Ole Sabaya kaa kimya uchunguzwe, acha kuchonganisha mamlaka za nchi. Utaingia matatizoni

Ole Sabaya kaa kimya uchunguzwe, acha kuchonganisha mamlaka za nchi. Utaingia matatizoni

Mimi bado nina mashaka naye kuwa ni Mtu wa Kitengo (bado kile kitambulisho alichoshikwa nacho cha kufoji cha TISS mwaka fulani) harafu akaachiwa bado napata mashaka!
Mambo yataishia uchunguzi bado unaendelea.
IMG-20210514-WA0040.jpg

Hana ukitengo wowote pimbi huyu na vitambulisho vyake vya kutengenezea stationary za ngaramtoni
 
Usitishe watu mjinga wewe,eti taasisi ya Raisi ina macho mengi,danganya wajinga,acha watu waongee wanachoamini,kamtishe mkweo huko
Nikiangalia hiyo Avarta yako ya " Nyamatare 1987". Nakumbuka juzi Sabaya akiwa Cloud TV alisema yeye ana MIAKA 34.

Pia namna ulivyojibu hapo inaonyesha Munkari wa Kimasai hivi.

Anyway ni Mtizamo wangu tu
 
Huyu jamaa ni mshirikina, sasa hivi anashinda kwa waganga likamatwe hili lijitu linyang'anywe ile pete pale kwenye kidole ndio inampa kiburi! Akijisahau akaivua ile pete, au yeyote akimvua anatiwa pingu fasta! Hata huku kutumbuliwa mama alimuwahi maana alitaka kumfanyia udunduwizi kama alivyomfanyia mwendazake! Hili kima ni lishirikina!
Hamuwezi mama. Si unaona mama baada ya Iddy ameenda mapumzikoni Zanzibar kusomewa dua nzito na wazee. Atakae mjaribu sasaiv kwisha habari yake.. tutamfukia
 
Inasikitisha sana kuona wananchi wakiteseka kwa sheria ambazo zimeekwa. Ifike wakati wananchi nao kwa umoja wao wajue tatizo liko wapi na wajaribu kutafuta suluhisho.

Mie kwa mtazamano wangu sheria zetu ni mbovu na nyingi ni za kijima. Sifahamu ni kwanini mtu kama DC/RC anapewa mamlaka kisheria ya kumueka ndani bila ya mahakama. Ziko nyingi sheria za kipuuzi puuzi kama hizi ambapo wananchi wanaishi kwa shida, wengine wakiambiwa hawapewi dhamana wanaita uhujumu uchimi, ugaidi .n.k

Nadhani iko haja ya wananchi kwa kutumia jumuiya za kiraia kuikalia serekali kooni, hadi iziondoshe. Inatia aibu kusikia TZ ati kuwa na blogi au youtube channel ni lazima uwe na leseni ya serekali!
 
Wakuu amani iwe juu yenu!

Hili naomba niliseme wazi na Sabaya mwenyewe najua yupo humu asome na asikie ujumbe impate. Kama hataki aache lakini matokeo atayapata muda sio mrefu. Hii ni tahadhari kwake kama ana masikio asikie, kama ana ubongo aelewe.

Kuna kundi la vijana wa CCM ambalo hata mimi nikiri mimi kwenye makundi hayo, wanafanya kazi kumsema Vibaya Mhe Rais wetu chini ya uamuzi wake wa kumsimashia Sabaya nafasi ya ukuu wa wilaya, makundi haya yanamtetea Sabaya kwa hali na mali akiyaandaa yeye mwenyewe. Kwa bahati mbaya sana kazi wanayofanya ni kudhihaki mamlaka za nchi. Wamesahau kuwa aliyemsimamisha kazi Sabaya si Samia Suluhu Hassan bali ni Rais Samia Suluhu Hassan. Urais ni taasisi kubwa ina macho yake ya kila aina na ni mengi.

Sabaya badala ya kutulia achunguzwe tuhuma dhidi yake ili ma majibu yajulikane na badala yake anatumia vijana kumsafisha aonekane kua hana hatia. Sabaya unataka kujihami na nini? What if matokeo ya uchunguzi yakasema aliharibu pakubwa na aende jela, wasafishaji wake watenda wapi hali ikiwa hivyo. Wewe wenzako wanatulia hata ili hata kama kuna makosa yatadhihiri hata busara inaweza kutumika kumuadhibu, leo wewe unaona umeonewa na kutuma vijana kumsema vibaya Mama?

Matukio yote unayotuhumiwa nayo Sabaya ni makubwa sana ni bora kukaa kimya. Muungwa huchutama pale akoseapo. Wajanja hukaa kimya ili hata kama kuna makosa waonewe huruma lakini wewe kichwa ngumu.

Hivi wewe unafikiri Mama hana faili lako? Unafikiri hakujui vizuri? Endelea kujiona unaonewa utapata mtu wa kukurudisha kwenye nafasi yako kama si jela.
hakuna mtu pale, kichwani bure kabisa, profesa assad ndio aliokuwa anamaanisha watu kama hawa kwenye serikali kuwa kichwani hazimo, bado analeta propaganda kutumia account feki nyingi nyingi mitandaoni
 
Hizo ni tabia za rika la Nyangoro kule umasaini, angekuwa real Laigwanani angechutuma.

Ninachokijua kuhusu Sabaya ni kwamba uchunguzi utafanyika tuhuma zitathibitika (kwa sababu ziko wazi)na atashitakiwa ikibidi ataenda jela. Hatofautiani sana na James Kaji tuhuma ni kama zinafanana na ukwasi is like the same sema kaji alikuwa anapiga kimya kimya.
Huyu James Kaji ni nani au alikuwa na ni kwani?
 
Back
Top Bottom