Orodha ya Mistari iliyo nichanganya kwenye Biblia takatifu kuhusu Ubatizo

Ahsante ndugu, na vipi kuhusu ubatizo wa MOTO
Tatizo unasoma Biblia kama unasoma gazeti. Sote tuliobatizwa kwa Yesu tumebatizwa kwa Roho Mtakatifu na Moto. Moto imetumika Kama lugha ya picha ikimaanisha mateso.
Ni wazi na hata Biblia imesema (sikumbuki vifungu maana huwa nasoma Biblia kuielewa na si kukariri) kuwa wote wampokeao Yesu Kristo hawana budi kuteseka kujaribiwa na ndio maana ya kubatizwa kwa Moto. Lakini tufurahi tupitiapo katika mateso na majaribu maana baada ya hayo yaja faraja. Ukristo sio mwepesi.
 
Mkuu huo ni ufahamu wako au ndio ufahamu wa Biblia? kwa hiyo wewe unaikosoa Biblia iliyo ainisha aina tatu za ubatizo bila ya kuunga unga maneno. Leta kifungu kinacho eleza hayo uliyo yanena hapa
 
Mkuu huo ni ufahamu wako au ndio ufahamu wa Biblia? kwa hiyo wewe unaikosoa Biblia iliyo ainisha aina tatu za ubatizo bila ya kuunga unga maneno. Leta kifungu kinacho eleza hayo uliyo yanena hapa
Ni wapi nilipoikosoa Biblia na uainishaji wa aina hizo za ubatizo ndugu? Hapo ninekuelewesha ufundi wa Biblia kutumia lugha ya picha kwani hilo ni jambo geni? Mbona ipo mifano mingi itumiayo aina ya lugha hiyo. Haya mfano ni the parable of the ten virgins na of talents pale Matthew 25.
 
Dhumuni la kubatizwa ni kuondolewa dhambi ya asili tuliyoirithi kutoka kwa Adamu na Hawa. Kwa mantiki hii ikiwa binadamu huzaliwa akiwa ni Muislamu basi uislamu ndio dhambi yenyewe ya asili. Basi nyinyi mwazaliwa dhambini na kufa dhambini. Poleni
🤣🤣🤣🙌🙌🙌
 
Huwa ni Shida mno kumuelewesha mtu aliekaririshwa!!
Ni vyema ukajikita kuchambua mambo yanayohusu Dini YAKO,ila uking'ang'ana na kuchambua Ukristo ambao sisi tunaongozwa na Roho😁hivyo tunaenenda kwa Imani,na ninyi mnaoongozwa na Sheria hautaambulia kitu.
 
Rejea kwenye hoja tafadhali, kunako ubatizo wa MOTO
 
Unataka uelezewaje??? C kuna wachangiaji wamekwisha kuielezea maana Yake?? Au unataka ujibiweje ndo uelewe???
Kama Vipi,njoo kesho kanisani Tukupe mafundisho kwa mapana zaidi
 
1. Kwanza kabisa napenda kukujuza Kuwa kauri ya kwamba Mtu huzaliwa mwisilamu akibatizwa ndiyo anakuwa mkiristo ni uongo. Lejea history ya uisilamu umeanza miaka 600 baada ya ukristo. Swali hapa kabla ya uisilamu kuja mtu alikuwa anazaliwa Kama Nani? Na kubatizwa anakuwa mkiristo.
2. Unachanganya Kati ya neno Moto na Roho Mtakifu. Maana yake Roho=Moto. Hivyo Roho Mtakifu pia huitwa upepo au moto. Rejea.
1.Waebrania 1:7
[7]Na kwa habari za malaika asema,
Afanyaye malaika wake kuwa pepo,
Na watumishi wake kuwa miali ya moto.
2.Matendo ya Mitume 2:1-3
[1]Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.
[2]Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.
[3]Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Hivyo Roho Mtakatimu ni upepo na ni moto.

Lakini nakukumbusha Kuwa Yesu akibatizwa kwa maji sema Kuwa ubatizo wake ulikuwa wa nguvu za Roho Mtakifu ambaye ni moto.
Rejea
1. Yohana 3:5-6
[5]Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
[6]Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
2.Yohana 3:5-6,22-23
[5]Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
[6]Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
[22]Baada ya hayo Yesu na wanafunzi wake walikwenda mpaka nchi ya Uyahudi; akashinda huko pamoja nao, akabatiza.
[23]Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji tele; na watu wakamwendea, wakabatizwa.

Yesu alibatiza kwa maji.

Pia mitume walibatiza kwa maji
Matendo ya Mitume 8:36-39
[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [
[37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
[38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
[39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
 
Nadhani mtoa mada unajichanganya mwenyewe na dhana ya uislamu, Islamu maana yake ni Amani.sasa kunatofauti kati ya dini ya Amani na AMANI yenyewe. Unaposema kila aliyezaliwa alikua muislam si kwamba alisilimiswa kuwa muumini wa imani ya kiislamu. Unapaswa utambue kwamba ubatizo ulikuja kama ishara ya kumtoa mtu katika matendo maovu na kumfanya upya. Hivyo ubatizo wa Yohana ulifanyika kama ondoleo la dhambi.Huo ulikua ni Toba waliofanya wayahudi. Yesu alibatiza watu katika( moto), pamoja na watu kubatizwa na Yohana bado hawakuziacha dhambi. Ndipo Yesu alipokuja kuziteketeza kazi za shetani kupitia jina lake leo tunaona makahaba wakiacha ukahaba na kuwa watu wema wanapompokea Yesu. Ubatizo wa Roho mtakatifu,ni uvuvio na ujazo wa nguvu za kimungu ndani ya mtu. Hivyo ubatizo wa maji pekee siyo njia ya kuishinda dhambi. Unatakiwa tamaa ya dhambi ichomwe na ujae nguvu za kimungu ndipo unaweza kushinda dhambi. Hoja ya kuzaliwa muislam ni dhaifu maana,huwezi kuwa muislam bila kuslimu. Story za kuokoteza eti kila mtu huzaliwa muislam maanayake makahaba,majambazi,mafitinishi,malevi,n.k yote ni maislum.Na maandiko yako wazi. Wagalatia 5:16....., Yohana 3:18. Watu wajinsi hiyo hawataingia mbinguni. Yohana hapo inafafanua unayemkataa Yesu tayari unatiketi ya jehanamu. Hivyo waislamu wote wanaenda jehanamu maana wanamkataa Yesu,nawewe umekiri kabisa watu wote wasiokoka ni waislamu. Chagua moja kwenda motoni au uokoke na ubatizwe uwe miongoni mwao watakao ingia mbinguni.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Powerfully💪💪
 
Wewe endelea tu kula nguruwe, biblia huiwezi.
 
Ungekuwa Mkristo unayehitaji msaada wa ufafanuzi wa kimaandiko ningekusaidia.
Wewe shika hiyo dini yako inayobariki uganga (maana masheikh wote Tz ni waganga kisirisiri) ila nguruwe haramu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…