Nyimbo gani umekua nazo na ukizisikia zinakukumbusha utoto au ujana wako?

Nyimbo gani umekua nazo na ukizisikia zinakukumbusha utoto au ujana wako?

View attachment 3261955Wataalam wanasema muziki uliousikiliza ukiwa na takribani miaka 13 ndio huwa taste yako ya muziki. Muziki wa kikongo ndio muziki ambao nimekuwa nao nyumbani kwetu miaka ya 1990 akisikiliza mzee. Pia Chaka Chaka, Whitney, Abba zilikuwa ni ngoma za mama yangu. Braza wangu mmoja ndiye aliyenitambulisha kwenye hip hop ya Tupac. Uncle wangu yeye alikuwa ni mzee wa reggae. No wonder hadi leo, Reggae, Rhumba Congolese na Rap ndio miziki niipendayo.

Hii album ya Koffi ya V12 ndio album naisikiliza toka niko Primary School Tabora 1990s hadi leo hii, 2025, March 06 saa 5 na dakika 48 usiku.
Mh! sidhani mi zamani nilikuwa sipendi R&B sasahivi sasa ndo zinanipa usingizi!
 
👉Usiusemee moyo-lady jaydee , nyambizi-duly sykes, maisha ni foleni ya bony mwaitege
👉Sauti ya manka-king crazy gk
Kwaya zote za catholic za 1995-2010
, 👉Bahati bukuku, upendo nkone
👉Njiwa peleka salamu - sikumbuki yule mama aliitwa nani
👉Vyonne chaka songs
👉Mafikizolo-meet up the river
👉Lucy dube-remember me
👉Mwanangu soma-von mwaitege


Kwa kifupi rest in peace my mother 🙏alifanya nikapenda sana hizo nyimbo twaja hapo juu
Nyimbo nzuri na kumbukumbu nzuri ya mama, May her soul rest in peace 🙏🏽
 
Linapokuja swala la muziki nafikiri napenda aina nyingi ya muziki ila zaidi napenda muziki mzuri uliopikwa ukapikika!, na pia muziki unaweza kueleza uwezo wa ufahamu wa mtu! namaanisha music is intelligent!.

Sipendi singeli ule sio muziki ni kelele zile!, muziki huwa unapangwa vizuri ki ustadi na kimaridadi!.


 
Back
Top Bottom