofautiana kimtazamo ni jambo la kawaida na
hiyo ndiyo afya ya demokrasia iache ichukue nafasi yake. Tupingane kwa hoja bila kuhatarisha amani ya taifa letu.

Hongera Mh. Raisi Dr. Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa uliyoifanya. Hili ni jambo la kihistoria ambalo halijawahi kutokea katika historia ya Taifa. Hii ni mara ya kwanza kwa Taifa letu kuandika katiba yake kwa kushirikisha wananchi wake. Yapo mataifa ambayo yaliwahi kuandika katiba zao kwa kutumia Bunge la katiba pekee, wapo waliogeuza Bunge la kawaida na kuwa Bunge la katiba. Kwa taifa letu, mchakato umekuwa wa kidemokrasia zaidi kiasi kwamba wapo wanazuoni, wanasiasa na mataifa mbalimbali ambao wameishangaa Tanzania kwa kuruhusu demokrasia kwa kiwango hiki. Kwa hakika Mh. Rais anastahili pongezi na daima watanzania tutakukumbuka na jina lako haliwezi kufutika katika fikra zao.

Tunaomba basi mtuwekee soft copy yake yenye ibara 296 maana ile ya Profesa si imefanyiwa marekebisho.
 
Planner huitaji ku compare rasimu ya warioba na ya sitta maana ziko tofauti sana. Na tofauti zake ziko waazi kabisa kwamba warioba rasimu yake ni ya serikali ya Muungano wakati ya chenge na sitta imechanganya muungano na tanganyika.

Wakati tume ya warioba ilijikita kwenye Muundo wa Muungano; Sita na wenzie wamekimbilia kwenye mambo ya Tanganyika. Kwa sababu hiyo basi COMPARE KATIBA YA CHENGE NA HII YA SASA ndio utajua hii ni mpya au ya zamani iliyotiwa viraka
 
Katiba ya kinafiki.Haina jipya la msingi.Hizo haki za wafugaji na wakulima ni hadaa tu.Tulitegemea katiba mpya ingefumua muundo wa uongozi ili kutatua kero sugu kama ufisadi, uwajibikaji , masuala ya muungano na muingiliano wa mihimili.
Katiba pendekezi imewabeba wenye mamlaka na kuwahadaa wananch wa kawaida.

neno kulinda muungano limetumika kutetea na kulinda maslahi ya tabaka tawala mwananchi wa kawaida ataendelea kubakia fukara na maskini huku watawala wakiendelea kunufaika na rasilimali za taifa kupitia mgongo wa wawekezaji tegemeeni kusikia kashfa nyingine kama zile za richmond, epa, kagoda nk
 
Katiba ya kinafiki.Haina jipya la msingi.Hizo haki za wafugaji na wakulima ni hadaa tu.Tulitegemea katiba mpya ingefumua muundo wa uongozi ili kutatua kero sugu kama ufisadi, uwajibikaji , masuala ya muungano na muingiliano wa mihimili.
Katiba pendekezi imewabeba wenye mamlaka na kuwahadaa wananch wa kawaida.
Sheria zilizopo zinatosha kuondoa ufisadi. Tatizo ni utekelezaji.
 
KATIBA INAYOPENDEKEZWA NI BORA KULIKO YA SASA, HONGERA MH. RAISI, HONGERA WATANZANIA.

Katika historia ya uandishi wa katiba mpya duniani hakuna nchi yeyote ambayo iliwahi kuandika katiba mpya ikakidhi matakwa ya wananchi wote na taifa kwa 100%. Katiba si msaafu wala si biblia kwamba haiwezi kufanyiwa maboresho. Leo hii jambo ambalo tumeliona lina tija na manufaa kwa taifa na tukaliingiza kwenye katiba, kesho tutaliona halina tija na tutakubaliana kuliondoa au kuliboresha. Vilevile jambo ambalo leo tumeliona halina tija na kutoliingiza ndani ya katiba kesho tutaona umuhimu wake na tutakubaliana kuliingiza ndani ya katiba yetu.

