Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Mpira ni taasisi yenye lugha yake, taratibu zake na sheria zake. Mpira ndio taasisi inayoruhusu mtu kuuzwa kwa mkataba fulani wa muda fulani kwa kiasi fulani. Hii inafanyika kwakuwa:

1. kila timu inataka wachezaji wazuri kuliko timu pinzani.

2. Wachezaji wazuri sio wengi sana kwenye jamii.

3. Kila timu inataka kushinda kwa gharama yoyote, haipendi kufungwa.

4. Mpira ni pesa, hivyo wachezaji ni pesa (bidhaa) pia.

Sababu hizi ndio zilizosababisha mpira ukawa na taasisi zake maalumu chini ya FIFA ambazo haziingiliwi na serikali na wanasiasa kwenye uendeshaji wake.

Ombi la Rais lazima liheshimiwe na Yanga na lazima litekelezwe kwa kufuata lugha na kanuni za kimpira kwakuwa utekelezaji wake utaacha alama, njia na utaratibu ambao utatumika kutatua matatizo mengine yajayo nchini yatayofanana na hili la Fei Toto na Yanga.

Ukweli ni kwamba Fei Toto:
1. Anatakiwa na timu nyingine ambayo haitakii kujitokeza wazi. Hiki ni kinyume.

2. Fei Toto ana mkataba mbichi na Yanga.

3. Fei Toto anataka kuvunja mkataba kwa unilaterally, kinyume na taratibu za mpira.

Swali hapa ni njia itakayotumiwa na Yanga kumaliza mgogoro na katoto Fei Toto itatoa SoMo gani kwa wachezaji wengine Yanga na timu nyingine nchini?

Je, njia hiyo inaweza kutumiwa tena kumaliza mgogoro mwingine unaofanana na huo kama ukijitokeza?

Soma:
- Rais Samia: Sifurahii Mgogoro wa Yanga na Feitoto. Nataka umalizike
 
Mpira ni taasisi yenye kugha yake, taratibu zake na sheria zake. Mpira ndio taasisi inayoruhusu mtu kuuzwa kwa mkataba fulani wa muda fulani kwa kiasi fulani. Hii inafanyika kwakuwa:


Je, njia hiyo inaweza kutumiwa tena kumaliza mgogoro mwingine unaofanana na huo kama ukijitokeza?
Ni lazima Yanga watasimamia kanuni tu
 
Nimeona wapambe wa fei toto wakifuraishwa sana na kauli ya Rais Samia juu ya kuiomba Yanga kumalizana Fei.

Nimeona baadhi ya wasioelewa wala kutambua hili jambo lipo kiutaratibu zaidi na sio kihisia wala kimihemko.

Ndiyo maana hata Rais katumia kauli ya kuomba na sio Amri akijua fika kuwa masuala ya soka ayaingiliwi kivyovyote na mambo ya kisiasa.

Na fei mwenyewe ndiye mwenye uwezo wa kulihitimisha ili jambo kwa kufuata utaratibu, sheria na kanuni za kimkataba aliousaini na sio vinginevyo.

Asitegemee kwamba ataachwa tu bure aondoke eti kwa kuwa Rais kasema iyo kitu aitokaa itokee.

Bahati nzuri yeye mwenyewe keshatamka hana tatizo lolote na Yanga wala mkataba wake.

Basi yeye mwenyewe ndiye anayeonekana ana ukorofi achutame kwa kufata utaratibu, na utaratibu ni kwenda pale yanga wamtajie dau wanalotaka kwa timu yoyote inayomuitaji iweke mpunga mezani aondoke zake.

Jambo analolazimisha kwamba aachwe tu bure kama anavyotaka yeye na wapambe wake waliomrubuni ili wampate bwerere alitowezekana na atateseka sana.

Viongozi wa yanga wako very clear na Fei angekuwa smart kichwani hili jambo lingekuwa lilishakwisha kitambo sana, lakini jeuri yake na wapambe wake ndio vimemfikisha hapa.

Anajua keshayakoroga pakubwa ndiyo maana anaona ata aibu kwenda pale yanga anapakwepa kama ugonjwa wa ukoma, na awezi kulimaliza hili bila kuihusisha yanga ambao ndio mwajiri wake.

Kwa maana hiyo napenda kuwaeleza waliofurahia kauli ya Rais ya kwamba fei mwenyewe ndiye mwenye utashi wa kulimaliza hilo jambo lake kwa kufata utaratibu na sio yanga.

Yanga wameshampa option 3 za kufata ili aondoke ivyo ni juu yake kusuka ama kunyoa itifaki inazingatiwa.
 
Ile ni order,kimsingi huelewi maana ya power ya rais,mtu mwenye nguvu kama Rais akikuomba kitu unakuwa hauko kwenye position ya kumkatalia kutokana na nguvu aliyo nayo na yeye analijua.Anaweza asiwe na mamlaka ya kuingilia maswala ya kimichezo ila anaweza kuumiza biashara za maboss zenu.
 
