Pamoja na mapungufu yanayosemwa na "CCM ya Makonda", CCM imefanya mengi kipindi cha Samia. Kwanini Makonda hajikiti kuyaeleza mbele ya watanzania?

Pamoja na mapungufu yanayosemwa na "CCM ya Makonda", CCM imefanya mengi kipindi cha Samia. Kwanini Makonda hajikiti kuyaeleza mbele ya watanzania?

Kuna jambo linatia tafakari kidogo, CCM pamoja na awamu ya sita, kwa kweli wamefanya mengi sana ya kimaendeleo. Ili kuitendea haki CCM na uongozi wa serikali, lazima yasemwe mikutanoni.

Hii ya kutembea na kuaminisha watu kwamba hakuna lililofanyika nadhani si sahihi. Unaita mtumishi mmoja, ana ka suala kamoja tu ka kiutendaji, unakashikia bango hako, husemi chochote kuhusu mengine mazuri yaliyofanywa na CCM eneo hilo. Mfano, Kagera, kuna miradi mipya lukuki imepelekwa na Samia, yakaangaliwa mabaya tu tena kwa lengo la kujitafutia umaarufu binafsi, hakuongelea meli mpya ukarabati mkubwa wa bandari, na kadhalika, ukiangalia, hii ni kwa mikoa yote anafanya hivyo.

Hata JPM, alijikita kwanza kuonyesha mafanikio ya CCM japo yamepatikana katika hali ya uchumi mgumu. Na kisha akasemea mapungufu, kwa nini huyu amejikita kwenye upande wa kuonyesha kwamba awamu ya sita haijafanya kitu kwamba kila sehemu ni shida tu?

Maana uongo ukirudiwa, unakuwa ukweli, sasa ukiwa ukweli wananchi tutawaambia nini 2025? Maana kiongozi wa CCM wa uenezi anasema serikali iko hovyo, na wapinzani wanasema iko hovyo, tunadhani wananchi wataamuaje? Hatukatai CCM kuyatambua mapungufu na kuyafanyia kazi, lakini mbona tunaweka nguvu kubwa kufanya mafanikio yaonekane kama hakuna?

Kuna mtu anajua kwamba wale wanaohamishwa bonde la msimbazi mama Samia, sio Benki ya Dunia, mama Samia kupitia ikulu katoa amri kila mmoja apewe milioni nne akanunue kiwanja kigamboni au chanika, hiyo ni mbali na fidia anayolipwa? Sawa, shida zipo, mbona mazuri huyasemi?

Tutumie asilimia 75 ya muda kuwaeleza wananchi nini tumefanya, tuwaeleze mapungufu, na na wao watueleze mapungufu, tuone namna ya kuyafanyia kazi.

Kwa hali ilivyo, sidhani kama kuna strategy ya mawasiliano ndani ya chama. Mwenenzi anasema akimaliza ziara anapeleka taarifa kwa Rais! Kwa nini isiwe kwa Katibu Mkuu, ambaye ndio immediate boss?

Ziara nzima hakuna anayeambiwa kuhusu SGR, Bwawa la Mwalimu Nyerere, shule nzuri hazitembelewi, anatembelea makaburi tu, wengine wanasema anatembelea makaburi kwa sababu za kishirikina tu, sijui kuchota mchanga apeleke kwa wataalamu ili wamchanganyie mavumba awe mkubwa kama hao viongozi, kwa nini hakuna sauti kubwa kwa miradi kama Kigongo Busisi, Lami,.miradi ya maji na kadhalika.

Hatumuoni anatembelea miradi ya mfano kwa kila wilaya au Halmashauri, iko mingi sana, ya kila aina, tena ya kisasa, ila yeye anatafuta sehemu za chokochoko tu dhidi ya serikali iliyo madarakani, na kudhoofisha imani ya wananchi kwa serikali. Sawa, atafute za chokochoko, lakini mbona nzuri hazisemi wala kuziona?

Chama kinatakiwa kuwa juu ya mtu, lakini naona mtu anataka kuwa juu ya chama.

Hii inaweka taswira kwamba, kwa mlango wa nyuma, anambomoa Samia kisiasa kwamba hajafanya kitu chochote, wakati wenzake ndani ya CCM wametumia muda mwingi kuonyesha Samia kafanya makubwa nchini.
Kwanza wewe ni adui namba moja wa MAKONDA hakuna sehemu umemsema vizuri MAKONDA,wewe ni kumshambulia tu,nakufuatilia kila angle,


Nije kwenye hoja yako,hakuna sehemu MAKONDA kaponda mema anayoyafanya rais Samia ,bali MAKONDA ana dili na viongozi wazembe,wapumbavu kama wewe,mnaomvika mama Samia kilemba cha ukoka huku jamii ikmtengenezea chuki kwa kushindwa kutatua kero kwa dhamana alizowapa.