Katiba inayopendekezwa imetambua haki za makundi mbalimbali kama vile wakulima, wafugaji, wafanyakazi, wasanii, vijana, wanawake na wengine. Pia katiba inayopendekezwa imetambua haki bunifu, mgombea, binafsi, maboresho katika muungano wetu sambamba na kuweka mfumo bora wa kusimamia rasirimali za taifa na kudhibiti mianya ya matumizi mabovu ya rasirimali. Kundi pekee ambalo linadhani halijatendewa haki katika katiba hii ni kundi la wanasiasa wachache ambao kwao tafsiri ya katiba bora ni ile inayokidhi maslahi yao ya kisiasa. Hili ni jambo ambalo watanzania hawana budi kulikataa.

Jambo la msingi ambalo kila mtanzania anapaswa kukubali ni kwamba katiba inayopendekezwa ni bora kuliko ile ya sasa. Wakati ambapo baadhi ya watu wakiipinga na kudai kwamba haiwezi kulivusha taifa letu, wapo watanzania tena asilimia kubwa ambao wanaiona katiba inayopendekezwa kuwa ni chombo madhubuti ambacho kitachochea maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja, na ikifika wakati watanzania wote tukawa na mawazo yanayofanana basi tujue kwamba tunapaswa kujitazama upya. Kutofautiana kimtazamo ni jambo la kawaida na
hiyo ndiyo afya ya demokrasia iache ichukue nafasi yake. Tupingane kwa hoja bila kuhatarisha amani ya taifa letu.

Hongera Mh. Raisi Dr. Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa uliyoifanya. Hili ni jambo la kihistoria ambalo halijawahi kutokea katika historia ya Taifa. Hii ni mara ya kwanza kwa Taifa letu kuandika katiba yake kwa kushirikisha wananchi wake. Yapo mataifa ambayo yaliwahi kuandika katiba zao kwa kutumia Bunge la katiba pekee, wapo waliogeuza Bunge la kawaida na kuwa Bunge la katiba. Kwa taifa letu, mchakato umekuwa wa kidemokrasia zaidi kiasi kwamba wapo wanazuoni, wanasiasa na mataifa mbalimbali ambao wameishangaa Tanzania kwa kuruhusu demokrasia kwa kiwango hiki. Kwa hakika Mh. Rais anastahili pongezi na daima watanzania tutakukumbuka na jina lako haliwezi kufutika katika fikra zao.
Ebu isome kwa kina bila mlengo na kutakafari. Hizo haki zilizomo ziangalie kwa kurejea Kifungu cha 20. Pia angalia madaraka ya Rais na kutenganisha vyombo vya cola.
 
SURA YA PILI MALENGO MUHIMU, MISINGI YA MWELEKEO WA SHUGHULI ZA SERIKALI NA SERA ZA TAIFA SEHEMU YA KWANZA MALENGO MAKUU


Malengo Makuu
11.-(1) Lengo la Katiba hii ni kulinda, kuimarisha na kudumisha, haki, usawa, udugu, amani, umoja na utangamano wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru lenye demokrasia, utawala bora, maendeleo endelevu na kujitegemea.
(2) Bila kuathiri masharti ya ibara ndogo ya (1), lengo hilo kuu litaendelezwa na kuimarishwa katika nyanja zote kuu, ikijumuisha nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kimazingira.
(3) Bunge litatunga sheria itakayofafanua juu ya utekelezaji wa malengo muhimu kwa mujibu wa Katiba hii.


