Nyerere, Mwinyi, Mkapa, na Kikwete waliwahi kuvaa Magwanda ya JWTZ walipokuwa Marais?

Nyerere, Mwinyi, Mkapa, na Kikwete waliwahi kuvaa Magwanda ya JWTZ walipokuwa Marais?

Rais aliyechaguliwa kidemokrasia kuvaa gwanda la kijeshi popote pale ni kuvunja misingi ya kanuni za "civilian control of the military".

Katika nchi za kidemokrasia, jeshi linamilikiwa na kuongozwa na raia. Ndiyo maana linaitwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

Rais kuvaa kiraia ni symbolism ya kuonesha raia wapo juu ya jeshi, wanaliongoza jeshi.

Rais akivaa kijeshi ni symbolism ya kwamba nchi haiongozwi kiraia tena, inaongozwa kijeshi, kitu ambacho hakitakiwi katika nchi ya kidemokrasia.

Una akili kubwa sana.

Kwa Muda mrefu sasa CCM wanaongoza nchi kijeshi .
Hata wanayoyafanya kwenye uchaguzi ni mapinduzi ya kiraia kutumia majeshi .

Nilipoona tu Dr.Samia akavaa magwanda ya Kijeshi kinyume kabisa na utaratibu wa tawala za kidemokrasia nikagundua kuwa yule mama ndani yake kuna udikteta mkubwa sana na anatamani kuongoza kwa kutumia mtutu wa Bastola.
Rais wa Marekani ni kama raisi wa Dunia. Taifa lenye jeshi kubwa na la kisasa kabisa duniani lakini hawezi kuvaa sare za kijeshi ili hali yeye ni Raia .

Rais anawakilisha wananchi kuongoza nchi na taasisi zote za serikali ikiwemo Jeshi . Kwa hiyo yule ni raia namba moja na sio mwanajeshi . Mwanajeshi namba moja ni CDF. Ndio maana Jeshi ni serikali mbadala muda wote . Kwa protocol za kijeshi kila cheo kina heshima yake . Na cheo kinavalishwa kwenye unifomu . Asiye na cheo kwenye unifomu basi atakua ndiye mdogo kabisa kwa cheo . Sasa wale madikteta uchwara sijui wanavaa vyeo gani kwenye unifomu zao ili wawe juu ya 4 star General.!!

Hii nchi, CCM kuna siku watampitisha kwa kishindo mgonjwa wa ubongo .Atavaa vip(as then it was) kichwani😂😂😂😂
 
Bora ata ungetuwekea linko ya igonga tukaona mambo
Kuliko kuandika hoja ambazo hazina ata mashiko sasa kosa liko wap kwa Raisi wa nchi kuvaa gwanda

Tz ina mambo meng sana makubwa na mazito yakuhoji sio izo hoja zaifu

Ni bora ata ungehoji Bajeti imetangazwa mwezi wa 7 ila ad leo hali ngumu na miradi mingi imesimama je izo pesa za bajeti hazijatoka au ndo zimehamishiwa ktk uchaguzi maana wazabuni wanadai, taasisi nying za serikal hazijaletewa pesa za maendeleo na miradi ming ilokua inaendelea imesimama
 
Mwalimu Nyerere ndiye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wa kwanza baada ya Tanganyika kupata Uhuru na Tanganyika ilipoungana na Zanzibar kuunda Tanzania.

Mwalimu yeye ndiye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wakati wa vita ya Kagera na kwenye harakati za ukombozi Kusini mwa Afrika.

Ukiachilia mbali Mwalimu, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Benjamini Mkapa, Jakaya Kikwete yeye alikuwa ni mwanajeshi kabla hajawa Rais.

Lakini sina kumbukumbu kama hao maris wanne wa Tanzania enzi wakiwa ni Marais wa Tanzania, waliwahi kuvaa sare za JWTZ kuonesha uamiri jeshi Mkuu wao.

Kama Kuna kumbukumbu za Nyerere, Mwinyi, Mkapa au Kikwete kuvaa sare za JWTZ kuonesha uamiri jeshi Mkuu wao, naomba niwekewe ili nibadili mafaili kwenye kumbukumbu za mbongo yangu.
Mimi sikuwahi ona.
 
