Oman yapiga Marufuku abiria yeyote kutoka Tanzania asikanyage kwao

Oman yapiga Marufuku abiria yeyote kutoka Tanzania asikanyage kwao

Siku mwanao akija na kukuonyesha matokeo amescore 7% ukamuhoji na akakwambia “tupo wengi tumepata 7% na wengine wamepata 3%”. nadhani wewe unaweza kuwa happy tu kwa kuwa “wapo wengi na hivyo sio shida” na life likasonga as if hakuna lililotokea

Two wrongs don’t make it a right. Look at the big picture!
Mlipuko huu wa Corona, kila mtu alinde abiria wake, Mimi Niko kijijini, Nimepiga marufuku mtu yeyote anayetokea mijini kukanyaga kwangu,

Wewe unaona ajabu Kwa Oman kulinda watu wake siyo???
 
Wewe umeona ni Tanzania tu iliyozuiliwa watu wake kuingia Oman
Yaani ni sawa na kusema. Mbona wote wanakufa ngoja na Mimi nife tu. Haya ni mawazo ya kijinga. A leader always struggled to overcome others not to be in the same pool .
 
Dunia nzima sasa inatuona Tanzania kama "NUKSI a.k.a MWAJUMA NDALA NDEFU". Mataifa yote duniani huko yanatu "NG'ONG'A NA KUTUSENGENYA".

Juzi African Union ilitoa tamko kwamba Tanzania tujichunge, tunahatarisha bara zima la Africa kwa ukaidi wetu wa kuchukua tahadhari dhidi ya hili janga la Covid-19.
Na ndio ukweli wenyewe. CHanjo hatutaki, kudhibiti misongamano hatutaki, na kuvaa barakoa ni kwa kulazimishana. Matokeo yake itafikia hatua hakuna Mtanzania ataruhusiwa kutoka kwenda nje ya nchi, kwa sababu atakuwa hajachanjwa na wala taarifa za afya yake hazijulikani. Siasa mbaya sana kwa kweli
 
Kama moja ya hatua ya kupambana na Covid-19 nchi ya Oman imezipiga marufuka nchi zipatazo 12 kufika kwao Tanzania ukiwemo.

Ikumbukwe kwamba Tanzania na Oman zina uhusiano wa karibu sana hususan Zanzibar ambao wameoleana sana. Hili litatuathiri sana.

Hii ni kwa sababu tunaonekana hatuko serious kupambana na janga la Corona kama mataifa mengine.

Chanzo: BBC
Wao hawaathiriki kwa hatua hiyo,?,kwanini mnapenda kujishusha sana ?
 
Kila kona tumekua kichekesho kwani tatizo liko wapi taifa kama taifa tukifanya jitiada kama zilizofanyika mwaka jana? Kwanini viongozi wamekua wazito sana juu ya hili? Sawa hatutaki chanjo kama wanavyojinasibu vipi hatu za kujirinda mbona nazo hazifanyiki? Kipi hasa kinakwamisha kuamasisha watu kuvaa barakoa, kunawa mikono na kuepuka misongamano isio ya lazima kama mwaka jana tu.. kunanini hapa kati mbona taifa kama taifa tunafanya vituko vya kijinga sana
 
Wanachoangalia ni wingi wa maambukizi maana watanzania wanaoingia Oman wakipimwa kule zaidi ya 18% wanapatikana na virusi vya korona.
18% tu?

Nikafikiri wote
 
Yeye ni mtanzania ameamua kuizungumzia nchi yake sasa kuna tatizo gani?Halafu Tanzania kuwekwa kundi moja na nchi kama South Africa ni hatari sana maana hilo Taifa limeathiriwa pakubwa.

Mpaka Oman kufikia kuiwekea vikwazo vya safari Tz basi ujue kuna tatizo kubwa ndani ya serikali hawalifanyii kazi.
Ghana, SA, na kwingineko nako selikali hazifanyi kazi?

Kama huyu Ghana si juzi tu mlimpigia hata kura ya kupata tuzo ya kiongozi bora? Vipi tena kiongozi bora corona inamtoa kamasi hadi anawekewa vikwazo vya usafiri?
 
kwa hito unataka tupate faraja kwa sababu ni nchi nyingi?!? swali hapa na masikitiko hapa ni WHY MY TANZANIA!?!? hata kama ingekuwa kwa siku moja tu WHY TANZANIA?!? mi naona ndio la msingi hapa
Kwanini usijiulize why hizo nchi nyingine?
 
Watetezi watakuja punde waseme “kwanza hatupo peke yetu by the way, zipo Nchi 10”

Kuna watu siku zote hutafuta namna ya kutetea tuuuu na hawaangalii picha kubwa
Kwani hizo nchi zingine zilizozuiliwau mleta uzi hazifahamu?,au anausongo na Tz tu?
 
Wanachoangalia ni wingi wa maambukizi maana watanzania wanaoingia Oman wakipimwa kule zaidi ya 18% wanapatikana na virusi vya korona.
Hapa ndio kwenye tatizo.. tumekua waze wakuamini ngano za maombi yatanusuru hili taifa.. namini hata Sir God uko alipo anatuona mazwazwa tumepewa ubongo wakuchakatua mambo lakini bado tunashindwa tatua changamoto zinazotukabiri nakujitia uvivu wa kufikili.. tuite wachungaji tanzania nzima wafunge na kuomba huenda janga likatoka nduki kama shida nimaombi
 
A leader always struggled to overcome

I am very pleased with the decision of the Ministry of Justice to change the use of English in court to bring it to our beloved Kiswahili language.

Meaning For most Tanzanians they do not know English like this relative

Use only Swahili
 
Wale ambao hatuna uhusiano huko tunaendelea kudunda ila Zanzibar itawacost sana
 
JF bwana, zamani ndiyo ilikuwa chanzo changu pekee cha habari.....
Mleta mada amaeishiwa wino wa kuandika nchi nyingine ambazo pamoja na Tanzania watu wake wamezuiwa kuingia Oman..
Aibu yako mleta mada!
Nikumbushe jambo moja Alexander The Great kuwenye mwili wako kuna kitu kinaitwa "subconscious mind" kwa kiswahili wanaita mawazo ya kina....sehemu ambapo vitu vyote vinafanyika bila utashi wako mfano kkupiga kope, kupumua, mapigo ya moyo, nk kuna kitu unaongeza ambacho kitakuwa kinafanyika bila utashi wako....yaani umekitengeneza au kwa kujua au bila kujua na kitakuwa kinafanyika automatically bila utashi wako maana "subconscious mind" huwa hajali unaigiza au unatania....yaani hata ikitokea fursa ya kukunufaisha kale ka element ka KUPOTOSHA mambo katakuwa kanajirudia bila wewe kujua....!
Kwani jamaa yuko nchi gani na wew uko nchi gani ambayo imepigwa ban lakini jamaa hajaisema?
Mataga ni hasara kwa taifa
 
Wewe umeona ni Tanzania tu iliyozuiliwa watu wake kuingia Oman
Kasema kabisa kuwa zipo nchi nyingine ikiwemo Tz, yeye ni Mtanzania na yuko Tz hivyo kaandika kuhusu Tz, kwanini na wew usiandike kuhusu hizo nchi nyingine? So ukiambiwa kwa mfano na Ghana wamepigwa ban so akili yako ita justify ujinga wako kwa sababu mjinga siyo wew pekee au?. Idiot
 
Back
Top Bottom