SEHEMU YA PILI MALENGO YA KISIASA


Lengo la Taifa Kisiasa
12.-(1) Lengo la Katiba hii kisiasa ni kudumisha demokrasia na kuondoa ubaguzi wa aina zote.
(2) Katika kuhakikisha utekelezaji wa lengo hilo, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili: (a) kuhakikisha kuwa inazuia na kuondoa dhuluma, vitisho, ubaguzi, unyanyasaji, rushwa, uonevu na upendeleo miongoni mwa wananchi kwa misingi ya itikadi, asili ya mtu, sehemu anayotoka, nasaba, kabila, jinsi, dini au imani yake;


(b) kuhakikisha kuwepo kwa amani na utulivu na kujenga utamaduni wa kuenzi, kuheshimu na kudumisha uzalendo, amani, umoja, utangamano, ushirikiano na uvumilivu wa kisiasa kwa madhumuni ya kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi; na (c) kuhakikisha kuwepo kwa usalama na ustawi wa watu na mali zao. SEHEMU YA


TATU MALENGO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KIUTAMADUNI Lengo la Taifa Kiuchumi


13.-(1) Lengo la Katiba hii kiuchumi ni kujenga uchumi wa kisasa utakaowezesha wananchi na Taifa kujitegemea kwa kuzingatia matumizi ya elimu ya sayansi na teknolojia katika nyanja zote za uzalishaji mali kwa kuhimiza mapinduzi ya kilimo, ufugaji na uvuvi, mapinduzi ya viwanda na kujenga sekta muhimu ya nishati, mawasiliano na miundo mbinu.
(2) Katika kuhakikisha utekelezaji wa lengo hilo, Serikali itachukua hatua zifuatazo:
(a) kuweka na kutekeleza mpango mkakati wa kutoa elimu ya kisasa yenye kusisitiza ubunifu, sayansi na teknolojia kuanzia ngazi ya msingi, sekondari, ufundi na amali hadi vyuo vikuu na katika shughuli za uchumi na maendeleo ya Taifa kwa ujumla;
(b) kuimarisha na kujenga uwezo wa vyama vya ushirika ili viwe vyombo madhubuti vya kueneza maarifa, mbinu na zana bora za kisasa katika kilimo, ufugaji na uvuvi ili kuongeza tija katika uzalishaji, kutoa mikopo, kutafuta na kuendeleza masoko ya mazao yao;
(c) kuweka utaratibu wa kujenga viwanda vya kati na viwanda vidogo vitakavyosindika na kuchakata bidhaa za kilimo, ufugaji, uvuvi, na madini ili kuziongezea thamani kwa ajili ya mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi;
(d) kuhakikisha kuwa wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao katika kukuza mazingira yaliyo bora kwa ajili ya kuhamasisha sekta binafsi katika uchumi, upangaji na usimamizi wa mizania ya bei za mazao na pembejeo;
(e) kuhamasisha uwekezaji wa pamoja baina ya raia na wasio raia katika miundombinu ya uchumi, uvunaji wa rasilimali na maliasili za Taifa;
(f) kuhakikisha kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo utajiri wa Taifa unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote na kuweka mazingira yatakayochochea maendeleo linganifu na kuwawezesha wananchi kuondokana na umaskini; na
(g) kuweka utaratibu wa usimamizi na udhibiti wa huduma za kijamii ili kuwezesha ushindani wenye haki na ubora wa viwango vya huduma zinazotolewa ili kuwalinda wananchi.


14.-(1) Lengo la Katiba hii kijamii ni kujenga jamii yenye ustawi na uwezo wa kushiriki katika shughuli za kimaendeleo katika nyanja mbalimbali.
(2) Katika utekelezaji wa lengo hilo, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili:
(a) kuhakikisha kwamba heshima ya binadamu inahifadhiwa na kudumishwa kwa kufuata mila, desturi na Kanuni za Tangazo la Dunia kuhusu Haki za Binadamu na mikataba mingine ya kimataifa iliyoridhiwa na Tanzania;
(b) kuhakikisha kwamba Serikali na vyombo vyake vyote vya umma vinatoa nafasi na fursa sawa kwa raia wote, bila ubaguzi;
(c) kuhakikisha kuwa huduma na hifadhi ya jamii inatolewa kwa watu wasiojiweza, wazee, watoto na watu wenye ulemavu;
(d) kuwezesha upatikanaji na utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria kwa wananchi wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za mawakili;
(e) kuweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kujipatia elimu na kuwa huru kupata fursa sawa ya kutafuta elimu katika fani anayoipenda hadi kufikia upeo wowote kulingana na uwezo wake; na
(f) kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora ya afya kwa watu wote ikiwa ni pamoja na afya ya uzazi salama.


