Uchaguzi 2020 Nyehunge: Dkt. Magufuli amuamrisha Mfugale atangaze ujenzi barabara ya Sengerema-Nyehunge (KM 46) kisha amuulize hela za kujengea

Uchaguzi 2020 Nyehunge: Dkt. Magufuli amuamrisha Mfugale atangaze ujenzi barabara ya Sengerema-Nyehunge (KM 46) kisha amuulize hela za kujengea

Hivi Mheshimiwa anajua nini maana ya kampeni za uchaguzi wa Rais? Na pia anatambua nini kinachopaswa kufanyika wakati wa shughuli za kampeni? Na kweli alisoma kwa kina na kuzielewa kanuni na maadili ya wagombea kutokana na tume ya uchaguzi?

Rais wa Tanzania ni kama Mfalme kutokana na katiba yetu ya leo.
 
DKT. Magufuli akiwa anaendelea na kampeni za uchaguzi 2020, amepita kijiji cha Nyehunge akiwa anaelekea Geita ambapo kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46. Alisimama kuongea na wananchi waliokuwa wakimsubiri barabarani, wakati anaielezea barabara hiyo ghafla aliomba simu yake na kumpigia mtu ambae baadae alijulikana ni mkurugenzi mkuu wa TANROADS, Injinia Mfugale na mazungumzo yao yalikuwa hivi.

Magufuli: Hallo, Chief executive

Mfugale: Naam mheshimiwa Rais

Magufuli: Hujambo

Mfugale: Sijambo mheshimiwa

Magufuli: Uko wapi?

Mfugale: Niko Dar es Salaam TANESCO tunazungumzia habari ya Nyerere dam.

Magufuli: Haya, sasa mimi niko Nyehunge, kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46, hii barabara tumeshaifanyizia feasibility study na detail design, nimesimama hapa na wananchi, nataka hii barabara, mimi si ndio Rais?

Mfugale: Ndio mheshimiwa(Wananchi kicheko cha furaha)

Magufuli: Nyehunge Oyee, Unanielewa Chief? Basi hii barabara uitangaze kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Huu ni mwezi wa ngapi? (Mfugale: Mwezi wa tisa). Haya uandae document zote kabla ya mwezi wa 12 haujafika na kandarasi apatikane, niulize hela nitazitoa wapi. Sawa Mfugale?

Mfugale: Nimekuelewa mheshimiwa Rais

Magufuli: Umenielewa, mueleze na Waziri kwamba hayo ni maagizo yangu wala yasibadilike, Asante sana.

MWISHO WA MAONGEZI
ukisikia uhuni ndiyo huu!
 
Mgombea aliyekuwa madarakani lakini kampeni zinampeleka puta hadi hadi amepaniki, tatizo aliaminishwa kuwa anapendwa sana!

Mabango makubwa njiani utasema ndo anagombea mara ya kwanza!!
 
Hiyi ndo dhana halisi ya kuwa na vyombo vya dola kama alivyosema Katibu Mkuu wa CCM lakini Chadema wakapotosha kwamba chombo cha dola ni Polisi. Ukiwa kwenye madaraka unakuwa na advantage kubwa ya kushinda uchaguzi maana utatoa maagizo kama haya na sheria inakuruhusu kufanya hivyo
Sasa kwaakili za kawaida (usifikiri kiccm) unaona kuna uwanja sawa wa kushindana na vyama vingine vya siasa?
 
Hapa ndipo umuhimu wa katiba mpya unapoonekana, kuwa Rais wa nchi halafu hapo hapo kuwa mwenyekiti wa chama cha siasa ni tatizo.

Hapo Magufuli anaamua kutumia kofia yake ya Urais kujinufaisha kisiasa kwenye kampeni zake, hiIi sio sawa.

Hizi bajeti siku zote zinatakiwa kupitishwa na bunge, sio mtu mmoja anajiamulia tu, hii nchi ina sheria na taratibu zake Magufuli akumbushwe kuzifuata.
Kama anatoa pesa yake kuna tatizo gani
 
Huyu jamaa hata akishindwa uchaguzi hatoki madarakani atalazimisha kuendelea

Atadai miradi alioianzisha ni mingi kwa hiyo atalazimisha kuwa lazima aione ikiisha

Miradi mingine itachukua hadi miaka 20 ijayo sasa Mtanzania piga mahesabu

Tayari Tanzania imempata raisi wa maisha Dikteta wa maisha
Miradi ipi inayoweza kuchukua miaka 20?
 