Ile ni order,kimsingi huelewi maana ya power ya rais,mtu mwenye nguvu kama Rais akikuomba kitu unakuwa hauko kwenye position ya kumkatalia kutokana na nguvu aliyo nayo na yeye analijua.Anaweza asiwe na mamlaka ya kuingilia maswala ya kimichezo ila anaweza kuumiza biashara za maboss zenu.
We mwehu kabisa umeisikia hotuba yake kuhusu wafanyabiashara kina gharibu waliowekeza pale yanga? Kawaambia wapige kazi akuna atakayewagusa wala kuwabinya waendelee kumwaga mpunga kwenye mpira na mungu aendelee kuwabariki, kwaiyo kauli yako ya kuumiza biashara zao inakufa kifo cha kawaida, Fei afate utaratibu vinginevyo ataendelea kuumia mwenyewe
 
We mwehu kabisa umeisikia hotuba yake kuhusu wafanyabiashara kina gharibu waliowekeza pale yanga? Kawaambia wapige kazi akuna atakayewagusa wala kuwabinya waendelee kumwaga mpunga kwenye mpira na mungu aendelee kuwabariki, kwaiyo kauli yako ya kuumiza biashara zao inakufa kifo cha kawaida, Fei afate utaratibu vinginevyo ataendelea kuumia mwenyewe
Kwa hiyo assuarance aliyowapa we unadhani watamkatalia hiyo simple request(order).Mbona unakuwa mjinga kiasi hiki,kwani una umri gani.
 
Kikubwa kwenye haya maisha tujifunze kuweka akiba ya maneno hata kama tumegombana kwa kiasi gani. Viongozi wa Yanga na hasa wasemaji wao walimaliza maneno na mpaka wakafikia kumtukana/kumdhalilisha Mama Fei vile vile Fei nae alimaliza maneno mpaka akafikia kuidhalilisha mojawapo ya taasisi kubwa sana hapa Tanzania Yanga. Sasa mheshimiwa raisi amewaambia viongozi wa Yanga wamalizane na Fei hapa nauona ugumu wa kuumaliza ugomvi wao kirahisi labda tu upande mmoja utumie busara na kukubali yaishe ili maisha yaendelee.
 
Ile ni order,kimsingi huelewi maana ya power ya rais,mtu mwenye nguvu kama Rais akikuomba kitu unakuwa hauko kwenye position ya kumkatalia kutokana na nguvu aliyo nayo na yeye analijua.Anaweza asiwe na mamlaka ya kuingilia maswala ya kimichezo ila anaweza kuumiza biashara za maboss zenu.
Raisi hana maslahi yoyote kwenye hili, na Yanga halazimishwi kufuata ombi la raisi, mpira ni biashara, tunaongelea mamilioni ya hela hapa

Yanga walishatoa options zao tatu, zote zinampa favour huyu dogo, labda watoe ya nne kuwa hawatampiga fine, atafute timu kabla mkataba wake haujaisha ije mezani
 
Raisi hana maslahi yoyote kwenye hili, na Yanga halazimishwi kufuata ombi la raisi, mpira ni biashara, tunaongelea mamilioni ya hela hapa

Yanga walishatoa options zao tatu, zote zinampa favour huyu dogo, labda watoe ya nne kuwa hawatampiga fine, atafute timu kabla mkataba wake haujaisha ije mezani
Mzee, lile ni ombi kweli ila hakuna wa kupinga na Zaid yanga ndo watafanya kila namna wamalizane na Feisal
 
Ile ni order,kimsingi huelewi maana ya power ya rais,mtu mwenye nguvu kama Rais akikuomba kitu unakuwa hauko kwenye position ya kumkatalia kutokana na nguvu aliyo nayo na yeye analijua.Anaweza asiwe na mamlaka ya kuingilia maswala ya kimichezo ila anaweza kuumiza biashara za maboss zenu.
Jamaa anashindwa kuelewa utofauti wa Rais wa Nchi na hawa Marais wa mitaa kama madee au ney,hapo ni Yanga wanatakiwa kumuacha feisal tena kwa taarifa yako tu Leo wawakilishwi wa feisal wameitwa kukutana na Viongozi wa yanga,mpaka wiki ijayo feisal atakuwa mchezaji Huru tayari kuvaa jezi ya Mnyama mkali
 
We mwehu kabisa umeisikia hotuba yake kuhusu wafanyabiashara kina gharibu waliowekeza pale yanga? Kawaambia wapige kazi akuna atakayewagusa wala kuwabinya waendelee kumwaga mpunga kwenye mpira na mungu aendelee kuwabariki, kwaiyo kauli yako ya kuumiza biashara zao inakufa kifo cha kawaida, Fei afate utaratibu vinginevyo ataendelea kuumia mwenyewe
We ndo huna akili kuwambia vile ni alert kuwa anao uwezo wa kukubinya any time na anao uwezo wa kutokukubinya any time .
Hapo ni fasihi tu .Sasa unawezaje kupinga ombi la rais na ukabak salama?
Jiongeze chakata akili Yako vzr .
 
Muwe Mnasikiliza vizuri.

Rais ALISEMA NYIE mmeniomba na Mimi niwaonbe jambo Moja.

KLABU kubwa kama yanga kuwa na migogoro na wachezaji haipendezo.
Akaomba wamalizane na Toto.

Rais AMETOA Ombi.
Kutoa ombi si AMRI.

HAJA VUNJA KANUNI YOYOTE ILE.
 
Back
Top Bottom