Tetesi: P Diddy ahusishwa na kifo cha Notorious B.I.G

Tetesi: P Diddy ahusishwa na kifo cha Notorious B.I.G

Wimbo unaitwa Get Money aliiba beat na Melody, huu wimbo pac alitaka kuutoa baada ya kutoka jela Ila kabla wimbo haujatoka Faith alivujisha kwa BIG na beat na Melody ilichukuliwa na Faith Evans ambae alikua anafanya ngoma na 2pac, BIG alipochukua ile Melody na beat akafanya na kundi lake jipya akaliita Junior M.A.F.I.A Ina maana yake na baada ya wimbo kutoka pac akawa amechukia maana Melody na beat ni ya kwake yeye kwa hio BIG aliiba ukiacha hivyo pac alikua na hasra alipopigwa risasi BIG alitoa wimbo unaitwa Who Shut You? Ikamuuma

Sasa baada ya BIG na Junior Mafia kutoa Get Money audio na video, pac alilalamika kua BiG kamkosea akasema isiwe kesi akaenda akafuta lyrics zoote za ile beat akatengeneza Diss Track pamoja na Crew yake yaan aliunda kundi na yeye akaliita Outlaws ambapo pindi inaundwa ilitambulika km Outlaw Immortalz yeye akiwa km Makaveli ambapo alikua anamhusudu mwanafalosofia Niccola Machiavelli akajiita pia Killuminati The Don (jina la album yake) na wengine ambao ni kundi aliloliunda wakiwa ni madikteta wa dunia, Big Marik aliejiita E.d.I Mean, na wengineo km Kastro alikua anajiita K-Dog huyu ni Fidel Castro wa Cuba, Yaki Karafi huyu ni Gadafi wa Libya, Mutah ambae baadae alibadiri kua Napoleon, pia walitambulika km Thoro Headz and Young Thugz

Baada ya kuunda hilo kundi pac akaingia booth kutengeneza wimbo ambao hio Crew yake mwanzo hawakujua wimbo ni wa nini ndio akawaambia ni Diss Track na inaenda kumpaka Matope BiG na wale wote walio na ubia na BiG akiwemo P Diddy na Bad Boy Crew nzima pamoja na Junior Mafia

Wakatengeneza Diss Track inaitwa Hit 'Em Up hii ndio Diss Track kali ya muda wote, unaambiwa wakati Pac anaingiza vocal mic zilikua zinazima kila wakati na mmoja wa wale waliounda group ya Outlawz aliwahi kuhojiwa akasema pamoja na mic kuzima zima Pac hakuacha kurekodi na ilikua lazima arekodi hakuna wa kumzia hata producer wa ngoma nae anasema alipokua anatengeneza hio ngoma kulikua na changamoto km hizo Ila Pac hakutaka kurudi nyuma

Hatimae ngoma ikawa tayari wakatafuta watu wa Video wakashoot video baada ya hapo ikatoka kitu video & audio at the same time, na katika kava ya audio ya kwanza kabisa kwenye Tape waliweka picha ya BIG akiwa ni nguruwe kaveshwa kichwa Cha BiG na P Diddy akawekwa nyoka kaveshwa kichwa Cha P Diddy ngoma ikaachiwa

Baada ya kifo cha BiG Faith Evans aliewahi kua mke wa BiG alitoa wimbo wa kumbukumbu kwa BIG akiwa na P Diddy unaitwa I Will Be Missing You

Walale wanapostahiri uko walipo

R.I.P
Naona humu kuna washabiki wengi wa Tupac
 
Haka katakuwa kalisoma gazeti la uwazi. Wakati mtandaoni kuna hadi picha za crime scene kabisa ambapo mauwaji yametokea kenyewe kanasema mtu ameshambuliwa ukumbini, ukumbi gani sasa huo, Diamond Jubilee au?!
😂😂😂 ulichoandika kimenichekesha sana
 
Nimekwenda kutazama nimegundua sipo sahihi ila siwezi kukubali kushindwa kinyonge ngoja nilete ligi tu na kubadilisha mada.

2pac amechezea jumla ya risasi 9, 5 ile siku aliposhambuliwa kwenye lift na 4 ile siku aliposhambuliwa kule Las Vegas jumla risasi 9,mbona tunabishana ndugu eti, eeeen si nakuuliza?!
Kwa hesabu hii hapo umenipata mkuu 😂😂
 
Msaani maarufu wa Marekani na producer wa label ya Bad Boy record, anaejulikana kwa jina maarufu la P diddy, sasa tumbo joto baada ya mama yake na Christopher Wallace almaarufu Notorious B.I.G kumuhusisha msaani huyo na kifo cha mwanae kilichotokea mwaka 1997 huko Los Angeles, CA.

