Tetesi: P Diddy ahusishwa na kifo cha Notorious B.I.G

Tetesi: P Diddy ahusishwa na kifo cha Notorious B.I.G

Aliyemshuti Pac pale new york studio ni member wa seti moja ya crips ya new york ila hajulikani na alipewa oder ya hit na OG a.k.a god father Kenneth Supreme Mcgriff wakawaibie wale wasanii kutoka west coast waliokuwepo pale new york kwenye ile studio siku ile.

Big alidandia tu upepo na kutoa""who shoot ya"" zikiwa ni hasira baada ya 2Pac kumlaumu wala hakuhusika na like tukio,ila story za kupotosha zimekua nyingi.Na aliyemuua 2Pac alikua Mac Andreson(Orlando) na washirika wake kutoka seti moja ya compton crips kwa ugomvi binafsi baada ya Pac na washikaji zake kumpiga pale Las Vegas wakimutuhumu kumuibia mmoja wa washikaji wa 2Pac anaitwa Daz dillinger kama sikosei jina lake cheni.Sema theory's nyingi hazisemagi ukweli.

Kumbuka 2Pac amekulia new york kabla ya kwenda vallejo California na yeye na Big na faith evans na keysha cole na ray ruv walikua marafiki toka high school,sema utafutaji katika maisha ndio uliowatenganisha.Kuna mahojiano Big anakiri kabisa kua 2pac alikua mshikaji wake sana sema tu ushindani wa mziki na gangs afliation,s ndio vilivyowatenganisha.
Kweli kabisa naikumbuka ile video wanachana wakiwa wamekaa kwenye meza eneo fulani hivi.
 
Ni vile tu TUPAC na BIG walikuwa watu maarufu sana lkn kimsingi Watu Weusi USA kuuana kwa kutumia Chuma ni sehemu ya Utamaduni wao!

Zipo theory zingine zinamtaja Snoopy km mtu alietia mkono wk ktk mauaji ya Pac. Binafsi nilimuona Pac akiwa kitandani Hospital, niliamini Mwamba hatoboi
Mwamba ni kweli ulimuona!? 1996 hiyo ujue!
 
Ya hilo la illuminati ni la kweli, 2pac alikataa kushikiwa akili na kundi hilo kama lilivyokuwa linawashikia kina Michael Jackson, Eddy Muphy nk.

Lakini sasa kwa pale Marekani hamna namna ambayo unaweza kulitanganisha kundi la illuminati na serikali ya Marekani.

Asilimia kubwa ya wanaoongoza Marekani kuanzia serikali, polisi, FBI, CIA, jeshi nk wote ni illuminati. Kwahiyo hao illuminati wanaweza kuwatumia FBI kufanya yao, maana ukigombana na polisi au FBI ni moja kwa moja umegombana na Illuminati. Pia ukigombana na hao illuminati ni moja kwa moja umegombana na serikali, polisi nk.

Kwahiyo yoyote anaweza kuhusika na mauaji hayo kwa kupitia kimvuli cha bifu la Big na 2pac au yule dogo Orlando.
Illuminati ni kitu cha ukweli!? Yaani kipo!? Au ni stori tu!?
 
Uvumi ni mwingi lakini mpaka recently imeshathibitishwa aliyemuua 2pac ni Orlando Anderson,yule jamaa aliyepigwa na 2pac mapema siku ile kwenye pambano la Tyson na Bruce Seldon.Na alikuwa mtu wake wa karibu.BIG alikufa sababu wapambe wa 2pac waliamini ye ndo alimuua.Kimsingi theories zipo nyingi Kuna hadi wanaoamini waliuawa na serikali ya marekani sababu ya bad influence Kwa vijana na makundi Yao ya east side na west side.Na Kuna wengine wanaoamini pia hakufa sababu hawakuona mazishi yake.

KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KUFA?
___________________

Watu wengi wamekuwa wakiniuliza maswali inbox, je, ni nini haswa kilisababisha ugomvi wa magwiji wawili duniani, Tupac Shakur na Notorious BIG kuchukiana mpaka kufa ?

Majibu ya swali hilo napenda niyaanzie mnamo February 13 mwaka 1993 wakati wamba hao wawili yaani Tupac na Biggie walipokutana kwa mara ya kwanza jijini Los Angeles.

Wakati huo Tupac tayari alikuwa ameshakuwa Staa wa filamu na muziki hivyo Biggie alitamani ukaribu naye kwa sababu naye alikuwa akiimba mtaani.

Kiroho safi, Tupac akamkaribisha Biggie nyumbani kwake na kisha wakala, kunywa na kuimba, huku wawili hao wakionekana kuzoeana kama walifahamiana muda mrefu.

Hata hivyo, Big alionekana kuhitaji msaada kwa Tupac wa kumshauri afanyaje ili naye aweze kuwa msanii mkubwa.? Tupac akamwambia Big "Usiwe na shaka, nitakusaidia".

Kwa mujibu wa Rapa wa kundi la Outlawz, E.D.I. Mean (Iddi Amini), anasema kuwa Tupac alitoa chupa ya Hennessy na kumpa Big kisha akawa anamsikiliza namna anavyorap.

Hata baada ya Tupac kutakiwa kutumbuiza kwenye tamasha la muziki huko Madison Square Garden, 'alimpa shavu' Big na kuweza kuimba naye pamoja.

