Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

Tufanye assumption wewe ndio Hersi, na umeshashiba pilau la Ikulu, Kataa ombi la raisi kwa kujaza sehemu iliyo wazi.

RAISI WA JMT: Naomba suala la Fei mlimalize.

Hersi:______________________
 
Linavunjaje kanuni za fifa? Yanga ndo mshika mkataba, sio fifa, akiamua kuachilia, hakuna shida.

Ni sawa na wewe ununue eneo utapeliwe, uamue kusamehe usiende mahakamani, hakuna sheria ta nchi imevunjwa
Huwezi kumwachia daudi aende halafu kumzuia masoud asiende kwa kosa au ombi kama lilelile la daudi. Huu ni wakati wa kutoa elimu hata kwa Rais wetu nae ajue namna suala Fei Toto linavyokuwa gumu kulitatua kwa wepesi kama anavyoomba.
 
Huwezi kumwachia daudi aende halafu kumzuia masoud asiende kwa kosa au ombi kama lilelile la daudi. Huu ni wakati wa kutoa elimu hata kwa Rais wetu nae ajue namna suala Fei Toto linavyokuwa gumu kulitatua kwa wepesi kama anavyoomba.
Andaeni press ya kumsahiiisha Rais kuwa alikosea alichosema na sheria za FIFA aziingiliani na serikali...nipo apa apa JF nasubiria mrejesho[emoji16][emoji16]
 
Nimeona wapambe wa fei toto wakifuraishwa sana na kauli ya Rais Samia juu ya kuiomba Yanga kumalizana Fei.

Nimeona baadhi ya wasioelewa wala kutambua hili jambo lipo kiutaratibu zaidi na sio kihisia wala kimihemko.

Ndiyo maana hata Rais katumia kauli ya kuomba na sio Amri akijua fika kuwa masuala ya soka ayaingiliwi kivyovyote na mambo ya kisiasa.

Na fei mwenyewe ndiye mwenye uwezo wa kulihitimisha ili jambo kwa kufuata utaratibu, sheria na kanuni za kimkataba aliousaini na sio vinginevyo.

Asitegemee kwamba ataachwa tu bure aondoke eti kwa kuwa Rais kasema iyo kitu aitokaa itokee.

Bahati nzuri yeye mwenyewe keshatamka hana tatizo lolote na Yanga wala mkataba wake.

Basi yeye mwenyewe ndiye anayeonekana ana ukorofi achutame kwa kufata utaratibu, na utaratibu ni kwenda pale yanga wamtajie dau wanalotaka kwa timu yoyote inayomuitaji iweke mpunga mezani aondoke zake.

Jambo analolazimisha kwamba aachwe tu bure kama anavyotaka yeye na wapambe wake waliomrubuni ili wampate bwerere alitowezekana na atateseka sana.

Viongozi wa yanga wako very clear na Fei angekuwa smart kichwani hili jambo lingekuwa lilishakwisha kitambo sana, lakini jeuri yake na wapambe wake ndio vimemfikisha hapa.

Anajua keshayakoroga pakubwa ndiyo maana anaona ata aibu kwenda pale yanga anapakwepa kama ugonjwa wa ukoma, na awezi kulimaliza hili bila kuihusisha yanga ambao ndio mwajiri wake.

Kwa maana hiyo napenda kuwaeleza waliofurahia kauli ya Rais ya kwamba fei mwenyewe ndiye mwenye utashi wa kulimaliza hilo jambo lake kwa kufata utaratibu na sio yanga.

Yanga wameshampa option 3 za kufata ili aondoke ivyo ni juu yake kusuka ama kunyoa itifaki inazingatiwa.
Hata Rais wetu afahamishwe kuhusu utaratibu wa timu kumpata mchezaji mwenye mkataba, labda Kuna watu wamempotosha. Fei Toto akitoka Yanga haendi kuvua samaki baharini bali Kuna timu itamsajili na kucheza mpira. Hiyo "timu" inatakiwa ijitokeze hadharani Sasa ili iuziwe mchezaji mzuri Fei Toto ambae bado Yuko kwenye mkataba na Yanga. Ikumbukwe kuwa Yanga imemuongezea thamani Fei Toto ndio maana hata timu nyingine inamtaka. Wachezaji ni bidhaa kama bidhaa nyingine kwenye tasnia ya mpira.
 
Chagueni kati ya kupewa eneo la kuongezea kujenga uwanja jangwani au mwacheni fei aende zake msimbazi.
Kwa mustakabali wa Yanga, mpira na uongozi ulioko madarakani ni heri kulikosa eneo kuliko kuivuruga Yanga kwa kuweka presidency ya hovyo itakayoivuruga klabu. Ni heri Hersi ajiuzulu kuliko kuivuruga timu.
 
Ile ni order,kimsingi huelewi maana ya power ya rais,mtu mwenye nguvu kama Rais akikuomba kitu unakuwa hauko kwenye position ya kumkatalia kutokana na nguvu aliyo nayo na yeye analijua.Anaweza asiwe na mamlaka ya kuingilia maswala ya kimichezo ila anaweza kuumiza biashara za maboss zenu.
Hata Rais hakuagiza Yanga imwachie Fei Toto aondoke kiholela kwenda Azam au Simba bwerere. Kuna maagizo lazima atampa Fei Toto pia. Kwakuwa Rais wetu anafahamu mambo mengi sana. Inawezekana anamjua hata yule aliyempa Fei sh.100,000,000 za kununulia mkataba wake Yanga.
 
Kwa hiyo assuarance aliyowapa we unadhani watamkatalia hiyo simple request(order).Mbona unakuwa mjinga kiasi hiki,kwani una umri gani.
kwani ukiitwa hasani lazima uwe mpumbavu kiasi hiki et?
 
Muwe Mnasikiliza vizuri.

Rais ALISEMA NYIE mmeniomba na Mimi niwaonbe jambo Moja.

KLABU kubwa kama yanga kuwa na migogoro na wachezaji haipendezo.
Akaomba wamalizane na Toto.

Rais AMETOA Ombi.
Kutoa ombi si AMRI.

HAJA VUNJA KANUNI YOYOTE ILE.
Hakuna ombi pale. Ni lugha rahisi yenye amri ndio maana kaomba apewe mrejesho. Sijuona sababu ya raisi kuingilia hili suala
 
Ni njia rahisi tu ambayo Fei Toto anatakiwa aifate ili aachiwe huru aondoke, nayo ni kwenda yanga kutajiwa thamani yake ambayo kwa upembuzi wa haraka haraka si chini ya milioni 350, alipe aondoke kiroho safi vinginevyo hakuna huruma itakayomuokoa.

Sheria, kanuni na miongozo ya FIFA na CAF iko wazi na sio suala la kihisia au huruma ya mtu!

Eng. Hersi shikilia hapo hapo dawa ya kiburi ni jeuri!
 
Ni njia rahisi tu ambayo Fei Toto anatakiwa aifate ili aachiwe huru aondoke, nayo ni kwenda yanga kutajiwa thamani yake ambayo kwa upembuzi wa haraka haraka si chini ya milioni 350, alipe aondoke kiroho safi vinginevyo hakuna huruma itakayomuokoa.

Sheria, kanuni na miongozo ya FIFA na CAF iko wazi na sio suala la kihisia au huruma ya mtu!

Eng. Hersi shikilia hapo hapo dawa ya kiburi ni jeuri!
ngoja tuone
 
Back
Top Bottom