Passo ikiwa kwenye speed ya 80km/h inakuwa sawa na V8 ikiwa kwenye speed hiyo hiyo?

umbali/muda = mwendokasi
Akili unazo afu unajitia wazimu. Mtoa mada kuna sehemu kazungumzia power?

Yeye kauliza kuhusu speed tu. So mada yetu imejikita katika speed basi.

Haijarishi ya Bugatti, Aston Martin, IST, Passo, March au VW chura.

Je, Aston Martin akiwa speed 80km/ na hiyo V8 yenu iko speed hiyohiyo, zitaenda sambamba?? Nijibu
 
Kwa laws za physics na mahesabu ni sawa lakini kiuhalisia sio sawa.
 
Hazitokwenda sawa mzee katika uhalisia, aerodynamics katika aston martin na LC ni tofauti, factors nyingi zinahusika, unless unazungumzia physics ambayo katika mazingira ya uhalisia haipo..
 
Hazitokwenda sawa mzee katika uhalisia, aerodynamics katika aston martin na LC ni tofauti, factors nyingi zinahusika, unless unazungumzia physics ambayo katika mazingira ya uhalisia haipo..
Unajitoa akili sijui kwanini!! Hivi trafiki akiwa anapima speed anakua na tochi za kila model ya gari??
 
Unajitoa akili sijui kwanini!! Hivi trafiki akiwa anapima speed anakua na tochi za kila model ya gari??
Katika uhalisia passo haiwezi kuizidi LC, achana na upuuzi wa physics ku ignore aerodynamic, hp torque,handling n.k...
Ninachozungumzia weka hapo passo yako iwe na inatembea 80km/hr n V8 itembee 80km/hr barabara imenyooka km 100... ndipo utagundua wewe ndiye unajitoa akili..

katika mazingira ya kufikirika na laws za physics kwenye karatasi zitakuwa sawa, kiuhalsia passo ni baiskeli..
 
Mbona unakwepa maswali ya msingi unayoulizwa?? Au huko na chuki binafsi na passo??

Unavijua ving'amuzi (GPS speedometer) vinavyowekwa kwenye magari especially mabasi ya kati na makubwa ya abiria?


Je vinatofautiana kulingana na gari??


Tuseme wanachoweka kwenye Tata Marcopolo ni tofauti na wanachoweka kwenye Scania irizar almaarufu Katarama??


Maana vinapima speed ya gari na hayo hapo juu ni magari tofauti tukizungumzia maswala ya Hp, torque, handling, shape nk....
 
Kwa laws za physics na mahesabu ni sawa lakini kiuhalisia sio sawa.
Kwa mujibu wa fizikia, kasi ya mwendo (velocity) ni kipimo cha jinsi kitu kinavyosafiri umbali fulani kwa muda fulani.

Inapimwa kwa kipimo cha umbali kwa muda, kama vile kilomita kwa saa (km/h) au mita kwa sekunde (m/s). Ikiwa Toyota Passo na Land Cruiser V8 zote zinasafiri kwa kasi ya 80 km/h, kasi zao za mwendo (velocities) ni sawa.

Kwa hiyo, kutoka kwa mtazamo wa fizikia, vitu hivi viwili vitasafiri umbali sawa kwa muda sawa kwa kuwa vina kasi sawa.

Katika kesi hii, tofauti katika muundo, uzito, au nguvu ya injini haziathiri umbali wanaosafiri kwa kila saa moja. Kasi ya mwendo hutegemea tu umbali unaofikiwa kwa muda, na siyo sifa za gari lenyewe.

Kwa kuzingatia kanuni ya mwendo ya Newton ya pili, nguvu (force) itakayohitajika ili kuendeleza mwendo wa magari haya kwenye kasi ya 80 km/h inaweza kutofautiana kwa sababu ya tofauti katika uzito na ukubwa wa magari hayo.

Lakini kama hakuna vikwazo (labda hali ya barabara), kasi inabakia ile ile, na magari haya mawili yatatembea sambamba umbali ule ule ndani ya muda ule ule kwa kuwa yana kasi sawa.

Ova
 
Akibisha na hapa nam- ignore
 
Na bado watakubishia.
Hapo ndio ujue kuwa elimu ya bongo ina shida.
Watakwambia hata magari yote yakiwa yamesimama (speed ya 0km/hr), Gari kubwa litasogea mbele kidogo🤣🤣🤣🤣
 
Msukuma aliyezaliwa mwaka 1990 na Mchaga aliyezaliwa mwaka 1990 nani kati yao atakuwa na umri wa miaka mingi?
Au muulize kilo 100 za sufu (pamba) na kilo 100 za mawe ni kipi kizito zaidi?
 
Tractor na Baiskeli vyote vikiwa kwenye speed ya 10km/hr, kipi kitamaliza umbali wa urefu wa football (100m) haraka?
 
Nenda moja kwa moja kwenye jibu! Speed ni speed tu 180km/h ya passo ni sawa sawa na 180km/h ya V8, ikiwa na maana kwa muda wa dakika 60 (saa moja) magari hayo yote mawili yatakuwa yametembea kilometer 180. Labda utofauti ni Revolution per second ya taili (taili ya v8 kwa vile ni kubwa) ikizunguka mzunguko hule hule teseme 180rev/sec sawa na passo, basi V8 itakuwa inaenda kwa speed kubwa zaidi ya passo crome20
 
Hivi jamani Passo ikiwa kwenye speed ya 80km/h inakuwa sawa na V8 ikiwa kwenye speed hiyo hiyo au kuna tofauti? Cse magari madogo mengi ni 180KMh, sawa na haya magarri yetu SUVs.

Sasa tofauti ni wapi?
ili kukamilisha uchunguz ongezea passo na v8 zkifika kwe bams inakuaje 😄
 
My very own, unajua halafu wala huna kelele.
I’m proud.
 
usitusahau 'maafisa usafirishaji'
boxer bm 150 speedometer 140 lakini wa gari ndogo hawampati kama akiamua kuiondolea unyonge.

 
Tractor na Baiskeli vyote vikiwa kwenye speed ya 10km/hr, kipi kitamaliza umbali wa urefu wa football (100m) haraka?
Mnachoshindwa kuelewa , katika uhalisia mambo kama aerodynamics yanahusika...

V8 ni gari yenye horse power kubwa na torque kubwa kuliko hio passo, kumbuka upepo huwa unaleta ukinzani kwenye gari inapotembea kitu kinachopelekea kuathiri mwendokasi na perfomance.

Katika mazingira ya uhalisia upepo pekee ni chanzo kitakachopelekea passo kushindwa ku perform vyema...

V8 ina nguvu kukabiliana na upepo kuliko passo... Passo itakuwa inapepesuka hovyo...

Aerodynamics ina affects speed ya gari na perfomance si kidogo...

Acheni mifano mfu na physics za uongo za ku assume na ku ignore real facts..
 
Ndio nasema katika uhalisia passo itabaki nyuma..

Kwa physics za darasani ku ignore uhalisia zitakuwa sawa...

Upepo tu pekee ni fact moja kubwa kwa passo kuzidiwa..
 
Haziwezi kuwa sawa mkuu
Hatua Yako na Usain bolt haziwezi kufanana ,hivyo mkiwa kwenye speed sawa lazima atakupita sababu ya urefu wa hatua zake
Complete frequency of V8 will cover more distance than Passo's tire
Speaking from thought not experience
Kwa muktadha wako huu...... je una maoni gani kwa trecta lenye tairi dogo mbele na kubwa nyuma lakini tracta lina speed ilele?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…