Inasemekana kwamba mama huyo amefanya uchunguzi wa kutosha na kujiridhisha kuwa huenda manager huyo wa Bad Boy record amehusika pakubwa na kifo cha mwanae, hivyo anapanga kufungua kesi ili ukweli ujulikane na kila aliehusika na kifo cha mwanae aweze kuchukiwa hatua za kisheria kutokana na mauaji hayo.

Ngoja tusubiri kitachotokea, maana kwa R Kelly ilianza hivi hivi kimzaa mzaa matokeo yake mpaka leo bado mfalme huyo wa R&B ananyea debe.
Mkiandika taarifa muweke link, au ni NDOTO ZAKO 😠😠😠😠
 
Hatari sana "then if you're down with bad boy then fu ... you too ..Chino excel... Mle mwamba katukana sana.

Ile nyimbo miaka hiyo ilikua juu hatari
Mwamba alikuwa jeshi la mtu mmoja ila aliwakalisha wasanii wote waliojaribu kumdiss akiwemo Jay z.
 
Vifo vyao vilipangwa ndomana vilifanana.
2pac gari yao ilipofika kwenye traffic light mataa ya kuruhusu upande wao kwenda yakafunga hivyo ikawalazimu kusimama. Ghafla wakatokea mabinti pembeni ya barabara wakaanza kuita 2pac.. 2pac.. 2pac... basi 2pac ile kushusha kioo awapungie mkono hapo hapo akaanza kushambuliwa na gari ya majamaa waliokuwa ubavuni kwao.

Big nae gari yao ilipofika kwenye traffic light mataa ya kuruhusu upande wao kwenda yakafunga hivyo ikawalazimu kusimama. Ghafla pia wakatokea mabinti pembeni ya barabara wakaanza kuita Big.. Big.. Big.. basi ile Big kushusha kioo awapungie mkono hapo hapo na yeye akaanza kushambuliwa na gari iliyokuwa pembeni yao hadi kusababisha umauti wake.
Noma mkuu
 
50cent kayafukua haya makaburi ya Diddy mana alianza kumweka wazi siri zake za ushoga ila sasa alipofikia kwenye hii kesi na kumtafuta LAPD officer aliyekuwa eyewitness wa shambulio kisha kuchukua video za Pac alizokuwa akieleza claims zake na kuwa Ana ushahidi na anajua mhusika wa shambulio tofauti tofauti ni Diddy ila iachwe na ibaki Kati Yao wawili.

Mzigo ukaja kwa Diddy kupigwa maswali kutokana na tuhuma hz..... Diddy anaonekana Ana kitu amekificha kwa muda mrefu kuhusiana na vifo viwili hivyo.
Na wanazidi kumtilia mashaka.
Asante mkuu kwa ufafanuzi mzuri. Diddy kwa sasa ni kama vile amekalia misumari, hana raha kabisa.
 
Angalau wewe umeandika vinavyoeleweka. Wengine walikuwa wanaposti longo longo tu, mara illuminati mara sijui FBI ...

KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KIFO ? (4)
_______________

Inaendelea......

Kutokana na Tupac kuhitaji bosi wa Death Row, Marion 'Suge' Knight apambane kumtoa ndani ili waweze kufanya biashara pamoja, Suge aliangaika huku na huko mpaka kufanikiwa kumchomoa Tupac jela.

Kiasi cha Dola Milioni 1.4 kilitolewa na Suge hivyo kufanikiwa kumtoa jela Tupac mwaka 1995, achilia mbali Dola 15,000 ambazo Suge alizitoa kumsaidia 'kishkaji' Tupac wakati akiwa jela.

Kimsingi Suge alikubali kujipukutisha fedha kwa sababu alijua kumwandika Tupac mkataba wa kumsimamia kupitia Death Row Records italipa. Knight alijua nini anafanya kwenye makubaliano hayo.

Makubaliano ya Tupac na Suge yakawa mazuri. Tupac akakubali kutengeneza albamu 3 chini ya Death Row Records lakini muda wote akihitaji Suge awe upande wake kwenye vita vyake dhidi ya Biggie.

Nyimbo ya kwanza ya Tupac kuitoa chini ya Death Row Records ikawa California Love. Kombinesheni ya Tupac, Dr Dre na Roger Troutman kwenye chorus ukawa unyama wa kufa mtu. Kwa hakika "The King was back from Jail''.

Ujio wa California love ulimtikisa kila mtu. Tupac alikuwa amejerea kuusimika upya ufalme wake uliotishiwa kuondoshwa kwa mtutu wa bunduki na vijana kutoka Pwani ya Mashariki (East Coast).

Marion Suge Knight na Tupac Shakur wakafanikiwa 'kuupika' mgogoro wa East Coast na West Coast ukapikika, mgogoro ambao chimbuko lake haswa ni chuki baina ya wasanii wawili, Notorious Big na Tupac Shakur.

