Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

Ombi la Rais kuhusu Fei Toto kwa Yanga ni agizo lakini lisivunje kanuni za FIFA

Mpira ni taasisi yenye kugha yake, taratibu zake na sheria zake. Mpira ndio taasisi inayoruhusu mtu kuuzwa kwa mkataba fulani wa muda fulani kwa kiasi fulani. Hii inafanyika kwakuwa:

1. kila timu inataka wachezaji wazuri kuliko timu pinzani.

2. Wachezaji wazuri sio wengi sana kwenye jamii.

3. Kila timu inataka kushinda kwa gharama yoyote, haipendi kufungwa.

4. Mpira ni pesa, hivyo wachezaji ni pesa (bidhaa) pia.

Sababu hizi ndio zilizosababisha mpira ukawa na taasisi zake maalumu chini ya FIFA ambazo haziingiliwi na serikali na wanasiasa kwenye uendeshaji wake.

Ombi la Rais lazima liheshimiwe na Yanga na lazima litekelezwe kwa kufuata lugha na kanuni za kimpira kwakuwa utekelezaji wake utaacha alama, njia na utaratibu ambao utatumika kutatua matatizo mengine yajayo nchini yatayofanana na hili la Fei Toto na Yanga.

Ukweli ni kwamba Fei Toto:
1. Anatakiwa na timu nyingine ambayo haitakii kujitokeza wazi. Hiki ni kinyume.

2. Fei Toto ana mkataba mbichi na Yanga.

3. Fei Toto anataka kuvunja mkataba kwa unilaterally, kinyume na taratibu za mpira.

Swali hapa ni njia itakayotumiwa na Yanga kumaliza mgogoro na katoto Fei Toto itatoa SoMo gani kwa wachezaji wengine Yanga na timu nyingine nchini?

Je, njia hiyo inaweza kutumiwa tena kumaliza mgogoro mwingine unaofanana na huo kama ukijitokeza?
Sina cha kuongezea nimefuta uzi wangu.
Nilitaka kuweka angalizo la kutumia vifungu na previous case studies
 
Ile ni order,kimsingi huelewi maana ya power ya rais,mtu mwenye nguvu kama Rais akikuomba kitu unakuwa hauko kwenye position ya kumkatalia kutokana na nguvu aliyo nayo na yeye analijua.Anaweza asiwe na mamlaka ya kuingilia maswala ya kimichezo ila anaweza kuumiza biashara za maboss zenu.
Kwani si wamesikia amesema" uzuri GSM hatumbinyi kwenye biashara zake"
 
We ndo huna akili kuwambia vile ni alert kuwa anao uwezo wa kukubinya any time na anao uwezo wa kutokukubinya any time .
Hapo ni fasihi tu .Sasa unawezaje kupinga ombi la rais na ukabak salama?
Jiongeze chakata akili Yako vzr .
Basi subilia embe chini ya mnazi kwa hizo akili zako, Usifikiri kila sehemu ombi la Rais linafanya kazi, ombi la Rais litafanyiwa kazi na fei mwenyewe kufata utaratibu na sio vinginevyo akatajiwe dau lake alipe aondoke zake
 
Jamaa anashindwa kuelewa utofauti wa Rais wa Nchi na hawa Marais wa mitaa kama madee au ney,hapo ni Yanga wanatakiwa kumuacha feisal tena kwa taarifa yako tu Leo wawakilishwi wa feisal wameitwa kukutana na Viongozi wa yanga,mpaka wiki ijayo feisal atakuwa mchezaji Huru tayari kuvaa jezi ya Mnyama mkali
Anadhani yule ni WCB president
 
Muwe Mnasikiliza vizuri.

Rais ALISEMA NYIE mmeniomba na Mimi niwaonbe jambo Moja.

KLABU kubwa kama yanga kuwa na migogoro na wachezaji haipendezo.
Akaomba wamalizane na Toto.

Rais AMETOA Ombi.
Kutoa ombi si AMRI.

HAJA VUNJA KANUNI YOYOTE ILE.
Mkatalieni muone mnavyorudi mtaani kuomba omba,Manake huyo boss wenu atahamisha Mali zake Zambia,kama kawaida ya ma boss zenu
 
Mpira ni taasisi yenye kugha yake, taratibu zake na sheria zake. Mpira ndio taasisi inayoruhusu mtu kuuzwa kwa mkataba fulani wa muda fulani kwa kiasi fulani. Hii inafanyika kwakuwa:

1. kila timu inataka wachezaji wazuri kuliko timu pinzani.

2. Wachezaji wazuri sio wengi sana kwenye jamii.

3. Kila timu inataka kushinda kwa gharama yoyote, haipendi kufungwa.

4. Mpira ni pesa, hivyo wachezaji ni pesa (bidhaa) pia.

Sababu hizi ndio zilizosababisha mpira ukawa na taasisi zake maalumu chini ya FIFA ambazo haziingiliwi na serikali na wanasiasa kwenye uendeshaji wake.