Lengo la Taifa Kiutamaduni
15.-(1) Lengo la Katiba hii kiutamaduni ni kukuza, kudumisha na kuhifadhi lugha ya Kiswahili, urithi wa asili na utamaduni wa wananchi.
(2) Katika kuhakikisha utekelezaji wa lengo hilo, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili: (a) kulinda na kuendeleza lugha ya Kiswahili;
(b) kulinda na kuhifadhi urithi wa asili, malikale na sehemu zenye umuhimu wa kihistoria ili kuepuka uharibifu, wizi au utoroshaji nje ya nchi;
(c) kulinda, kuhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii mbalimbali;
(d) kujenga utamaduni wa kuwepo ushirikiano, maelewano, maridhiano, uvumilivu na kuheshimu mila, desturi na imani ya dini ya kila mtu; na
(e) kuweka mazingira yatakayowezesha wasanii kutumia fursa zilizopo na vipaji vyao katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na mabadiliko katika jamii.


SEHEMU YA NNE
UTAFITI, DIRA YA MAENDELEO, MIPANGO NA UTEKELEZAJI WA MALENGO YA TAIFA Utafiti na Maendeleo
16. Katika kuweka mipango ya Taifa, Serikali itatoa kipaumbele kwenye shughuli za utafiti na maendeleo kwa lengo la kupata taarifa zitakazowezesha upatikanaji wa maendeleo ya kiuchumi nchini.
17.-(1) Kutakuwa na Dira ya Taifa ya Maendeleo katika nyanja mbalimbali kwa kuzingatia haki na wajibu wa kila raia kupata maendeleo.
(2) Katika kutekeleza ibara ndogo ya
(1), Mamlaka za Serikali zitaweka mipango ya kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo. Tume ya Mipango ya Jamhuri ya Muungano
18.-(1) Kutakuwa na Tume ya Mipango ya Jamhuri ya Muungano itakayoitwa “Tume ya Mipango” ambayo itakuwa ndicho chombo cha juu cha kupanga na kusimamia utekelezaji wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya Taifa.
(2) Bunge litatunga sheria kwa ajili ya utekelezaji wa Ibara hii. Utekelezaji wa Malengo ya Taifa


19.-(1) Malengo ya Taifa yaliyoainishwa ndani ya Katiba hii yatakuwa ni mwongozo kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kwa wananchi katika matumizi au kutafsiri masharti ya Katiba hii au sheria nyingine yoyote au katika utekelezaji wa maamuzi ya kisera kwa madhumuni ya kujenga jamii iliyo bora, huru na makini.
(2) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itawasilisha katika Bunge mara moja kwa mwaka, taarifa ya hatua ilizozichukua katika utekelezaji wa malengo ya Taifa. Matumizi ya masharti ya Sura ya Pili


20.-(1) Bila kuathiri masharti ya ibara ndogo ya (2), Serikali, vyombo vyake vyote na watu au mamlaka yoyote yenye kutekeleza madaraka ya utawala, kutunga sheria au ya utoaji haki, vitakuwa na jukumu na wajibu wa kuzingatia na kutekeleza masharti yote ya Sura hii.
(2) Masharti ya Sura hii hayatatiliwa nguvu ya kisheria na Mahakama yoyote. Mahakama yoyote nchini haitakuwa na uwezo wa kuamua juu ya suala kama kutenda au kukosa kutenda jambo kwa mtu au mahakama yoyote au kama sheria au hukumu yoyote inaambatana na masharti ya Sura hii.

