Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,916
- 43,505
Mwana JF nguli, Akihojiwa Radio DW Pascal Mayala, amemchambua Dr Bashiru. Amesema Dr Bashiru kapata ajali kubwa Sana kisiasa na hatoinuka tena. Pia kadai Magufuli amiini usiamini alikuwa akimwandaa Dr Bashiru kuwa Rais 2025.
Mayala amedai Dr Bashiru aliyeibukia kuwa Katibu Mkuu wa CCM baada ya kuhakiki Mali za chama hicho alichukuwa mno kutokana na style ya uongozi.
Amesema amekinyoosha mno chama hadi kupitiliza na kusababisha kuchukiwa mno kuliko Katibu Mkuu yeyote ktk Historia ya CCM. Pia amedai Dr Bashiru no mjamaa mno au Mnyerere na Marehemu Magufuli alimkubali na kumpenda Sana na alipanga kumuacha Urais 2025.
Mayala amedai pia haoni njia ya Bashiru kufufuka tena kisiasa na ndiyo hivyo Mama Samia Suluhu ameshampoteza na Wana CCM wamefurahi mno.
Amesema kwa uhakika utawala wa Mama Samia Suluhu atakuwa Rais mzuri Sana kuliko Rais Magufuli.
Source: Radio DW Swahili, Leo mchana saa Saba, 01/04/2021.
Naheshimu maoni ya Pascal na wengine napia nitaendelea kumuheshimu Dr Bashiru maana amefanya kazi kubwa ndani ya chama!
Kidumu chama cha Mapinduzi