Matatizo binafsi ya Biggie na Tupac yakajikuta yakirithiwa na hata wengine 'yasiyowahusu'. Wasanii wa East na West wakaonekana kuchukiana katika kiwango kilichotisha kabisa.

Wakati mgogoro huu ukikua na kuzidisha uhasama kwa wasanii, Serikali mwanzo ilionekana kama kupuuza, lakini kadiri hali ilivyozidi kuwa mbaya na viongozi walilazimika kusema chochote.

Lakini kabla ya kusema chochote, huko nyuma Tupac alikuwa ameshaingia kwenye mgogoro mara kadhaa na serikali kutokana na misimamo yake, harakati zake na maisha yake.

Nyimbo zake kupitia albamu yake ya 2Pacalypse ziliichefua sana serikali. Tupac alizungumzia zaidi Siasa, Ubaguzi na umasikini katika namna ambayo ilionekana kama kuchochea chuki kwa raia.

Mshtuko mkubwa ulitokea baada ya kijana mmoja mdogo kumpiga risasi polisi na kumuua kisha baada ya kukamatwa na kuhojiwa akathibitisha kufanya hivyo baada ya kusikiliza albamu ya Tupac iitwayo 2Pacalypse.

Tukio hilo lilikuwa gumzo nchini Marekani. Aliyekuwa Makamu wa Rais wakati huo, Bw Dan Quayle akatangaza kupigwa marufuku kwa nyimbo za Tupac kusikilizwa kwenye Jamii ya wamarekani.

Bw. Quayle alisema Tupac ni msanii asiyefaa kabisa kusikilizwa. Nyimbo zake zimejaa chuki na kuchochea uovu kwenye jamii. Akaanzisha kampeni za kuhakikisha jamii inamchukia na haipati nafasi ya kumsikiliza Tupac.

Masikini Quayle hakuwa amejua kuwa wakati anasema hayo, Tupac alikuwa ameshaiteka sehemu kubwa ya jamii ya wamarekani kuliko anavyodhani. Mahojiano yake na MTV ya mwaka 1993 yamlitosha kabisa kumfanya asimjibu lolote.

"Siwezi kuitawala dunia wala siwezi kuubadilisha ulimwengu, bali nichoweza kufanya ni kutema cheche zitakazofanya bongo za watu kuibadilisha dunia"..hii ndiyo kazi yetu tunayopaswa kufanya, kuamsha mtu mwingine anayetutazama".

Tupac alikiambia kituo cha televisheni cha MTV mwaka 1993 katika moja kati ya mahojiano yake yanayoendelea kukumbukwa mpaka leo. Quayle alishindwa vibaya katika kampeni ya kumaliza Tupac, lakini inaelezwa alichangia mno kupromoti mauzo ya kazi zake bila ya yeye kujua.

Watu mashuhuri mbalimbali waliyataja maneno hayo machache ya Tupac kama maneno bora zaidi kuwahi kutolewa na mtu "asiyetegemewa" na wengi kusema hivyo. Wengi waliyatumia kama rejea kwenye maeneo yao mbalimbali.

"Inawezekana baadhi yetu tusiwe watu wa kuibadilisha dunia, lakini tunapaswa kujaribu kila wakati kushawishi mtu mwingine kuchukua hatua zitakazoweza kuibadili dunia".

Maneno haya ya Tupac hata kwangu binafsi bado yanaishi sana.!

Itaendelea........[emoji3578]

#Balozi
 
Hata na mimi nakubaliana kwa namna fulan ya kile ulichoandika. Ila kusema kuwa gangs wa LA watakuwa wamehusika ma mauaji hayo kidogo inanifanya nisikubaliane na wewe moja kwa moja.

2pac pale LA ndio alikuwa kama ngao yao kimziki na kingome. Pac alikubalika sana LA mpaka akajiona kama vile pale ndipo alipopaswa kuzaliwa.

Shambulio la 2pac lilifanyikia Nevada katika jimbo la Texas. Sheria za Texas haziruhusu mtu yoyote kutoka nje ya jimbo hilo kuingia na silaha ndani ya jimbo lao, na hiyo ndio sababu iliyosababisha kina 2pac na ulinzi wao wasiingie na silaha jimboni humo.

Lingine unafikiri hao wauaji walijuaje kama 2pac hakuwa na kinga ya kuzuia risasi kama sio mpango mahususi ulipangwa na watu wakubwa. Ukiangalia ile historia ya 2pac ambayo alikuwa anasimulia mwenyewe maisha yake toka utoto hadi kifo kilipotokea, utaona kuna sehemu wakati kina 2pac wakienda club walikutana na polisi wale wa beskeli, wale polisi wakaongea kwa muda na kina 2pac afu wakawaruhusu waendelee na safari yao.

