Ombi: Serikali ituruhusu wananchi kutumia uwanja wa ndege Chato kuanikia mpunga, mihogo na mahindi wakati huu hakuna ndege

Ombi: Serikali ituruhusu wananchi kutumia uwanja wa ndege Chato kuanikia mpunga, mihogo na mahindi wakati huu hakuna ndege

Sasa ni msimu wa mavuno kwetu wakazi wa Chato, mahindi,mpunga na mihogo iko kwa wingi, naomba serikali ituruhusu kutumia uwanja was ndege kuanikia mpunga, mahindi na mihogo,inatoka vizuri bila mchanga.

Ni ombi letu sisi wanyonge na masikini.

Kidumu CCM
#matege
Inaitwa legacy ya kufa kufaana 😂😂😂
 
Subiri kidogo, kwani michembe siku hizi haianikwi juu ya paa? hukumsikia polepole akisema huo uwanja utatumika na ndege zinazohitaji kutua kwa dharura.....wasiwasi wangu unaweza usipate ndege yenye dharura kwa zaidi ya miaka 20, itabidi awepo mtu wa kufyeka nyasi na vichaka....
 
Sasa ni msimu wa mavuno kwetu wakazi wa Chato, mahindi,mpunga na mihogo iko kwa wingi, naomba serikali ituruhusu kutumia uwanja was ndege kuanikia mpunga, mahindi na mihogo,inatoka vizuri bila mchanga.

Ni ombi letu sisi wanyonge na masikini.

Kidumu CCM
#matege
Usisahau na dagaa tena kwenye lami zinakauka vizuri Sana bila mchanga.
Mbunge awasilishe hoja
 
Hilo wazo ni zuri litapunguza gharama za kuwalipa wafyeka nyasi
 
Ukiachana na hilo,naomba kujuzwa fursa za kiuchumi zilizoko hapo Chato.Hivi karibuni nitahamishiwa huko kikazi.

Huku niliko nilikuwa najishughulisha sana na kilimo cha karanga,mahindi na ufuta. Sasa huko Chato mmetaja panalimwa mahindi,mpunga na mihogo kwa wingi.Je,ni kata zipi zinafanya vyema kwenye kilimo cha mazao hayo? Na je,ardhi inaweza kuniruhusu kuendeleza kilimo cha karanga na ufuta huko?
Fursa tele we njoo sehemu ya kuanikia ipo
 
Naona historia inajirudia! Huenda wewe mleta mada ni kijana uliyezaliwa awamu ya Mkapa! Kama umekula chumvi kidogo, utajua kwamba historia hujirudia, ulipojengwa KIA (Kilimanjaro International Airport) ulipomalizika, ulikosa ndege maana EMBAKASI ya Nairobi ndiyo ilikuwa inajulikana/inavuma. Lawama nyingi sana na kashfa kemkem /kejeri zilitolewa kwamba serikali imekurupuka kujenga KIA! Enzi hizo watalii wa mbuga na vivutio vyetu walikuwa wanatua Nairobi/EMBAKASI! Safari zinapangwa kuanzia huko, Hata mlima Kilimanjaro ilikuwa unapandiwa upande wa Kenya!
To cut a long story short, sasa hivi KIA Inafanya vizuri Sana.
Kwa hiyo subiri kidogo Chato itatoboa,usikejeri
Ujamuelewa mtoa mada ule uwanja ukiachwa hivi hivi utaharibika kwa nyasi nk.Wananchi wakipewa kuanikia mazao watausafisha na watautunza hadi ikifika muda wa kutumika tena
 
Umenikumbusha miaka ya 2004, 2005, 2006 Maeneo ya Maseyu na vijiji fulani kabla ya kufika Morogoro ukitokea Dar walikuwa wanaanika mazao yao kandokando ya highway ya Dar - Moro (nje ya ule mchirizi wa njano)
Mpala leo hii kwa wakazi wa kuanzia nzega mpaka tinde nao hufanya hivyo hivyo 😀
 
Sasa ni msimu wa mavuno kwetu wakazi wa Chato, mahindi,mpunga na mihogo iko kwa wingi, naomba serikali ituruhusu kutumia uwanja was ndege kuanikia mpunga, mahindi na mihogo,inatoka vizuri bila mchanga.

Ni ombi letu sisi wanyonge na masikini.

Kidumu CCM
#matege
Senge unataka kuanika matako?laana ya mungu itakufikia ulipo pumbavu
 
Je kabla ya uwanja kujengwa hawakuwa na mahali pa kuanika mazao mpaka waende uwanja wa ndege?
walianika majumbani, ila tatizo mazao yalichanganyika na vijiwe/mchanga.Kuanika pale airport kero ya michanga kwenye mpunga ndio basi tena. Nadhani umeelewa.Mfano mzuri wa resource sharing- with proper schedulling mukulima anafaidi ,msafiri anafaidi.
 
Sasa ni msimu wa mavuno kwetu wakazi wa Chato, mahindi,mpunga na mihogo iko kwa wingi, naomba serikali ituruhusu kutumia uwanja was ndege kuanikia mpunga, mahindi na mihogo,inatoka vizuri bila mchanga.

Ni ombi letu sisi wanyonge na masikini.

Kidumu CCM
#matege
Siyo mbaya sirkali ingewatoza angalau 200/=@mkulima kwa siku itapata mapato kuliko kukaa bila kazi ya kutua ndege

Sent from my TECNO LA7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom