igogondwa
JF-Expert Member
- Aug 1, 2021
- 2,597
- 3,373
Sanaa DED hawezi kumpangia DC watumishi wake, kwanza hata mishahara hizo ofisi mbili kila mmoja anajitegemea.Jenerali Lengai Ole Sabaya anajichanganya kweli kweli!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sanaa DED hawezi kumpangia DC watumishi wake, kwanza hata mishahara hizo ofisi mbili kila mmoja anajitegemea.Jenerali Lengai Ole Sabaya anajichanganya kweli kweli!
Hakuna kitu hapooo, DED hana mamlaka ya kupeleka mtumishi ofisi ya DCWewe labda hujui namna ya kutoa usjahidi yupo very composed na ushahidi wake kashauset na anauhakika wa anachokifanya kipo relevant katika ku disprove allegations against him
Kaulizwa kwa nini ulipokuwa unaenda huko Arusha ulikuwa humjulishi bosi wako (RC Kilimanjaro)? Eti anajibu iulizwe mamlaka ya uteuzi [emoji1787][emoji1787]Huyu akicheza anafungwa. Haiwezekani mahakamani useme ni siri halafu eti unasema mtu alipangiwa kwako na ofisi ya Mkurugenzi lakini haujui majukumu yake ni yapi. Lengai Lengai umeanza kuchanganyikiwa.
Si ndiyo maajabu hapo? DC ni ofisi inayojitegemea kwa kila kitu na Mgt yake na ajira zake.Dc anapangiwa mtumishi na DED? Hii inaitwaje kiporotokali wewe mjuaji?
Labda atashinda njaa.Tuweke chuki pembeni ole sabaya na mawakili wake wako vizuri , wasipo angalia . dogo anashinda kwa kishindo.
Kuchanganyikiwa huyu dogoKaulizwa kwa nini ulipokuwa unaenda huko Arusha ulikuwa humjulishi bosi wako (RC Kilimanjaro)? Eti anajibu iulizwe mamlaka ya uteuzi [emoji1787][emoji1787]
Kapoteza kumbukumbuArusha .
Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro Lengai o Sabaya amemkana mshirika wake katika kesi hiyo ya unyang'anyi wa matumizi, Sylvester Nyegu, kuwa hakuwa msaidizi wake.
Sabaya na wawili wawili, Nyegu ambaye anadaiwa na upande wa mashtaka kuwa msaidizi wake binafsi na Daniel Mbura aliweza kuona kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha, inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo.
Katika kesi hiyo ambayo iko katika hatua ya utetezi, washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matatu ya unyang'anyi wa kutumia silaha katika duka la Mohamed Saad eneo la bondeni jijini Arusha.
Akihojiwa na mwendesha mashtaka, Wakili wa Serikali Baraka Mgaya leo Jumatano Agosti 18, 2021 kuhusu uhusiano wake na mshtakiwa huyo wa pili, Sabaya ameeleza mahakama hiyo kwa kuwa anajua Nyegu lakini hakuwa msaidizi wake binafsi.
Amedai kuwa alipangiwa kufanya naye kazi na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Hai.
Lakini alipoulizwa kuwa Nyegu alipangiwa na mkurugenzi kufanya naye kazi kama nani, Sabaya amedai kuwa hafahamu kuwa alipangiwa kama nani huku akimrushia mpira Nyegu mwenyewe kuwa ndiye anayeweza kueleza.
Sabaya ambaye ni shahidi wa kwanza katika kesi hiyo ya upande wa utetezi, alikuwa akihojiwa na upande wa mashtaka baada ya kumaliza kukamilisha kutoa utetezi wake ambapo hata hivyo amekwepa kujibu maswali mengi akidai kuwa hawezi kuelezea kwa kuwa siri
[emoji2398] Mwananchi