Mwalimu Nyerere ndiye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wa kwanza baada ya Tanganyika kupata Uhuru na Tanganyika ilipoungana na Zanzibar kuunda Tanzania.

Mwalimu yeye ndiye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wakati wa vita ya Kagera na kwenye harakati za ukombozi Kusini mwa Afrika.

Ukiachilia mbali Mwalimu, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Benjamini Mkapa, Jakaya Kikwete yeye alikuwa ni mwanajeshi kabla hajawa Rais.

Lakini sina kumbukumbu kama hao maris wanne wa Tanzania enzi wakiwa ni Marais wa Tanzania, waliwahi kuvaa sare za JWTZ kuonesha uamiri jeshi Mkuu wao.

Kama Kuna kumbukumbu za Nyerere, Mwinyi, Mkapa au Kikwete kuvaa sare za JWTZ kuonesha uamiri jeshi Mkuu wao, naomba niwekewe ili nibadili mafaili kwenye kumbukumbu za mbongo yangu.
Kuvaa magazine ya kijeshi wakati wewe ni kiongozi wa kiraia ni kutisha wananchi! Ila nadhani Mama yeye hana nia hiyo machawa ndio wanampotosha aige mambo ya Magufuli pengine atapata umaarufu.
 
Walikuwa wanajielewa, once you know ur strength, you don't have to brag about it, make a lot of show off,
Maghu alikuwa anataka watu wamuogope kwa kuwa Tisha, kuumiza, alichukulia kuvaa magwanda kama nembo ya kuonyesha yeye ni tishio kwa kila mtu, deep inside alikuwa dhaifu, kimwili na kiakili,
Samia, ndio kilaza kabisa, ki elimu, ki upeo, na a najua wasaidizi wake wanamdharau, wanampa tu masifa ya juu juu, sasa ili ajiboost, ndio kila wakati kupanga apewe degree za heshima, aitwe DR wakati hata masters Hana, anajivalia magwanda ili kujiboost tu
Ukiondoa hayo maneno yako yanayoonyesha chuki za wazi kwa Rais SSH, unaweza kuweka wazi amevunja kipengele kipi cha katiba ya mwaka 1977?.
 
Rais aliyechaguliwa kidemokrasia kuvaa gwanda la kijeshi popote pale ni kuvunja misingi ya kanuni za "civilian control of the military".

Katika nchi za kidemokrasia, jeshi linamilikiwa na kuongozwa na raia. Ndiyo maana linaitwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

Rais kuvaa kiraia ni symbolism ya kuonesha raia wapo juu ya jeshi, wanaliongoza jeshi.

Rais akivaa kijeshi ni symbolism ya kwamba nchi haiongozwi kiraia tena, inaongozwa kijeshi, kitu ambacho hakitakiwi katika nchi ya kidemokrasia.
mkuu uzi ufungwe umeshatoa majb stahiki,
 
Mwalimu Nyerere ndiye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wa kwanza baada ya Tanganyika kupata Uhuru na Tanganyika ilipoungana na Zanzibar kuunda Tanzania.

Mwalimu yeye ndiye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wakati wa vita ya Kagera na kwenye harakati za ukombozi Kusini mwa Afrika.

Ukiachilia mbali Mwalimu, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Benjamini Mkapa, Jakaya Kikwete yeye alikuwa ni mwanajeshi kabla hajawa Rais.

Lakini sina kumbukumbu kama hao maris wanne wa Tanzania enzi wakiwa ni Marais wa Tanzania, waliwahi kuvaa sare za JWTZ kuonesha uamiri jeshi Mkuu wao.

Kama Kuna kumbukumbu za Nyerere, Mwinyi, Mkapa au Kikwete kuvaa sare za JWTZ kuonesha uamiri jeshi Mkuu wao, naomba niwekewe ili nibadili mafaili kwenye kumbukumbu za mbongo yangu.
Hizo codes nimezielewa nakupa A top
 
Nikasema huyu ndezi, si bure.

Unasema hapa inawezekana napiga kelele na mtoto wa miaka 14, tena mtoto mjinga.