Mara zote Tupac alitembea na Big kwenye Limousine, huku akimchukua kutumbuiza naye, japo Big alikuwa underground huku Tupac akiwa msanii mkubwa.

Wakiwa nyumbani, Tupac akamwambia Big, "Wacha leo nikupe siri hii.. kama unataka kupata pesa, hakikisha nyimbo zako huwaimbii Masela bali unawaimbia mademu".

Tupac akaendelea kumwambia Big kuwa, "Masela siku zote hupenda kuwanunulia mademu vitu wanavyotaka, hivyo mademu wakipenda kazi zako masela watawanunulia tu".

Big alikuwa makini sana kumsikiliza Tupac anachomshauri. Albamu yake ya kwanza ya 'Ready to Die' ikawa na kibao cha 'Big Poppa' kilichoonekana kupendwa mno na mademu.

Kabla ya Big kuachia albamu hiyo ya 'Ready to Die' alikuwa na wasiwasi wa kushindwa 'kutoboa' kutokana na record label iliyokuwa ikimsimamia ya Bad Boy Record kutokuwa maarufu.

Big akatoa pendekezo kwa Tupac kuomba kuwa meneja wake badala ya Sean Combs (Puff Daddy), lakini Tupac akamwambia "Hapana, fanya kazi na Puff Daddy, usimwache..ni mzuri...atakufanya kuwa Staa".

Big na Tupac wakaendelea kuwa washkaji wa karibu, walioshirikiana katika mambo mbalimbali ya muziki, wala haikuwepo dalili kama ipo siku watakuja kukorofishana.

Mapema mwaka 1994, Tupac akiwa jijini New York ku-shoot muvi ya 'Above the Rim' aliingia kwenye klabu moja na kumkuta jamaa flani akiwa kazungukwa na mademu huku meza yake ikichafuka kwa vinjwaji vya gharama.

Tupac akajikuta akishoboka kutaka kumjua jamaa huyo ni nani. Hakujua kumbe kijana huyo alikuwa mtu hatari sana pale Manhattan anayefahamika kwa jina la Jaques Agnant maarufu kama 'Haitian Jack'

Kando ya meza ya 'Haitian Jack' ilikuwepo chafu nyingine inayofahamika kwa jina la Jimmy Henchman. Big aliyekuwepo ndani ya klabu ile na Tupac, alishtushwa na Tupac kutaka ukaribu na watu wale.

Big akamwita Pac na kumwambia kuwa asithubutu kuhitaji ukaribu na Jack na Jimmy, lakini Tupac hakusikia na kuendeleza ukaribu na watu wale aliokutana nao klabu juu juu bila kuwajua vizuri.

Big alimtahadharisha Tupac kuhusu kutokuwa na ukaribu na Jack 'Haitian' na Jimmy, kwa sababu watu hao ni hatari na wangeweza kutumia fursa ya ukaribu wao na Tupac kujipatia pesa hata kwa njia za hatari.

Hata hiyo, siku iliyofuata Tupac na Jack wakakutana kwenye baa moja maarufu iitwayo Queens. Ndani ya baa hiyo walikuwapo wanamuziki mastaa Lady Madonna, Shaba Ranks na Buju Banton nao wakipata kilaji.

Itaendelea........[emoji3578]

#Balozi
 
KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KUFA.? (2)
___________________

(Inaendelea ilipoishia sehemu ya kwanza....)

Ushirika wa ghafla wa Tupac na Haitian Jack ulizidi kupamba moto licha ya Big kumsihi Tupac kukaa mbali na Jack. Wawili hao wakawa watu wa starehe na kujirusha viwanja mbalimbali.

Jambo hili lilionekana kumfadhaisha sana Big, kwanza ushauri wake ulipuuzwa, lakini pili alihisi huenda Tupac akamwambia Jack kuhusu Big alivyomsagia kunguni. Big akaamua kuwa kimya.

Haitian Jack alikuwa promota wa muziki, mtu mwenye pesa na mpenda sana matanuzi. 'Upedeshee' huo ulimpelekea kuwa karibu na mastaa wengi akiwemo hata bingwa wa zamani wa masumbwi, Mike Tyson.

Kwa kifupi, Tupac alijiona yupo kwenye mikono salama sana kwa kuwa karibu na mtu mwenye pesa anayeweza kufanya naye biashara na mambo yake yakamwendea.

Kumbe masikini upande wa pili wa Haitian Jack ambao Big anaujua vizuri Tupac hakuujua. Tatizo moja la Pac ni kuwa mtu wa kupuuzia sana ushauri pale akili yake inapomwaminisha kuwa yupo sahihi.

Mnamo mwezi November 1993, Tupac na Haitian Jack walikuwa kwenye Klabu moja iitwayo Nell's huko Manhattan. Ghafla macho ya Tupac yakajikuta yakiganda sehemu moja kumwangalia binti mmoja mrembo.

Binti huyo alionekana kumtazama kwa mahaba Tupac, huku Haitian Jack akimtazama Tupac jinsi anavyobabaika. Jack akamwita yule binti na kumkaribisha kwenye meza yao kisha kumtambulisha kwa Tupac.

Kilichoendelea ni Tupac kuanza kuchonga naye kiutu uzima, huku Jack akionekana kuwa bize kuendelea na starehe zake. Tupac akakolea na kuomba kucheza muziki na binti yule huku kila kitu kikiwekwa sawa.

Siku nne baadae, Tupac akamualika binti yule nyumbani kwake. Ikafahamika kuwa binti yule anaitwa Ayanna Jackson na umri wake ulikuwa miaka 19 tu.

Ayanna akawasili nyumbani kwa Tupac na kukuta kukiwa na wanaume kadhaa chumbani (tazama moja ya picha kwenye post hii), cha kushangaza Tupac akaendelea kuwa bize na mambo mengine.

Baada ya dakika chache, Ayanna akatoka nje na kuzungumza na simu, kisha akarejea ndani na kuketi na washkaji kama kawaida, ghafla Polisi wakavamia na kuwaweka wote chini ya ulinzi.

Msichana yule akaanza kuwaambia Polisi kuwa Tupac alimuita ndani mule ili ambake na wenzie watatu akiwemo Haitian Jack, na wote walimlazimisha kufanya ngono ya mdomo kitendo ambacho yeye alikigomea.

Tupac, Haitian Jack na Charles Fuller wakakamatwa na kufungukiwa mashtaka ya unyanyasaji wa kijinsia na walipopekuliwa wakakutwa na silaha wanazozimilki kinyume cha sheria. Suala hilo likaongezwa pia kwenye mashtaka yao.

Akiwa mahakamani, Tupac akajitetea kuwa alikuwa amelala chumba tofauti wakati madai ya Ayanna kubakwa yakitokea, lakini aliulizwa je, alifanya jitihada gani kuzuia tukio hilo kutokea wakati pale ni nyumbani kwake.?

Mawakili wa Ayanna wakaiambia mahakama kuwa inaonekana Tupac alipanga kula njama za kumchukua binti huyo na kumtoa kama zawadi kwa marafiki zake aliowajaza chumbani humo, japo Tupac aliendelea kukana.

Mahakama ikajiridhisha na kumshtaki Tupac kwa makosa ya unyanyasaji wa kijinsia, ulawiti na kumiliki silaha kinyume cha sheria, huku Jack akikiri makosa mawili na kulipa faini yeye na Fuller ili kuepuka kifungo.

Tupac alilalamika kuwa rafiki yake Haitian Jack alisuka dili la kesi hiyo na kumpanga Ayanna Jackson kucheza mchezo mzima ili kumpukutisha pesa zake. Wawili hao wakageuka maadui na kumwagana.

Japo kuwa Tupac alikuwa na pesa, akaunti yake ililazimika kupukutika mara kwa mara kutokana na kuwalipa wanasheria na mawakili kusimamia kesi zake zisizo na mwisho. Kwa kifupi mtindo wake wa maisha ulichangia mno kumfilisi.

Akauti ya Tupac ikapukutika haswa. Tupac alihitaji pesa ili kuweza kukabiliana na mwenendo wa kesi na masuala yake mengine muhimu. Rafiki wa karibu wa Haitian Jack, Jimmy 'Henchman' Rosemond akamfuata Pac na kumpa wazo.

Wazo lenyewe ni kumtaka Tupac ashiriki kurekodi track na msanii Little Shawn ambaye yeye (Henchman) ndiye meneja wake. Rapa huyo ni mtu wa karibu na Biggie na Puff Daddy ambao kipindi hicho wote walikuwa bado washkaji.

Tupac akaiona fursa ya kupata pesa muhimu anazozihitaji ili kutatua changamoto zake. Akaombwa alipwe Dola 7,000 ili kurekodi na Little Shawn track hiyo, Henchman akakubali kumpa pesa hizo Tupac ili mradi kazi ifanyike.

Mnamo November 30 ikafika. Siku ambayo ilikuwa ya miadi kwa Tupac na Little Shawn kurekodi pamoja. Tupac akawasili kwenye studio za Quad Record huko Times Square na hapo ndipo chanzo matatizo yote kilipotokea.

Akiwa na walinzi wake wawili, Tupac akakutana na vijana watatu waliovalia mavazi ya rangi za kijeshi (kombati) ambayo kwa wakati huo yalikuwa ni fasheni sana kwa vijana wa Brooklyn. Tupac akawasalimu kwa kujua ni wasanii walioenda pia kurekodi.

Wakiwa bado wapo eneo hilo, Tupac akakutana na Rapa wa Bad Boy, Lil Cease aliyemwambia kuwa Biggie yupo studio za ghorofani akirekodi, hivyo kumfanya Tupac kuamini kuwa vijana wale kama si wasanii, basi wapo pamoja na Biggie kumsubiria.

Hakika haikuwa hivyo..!
Wakati Tupac akielekea kwenye lift ili kuingia studio zilizopo ghorofani mwa jengo hilo, Vijana wale wakachomoa silaha na kumshambulia nazo Tupac.

Tupac akaanguka chini na kulala sakafuni baada ya risasi kumjeruhi maeneo kadhaa. Vijana wale wakamsogelea na kumpora vito vyote vya thamani alivyokuwa amevaa, huku Tupac akitulia tuli chini kuigiza kama amekufa.

Baada ya wakora wale kuondoka, Tupac akainuka sakafuni na kukimbilia kwenye lifti huku akivuja damu kutokana na majeraha kadhaa ya risasi aliyoyapata katika shambulio lile.

Akiwa amefika eneo hilo, milango ya lifti ikafunguka na ghafla Biggie, Puffy na Henchman wakashuka na kukutana uso kwa macho na Tupac akiwatazama kwa hasira huku akivuja damu.

Itaendelea.........[emoji3578]

#Balozi
 
KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KIFO ? (3)
__________________

(Inaendelea ilipoishia..)