Haikupita muda wakafika katika mataa na kukuta mataa ya upande wao yamefunga, hivyo ikawalazimu wasubiri mataa yaruhusu ndo waendelee na safari. Sasa katika mazingira hayo ndio shambulizi lilipotokea.

Kwahiyo inaweza kuwa kweli vijana wamepewa deal na wakubwa kwa ahadi kwamba hawatafuatiliwa na vyombo vya usalama. Kwahiyo na wao kwa makubaliano hayo wakafanya yao na jumba bovu kuangushiwa kina Orlando na Big ambao hawajui hili wala lile.

Wahenga walisema mdomo uliponza kichwa. Nyimbo ya Big who shot ya imemponza, na dogo Orlando lile pambano likatumiwa kama njia ya wauaji kufikia malengo yao.
Las Vegas ipo Nevada sio Texas, story yako haipo sawa kwa asilimia kubwa sana.
 
Pddy hawezi kumuu BIGGIE nakataa,kwenye gari alipokuwepo BIGGIE Kulikua na ndugu yake wa damu..

Eugene deal ambae ni bondia wa pddy(Mtoto wa kaka yake)
Lil cease mjomba wa B.I.G na member wa JUNIOR M.A.F.I.A wote walifia humo..

labda bimkubwa ameona mwanae amesahaulika anataka kumrudisha kwenye trend ya vichwa vya habari...
pia inaweza kuwa ni mpango wa SUGE KNIGHT kama rivarls kwa PDDY...

Pddy ndio power control kwenye kesi ya SUGE Na anamchomekea kweli,halafu mwezi uliopita mama yake B.I.G Alikutana na SUGE mahakamani na waliondoka pamoja..

BEEF YA SUGE KNIGHT NA P.DIDDY HAIWEZI KUISHA
Gene Deal hana undugu wowote na puffy, alikuwa bodyguard na ata sasa amekuwa akimsagia kunguni puff kila siku. Lil Cease pia sio ndugu wa damu, ni rafiki wa utotoni wa karibu sana. Suge aondoke mahakama ipi? We jamaa muongomuongo sana, mwenzio yupo jela ana miaka zaidi ya 25 inamsubiri eti alikutana na mama yake Biggie wakaondoka wote, we ni mzima au umekula kitu wewe? Dah 🤣
 
FBI walifanya upelelezi wao wakashindwa kujua muuaji ndo kusema huyu mama kawazidi ujuzi?
Toka lini muuaji akajichunguza mwenyewe ili ajikamate. FBI ndio wahusika wakuu wa hayo yaliotokea ndomana mpaka leo unaona kesi zinapigwa danadana. We kwa akili ya haraka haraka unaona shirika kubwa la upelelezi duniani kama FBI wangeshindwa kutambua wahusika wa mauaji ya ndani tena katika traffic light barabarani sio uchochoroni?
 
Mwamba alikuwa jeshi la mtu mmoja ila aliwakalisha wasanii wote waliojaribu kumdiss akiwemo Jay z.
Kwenye kuandika hio Diss Track ya Hit 'Em Up aliweka line ikisema fack Jay-Z wakamwambia Jay-Z usimdiss hausiki na Bad Boy Crew kipindi hicho Jay Z alikua anataka kufanya project na Bad Boy kwa akafuta ile line ya fack Jay-Z akaandika fack Chino XL, huyu mwamba Chino XL alipokua jela Pac jamaa alitoa ngoma katika lyrics zake akasema kwamba hawezi kwenda ili akabakwe km 2Pac yaan akimaanisha kwamba Pac alipokua jela alitatuliwa Malinda kwa hio Pac alipotoka akaongezea hio Fack Chino XL, lakini baadae walikuja kukutana California Chino XL na Pac wakaongea wakayamaliza haikua bifu kiivyo

Na Jay-Z kuna ngoma yake moja inaitwa Jocking Jay-Z mwanzo ukiipata OG yenyewe utamsikia km Pac akisema Fack Jay-Z Ila Jigga akai-translate vingine akaweka Jocking Jay-Z na hio track ipo ndani ya album ya Jigga Blueprint 3
 
Tupac alikuwa na hasira baada ya kutokea ugomvi baina yake na BIG kuhusu utunzi wa wimbo fulani, alikwenda kwenye vyombo vya habari na kuanza kujisifu kuwa amelala na Faith Evans mke wa BIG.

BIG akaona isiwe shida ammalize tu. Kundi la Tupac likaamua nalo lilipize kisasi na vijana wawili wadogo wakaondoka kiurahisi sana.

Faith Evans akatoa wimbo mmoja mkali sana wa kumkumbuka BIG chini ya uongozi wa P Didy....
Ile nyimbo kalii sanaa
 
Back
Top Bottom