Uchaguzi 2020 Omary Kumbilamoto atoboa siri za CHADEMA kuhujumu Miradi ya Awamu ya Tano

Uchaguzi 2020 Omary Kumbilamoto atoboa siri za CHADEMA kuhujumu Miradi ya Awamu ya Tano

Said Stuard Shily

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2017
Posts
2,396
Reaction score
2,108
Leo eneo la Kinyerezi kwenye kampeni za Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi ambaye ndie Rais Mtarajiwa hilo halina ubishi, Kumbilamoto amemuomba msamaha Dkt. Magufuli kuwa walifanya makosa makubwa sana akiwa Meya wa Ilala kupitia CHADEMA kuhujumu miradi ya Serikali ili kuonesha Rais Magufuli hawezi kutatua matatizo ya wananchi, hivyo amesema CHADEMA ni Chama kinachozungukwa na watu wasiolitakia Taifa letu mema hasa sisi wanyonge.

===

Kumbilamoto.jpg

Aliyekuwa Mstahiki Meya Manispaa ya Ilala, ambaye pia alikuwa ni Diwani wa Vingunguti, Omar S. Kumbilamoto amumomba radhi Dkt. Magufuli leo katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kinyerezi

Kumbilamoto ameomba radhi kwa kuwa alikuwa Upinzani katika Umoja uliojulikana kama UKAWA katika Uchaguzi Mkuu wa 2015

Kwasababu hiyo ameomba radhi kwa Rais, CCM, wananchi na viongozi wa Ilala kwa mabaya waliowafanyia kipindi yuko upinzani

Ameyasema hayo alipopewa muda wa kuzungumza kwenye mkutano wa kampeni

Nukuu:
Kabla sijaongea, nichukue fursa hii kwanza kukuomba msamaha wewe binafsi, Chama cha Mapinduzi na wananchi kwa ujumla kwa mabaya tuliyowafanyia wakati tupo upinzani. Naomba sana unisamehe Mheshimiwa Mwenyekiti.

Mheshimiwa Rais, katika manispaa yetu uliingiza miradi ya Soko la Kisutu, Machinjio ya Vinginguti na Hospitali ya Kivule.

Ukaingiza bilioni 17.6 ujenzi wa daraja la Ulongoni, bilioni 4.3 ujenzi wa Daraja la Zimbili na uliingiza takribani bilioni 115 ya barabara za BMDP.

Nisikufiche Mheshimiwa Rais, miradi hii ilikwama kwa maelekezo kwamba tukifanya sisi kama ukawa tutakupa kiki wewe Rais Magufuli. Ilibidi na sisi tutii, tukakuhujumu. Kwahiyo naomba unisamehe sana.

Baada ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala sisi kurudi, miradi hii yote tukaikwamua na hivi sasa ipo kwenye maendelezo na mingine imeshakamilika.

Lakini kubwa zaidi Rais kilichotuuma sisi tukawa upinzani kulikuwa na mikopo ya Asilimia 10 ambapo mikopo hii ilikuwa haitoki na wala wananchi hawaijui – 2010 hadi 2015. Ulipoingia ukaagiza itoke hii mikopo takribani bilioni 10 na hapa nimpongeze Mkurugenzi , pesa hizi zimewafikia wananchi wa kawaida – mama lishe na bodaboda.
 
Leo eneo la Kinyerezi kwenye kampeni za Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi ambaye ndie Rais Mtarajiwa hilo halina ubishi, Kumbilamoto amemuomba msamaha Dkt. Magufuli kuwa walifanya makosa makubwa sana akiwa Meya wa Ilala kupitia CHADEMA kuhujumu miradi ya Serikali ili kuonesha Rais Magufuli hawezi kutatua matatizo ya wananchi, hivyo amesema CHADEMA ni Chama kinachozungukwa na watu wasiolitakia Taifa letu mema hasa sisi wanyonge.
Malaya tu huyu wa siasa CHADEMA WANA UWEZO WA KUHUJUMU MAENDELEO
 
Kwa hali hii naanza kuamini kwanini wakati mwingine hawa mameya wa kutoka vyama vya upinzani walikuwa wanaporwa nyadhifa/ madaraka yao kwa nguvu na kuvyrushwa ofisini.
 
Zimemwagwa siri kibao kuwa stendi ya MBEZI tu ilisumbua kujenga sababu kila diwani wa CHADEMA alikuwa na kampuni yake aliyotaka ipate tenda sababu wao ndio walikuwa wengi wakawa wanavutana tu wenyewe kwa wenyewe kwenye vikao vya jiji hadi hela ikawa haiwezi tumika.
 
Jomba hua anapenda kusamehe.

Nimemsamehe Kinana

Nimemsamehe Nape

Nimemsamehe Commisioner Andengenye

Nimemsamehe Wanaonichukia

Nimesamehe waliochagua upinzani 2015

Nimemsamehe.................Itaendea
Apparently, yeye ni Mkuu wa Malaika kwenye next life .......................!!
 
Kama no muunga juhudi,yeye apambane na half take na asiwasingizie wengine.
 
Huyu apewe ulinzi...wanaofanana na wale waliojulikana kule Tunduma na Njombe wako wengi katika chama hicho.
 
Kumbuka yeye ni kiranja wa Malaika huko mbinguni...kwamujibu wa maneno yake.
Jomba hua anapenda kusamehe.

Nimemsamehe Kinana

Nimemsamehe Nape

Nimemsamehe Commisioner Andengenye

Nimemsamehe Wanaonichukia

Nimesamehe waliochagua upinzani 2015

Nimemsamehe.................Itaendea
 
Wanauangalia uzi huu kwa machungu! ushaidi wa aliyoyasema Omary ni michango ya member wengi wa JF kila jambo linalofanywa na serikali ni kupinga tu!
 
Back
Top Bottom