Macho ya Tupac yalikuwa bado yakiendelea kuwatazama Biggie, Puff na Henchman kwa hasira. Hisia za Tupac zilimpa mtazamo kuwa tukio lile lilipangwa na washirika hao ili kumuua.

Biggie, Puff na Henchman walikuwa bado wamepigwa butwaa. Tupac alisema "Niliwatazama machoni wote watatu, walionekana kujua mpango mzima wa tukio..macho huwa hayafichi kitu".

Akihojiwa na gazeti la Vibe mwaka 2005, Henchman alisema "Hakuna aliyepanga kumwibia (Tupac) vito vyake wala kumuua kwenye tukio lile, kilichofanyika vijana walikuja kumfunza adabu tu".

Kauli hii ya Henchman ambaye ndiye aliyeratibu Tupac kurekodi na Shawn kwa malipo ya Dola 7,000 inaonesha wazi kuwa alilifurahia tukio lile na si dhambi ikisemwa kuwa lilipangwa kusudi kumhujumu Tupac.

Wakati tukio hilo liki-trend kwenye vyombo vya habari. Puff na Biggie walikana mara zote kuhusika na njama za kumshambulia Tupac, hata Haitian Jack alipohojiwa naye alikana, japo baada ya hukumu alirudishwa nchini kwao Haiti.

December 1, 1994 Tupac akafikishwa mahakamani akiwa kwenye kiti cha magurudumu (wheelchair) ili kuendelea na kesi yake. Mahakama ikamkuta na hatia dhidi ya makosa ya unyanyasaji kingono kwa binti Ayanna Jackson.

Hukumu dhidi yake ikasomwa. Mashtaka ya kulawiti na kumiliki silaha yakafutwa kwenye hukumu, lakini lile la unyanyasaji kingono likaachwa, akahukumiwa mwaka mmoja na nusu jela.

Rufaa dhidi ya hukumu yake iliachwa wazi kwa sharti la kutakiwa kulipa Dola milioni 3. Tupac hakuwa na pesa kabisa, kwa sababu hata dili lake la kurekodi na Shawn kwa malipo ya Dola 7,000 liligonga mwamba.

Hatimaye Tupac akaanza maisha yake mapya kwenye gereza lenye ulinzi mkali la Clinton Correction Facility lililopo jijini New York, huku akiacha nyimbo kadhaa studio zilizokuwa tayari kutoka.

Akiwa jela, huku nyuma hasimu wake anayemtuhumu kupanga njama za kumuua (Biggie) akatoa track aliyoiita "Who Shot Ya". Track hiyo ilionekana kuwa dongo kwa Tupac, taarifa zilimfikia Tupac na alikasirika sana.

Tupac alifikiria namna alivyomsaidia Biggie since day one wanakutana mpaka kupelekea kuanza kupata pesa na umaarufu na akifikiria namna zilivyosukwa njama ili kumuua hakuona lilipo kosa lake.

Hata baada ya Biggie na Puff kuhojiwa kuhusu Track hiyo ya "Who Shot Ya" inayoonekana kumshambulia Tupac ambaye yupo gerezani, wote walikanusha kuhusu wimbo huo kuwa dongo kwa Tupac.

Biggie alieleza kuwa mashairi ya wimbo huo aliyatunga muda mrefu kabla hata ya tukio la Tupac kupigwa risasi, huku akisisitiza kuwa yeye na Pac bado ni washkaji na hakuna tatizo lolote juu ya urafiki wao.

Hasira za Tupac juu ya wimbo wa Biggie "Who Shot Ya" zinadhihirika kupitia Track yake "Hit Em Up". Kwenye track hiyo Tupac aliyoshirikiana na Outlawz hakuna ambacho Biggie na Bad Boy nzima walibakishwa.

Akiwa gerezani, Tupac alikuwa akibiliwa na ukata mkubwa. Pesa zilimuishia kwa sababu ya kesi zake na hata ikapelekea nyumba yake kuwa hatarini kuuzwa ili kufidia baadhi ya mambo.

Wazo la uhitaji pesa likamuumiza sana kichwa na hatimaye akapata suluhisho la kuweza kumaliza changamoto hiyo. Tupac akakumbuka kuwa lipo jitu moja la miraba minne linaloweza kumaliza matatizo yake.

Marion 'Suge' Knight. Mkurugenzi wa Death Row Records likawa ndiyo chaguo la Tupac kumweleza yote yanayomsibu. Suge akapokea ujumbe kutoka gerezani kupitia kwa Keisha Morris.

Ndani ya ujumbe huo, Tupac alimwomba 'Suge' amsaidie kiasi cha Dola 15,000 kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali zinazomkabili. Knight hakuwa na hiyana, alimtupia pesa hizo Tupac kwa kuziweza kwenye vitabu.

Tupac hakuamini..alimshukuru sana Knight kwa msaada wake, lakini akampa Ofa nyingine ya kumuomba wakutane kwenye chumba maalum kwenye gereza la Dannemora jijini New York kwa ajili ya mazungumzo zaidi.

Mazungumzo ya Tupac na Knight yakafanikiwa. Knight akakubali kulibeba jukumu la kumsaidia Tupac kumaliza changamoto zake. Wakili wa Death Row, David Kenner akaanza kufuatilia rufaa za Tupac kuhakikisha anatoka kifungoni.