Soma ibara ya 20(2) hapo , hakuna haki za wavujishwa,wafugaji,Wazee, wanawake, uzazi salama, vijana , etc ....ni kuzuiwa Mbuzi kwenye gunia .
 
Bingo movie na bongo flavor za wabeba mzigo sawa poa ndani ya katiba.waislam nusu ya raia wa nchii hii hapana " tutawaundia sheria"
Kwani hakuna sheria ya haki miliki ? Kwani hii nchi ya wapuga vinanda peke yao
 
Nimejitahidi kusoma katiba pendekezwa. Tofauti yake na ile ya 1977 ni ndogo sana. Bado Rais anaendelea kuwa na madaraka makubwa, yaani Rais anateua watendaji wengi ambapo Wananchi hawawezi kuwaondoa, Rais ameendelea kuwa mfalme.
Waziri kaendelea kuwa Mbunge wa kawaida
Wateule wa Rais hawadhibitishwi na Bunge kama ilivyo kuwa katika Rasimu ya Warioba
Wabunge wameongezwa zaidi, hii ni mzigo kwa walipa kodi


Kwa ujumla ni propaganda tu za kusema eti haki za wafugaji. Hii katiba pendekezwa imekidhi matakwa ya watawala na wala si Raia wa kawaida
Na pia Rais ni sehemu ya bunge sasa kikatiba, wakati huo huo rais ana nguvu za uteuzi wa viongozi na watendaji wa Mahakama. Katiba hii sasa inafanya mihimili mitatu ya dola kuingiliana.
 
Wale jamaa wa upande mwingine walidhani wakisusa basi hakuna katiba itayotengenezwa.
Lkn ni jambo la heri leo hii tuna katiba iliyo pendekezwa na ni nzuri kwa ssbabu imeshika kila mahali.
Ni jambo la kushangaza pale mwana siasa anaposimama na mishipa kumtoka akisema eti usawa wa kijinsia yaani 50 kwa 50 itanufaisha wachache halafu yeye mwenyewe ni mwanamke? Unajiuliza hawa watu wapo serious kweli???
Nasema hongera wabunge wote mliomaliza kazi hii na hongera saaana mh. Sitta na samie.

Kama unaamini kuwa hiyo 50 kwa 50 ina faida, basi fikiria tena. Tafsiri yake ni "jaza tu maembe mradi kapu lijae, hata mabovu" maana hapa haki inayotafutwa si ile inayotokana na merit, bali numeric in the context of affirmative action. Huwa hailipi na kwa yeyeote anayeshabikia asubirie matokeo yake.
 
Sheria zilizopo zinatosha kuondoa ufisadi. Tatizo ni utekelezaji.

Ndiyo maana hata mahakama inakimbia kesi na kudai ni za kisiasa. Tutajikongoja huku tukirudi nyuma hadi tupotee kwenye ramani ya dunia.
 
Hakuna jipya ni ushenzi mm nafanya yangu naona hii nchi mpaka atokee gaidi aiongeze mana viongozi wamejisahau ila kuna siku viti vitakuwa vya moto.
 
neno kulinda muungano limetumika kutetea na kulinda maslahi ya tabaka tawala mwananchi wa kawaida ataendelea kubakia fukara na maskini huku watawala wakiendelea kunufaika na rasilimali za taifa kupitia mgongo wa wawekezaji tegemeeni kusikia kashfa nyingine kama zile za richmond, epa, kagoda nk

