Nyimbo za utotoni za zamani ambazo watoto wa leo hawazijui

Nyimbo za utotoni za zamani ambazo watoto wa leo hawazijui

Aah umeruka mstari...
Chanuo kampa nani ? Chanuo kampa nani?
Kampa msusi kampa msusi....
Mafuta kampa nani? Mafuta kampa nani?
Kampa msusi kampa msusi...
Ahsante mkuu kwa kunikumbushia huo ubeti,si unajua kitambo sana
 
Ndege wengi wamekimbia, Dar wamejenga hadi mabondeni ambako wale ndege walikuwa wanakaa, unakumbuka mbayuwayu ikifika jioni wanakatiza mtaani kimo cha mbuzi!
Zile ndege angani tulikuwa tunadanganyana ni roketi kumbe ndege za kawaida zinapita anga la kimataifa(halina mwenyewe) mfano ndege za SA zamani zilikuwa haziruhusiwi kupita anga la Tz hivyo inabidi ziruke juuu sana kwenye anga la kimataifa, ule moshi ni hewa ya moto kutoka kwenye engine ikikutana,na hewa ya baridi angani. Mfano ukienda Makambako watu wakiongea asubuhi utaona ule 'moshi'
Kumbee mi mpka leo nilijua zile ndege za Urusi labda wamebadili teknolojia hahahaha!!! Nawakumbuka Sana hao mbayuwayu... Ww utakuwa mhenga lol
 
Hello mambo, za mwananyamala....

Ulishawahi kucheza kibumzi kibumzi
Chameemee Chameemee
Halafu kika mtu anaulizwa kimya kimya ataje mchumba ake hahahahahahhaaa hapo sasa kama kuna kavulana unakapenda mtaani unakasema.

Halafu muimbishaji anaanza kutaja.

Nilonge nisilongeee loongaaaa
Nisemeee nisiseemeeee seemaaaa
Mwenzetu Kasie. .... mchumba ake....

Asprin basi watu eeehhh yeeeyyy hapo kama kulikuwa na kaschana kingine kanampenda basi ananuna. Na ukikuta kavulana na kenyewe kanakupenda basi kanaanza uchokozi mara akuvute nywele mara akidalike mara akufinye au akutekenye....

Basi wewe unajidai banaa niniiii mii staakiiiiii ntakusemea. .... Hahahahahahhahaaa ilikuwa raha sana. Hapo kama kavulana kababe mtaani huwezi kuonewa au kupigwa lazima akutetee. Asipokuona mtaani anakuja kukuulizia kwenu na siku kwao kukipikwa maandazi basi atakuibia moja akuletee uonje hehehehehehehhee


Those were innocent pure love.


Umenikumbusha mbaali saana
 
Nasakaa mke wangu....nasaka mke wangu,haaapa hayupo haaapa hayupo...kaeeenda wapi?...kaeenda wapi?,kaeenda kusuka..kaeenda kasuka,kachukuaa... nini? na nini?,kachukuaa chanuuuo na mafutaa
mafuta kampa nani mafuta kampa nani.....kampa msusi kampa msusi
chanuo kampa nani chanuo kampa nani.......kampa msusi kampa msusi
 
Hahahahaaa Hahahaaa hivi tunao changia huu uzi tukisema tukutane leaders club halafu tuanze kuimba hizo nyimbo heheheeee er ntacheka nahisi hadi nijikojolee heheheheheee

Itakuwa bonge la burudani, ila saa hizi hutoruhusiwa kuchungulia chupi tukiwa tunaruka kamba.
Old School Re-union...
 
Mwenzenu mimiii eeeeeeeeeee mchumba wangu eeeeeeeeeee ni simatiiiii eeeeeeeeeeeeeee lol pronunciations za kitoto simati


Cc Smart911
 
Its complicated sijui nianzie wapi. Mnaozinga mko wawili, mnaowawinda wanakuwa wanazunguka kwenye umbo mstatili.