Ni kama kila mtu aliiona fursa iliyo kwa mwenziye na kuitumia. Tupac akamwambia Knight inakuwa vyema endapo watafanya kazi pamoja kupitia lebo yake ya Death Row Records. Knight naye hakuiacha fursa hiyo kumpita.

Akiwa gerezani, Albamu yake ya tatu iitwayo "Me Against The World" iliyokuwa chini ya kampuni ya Interscope ikatolewa tarehe 14 March mwaka 1995. Albamu hiyo ilipata mafanikio makubwa kitu ambacho kilimshawishi sana Knight kuhitaji kufanya kazi na Pac.

Baada ya kumaliza mazungumzo na Tupac gerezani, Knight akaelekea kwenye ukumbi wa Madison Square Garden kuhudhuria Tuzo za kila mwaka za jarida la Hip Hop la The Source. Ikumbukwe kuwa Knight Biggie na Puff hawakuwa na uadui wowote hata kidogo.

Lakini akirejea makubaliano yake na Tupac kuhusu kumsaini kwenye lebo yake ya Death Row aliona bora afanye anachotaka Tupac ili mradi suala lao lina maslahi mapana kwao wote. Pac alimwambia Knight kuwa Bad Boy walipanga kumuua hivyo hasira zake atazimalizia akiwa Death Row.

Ilikuwa ni vigumu kufanya kazi na msanii anayeishambulia Bad Boy nawe bosi wake ukaendelea kuwa peace na wanaoshambuliwa. Huu ni unafiki ambao Knight aliamua kuachana nao kwa kuamua kuuingia mzozo binafsi ambao kimsingi ulikuwa wa Pac na Bad Boy.

Itaendelea......[emoji3578]

#Balozi
 
Hawa madogo wanahadithia hapa ukute hata mmoja hawakuwepo dunian siku hawa jamaa wanakufa, story wamekuta hapa dunian ila kama walikuwepo kwenye tukio
Binafsi Naamini wengi wanaomzungumzia 2Pac na Biggie hapa walikuwa mashabiki wao kabla hata hawajauawa.
 
Vifo vyao vilipangwa ndomana vilifanana.
2pac gari yao ilipofika kwenye traffic light mataa ya kuruhusu upande wao kwenda yakafunga hivyo ikawalazimu kusimama. Ghafla wakatokea mabinti pembeni ya barabara wakaanza kuita 2pac.. 2pac.. 2pac... basi 2pac ile kushusha kioo awapungie mkono hapo hapo akaanza kushambuliwa na gari ya majamaa waliokuwa ubavuni kwao.

Big nae gari yao ilipofika kwenye traffic light mataa ya kuruhusu upande wao kwenda yakafunga hivyo ikawalazimu kusimama. Ghafla pia wakatokea mabinti pembeni ya barabara wakaanza kuita Big.. Big.. Big.. basi ile Big kushusha kioo awapungie mkono hapo hapo na yeye akaanza kushambuliwa na gari iliyokuwa pembeni yao hadi kusababisha umauti wake.
Ila duuuh,we umeipata wapi hii?
 
KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KIFO ? (3)
__________________

(Inaendelea ilipoishia..)

Macho ya Tupac yalikuwa bado yakiendelea kuwatazama Biggie, Puff na Henchman kwa hasira. Hisia za Tupac zilimpa mtazamo kuwa tukio lile lilipangwa na washirika hao ili kumuua.

Biggie, Puff na Henchman walikuwa bado wamepigwa butwaa. Tupac alisema "Niliwatazama machoni wote watatu, walionekana kujua mpango mzima wa tukio..macho huwa hayafichi kitu".

Akihojiwa na gazeti la Vibe mwaka 2005, Henchman alisema "Hakuna aliyepanga kumwibia (Tupac) vito vyake wala kumuua kwenye tukio lile, kilichofanyika vijana walikuja kumfunza adabu tu".

Kauli hii ya Henchman ambaye ndiye aliyeratibu Tupac kurekodi na Shawn kwa malipo ya Dola 7,000 inaonesha wazi kuwa alilifurahia tukio lile na si dhambi ikisemwa kuwa lilipangwa kusudi kumhujumu Tupac.

Wakati tukio hilo liki-trend kwenye vyombo vya habari. Puff na Biggie walikana mara zote kuhusika na njama za kumshambulia Tupac, hata Haitian Jack alipohojiwa naye alikana, japo baada ya hukumu alirudishwa nchini kwao Haiti.

December 1, 1994 Tupac akafikishwa mahakamani akiwa kwenye kiti cha magurudumu (wheelchair) ili kuendelea na kesi yake. Mahakama ikamkuta na hatia dhidi ya makosa ya unyanyasaji kingono kwa binti Ayanna Jackson.

Hukumu dhidi yake ikasomwa. Mashtaka ya kulawiti na kumiliki silaha yakafutwa kwenye hukumu, lakini lile la unyanyasaji kingono likaachwa, akahukumiwa mwaka mmoja na nusu jela.

Rufaa dhidi ya hukumu yake iliachwa wazi kwa sharti la kutakiwa kulipa Dola milioni 3. Tupac hakuwa na pesa kabisa, kwa sababu hata dili lake la kurekodi na Shawn kwa malipo ya Dola 7,000 liligonga mwamba.

Hatimaye Tupac akaanza maisha yake mapya kwenye gereza lenye ulinzi mkali la Clinton Correction Facility lililopo jijini New York, huku akiacha nyimbo kadhaa studio zilizokuwa tayari kutoka.