Hoja yenyewe inayotumika kuulinda huo muungano mi naiona ya kipuuzi kabisa.
1. Kama serikali tatu ni kuvunja muungano, kwa nini isingekuwa moja ili tuamini kabisa kuwa sasa tumeamua kuungana? Hizi mbili za kiwizi-wizi ambazo hata hazieleweki misingi yake ndio chanzo cha migogoro, na ndio itapelekea hata matatizo zaidi siku za usoni.
2. Hoja kwamba kungeibuka hisia za utaifa ni kituko. sasa kuwa mzalendo kwa taifa lako imekuwa kosa? Kwani sasa hivi hizo hisia hazipo? Na kama kweli ingekuwa kuwa na hisia hizo ni 'dhambi' mbona JK Nyerere alitoa sababu ya kutofanya serikali iwe moja eti ni kuogopa Zanzibar kumezwa na Tanganyika? Hapo si yeye mwenyewe ndiye alianzisha hisia za uzanzibari. Kama wameungana na kuunda Tanzania, Tanganyika ingetoka wapi? Tanganyika inaendelea kudaiwa na watu kwa sababu Zanzibar ipo. Kwa hiyo mimi naona chanzo kikubwa kabisa cha matatizo ya muungano ambacho ndicho kinasababisha hata katiba hii kuwa magumashi, ni Mwalimu Nyerere mwenyewe. Yeye na mwenzake walitutengenezea muungano WA KINAFIKI USIO NA MANTIKI KABISA. Na kuhusu hili, kila anayetetea huwa hawezi kutoa sababu za kueleweka zaidi ya kusema alikuwa na malengo mazuri...

Matokeo yake leo tunaambiwa muundo wa muungano hauwezi kubadilishwa kwa kuwa eti baba wa Taifa alisema... Yaani ni hilo tu wameona la kushikilia kati ya yote aliyoagiza baba wa taifa, mengine yote kuhusu uadilifu wanamwona kiazi tu!
 
Support this campaign of 'VOTE NO FOR THE CONSTITUTIONAL DRAFT BY SITTA'

Tell all friends in your phonebook. Tell your friends and neighbours
 
Ndugu zangu Watanganyika na Wazanzibari, kitendo cha kuengua maadili na miiko ya uongozi yaliyokuwa yamesheheni kwenye rasimu ya pili ya tume ya jaji Warioba na kuturundikia kinachoitwa "haki za makundi mbalimbali" kama vile wavuvi, wakulima, wafugaji nk, ni changa la macho na ni danganya toto.

Kilichoua viwanda vyetu vikiwemo vile vya pamba, korosho, nk ni ufisadi uliotamalaki hasa baada ya kulichinjilia mbali Azimio la Arusha kule Zanzibar na kuiacha nchi ikiwa "utupu" bila kuwa na miiko ya uongozi.

Hali hii imepelekea kufilisika kwa vyama ushirika pamoja na wakulima kuibiwa fedha zao za ruzuku ya pembejeo, kuuziwa mbegu mbovu zisizoota, kuletewa mbolea feki, kupunjwa kwenye mizani wakati wa kuuza mazao yao, kupunjwa bei na kutolipwa kwa wakati,mazao kutonunuliwa kwa wakati, mambo ambayo yamewaacha ndugu zetu vijijini wakiwa hoi bin taabani kiuchumi kiasi cha kuwafanya wawe ombaomba kwa ndugu zao walio mijini ambao nao wamepigika vilevile kutokana na mikataba mibovu na uporaji wa IPTL/ESCROW ACCOUNT, DOWANS/RICHMOND, EPA,KAGODA AGRICULTURAL, BUZWAGI, NORTH MARA, MWADUI, GGM,KIWIRA, STATOIL & ASSOCIATES, NET GROUP SOLUTIONS, MKATABA WA UBINAFSISHAJI WA NBC & ATC, DEEP GREEN, MEREMETA, MIKATABA 17 YA SIRI NA RAIS WA CHINA, MRADI WA POWER TILLER, MRADI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA NK.

Katika utekelezaji wa amri ya kiongozi mmoja wa ngazi ya juu, wazee wetu ambao zamani walikuwa ni hazina yetu, siku hizi nao eti wanatwangwa kisawasawa akiwemo waziri mkuu mstaafu, makamu wa kwanza wa rais mstaafu na mwanasheria mkuu mstaafu mzee wetu Warioba pamoja na wastaafu wa iliyokuwa EAC ambao wanapigwa mabomu ya machozi ili kuwazuia wasidai mafao yao. Hii siyo laana kweli!