Anachokifanya MAKONDA ni kuwaanika wahuni nyie

Mwisho acha MAKONDA aseme mabaya ya Samia kama akili yako imekutuma hivyo,halafu wewe jikite kusema mazuri ya rais Samia,usimpangie gororko wewe
 
Unapomsikiliza utulie. Makonda ndo mtu pekee anyetangaza kazi nzuri za mama!! Lakini kumbuka yupo pia KM CCM na Viongozi wengine wa Chama na Serikali, wao wanafanya kazi gani? Unamuona Makonda tu?

Tuliza Makalio wewe CHAWA wa Wahuni.
we una ndizi, ni zombie km huyo Bashite
 
Hata Mrema alikuwa anajifanya kumsemea Mwinyi sana, lakini akaja kuongoza uasi mkubwa dhidi ya CCM. Na ndivyo itakavyokuwa kwa Makonda.
Ahsante mkuu, mi napenda watu wenye akili kubwa km wewe. Makonda ni kaburi la Samia. Ni kijana asiye na adabu, sijui amelelewa wapi, hata akiwa mkuu wa mkoa wa Dsm alikuwa juu ya mawaziri, hata sahivi anajiona yuko juu yao, anawapigia simu hadharani kuwadhalilisha na kujipa cheap popularity. Haheshimu wala hatambui taratibu, lile kwanza ni jinga kubwa. Na mtu mpumbavu mwepuke ataangamiza Taifa. Tusubiri Samia aendelee naye atajua kuwa hajui.
 
Tulishasema Samia atajuta kumweka pale huyo Bashite. Yule jamaa kwanza ni akili ndogo sana sana. Hakuna kitu pale. Bashite kwanza anautukuza usukuma, anamtukuza yule mfu wake, yukp kummaliza Samia ataamini siku maji yakimfika shingoni. Anajenga umaarufu binafsi, vilevile wako watu nyuma yake na si wengine na wale sukuma gang. Makonda hana akili. uwezo wake ni mdogo sana anategemea ushirikina. Ogopa mtu anayemtaja sana Mungu, ni hatari, ni mnafiki. Amefika Mbeya alichofanya ni kuchonganisha wizara ya Ardhi na Wizara ya Kilimo. Hamtambui Katibu Mkuu. Nchi imekuwa km ya mazombie, mataahira, mazuzu, wehu.

Samia anataka kuipeleka wapi nchi yetu? Makonda ni zero brain, ni aibu kuongozwa na jitu km lile. Kwanza limeshaua pamoja na yule shetani wake mpaka Marekani wakampiga ban kukanyaga kwao. Huyu mama atuachie nchi yetu iongozwe na watu wenye akili. Makonda hawezi kumkaribia Hussein Bashe kwa uwezo kichwani, Bashite ni zero anatuharibia nchi yetu. Anamdharau katibu mkuu, hata Samia anamdharau ni kwamba tu hajasema hadharani. Bashite alitakiwa awe mahakamani. Nimemchukia Samia kwasababu ya huyo mpumbavu wenu.
Umeona slogan ya CCM MBELE KWA MBELE inaigharimu nchi.
 
Kwanza wewe ni adui namba moja wa MAKONDA hakuna sehemu umemsema vizuri MAKONDA,wewe ni kumshambulia tu,nakufuatilia kila angle,


Nije kwenye hoja yako,hakuna sehemu MAKONDA kaponda mema anayoyafanya rais Samia ,bali MAKONDA ana dili na viongozi wazembe,wapumbavu kama wewe,mnaomvika mama Samia kilemba cha ukoka huku jamii ikmtengenezea chuki kwa kushindwa kutatua kero kwa dhamana alizowapa.

Anachokifanya MAKONDA ni kuwaanika wahuni nyie

Mwisho acha MAKONDA aseme mabaya ya Samia kama akili yako imekutuma hivyo,halafu wewe jikite kusema mazuri ya rais Samia,usimpangie gororko wewe
Konyo, nenda kamtawaze kama wanavyofanya wenzako, kisha wanampa uchifu
 
Back
Top Bottom