Akiwa jela, huku nyuma hasimu wake anayemtuhumu kupanga njama za kumuua (Biggie) akatoa track aliyoiita "Who Shot Ya". Track hiyo ilionekana kuwa dongo kwa Tupac, taarifa zilimfikia Tupac na alikasirika sana.

Tupac alifikiria namna alivyomsaidia Biggie since day one wanakutana mpaka kupelekea kuanza kupata pesa na umaarufu na akifikiria namna zilivyosukwa njama ili kumuua hakuona lilipo kosa lake.

Hata baada ya Biggie na Puff kuhojiwa kuhusu Track hiyo ya "Who Shot Ya" inayoonekana kumshambulia Tupac ambaye yupo gerezani, wote walikanusha kuhusu wimbo huo kuwa dongo kwa Tupac.

Biggie alieleza kuwa mashairi ya wimbo huo aliyatunga muda mrefu kabla hata ya tukio la Tupac kupigwa risasi, huku akisisitiza kuwa yeye na Pac bado ni washkaji na hakuna tatizo lolote juu ya urafiki wao.

Hasira za Tupac juu ya wimbo wa Biggie "Who Shot Ya" zinadhihirika kupitia Track yake "Hit Em Up". Kwenye track hiyo Tupac aliyoshirikiana na Outlawz hakuna ambacho Biggie na Bad Boy nzima walibakishwa.

Akiwa gerezani, Tupac alikuwa akibiliwa na ukata mkubwa. Pesa zilimuishia kwa sababu ya kesi zake na hata ikapelekea nyumba yake kuwa hatarini kuuzwa ili kufidia baadhi ya mambo.

Wazo la uhitaji pesa likamuumiza sana kichwa na hatimaye akapata suluhisho la kuweza kumaliza changamoto hiyo. Tupac akakumbuka kuwa lipo jitu moja la miraba minne linaloweza kumaliza matatizo yake.

Marion 'Suge' Knight. Mkurugenzi wa Death Row Records likawa ndiyo chaguo la Tupac kumweleza yote yanayomsibu. Suge akapokea ujumbe kutoka gerezani kupitia kwa Keisha Morris.

Ndani ya ujumbe huo, Tupac alimwomba 'Suge' amsaidie kiasi cha Dola 15,000 kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali zinazomkabili. Knight hakuwa na hiyana, alimtupia pesa hizo Tupac kwa kuziweza kwenye vitabu.

Tupac hakuamini..alimshukuru sana Knight kwa msaada wake, lakini akampa Ofa nyingine ya kumuomba wakutane kwenye chumba maalum kwenye gereza la Dannemora jijini New York kwa ajili ya mazungumzo zaidi.

Mazungumzo ya Tupac na Knight yakafanikiwa. Knight akakubali kulibeba jukumu la kumsaidia Tupac kumaliza changamoto zake. Wakili wa Death Row, David Kenner akaanza kufuatilia rufaa za Tupac kuhakikisha anatoka kifungoni.

Ni kama kila mtu aliiona fursa iliyo kwa mwenziye na kuitumia. Tupac akamwambia Knight inakuwa vyema endapo watafanya kazi pamoja kupitia lebo yake ya Death Row Records. Knight naye hakuiacha fursa hiyo kumpita.

Akiwa gerezani, Albamu yake ya tatu iitwayo "Me Against The World" iliyokuwa chini ya kampuni ya Interscope ikatolewa tarehe 14 March mwaka 1995. Albamu hiyo ilipata mafanikio makubwa kitu ambacho kilimshawishi sana Knight kuhitaji kufanya kazi na Pac.

Baada ya kumaliza mazungumzo na Tupac gerezani, Knight akaelekea kwenye ukumbi wa Madison Square Garden kuhudhuria Tuzo za kila mwaka za jarida la Hip Hop la The Source. Ikumbukwe kuwa Knight Biggie na Puff hawakuwa na uadui wowote hata kidogo.

Lakini akirejea makubaliano yake na Tupac kuhusu kumsaini kwenye lebo yake ya Death Row aliona bora afanye anachotaka Tupac ili mradi suala lao lina maslahi mapana kwao wote. Pac alimwambia Knight kuwa Bad Boy walipanga kumuua hivyo hasira zake atazimalizia akiwa Death Row.

Ilikuwa ni vigumu kufanya kazi na msanii anayeishambulia Bad Boy nawe bosi wake ukaendelea kuwa peace na wanaoshambuliwa. Huu ni unafiki ambao Knight aliamua kuachana nao kwa kuamua kuuingia mzozo binafsi ambao kimsingi ulikuwa wa Pac na Bad Boy.

Itaendelea......[emoji3578]

#Balozi
Madini madini madiiini . safi sana.
 
*uck Mobb Deep, *uck Biggie
uck Bad Boy as a staff, record label and as a mother*ucking crew
And if you want to be down with Bad Boy, then *uck you too
Chino XL, *uck you too
All you mother*uckers, *uck you too..Hapo imetukanwa label ya bad boys na wafanyakazi wake wote hadi wafagiaji,Mobb Deep nao wakaingizwa humohumo na yeyote anayejihusisha au kuihusudu Bad Boy nae kaingizwa ilikuwa hatar sana hii😀
Huyo mwamba alikuwa anawachana kinomanoma kummqe,he feared no one
 
KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KIFO ? (3)
__________________

(Inaendelea ilipoishia..)

