Hello mambo, za mwananyamala....
Ulishawahi kucheza kibumzi kibumzi
Chameemee Chameemee
Halafu kika mtu anaulizwa kimya kimya ataje mchumba ake hahahahahahhaaa hapo sasa kama kuna kavulana unakapenda mtaani unakasema.
Halafu muimbishaji anaanza kutaja.
Nilonge nisilongeee loongaaaa
Nisemeee nisiseemeeee seemaaaa
Mwenzetu Kasie. .... mchumba ake....
Asprin basi watu eeehhh yeeeyyy hapo kama kulikuwa na kaschana kingine kanampenda basi ananuna. Na ukikuta kavulana na kenyewe kanakupenda basi kanaanza uchokozi mara akuvute nywele mara akidalike mara akufinye au akutekenye....
Basi wewe unajidai banaa niniiii mii staakiiiiii ntakusemea. .... Hahahahahahhahaaa ilikuwa raha sana. Hapo kama kavulana kababe mtaani huwezi kuonewa au kupigwa lazima akutetee. Asipokuona mtaani anakuja kukuulizia kwenu na siku kwao kukipikwa maandazi basi atakuibia moja akuletee uonje hehehehehehehhee
Those were innocent pure love.