Oman: Rais Samia ataka kuwepo Maritime transport ya kusafirishia Wanyama wakiwa hai kutoka Tanzania kwenda Oman

Mchakato mzima wa biashara ya wanyama hai unahusisha idara nyingi mfano wafugaji wenyewe, mabwana mifugo, afya ya mifugo, kunenepesha mifugo, usafiri rafiki mpaka bandarini na kisha kupakiwa ktk meli . Ni zoezi linalotakiwa wadau wengi kujiweka ktk utayari kufanikisha azma hiyo ya biashara ya wanyama hai kufanyika.

 
Hilo la wanyama pori umelitoa wapi?
Hizo chuki zenu huwa zinawasaidia kulamba asali?

Hilo la Wanyamapori hai umelitoa wapi?

Kwa Samia mtahangaika Sana aisee
 
Shamba la ngombe la Hussein Bashe huko Bagamoyo ni mfano wa jinsi ya kujitayarisha kwa Tanzania kuingia ktk biashara ya wanyama hai

 
Kama tunahitaji joint vencher basi tunahitaji walete mitaji siyo kutegemea mabenki yetu. Mabenki yetu yaje kutoa support baada ya production kuanza yonde yonde Mama asiwape open cheque
 
😂😂😂tushauzwa kwa waarabu,, nisivyowapenda waarabu mimi
Lazima uwachukie tu, kwa kivazi kama ulichoweka kwenye avatar inaonyesha unapenda mambo ya kujiachia viuongo vyako vya ndani hovyo kwa namna hiyo ni ngumu kuishi sehemu zenye ustaarabu mzuri .
 
Wanyama hai sawa..ila tutapigwa sana...mana watachukua faida yote kutoka kwenye kwato..pembe..ngozi na offals.

Sikubaliani nalo hili.

Wauziwe meat and meat products sio myama hai.

Haya mambo JPM aliyakataa ya kuuza malighafi...hatuwezi kuza viwanda vya ndani na raia wetu watakosa kazi na ajira.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mama anafungua nchi, tumuunge mkono
 
NJIA ZA HIFADHI MAALUM ZA KUSWAGA MIFUGO ZIANDALIWE

Wafugaji wa Handeni, Kilindi, Manyara, Maswa, Bariadi nao wasisahauliwe waunganishwe katika biashara kwa kuwepo special corridor ya kusafirisha wanyama hai watakaoswagwa na wachuga ngombe mpaka bandarini Bagamoyo.

Mikoa na wilaya husika pamoja na serikali kuu ianze kujipanga kuweka beacons / mawe ya kuhifadhi mipaka ya njia hizi kufanikisha mnyororo wa biashara hii iweze kwenda shwari bila malalamiko ya uvamizi kwa ujenzi wa nyumba za makaazi au wakulima kulima katika njia za kupitisha mifugo hii hadi bandari za pwani au lawama za TANROAD kuwa kwato za ngombe zinaharibu lami n.k

Kama mfanyabiashara Tippu Tip aliweza kuwa na njia zake kufikisha pembe za ndovu na watumwa pwani Bagamoyo The Central Slave and Ivory Trade Route - UNESCO World Heritage Centre , sisi dunia hii ya GPS, smartphone na maofisa ardhi wa kisasa tutashindwa kuandaa njia za misafara ya mifugo kuelekea Bagamoyo na miji mingine ya pwani yenye bandari ? Tuanze sasa nchi imefunguliwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…