Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

Nimeona wapambe wa fei toto wakifuraishwa sana na kauli ya Rais Samia juu ya kuiomba Yanga kumalizana Fei.

Nimeona baadhi ya wasioelewa wala kutambua hili jambo lipo kiutaratibu zaidi na sio kihisia wala kimihemko.

Ndiyo maana hata Rais katumia kauli ya kuomba na sio Amri akijua fika kuwa masuala ya soka ayaingiliwi kivyovyote na mambo ya kisiasa.

Na fei mwenyewe ndiye mwenye uwezo wa kulihitimisha ili jambo kwa kufuata utaratibu, sheria na kanuni za kimkataba aliousaini na sio vinginevyo.

Asitegemee kwamba ataachwa tu bure aondoke eti kwa kuwa Rais kasema iyo kitu aitokaa itokee.

Bahati nzuri yeye mwenyewe keshatamka hana tatizo lolote na Yanga wala mkataba wake.

Basi yeye mwenyewe ndiye anayeonekana ana ukorofi achutame kwa kufata utaratibu, na utaratibu ni kwenda pale yanga wamtajie dau wanalotaka kwa timu yoyote inayomuitaji iweke mpunga mezani aondoke zake.

Jambo analolazimisha kwamba aachwe tu bure kama anavyotaka yeye na wapambe wake waliomrubuni ili wampate bwerere alitowezekana na atateseka sana.

Viongozi wa yanga wako very clear na Fei angekuwa smart kichwani hili jambo lingekuwa lilishakwisha kitambo sana, lakini jeuri yake na wapambe wake ndio vimemfikisha hapa.

Anajua keshayakoroga pakubwa ndiyo maana anaona ata aibu kwenda pale yanga anapakwepa kama ugonjwa wa ukoma, na awezi kulimaliza hili bila kuihusisha yanga ambao ndio mwajiri wake.

Kwa maana hiyo napenda kuwaeleza waliofurahia kauli ya Rais ya kwamba fei mwenyewe ndiye mwenye utashi wa kulimaliza hilo jambo lake kwa kufata utaratibu na sio yanga.

Yanga wameshampa option 3 za kufata ili aondoke ivyo ni juu yake kusuka ama kunyoa itifaki inazingatiwa.
Wewe ndio hujui chochote, hakuna sehemu fei anataka kuachwa bure kama ulivyoeleza, fei aliwalipa yanga 112M sasa ndio bure hiyo? Na kama hujui kauli ya rais kwa nchi za kiafrika ina nguvu kiasi gani basi subiri muda uamue,
 
We mwehu kabisa umeisikia hotuba yake kuhusu wafanyabiashara kina gharibu waliowekeza pale yanga? Kawaambia wapige kazi akuna atakayewagusa wala kuwabinya waendelee kumwaga mpunga kwenye mpira na mungu aendelee kuwabariki, kwaiyo kauli yako ya kuumiza biashara zao inakufa kifo cha kawaida, Fei afate utaratibu vinginevyo ataendelea kuumia mwenyewe
Una kichwa kigumu balaa
 
Kikubwa kwenye haya maisha tujifunze kuweka akiba ya maneno hata kama tumegombana kwa kiasi gani. Viongozi wa Yanga na hasa wasemaji wao walimaliza maneno na mpaka wakafikia kumtukana/kumdhalilisha Mama Fei vile vile Fei nae alimaliza maneno mpaka akafikia kuidhalilisha mojawapo ya taasisi kubwa sana hapa Tanzania Yanga. Sasa mheshimiwa raisi amewaambia viongozi wa Yanga wamalizane na Fei hapa nauona ugumu wa kuumaliza ugomvi wao kirahisi labda tu upande mmoja utumie busara na kukubali yaishe ili maisha yaendelee.
Na rais katoa oda kwa yanga watumie busara
 
Wanajifanya kubisha tu lakini ukweli remote control ya Hersi ni Ghalib na yeye hayupo tayari kuharibu mahusiano yake na mamlaka kwa kushupaza shingo.Kitendo cha Hersi kuinuka na kuinamisha kichwa wakati Rais anatoa 'ombi' lake inatosha kusema Yanga 'watatumia busara' na kulimaliza hili swala mapema na kupeleka mrejesho kwa Mama haraka iwezekanavyo.
Na mpira wetu tushazoea mambo ya busara kutumika, hapo yanga watamuacha free of charge. Raisi wa nchi ndio kila kitu mzee
 
Basi subilia embe chini ya mnazi kwa hizo akili zako, Usifikiri kila sehemu ombi la Rais linafanya kazi, ombi la Rais litafanyiwa kazi na fei mwenyewe kufata utaratibu na sio vinginevyo akatajiwe dau lake alipe aondoke zake
Mama sio chizi kuwaomba yanga watumie busara, angetaka fei afuate utaratibu angemuomba fei afate utaratibu.
 
Ni njia rahisi tu ambayo Fei Toto anatakiwa aifate ili aachiwe huru aondoke, nayo ni kwenda yanga kutajiwa thamani yake ambayo kwa upembuzi wa haraka haraka si chini ya milioni 350, alipe aondoke kiroho safi vinginevyo hakuna huruma itakayomuokoa.

Sheria, kanuni na miongozo ya FIFA na CAF iko wazi na sio suala la kihisia au huruma ya mtu!