Mzee mzima unajipinda kufungua Clausewitz na Clark (just to stay in C) halafu kumbe mwenzako hata Kiingereza hajui. Unarudia rudia tu "civilian control of the military" kumbe mwenzako hata kuitamka tu hawezi!
Tatizo ni kwamba siku hizi JF wajinga wamekuwa wengi mno kuliko wenye uelewa na mbaya zaidi ni wajinga wanaouamini na kuutetea ujinga wao kwa nguvu zote bila kukubali kueleweshwa,

Kwahyo muda mwingne ukiona mtu unamletea Facts yeye amekazana na nadharia za kusadikika ni heri unampuuza tu, mmojawapo ni kama huyo bwana mdogo uliyemuelezea hapo.
 
Tatizo ni kwamba siku hizi JF wajinga wamekuwa wengi mno kuliko wenye uelewa na mbaya zaidi ni wajinga wanaouamini na kuutetea ujinga wao kwa nguvu zote bila kukubali kueleweshwa,

Kwahyo muda mwingne ukiona mtu unamletea Facts yeye amekazana na nadharia za kusadikika ni heri unampuuza tu, mmojawapo ni kama huyo bwana mdogo uliyemuelezea hapo.
Huyo anaonekana kabisa anawayawaya.
 
Rais anapata wapi ushauri wa mambo ya jeshi? And why anapata ushauri why asiamue tu
Kumbe hata hujui kuwa Kuna baraza la usalama la Taifa.

Nimekwambia kuwa kwa mujibu wa Katiba ya JMT Rais halazimiki kuchukua ushauri wa mtu yeyote yule.

Majenerali kumshauri haiwapi nafasi ya rais kuwa na utii kwao. Bali majenerali ndiyo wanatakiwa wawe na utii Kwa Rais.

Mantiki nyepesi hii kwa nini unashindwa kuielewa?
 
Bado tu mnajadili amiri jeshi mkuu kuvaa magwanda ya jeshi kwenye shughuli za kijeshi,na mnajiaminisha ni akili kubwa/great thinkers!?
Kwa nini avae nguo za kijeshi? Akili kubwa ni kutaka kujua inakuwaje raia avae nguo za kijeshi wakati yeye si mwanajeshi?

Mtu akiwa Amiri Jeshi Mkuu hakumfanyi awe mwanajeshi
 
Kumbe hata hujui kuwa Kuna baraza la usalama la Taifa.

Nimekwambia kuwa kwa mujibu wa Katiba ya JMT Rais halazimiki kuchukua ushauri wa mtu yeyote yule.

Majenerali kumshauri haiwapi nafasi ya rais kuwa na utii kwao. Bali majenerali ndiyo wanatakiwa wawe na utii Kwa Rais.

Mantiki nyepesi hii kwa nini unashindwa kuielewa?


Uko sahihi katiba inasema hivyo

But nikwambie Tu, Rais wa jamhuri ya Tanzania uwa anaomba ushauri na anashauriwa na anasikiliza ushauri anaopewa

And I'm very sure before ya kuvaa uniform za Jeshi pamoja na kwamba katiba inamtaka asiombe ushauri Kwa mtu yoyote Yule Ila Kwa hili aliomba ushauri na alipata ushauri kuwa hakuna shida yoyote yeye kuvaa uniform za Jeshi kwenye tukio la jeshi

Unataka kutengeneza Jambo au kutuaminisha kilichopo kwenye akili yako but haiwezekani watu wote wasione hiyo shida uje kuona wewe Tu
 
Unataka kutengeneza Jambo au kutuaminisha kilichopo kwenye akili yako but haiwezekani watu wote wasione hiyo shida uje kuona wewe Tu
Usitake kusema "watu wote" kama vile ushafanya sensa ya kujua ni wangapi wanaona ni Sawa au wangapi wanaona si sawa raia kuvaa nguo za jeshi.

Rais ni raia tu kama Mimi na wewe na si mwanajeshi. Inakuwaje avae sare za jeshi?
 
Kwa mfano huyu mama wa zenji analikosea saana jeshi letu.

Yaani analirembulia vazi la wagumu.
 
Back
Top Bottom