Hakuna anayeweza kudhibiti rushwa na ufisadi nchi hii sababu jamii yenyewe inaabudu mafisadi japo inapiga na kuua vibaka wa kuku na wakwapua simu. Itokee siku moja fisadi likamatwe na wananchi wenye hasira halafu livishwe tairi shingoni kisha limwagiwe petroli na kutiwa kiberiti mchana peupe ndiyo labda tutaanza kuona mabadiliko.
Sasa hivi ukipewa madaraka ukawa mwadilifu kabisa kabisa ukaja kuyaacha ukiwa bado hujajilimbikizia mali jamii hiyo hiyo inakucheka kuwa we ni boya ulizubaa. Hakuna incentives zo zote za kuwa mwadilifu. Wakati huo huo ukiiba sawasawa unasifiwa kuwa we ndo mtoto wa mjini...na hata ukitajwa kwenye ripoti ya CAG mara mia hakuna ambacho utafanywa.
Kuwa mkali na kubweka bweka kidogo pengine inasaidia lakini hii ya kuambiana kabisa kuwa eti kuleni kwa urefu wa kamba zenu sijui itakuwaje. Nchi inasikitisha sana hii !!!
View attachment 2200569