Eng. Hersi shikilia hapo hapo dawa ya kiburi ni jeuri!
Hahahaa, mwenye thamani ya mil350 hawezi lipwa 4m kwa mwezi, mwenye thamani ya 100m ndio hulipwa 4m kwa mwezi.
 
Wewe ndio hujui chochote, hakuna sehemu fei anataka kuachwa bure kama ulivyoeleza, fei aliwalipa yanga 112M sasa ndio bure hiyo? Na kama hujui kauli ya rais kwa nchi za kiafrika ina nguvu kiasi gani basi subiri muda uamue,
Fei hauzwi 112m.
 
yatamalizwa km raisi anavyotaka ila kwa taratibu zinavyotaka
Bila hivyo viongozi wa Yanga watalitema bungo. Timu za wanachama hazina mambo mengi ni NO or YES basi. Wanaweza kuwapa mwanya wale wasiowatakia mema.
 
Yanga wanaweza kumuachia ata Bure lakini Kwa kiasi flani ameharibu brand yake maana Kwa timu ambayo Iko makini haiwezi kumchukua mchezaji aina yake wanavunja mkataba kienyeji kwaiyo mpaka apo Fei ndio kapoteza zaidi kuliko yanga
 
Fei hauzwi 112m.
Kuuzwa kwani kuna timu inataka kumnunua? Na wala fei hataki kununua mkataba wake bali anataka kuuvunja kwa mujibu wa vipwngele vilivyomo na sio kukaa mezani kujadili, vipengele vipo wazi mnataka kujadili nini? Hivi ulishawaza kwanini fei aliweka 112m na sio laki moja au bilioni mbili?
 
I'm
Kuuzwa kwani kuna timu inataka kumnunua? Na wala fei hataki kununua mkataba wake bali anataka kuuvunja kwa mujibu wa vipwngele vilivyomo na sio kukaa mezani kujadili, vipengele vipo wazi mnataka kujadili nini? Hivi ulishawaza kwanini fei aliweka 112m na sio laki moja au bilioni mbili?
angekuwa yuko sahihi niijuavyo mimi tff hii ingeshasema Fei ni mchezaji huru kitambooo.
 
Kuuzwa kwani kuna timu inataka kumnunua? Na wala fei hataki kununua mkataba wake bali anataka kuuvunja kwa mujibu wa vipwngele vilivyomo na sio kukaa mezani kujadili, vipengele vipo wazi mnataka kujadili nini? Hivi ulishawaza kwanini fei aliweka 112m na sio laki moja au bilioni mbili?
Nijuavyo mm namna mpira wetu ulivyosogea mbele hakuna timu imara na makini itamsajili Fei Toto ikawa na matumizi nae kama aliyokuwanayo Nabi. Niite mbwa nimekaa paleee,
 
Nijuavyo mm namna mpira wetu ulivyosogea mbele hakuna timu imara na makini itamsajili Fei Toto ikawa na matumizi nae kama aliyokuwanayo Nabi. Niite mbwa nimekaa paleee,
Hayo mambo ya sheikh yahya hatuyataki
 
yale mabango ya kisiasa uwanjani yanawaumiza wao wenyewe.

Hakuna ombi hapo. Issue ya feedback ni Amri🤣🤣🤣🤣
Hakuna kocha wala ofisa makini angependa kukaa mahali ambapo kazi ya mpira imechanganyika na siasa, wataondoka tu. Pale Chelsea Uingereza ilichanganya siasa na mpira, sasa hivi chelsea imepoteza uelekeo. Chelsea ilitekeleza maagizo ya Serikali kumfukuza Abramovic kwaajili ya Ukraine.

Fei toto ameondoka kwa njia ile, Yes!! lakini njia ile ina consequences zake kwa wachezaji, benchi la ufundi na uongozi kwakuwa lazima kutatokea mgongano wa mawazo na maoni ndani ya wachezaji, benchi la ufundi, mashabiki na viongozi kuhusu kutekeleza ombi lile la Mkuu. Kuna wakati Yanga italazimika kutumia fedha nyingi sana msimu huu kuliko ambavyo ingekuwa kuwabakiza wachezaji, makocha na hata viongozi wakuu.
 
Chagueni kati ya kupewa eneo la kuongezea kujenga uwanja jangwani au mwacheni fei aende zake msimbazi.
Nilisemaga humu wakati uleeee kuwa sakata la Toto na namna alivyohamia Azam litautesa mpira wetu. Watu walinichukilia poa. Hebu ona Simba nao wanatarajia sauti ya Rais Samia kumaliza swala la Awesu Awesu, maana linafanana kabisaaaaaaaaaa na lile la Fei Toto.
 
Nilisemaga humu wakati uleeee kuwa sakata la Toto na namna alivyohamia Azam litautesa mpira wetu. Watu walinichukilia poa. Hebu ona Simba nao wanatarajia sauti ya Rais Samia kumaliza swala la Awesu Awesu, maana linafanana kabisaaaaaaaaaa na lile la Fei Toto.
Hakika....sasa yametimia
 
yale mabango ya kisiasa uwanjani yanawaumiza wao wenyewe.

Hakuna ombi hapo. Issue ya feedback ni Amri🤣🤣🤣🤣
Kama Awesu nae mzanzibar anatarajia the same to happen . Sio sawa
 
Back
Top Bottom