Hahahahaaa yaani wewe unakumbuka kabisaa na ilikuwa atakayecheza hadi kufikia 100 kwa kuhesabu vile vyumba vya mstatili kwenye kila pembe au kona anakuwa kawaokoa wengine wote waliobabuliwa. Mnaozinga msipokuwa na ushirikiano mtazinga hata mara tatu. Hapo ndo kubabuana mabomba kanaanza na mpira ujazwa mchanga hahahahhaaa ukibabuliwa la uso lazima ukae chini kwanza hahahahahaa.

Ila napenda kwasababu inakupa akili ya mahesabu na kufikiria nawamalizaje hawa kisha nami niingie kucheza,mie nilikuwa nikizinga nahakikisha nimewababua kwanza wanaojua kucheza wenye machejo. Halafu wale ambao hawana machejo aaah unawamaliza fasta. Aliyetoka wa kwanza na wa mwisho ndo wanazinga.

Sasa nikiingia kucheza nahakikisha napambana sibabuliwi wa kwanza na pia nachezaaa nikiona watu wanakaribia kuisha najibabulisha ili nisizinge hehehehehehehehee. Hesabu za kitaani hizo zinaitwa.

Sasa itokee waliobabuliwa ifike zamu yao kuzinga halafu wajidai wameitwa kwao weeeh lazima tuwababue kwa mpira na wakija siku ingine lazima waanzie kuzinga.

Na ikitokea mti kaja kakuta mchezo ushaanza na anataka kuingia basi anaambiwa aingie kuzinga kwanza kisha ndo acheze wakifanikiwa kuwababua wote.

Mkifika siku ingine ndo mnaanza mnapinga inkseeksooo mnakuwa wanne, wataonyanyua viganja juu timu moja wataofunika viganja timu ya pili weeeh ilikuwa raha. Hiyo tuliitumia kwe ye rede ya mateka. Daaah those days....
 
Vipi yange yange walishawahi kukupa kucha nyeupe? Wakipita juu tulikuwa tubaimba
Yange yange nipe kucha nyeupeee....
Cha ajabu kweli kwenye kucha kunatokea vidoa vyeupe!

Hahahahaaa daaah ungekuwa Nyani Ngabu ningekwambia fcuk you. .... unajua kwanini......
We nahisi tulikaa mtaa mmoja au ulikuja kuhamia mtaa ambao sie tulihama hahahahhahahaaa

Hiyo ya yangeyange nipe kucha nyeupe nimefanya sana. Tena nikiwa na kaka zangu, tukienda kwa babu yetu Upanga mtaa wa Malik sijui ule karibu na kwa baba taibali jioni wanapita yangeyange weengiii. Basi tunaanza yangeyange nipe kucha nyeupee hahahahahaha na kweli.....

Huwezi amini hadi sass hivi kucha zangu kama sijapaka hina au rangi ya kucha hizo alama nyeupe zinaonekana daaah

Hahahahahahahahahahaaaa
 
Pepsi mirinda mbooo inadinda mpka kwenye mimba


Kuna mpuuzi mmoja alikuwa katuzidi miaka alikuwa anatufundisha matusi huyo nyingi nmesahau ila hyo moja hapo juu naikumbka kwasababu nilipigwa collabo ya kipigo na mshua na maza nilipita naimba bila wasiwasi nikavutiwa ndani

Aaahahahahahhahahahahahaaa aahahahahahhaahahhaahhahahahaa eehehehehehehehehheheheeeee yaani weweee umenifanya nicheke kwanguvu hapa nilipo loooh
Nimevuta taswira jinsi ulivokuwa unaimba huo wimbo kwanguvu bila wasiwasi unashangaa unavutwa ndani paaah paaah kichapo loooh.

Pole mwaya looh nimecheka hadi machozi looh.
 
Back
Top Bottom