Ndo tunageuza kurudi vijijini kwetu muda huu
IMG_20200908_175425.jpg
 
Ni tatizo la katiba Mgombea Urais wakati huo huo ni Rais ndo madhara yake haya.
Katiba ya marekani inasemaje maana uchaguzi ni mwaka huu na trump anaachia lini madaraka kabla ya uchaguzi.
 
DKT. Magufuli akiwa anaendelea na kampeni za uchaguzi 2020, amepita kijiji cha Nyehunge akiwa anaelekea Geita ambapo kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46. Alisimama kuongea na wananchi waliokuwa wakimsubiri barabarani, wakati anaielezea barabara hiyo ghafla aliomba simu yake na kumpigia mtu ambae baadae alijulikana ni mkurugenzi mkuu wa TANROADS, Injinia Mfugale na mazungumzo yao yalikuwa hivi.

Magufuli: Hallo, Chief executive

Mfugale: Naam mheshimiwa Rais

Magufuli: Hujambo

Mfugale: Sijambo mheshimiwa

Magufuli: Uko wapi?

Mfugale: Niko Dar es Salaam TANESCO tunazungumzia habari ya Nyerere dam.

Magufuli: Haya, sasa mimi niko Nyehunge, kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46, hii barabara tumeshaifanyizia feasibility study na detail design, nimesimama hapa na wananchi, nataka hii barabara, mimi si ndio Rais?

Mfugale: Ndio mheshimiwa(Wananchi kicheko cha furaha)

Magufuli: Nyehunge Oyee, Unanielewa Chief? Basi hii barabara uitangaze kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Huu ni mwezi wa ngapi? (Mfugale: Mwezi wa tisa). Haya uandae document zote kabla ya mwezi wa 12 haujafika na kandarasi apatikane, niulize hela nitazitoa wapi. Sawa Mfugale?

Mfugale: Nimekuelewa mheshimiwa Rais

Magufuli: Umenielewa, mueleze na Waziri kwamba hayo ni maagizo yangu wala yasibadilike, Asante sana.

MWISHO WA MAONGEZI
Hii barabara ya Sengerema nyehunge nkome nzela inapita kandokando mwa ziwa na hasa eneo la nkome ni swamp, hii swamp inaenda kasamwa mgoma salawe hadi mwakitolyo. ikijengwa kwa lami haitadumu.

Mie napendekeza ijengwe kwa zege, kwanza tutakuwa tumeokoa fedha zetu za kigeni na itadumu muda mrefu sana kwani cement na maji ni kama pilau na kachumbari wanapendana sana.

Uhai wa barabara ya Zege ni miaka 45 tofauti na lami ni miaka minane unaanza viraka. Na kwa hii barabara ni miaka miwili tunaanza kuziba viraka.
 
Hii na ule ubwabwa wa Hashim Rungwe Spunda tofauti ni ipi? TAKUKURU wataingia chini ya carpet
 
Ni tatizo la katiba Mgombea Urais wakati huo huo ni Rais ndo madhara yake haya.
Sasa mbona mtu kama huyu kushindwa uchaguzi ni ngumu sana, hii ni rushwa.
 
Hivi Mheshimiwa anajua nini maana ya kampeni za uchaguzi wa Rais? Na pia anatambua nini kinachopaswa kufanyika wakati wa shughuli za kampeni? Na kweli alisoma kwa kina na kuzielewa kanuni na maadili ya wagombea kutokana na tume ya uchaguzi?
Wewe unayeyajua hayo upo wapi? Katiba bado inamtambua kuwa yeye ni rais mpaka atakapovunja baraza la mawaziri!

Fuatilia mazungumzo uone kama kuna mahali ametajwa kuwa ni mgombea! Hii ndio tz, kwingine kungetokea maandamano ya kudai pingamizi!
 
Back
Top Bottom