Paka kuchukuliwa kama mwanafamilia kwa kutengewa bajeti yake, inakubalika?

Paka kuchukuliwa kama mwanafamilia kwa kutengewa bajeti yake, inakubalika?

Mtafuga na majini bure
Mimi kwangu sifugi mnyama tofauti na mbuzi,ng'ombe na kuku.
 
Kuna paka na mbwa hapa nyumbani kwangu, Sina tatizo na gharama za mbwa kwa sababu ana msaada kiasi kwenye swala la ulinzi.

Kwa huyu paka huwa inanifikirisha sana maana hatuna tatizo la panya ila watoto wangu kwa kuwa wanapenda paka nikaamua niwarusu wamfuge.

Kimbembe kipo huku mama yao (mke wangu) amekuwa akiteketeza pesa kwenye matumizi ya huyo paka.

Bili ya maziwa imeongezeka kwa sababu paka nae anahesabiwa, anapewa maziwa asubuhi na jioni.

ananunuliwa samaki hawa wadogo wadogo kama chakula.

Matibabu nayo baada ya miezi kadhaa check up, n.k

Kuna paka waliwahi kumfuga ila alikufa, haikuchukua hata siku 2 akaletwa mwengine, Kiukeli hawa paka kazi pekee wanayojua ni kupumzika na kujizungusha chini ya miguu, Mbaya zaidi wanahisi wanakutawala ukiwaendekeza kuwapa wanachohitaji

Hii imekaaje
Chuna ngozi huyo paka kawauzie Wachina, kama nyumba haina panya hakuna sababu ya kukaa na paka.....hana faida hata kidogo.
 
Kama uwezo wa kumhudumia unao, Basi kubali aendelee kufugwa.

Yawezekana huoni faida yake lakini haujajua kuwa furaha inayopatikana ndani ya ndoa yako imekamilika kupitia paka huyo.

Humtaki paka kwa kuwa ndani mwako hamna panya?

Kazi ya paka siyo kukamata panya tu, Penye paka huwezi muona nyoka.

NOTE: Kama matunzo ya paka huyo yana gharama kubwa basi mshauri mkeo kwa busara apunguze bajeti kwa paka huyo, Maana ukitumia mabavu ukamuondoa paka ujue watoto wako na mkeo watakuchukia na huo ndo utakuwa mwanzo ndoa yako kuparaganyika.
Safi kabisa, baba anafikiri anachokipenda yeye na familia itakipenda, kutunza familia siyo chakula na mavazi tu. Hata kuheshimu na kujali hobbies za wanafamilia ni sehemu ya majukumu ya baba, utakuta wengine wanachinja wanyama nyumbani huku watoto wanaona na wanaanza kulia sana, sababu wanawapenda wanyama. Watanzania wengi hawana elimu kuhusu tabia za viumbe na ndiyo maana bundi na paka wanahusishwa na Imani potofu za kishirikina.
 
Nimesoma Uzi nzima watu wamekalili kuwa kazi ya paka ni kuua panya tu,ok fine,sipendi paka lakini paka ni kiumbe mzuri Sana ,mwaka elfu 2000 nilikuwa kwa Bibi yangu tumelala chini ,na Bibi alipenda Sana kufuga paka,Ile naamuka asubuhi pale chini usawa wa godoro nilishangaa kuona nyoka amekufa,isingekuwa paka nyoka yule angetuuma.


Tena nakumbuka mwaka 2018 nikiwa Lindi ,ghafula paka wa jirani yangu alianza kutoa sauti ya kuashiria hatari,nilipo toka nje sikuamini macho yangu,nilimkuta paka anapambana na nyoka mkubwa Sana aliyekuwa akihangaika kuingia ndani ya nyumba,paka alikuwa akimzui,nilipambana naye na kumuua yule nyoka.

Paka Ni wazuri Sana,tuache kukalili kuwa kazi yao Ni kupambana na panya tu!
 
Kuna paka na mbwa hapa nyumbani kwangu, Sina tatizo na gharama za mbwa kwa sababu ana msaada kiasi kwenye swala la ulinzi.

Kwa huyu paka huwa inanifikirisha sana maana hatuna tatizo la panya ila watoto wangu kwa kuwa wanapenda paka nikaamua niwarusu wamfuge.

Kimbembe kipo huku mama yao (mke wangu) amekuwa akiteketeza pesa kwenye matumizi ya huyo paka.

Bili ya maziwa imeongezeka kwa sababu paka nae anahesabiwa, anapewa maziwa asubuhi na jioni.

ananunuliwa samaki hawa wadogo wadogo kama chakula.