Macho ya Tupac yalikuwa bado yakiendelea kuwatazama Biggie, Puff na Henchman kwa hasira. Hisia za Tupac zilimpa mtazamo kuwa tukio lile lilipangwa na washirika hao ili kumuua.

Biggie, Puff na Henchman walikuwa bado wamepigwa butwaa. Tupac alisema "Niliwatazama machoni wote watatu, walionekana kujua mpango mzima wa tukio..macho huwa hayafichi kitu".

Akihojiwa na gazeti la Vibe mwaka 2005, Henchman alisema "Hakuna aliyepanga kumwibia (Tupac) vito vyake wala kumuua kwenye tukio lile, kilichofanyika vijana walikuja kumfunza adabu tu".

Kauli hii ya Henchman ambaye ndiye aliyeratibu Tupac kurekodi na Shawn kwa malipo ya Dola 7,000 inaonesha wazi kuwa alilifurahia tukio lile na si dhambi ikisemwa kuwa lilipangwa kusudi kumhujumu Tupac.

Wakati tukio hilo liki-trend kwenye vyombo vya habari. Puff na Biggie walikana mara zote kuhusika na njama za kumshambulia Tupac, hata Haitian Jack alipohojiwa naye alikana, japo baada ya hukumu alirudishwa nchini kwao Haiti.

December 1, 1994 Tupac akafikishwa mahakamani akiwa kwenye kiti cha magurudumu (wheelchair) ili kuendelea na kesi yake. Mahakama ikamkuta na hatia dhidi ya makosa ya unyanyasaji kingono kwa binti Ayanna Jackson.

Hukumu dhidi yake ikasomwa. Mashtaka ya kulawiti na kumiliki silaha yakafutwa kwenye hukumu, lakini lile la unyanyasaji kingono likaachwa, akahukumiwa mwaka mmoja na nusu jela.

Rufaa dhidi ya hukumu yake iliachwa wazi kwa sharti la kutakiwa kulipa Dola milioni 3. Tupac hakuwa na pesa kabisa, kwa sababu hata dili lake la kurekodi na Shawn kwa malipo ya Dola 7,000 liligonga mwamba.

Hatimaye Tupac akaanza maisha yake mapya kwenye gereza lenye ulinzi mkali la Clinton Correction Facility lililopo jijini New York, huku akiacha nyimbo kadhaa studio zilizokuwa tayari kutoka.

Akiwa jela, huku nyuma hasimu wake anayemtuhumu kupanga njama za kumuua (Biggie) akatoa track aliyoiita "Who Shot Ya". Track hiyo ilionekana kuwa dongo kwa Tupac, taarifa zilimfikia Tupac na alikasirika sana.

Tupac alifikiria namna alivyomsaidia Biggie since day one wanakutana mpaka kupelekea kuanza kupata pesa na umaarufu na akifikiria namna zilivyosukwa njama ili kumuua hakuona lilipo kosa lake.

Hata baada ya Biggie na Puff kuhojiwa kuhusu Track hiyo ya "Who Shot Ya" inayoonekana kumshambulia Tupac ambaye yupo gerezani, wote walikanusha kuhusu wimbo huo kuwa dongo kwa Tupac.

Biggie alieleza kuwa mashairi ya wimbo huo aliyatunga muda mrefu kabla hata ya tukio la Tupac kupigwa risasi, huku akisisitiza kuwa yeye na Pac bado ni washkaji na hakuna tatizo lolote juu ya urafiki wao.

Hasira za Tupac juu ya wimbo wa Biggie "Who Shot Ya" zinadhihirika kupitia Track yake "Hit Em Up". Kwenye track hiyo Tupac aliyoshirikiana na Outlawz hakuna ambacho Biggie na Bad Boy nzima walibakishwa.

Akiwa gerezani, Tupac alikuwa akibiliwa na ukata mkubwa. Pesa zilimuishia kwa sababu ya kesi zake na hata ikapelekea nyumba yake kuwa hatarini kuuzwa ili kufidia baadhi ya mambo.

Wazo la uhitaji pesa likamuumiza sana kichwa na hatimaye akapata suluhisho la kuweza kumaliza changamoto hiyo. Tupac akakumbuka kuwa lipo jitu moja la miraba minne linaloweza kumaliza matatizo yake.

Marion 'Suge' Knight. Mkurugenzi wa Death Row Records likawa ndiyo chaguo la Tupac kumweleza yote yanayomsibu. Suge akapokea ujumbe kutoka gerezani kupitia kwa Keisha Morris.

Ndani ya ujumbe huo, Tupac alimwomba 'Suge' amsaidie kiasi cha Dola 15,000 kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali zinazomkabili. Knight hakuwa na hiyana, alimtupia pesa hizo Tupac kwa kuziweza kwenye vitabu.

Tupac hakuamini..alimshukuru sana Knight kwa msaada wake, lakini akampa Ofa nyingine ya kumuomba wakutane kwenye chumba maalum kwenye gereza la Dannemora jijini New York kwa ajili ya mazungumzo zaidi.

Mazungumzo ya Tupac na Knight yakafanikiwa. Knight akakubali kulibeba jukumu la kumsaidia Tupac kumaliza changamoto zake. Wakili wa Death Row, David Kenner akaanza kufuatilia rufaa za Tupac kuhakikisha anatoka kifungoni.