Ombi la Rais lazima liheshimiwe na Yanga na lazima litekelezwe kwa kufuata lugha na kanuni za kimpira kwakuwa utekelezaji wake utaacha alama, njia na utaratibu ambao utatumika kutatua matatizo mengine yajayo nchini yatayofanana na hili la Fei Toto na Yanga.

Ukweli ni kwamba Fei Toto:
1. Anatakiwa na timu nyingine ambayo haitakii kujitokeza wazi. Hiki ni kinyume.

2. Fei Toto ana mkataba mbichi na Yanga.

3. Fei Toto anataka kuvunja mkataba kwa unilaterally, kinyume na taratibu za mpira.

Swali hapa ni njia itakayotumiwa na Yanga kumaliza mgogoro na katoto Fei Toto itatoa SoMo gani kwa wachezaji wengine Yanga na timu nyingine nchini?

Je, njia hiyo inaweza kutumiwa tena kumaliza mgogoro mwingine unaofanana na huo kama ukijitokeza?
We Unafikiri alipokuwa anamwambia "Ghalib sitakubana, wewe fanya biashara" alikuwa anamaanisha nini??

Ghalib mwenyewe atachagua Kati ya Feitoto na "Kutokubanwa kibiashara" alafu ataamua....
 
Mikataba ya Ajira za mipira lazima ziwe na vipengele vya kumruhusu mchezaji kuondoka kama atahisi kudhalilika katika kazi yake.

Timu pia lazima iwe na vipengele vya kumwacha mchezaji kama atakiuka misingi ya timu.

Ajira za "huruhusiwi kutoka hadi mwisho wa mkataba wako" zimepitwa na wakati.
 
Chagueni kati ya kupewa eneo la kuongezea kujenga uwanja jangwani au mwacheni fei aende zake msimbazi.
🤣🤣Hawa maskin wanadhan wanaweza mdindia rais🤔 feitoto kashasema hataki kucheza yanga,na Kama bado mna mahaba naye huyo injinia wenu uchwara aondoke yanga,full stop🏌️🏌️🏌️🏌️🏌️
 
We Unafikiri alipokuwa anamwambia "Ghalib sitakubana, wewe fanya biashara" alikuwa anamaanisha nini??

Ghalib mwenyewe atachagua Kati ya Feitoto na "Kutokubanwa kibiashara" alafu ataamua....
Wanajifanya kubisha tu lakini ukweli remote control ya Hersi ni Ghalib na yeye hayupo tayari kuharibu mahusiano yake na mamlaka kwa kushupaza shingo.Kitendo cha Hersi kuinuka na kuinamisha kichwa wakati Rais anatoa 'ombi' lake inatosha kusema Yanga 'watatumia busara' na kulimaliza hili swala mapema na kupeleka mrejesho kwa Mama haraka iwezekanavyo.
 
Ukisikiliza vizuri maneno ya rais ni kama ametumia fasihi TU kufikisha amri yanga lazima wamuachie Feisal la sivyo GSM yatamkuta yaliyomkuta manji atahamia Zambia very soon Tena kasema hafurahishwi na Hilo na anataka mrejesho haraka
 
Linavunjaje kanuni za fifa? Yanga ndo mshika mkataba, sio fifa, akiamua kuachilia, hakuna shida.

Ni sawa na wewe ununue eneo utapeliwe, uamue kusamehe usiende mahakamani, hakuna sheria ta nchi imevunjwa
Tapeli anakuwa amevunja sheria. Au kwako sheria unaitazama kwa mtapeliwa pekee?
 
We Unafikiri alipokuwa anamwambia "Ghalib sitakubana, wewe fanya biashara" alikuwa anamaanisha nini??

Ghalib mwenyewe atachagua Kati ya Feitoto na "Kutokubanwa kibiashara" alafu ataamua....
Achana nao mkuu awajui kauli za Rais nguvu iliyonayo ile tayari ni order tusubirie uyo wa kukataa agizo la Rais..GSM ataambiwa chagua moja kubaki na fei toto au tuvuruge biashara zako
 
Kwa maana hiyo napenda kuwaeleza waliofurahia kauli ya Rais ya kwamba fei mwenyewe ndiye mwenye utashi wa kulimaliza hilo jambo lake kwa kufata utaratibu na sio yanga.
Kama mwenye kulimaliza tatizo hilo ni fei basi Samia hangetumia hela zake kuwaandalia msosi hao wenye njaa, kisha awasimange kwa jambo lisilowahusu 😂😂

Pole sana kwa uelewa haba ulionao kuhusu amri na mamlaka ya watawala.

Ni vyema ukitambua tu kuwa Samia keshawatukana viongozi wa Yanga wanaosumbuana na hako katoto 😂😂
 
Back
Top Bottom