Kutujazia haki kibao kwenye kinachoitwa "Katiba inayopendekezwa" ambazo hazitekelezeki kwa sababu ya ufisadi uliokithiri na ambao umejengewa mazingira mazuri ya kustawi vizuri kwenye hiyo katiba inayopendekezwa, ni ulaghai, ni uongo, ni uzushi, ni utapeli na ni ubabaishaji uliopindukia.

Ni afadhali kufutilia mbali hizo zinazoitwa "haki za makundi mbalimbali" na kurejesha miiko na maadili ya uongozi kwa sababu hakuna haki ya msingi kwa mwanachi inayozidi kupata huduma ya maji, umeme wa bei nafuu, barabara, huduma za afya NA KUPATA HAKI POLISI NA MAHAKAMANI BILA KUOMBWA AU KULAZIMIKA KUTOA RUSHWA.

Walioua Azimio la Arusha kule Zanzibar ndio hao hao walioikata kichwa (na kuiachia kiwiliwili kisicho na uhai) Rasimu ya jaji Warioba kule Dodoma halafu leo bila hata chembe ya aibu wanatuambia eti tuipigie kura ya NDIO. Sasa haya kama siyo matusi na masimango tutayaita jina gani sasa?

Sasa wanataka kuipitisha kwa mbinu zote ikiwa ni pamoja na KU-INFLUENCE VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI ACHILIA MBALI HILI LA KUWAJAZA WATOTO WETU UJINGA KWA KUWAIMBISHA MASHAIRI YASIYO NA KICHWA WALA MIGUU ILI KUITETEA HIYO KATIBA YA KIKUNDI CHA WATU WACHACHE ISIYOBEBA MAUDHUI NA MAONI YETU YA MSINGI KAMA YALIVYOWASILISHWA KATIKA RASIMU BYA PILI YA JAJI NWARIOBA HALAFU MWISHO WA SIKU WATAPEWA "A" KWENYE MITIHANI YAO KWAMBA WAMEFAULU. ACHA TU ELIMU YETU IJIFIE-KALAGABAHO!

HISTORIA ITAMHUKUMU SAMWELI SITA, CHENGE NA GENGE LAO LOTE WALIOTUPORA (angalau kwa sasa) FURSA YETU ADIMU YA KUPATA KATIBA MPYA. MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBAR, MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Naomba kuwasilisha.
 
Ndugu Mwananchit

Watanzania wengi tuna tatizo la kudhani tunafahamu wakati kiuhalisiasa hatufahamu lolote!

Ulichoandika hapa na kutoa malalamiko kinaonyesha kuwa, hujaisoma hata hiyo Katiba Inayopendekezwa ambayo unaipigia kelele.

Nenda kwanza ukaisome ili upate uwanja mpana kifikra katika kuchambua masuala mbali mbali kuhusiana na hoja yako.

Kwa kukusaidia, nenda ukasome Katiba Inayopendekezwa katika Sura ya Nne katika kifungu cha 28-31 kinachohusu Maadili ya Uongozi na Utumishi wa Umma ambacho kinajibu hoja zako.
 
Mwanadiwani katiba ni mkataba kati ya watawala na wtawaliwa.
kama utatoa mengi yanayotupa mamlaka akaweka yanayokupa mamlaka nikutu bure.halafu hii katiba penekezwa sio kwamba hatujaisoma ila ina ibara tatanishi,tulitaka kutenganisha mihimili3 kila mmoja uwe na mamlaka badala yake ipo miwil( mahakama na serikal iliyojichanganya na bunge) kumfanya mbunge awe wazir ni kuchanganya mihimili.(tusipotoshane kwa kutaja ibara bila kueleza kilichomo ndan ni kuyumbishana)
 
Natafuta nakala ya katiba iloyopendelezwa, zinapatikana wapi, tulibiwa zitagawiwa kwa wananchi
 
Back
Top Bottom