Matibabu nayo baada ya miezi kadhaa check up, n.k

Kuna paka waliwahi kumfuga ila alikufa, haikuchukua hata siku 2 akaletwa mwengine, Kiukeli hawa paka kazi pekee wanayojua ni kupumzika na kujizungusha chini ya miguu, Mbaya zaidi wanahisi wanakutawala ukiwaendekeza kuwapa wanachohitaji

Hii imekaaje
Ongea na wife na watoto mpate suluhisho. Mwambie ukweli wako unavyofikiri.
 
Zamani nilikuwa nafunga mbwa kwa ajili ya kuwinda na ulinzi ,paka naye alikwepo ila anajitafutia chakula kivyake maana siyo panya tu anakamata njiwa ,hadi kware .Ila jioni na asubuhi mnapokamua ng'ombe anakuja pale kulia anataka maziwa tunampa hata nusu lita anajipigia zake anaondoka but maisha ya Sasa yamebadilika ,paka na mbwa wamekuwa kama mapambo tu,unakuta paka hali nyama mbichi anataka vilivyokaangwa
 
Safi kabisa, baba anafikiri anachokipenda yeye na familia itakipenda, kutunza familia siyo chakula na mavazi tu. Hata kuheshimu na kujali hobbies za wanafamilia ni sehemu ya majukumu ya baba, utakuta wengine wanachinja wanyama nyumbani huku watoto wanaona na wanaanza kulia sana, sababu wanawapenda wanyama. Watanzania wengi hawana elimu kuhusu tabia za viumbe na ndiyo maana bundi na paka wanahusishwa na Imani potofu za kishirikina.
Hakika mkuu kwa waswahili paka mweusi na bundi anaonekana ni msala lkn kiuhalisia hawa viumbe ni wazuri kudhibiti wadudu hatari ndani ya nyumba tunahitaji elimu kuhusu hawa wanyama
 
Kuna paka na mbwa hapa nyumbani kwangu, Sina tatizo na gharama za mbwa kwa sababu ana msaada kiasi kwenye swala la ulinzi.

Kwa huyu paka huwa inanifikirisha sana maana hatuna tatizo la panya ila watoto wangu kwa kuwa wanapenda paka nikaamua niwarusu wamfuge.

Kimbembe kipo huku mama yao (mke wangu) amekuwa akiteketeza pesa kwenye matumizi ya huyo paka.

Bili ya maziwa imeongezeka kwa sababu paka nae anahesabiwa, anapewa maziwa asubuhi na jioni.

ananunuliwa samaki hawa wadogo wadogo kama chakula.

Matibabu nayo baada ya miezi kadhaa check up, n.k

Kuna paka waliwahi kumfuga ila alikufa, haikuchukua hata siku 2 akaletwa mwengine, Kiukeli hawa paka kazi pekee wanayojua ni kupumzika na kujizungusha chini ya miguu, Mbaya zaidi wanahisi wanakutawala ukiwaendekeza kuwapa wanachohitaji

Hii imekaaje
Hausumbuliwi na panya kwa sababu paka yupo,waenga sio wajinga walisema "paka akitoka(kuondolewa au kufa)panya utawala "
 
Kuna paka na mbwa hapa nyumbani kwangu, Sina tatizo na gharama za mbwa kwa sababu ana msaada kiasi kwenye swala la ulinzi.

Kwa huyu paka huwa inanifikirisha sana maana hatuna tatizo la panya ila watoto wangu kwa kuwa wanapenda paka nikaamua niwarusu wamfuge.

Kimbembe kipo huku mama yao (mke wangu) amekuwa akiteketeza pesa kwenye matumizi ya huyo paka.

Bili ya maziwa imeongezeka kwa sababu paka nae anahesabiwa, anapewa maziwa asubuhi na jioni.

ananunuliwa samaki hawa wadogo wadogo kama chakula.

Matibabu nayo baada ya miezi kadhaa check up, n.k

Kuna paka waliwahi kumfuga ila alikufa, haikuchukua hata siku 2 akaletwa mwengine, Kiukeli hawa paka kazi pekee wanayojua ni kupumzika na kujizungusha chini ya miguu, Mbaya zaidi wanahisi wanakutawala ukiwaendekeza kuwapa wanachohitaji

Hii imekaaje
Mnyama yeyote afugwae ni mmoja ya familia, kinachofanyika hapo kwako ni jambo jema sana na lakiimani sana kuhudumia mfugo ni wajibu na ni sehemu ya jukumu letu wanadamu, nikuombe tu usivunjike moyo wasapoti wanafamilia kwa hilo la kupenda wanyama na uwekeze ktk kuwajali na kuwatizama vyema.
WATAZAMENI NDEGE WA PORINI HAWAVUNI WALA HAWASOKOTI LAKINI BABA WA MBINGUNI ANAWAPA KULA KULALA KUNYWA NA UHAI.
 
Back
Top Bottom