Ni kama kila mtu aliiona fursa iliyo kwa mwenziye na kuitumia. Tupac akamwambia Knight inakuwa vyema endapo watafanya kazi pamoja kupitia lebo yake ya Death Row Records. Knight naye hakuiacha fursa hiyo kumpita.

Akiwa gerezani, Albamu yake ya tatu iitwayo "Me Against The World" iliyokuwa chini ya kampuni ya Interscope ikatolewa tarehe 14 March mwaka 1995. Albamu hiyo ilipata mafanikio makubwa kitu ambacho kilimshawishi sana Knight kuhitaji kufanya kazi na Pac.

Baada ya kumaliza mazungumzo na Tupac gerezani, Knight akaelekea kwenye ukumbi wa Madison Square Garden kuhudhuria Tuzo za kila mwaka za jarida la Hip Hop la The Source. Ikumbukwe kuwa Knight Biggie na Puff hawakuwa na uadui wowote hata kidogo.

Lakini akirejea makubaliano yake na Tupac kuhusu kumsaini kwenye lebo yake ya Death Row aliona bora afanye anachotaka Tupac ili mradi suala lao lina maslahi mapana kwao wote. Pac alimwambia Knight kuwa Bad Boy walipanga kumuua hivyo hasira zake atazimalizia akiwa Death Row.

Ilikuwa ni vigumu kufanya kazi na msanii anayeishambulia Bad Boy nawe bosi wake ukaendelea kuwa peace na wanaoshambuliwa. Huu ni unafiki ambao Knight aliamua kuachana nao kwa kuamua kuuingia mzozo binafsi ambao kimsingi ulikuwa wa Pac na Bad Boy.

Itaendelea......[emoji3578]

#Balozi
Angalau wewe umeandika vinavyoeleweka. Wengine walikuwa wanaposti longo longo tu, mara illuminati mara sijui FBI ...
 
Tupac alikuwa na hasira baada ya kutokea ugomvi baina yake na BIG kuhusu utunzi wa wimbo fulani, alikwenda kwenye vyombo vya habari na kuanza kujisifu kuwa amelala na Faith Evans mke wa BIG.
Wimbo unaitwa Get Money aliiba beat na Melody, huu wimbo pac alitaka kuutoa baada ya kutoka jela Ila kabla wimbo haujatoka Faith alivujisha kwa BIG na beat na Melody ilichukuliwa na Faith Evans ambae alikua anafanya ngoma na 2pac, BIG alipochukua ile Melody na beat akafanya na kundi lake jipya akaliita Junior M.A.F.I.A Ina maana yake na baada ya wimbo kutoka pac akawa amechukia maana Melody na beat ni ya kwake yeye kwa hio BIG aliiba ukiacha hivyo pac alikua na hasra alipopigwa risasi BIG alitoa wimbo unaitwa Who Shut You? Ikamuuma

Sasa baada ya BIG na Junior Mafia kutoa Get Money audio na video, pac alilalamika kua BiG kamkosea akasema isiwe kesi akaenda akafuta lyrics zoote za ile beat akatengeneza Diss Track pamoja na Crew yake yaan aliunda kundi na yeye akaliita Outlaws ambapo pindi inaundwa ilitambulika km Outlaw Immortalz yeye akiwa km Makaveli ambapo alikua anamhusudu mwanafalosofia Niccola Machiavelli akajiita pia Killuminati The Don (jina la album yake) na wengine ambao ni kundi aliloliunda wakiwa ni madikteta wa dunia, Big Marik aliejiita E.d.I Mean, na wengineo km Kastro alikua anajiita K-Dog huyu ni Fidel Castro wa Cuba, Yaki Kadafi huyu ni Gadafi wa Libya, Mutah ambae baadae alibadiri kua Napoleon, pia walitambulika km Thoro Headz and Young Thugz

Baada ya kuunda hilo kundi pac akaingia booth kutengeneza wimbo ambao hio Crew yake mwanzo hawakujua wimbo ni wa nini ndio akawaambia ni Diss Track na inaenda kumpaka Matope BiG na wale wote walio na ubia na BiG akiwemo P Diddy na Bad Boy Crew nzima pamoja na Junior Mafia

Wakatengeneza Diss Track inaitwa Hit 'Em Up hii ndio Diss Track kali ya muda wote, unaambiwa wakati Pac anaingiza vocal mic zilikua zinazima kila wakati na mmoja wa wale waliounda group ya Outlawz aliwahi kuhojiwa akasema pamoja na mic kuzima zima Pac hakuacha kurekodi na ilikua lazima arekodi hakuna wa kumzia hata producer wa ngoma nae anasema alipokua anatengeneza hio ngoma kulikua na changamoto km hizo Ila Pac hakutaka kurudi nyuma

Hatimae ngoma ikawa tayari wakatafuta watu wa Video wakashoot video baada ya hapo ikatoka kitu video & audio at the same time, na katika kava ya audio ya kwanza kabisa kwenye Tape waliweka picha ya BIG akiwa ni nguruwe kaveshwa kichwa Cha BiG na P Diddy akawekwa nyoka kaveshwa kichwa Cha P Diddy ngoma ikaachiwa

Baada ya kifo cha BiG Faith Evans aliewahi kua mke wa BiG alitoa wimbo wa kumbukumbu kwa BIG akiwa na P Diddy unaitwa I Will Be Missing You

Walale wanapostahiri uko walipo

R.I.P
 
Back
Top Bottom