Je ukiota unakula mahindi ya kukaangwa yatokayo kwenye ghorofa reefu kupita yote duniani kama mnara, ila anayeyateremsha haonekani zaidi ya kuona tu uwazi wa katikati ya hilo ghorofa afu unakinga kwa sufuria na kukaa chini unaanza kula?

Tafadhali msaada wa tafsiri ya hiyo ndoto Chifu.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Utapata neema

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Pole sana ndugu yangu, sasa sijui tuna wito wa kuingia jeshini ama ni vipi. Maana Da! Siyo mchezo
 
Nimeota nakutana na mwanamke mfupi sana kwenye ndoto nikawa namkemea, kwenye ndoto nilikuwa nawaza ni kibwengo.
 
Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umepatwa na jua, au mwezi umekua mwekundu, au mwezi umekua mweusi, basi Njozi hiyo inakujulisha kua:
"Hayo ni maharibiko katika maisha yako"
 
Je ukiota unakojoa?

Kuota unakojoa au kujisaidia mara kwa mara si vizuri.​

Kuota unakojoa si vizuri ila ni hatari sana kwa maisha yako, hii ni dalili za nguvu za giza ikiwemo mikosi na nuksi.

Ninakwambia jitahidi kufuatilia ndoto hizi ambazo ni mbaya kiafya katika ulimwengu wa kiroho:-

  • Kuota unakojoa, unajisaidia au uko sehemu chafu
  • Kuota unakula vitu au chakula mara kwa mara
  • Kuota maiti na watu waliokufa siku nyingi
  • Kuota vifo vya jamaa waliokaribu na wewe
  • Kuota nyoka na paka weusi mara kwa mara
  • Kuota unashambuliwa na watu
  • Kuota uko msituni na watu usio wajua
 
1. Kuota mwezi kunajulisha waziri, mfalme mkubwa, au sultani, nakama mwezi utakua umeambatana pembezoni mwake nyota basi ni kiongozi Na askari wake, Na inajulisha makazi ya kiongozi huyo Na maskani yake Na wakeze Na jirani zake.

2. Lakini huenda Njozi ya mwezi ikajulisha elimu, fiqih, na kila kinachojulisha uongofu Kwa mtu akaongoka kwacho katika magiza ya bara Na bahari.

3. Lakini pia mwezi unajulisha mtoto au mume au bwana.

4. Lakini pia nuru ya mwezi unajulisha uzuri Wa wanawake Na uzuri wa wanaume.

5. Lakini pia mwezi unajulisha kuongezewa kipato au kupungukiwa kipato, kwakua mwezi kawaida yake huongezeka ukubwa na unapungua ukubwa, kama jinsi zilivyo kazi za watu, huongezekewa Na kazi Na hupungukiwa kazi, huongezekewa na kipato Na hupungukiwa Na kipato.

6. Lakini pia kama utauona mwezi ukiwa kipande basi Njozi inakujulisha kupungukiwa umri na kukaribia ajali yako, kulingana Na masiku yaliyobaki ya mwezi huo kipande tokea ulipo uona.

7. Lakini pia utakapouona mwezi ukiwa umechomoza tena Kwa kujificha katika mawingu, basi utatoka maeneo yako na utasafiri.

8. Lakini pia utakapo uona mwezi ukiwa ndio umefikia siku ya mwisho wa mwezi, utasfiri safari ya mbali kutoka katika mji wako.

9. Lakini pia utakapouona mwezi upo nyumbani kwako, au chumbani kwako, au upo mkononi kwako, basi utaoa mke mzuri au utaolewa Na mume mzuri kulingana na ukubwa Wa mwanga wa mwezi Na kulingana Na ukubwa wa nuru ya mwezi.

10. Lakini pia ukiuona mwezi unazama mpaka ukapotea, basi jambo ambalo ulilokua ukilitafuta la Kheri au la shari limekwisha malizika.

11. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umekamilika duara lake Na mwezi huo upo katika anga la nyumbani kwake, basi Njozi inakujulisha kua:
"Hakika waziri Wa mfalme, au waziri Wa raisi atawanufaisha watu Wa sehemu hiyo"

12. Mtu anapolala kisha akaota kua, kautazama mwezi kisha akajiona sura yake katika mwezi, basi Njozi inakujulisha kua:
"Ajali yako imekaribia"

13. Mtu anapolala kisha akaota kua, Amening'inia mwezini, basi Njozi inamjulisha kua:
"Utapata Kheri nyingi kutoka Kwa sultani, raisi, waziri"

14. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi mwezi umefifia na akaona malaika akitoka mwezini, basi Njozi inakujulisha kua:
"Wachungwa wake watamuudhi Na watamkana"

15. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umegeuka na umekua jua, basi Njozi inakujulisha kua:
"Muotaji atapata Kheri nyingi, atapata utukufu mkubwa, atapata Mali nyingi, yote hayo kutoka umamani kwake au Kwa mwanamke wake"

16. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umejificha mawinguni, basi Njozi inakujulisha kua:
"Hayo ni maradhi yatakayompata waziri, na atapona baadae"

17. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi unakatiza mawinguni, basi Njozi inakujulisha kua:
"Utajiuzuru kazi ya uongozi"

18. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umemuongelesha, basi Njozi inakujulisha kua:
"Utapata cheo Na utasogezwa karibu Na waziri, au raisi"

19. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi upo nyumbani kwake, na huyo muotaji ni mwanamke mjamzito, basi Njozi inakujulisha kua:
"Utazaa mtoto wa kiume"

20. Mtu anapolala kisha akaota kua, analisujudia jua au anausujudia mwezi, basi Njozi inakujulisha kua:
"Unapandanisha madhambi juu ya madhambi, au unamtii mfalme au raisi au kiongozi katika batili"

21. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi na jua vinamsujudia, basi Njozi inakujulisha kua:
"Wazazi wako wawili wamekuridhia"

22. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi unang'ara vizuri, lakini yeye mwenyewe muotaji yupo gizani, basi Njozi inakujulisha kua:
"Nimaongezi yatakayoongelewa Kwa waziri au raisi au kiongozi yatakutia matatani"

23. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umepasuka vipande viwili, basi Njozi inakujulisha kua:
"Mfalme, au raisi, au waziri ataangamia"

24. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umegeuka muonekano wake ikawa unaonekana Kwa sura ya mtu unaemjua, basi Njozi inakujulisha kua:
"Waziri, au raisi, au kiongozi atajiuzulu nafasi yake"

25. Mtu anapolala kisha akaota kua, kauona mwezi nae akawa anafanya siri wenzie wasiuone mwezi, basi Njozi nakujulisha kua:
"Siri zako zitafichuka"

26. Mtu anapolala kisha akaota kua, mwezi umepatwa na jua, au mwezi umekua mwekundu, au mwezi umekua mweusi, basi Njozi hiyo inakujulisha kua:
"Hayo ni maharibiko katika maisha yako"
MENGINEYO:
 
Je ukiota upo kanisani au msikitini? Na pia ukiota unaongea na kiongozi wa nchi ?msaada
 
mkuu mimi nimeota nipo uwanja wa ndege napanda ndege nasafiri na sijui naelekea wapi lakini watu wananiaga kwa kufaraha na wanasherekea mimi kuondoka huku wakinipa baraka zote
 
Sigmund Freud laiti akiona uliyooandika atabaki mdomo wazi, quite typically magic pseudo article of no scientific value.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…