TANZIA Patrick Mfugale wa TANROADS afariki dunia Jijini Dodoma

TANZIA Patrick Mfugale wa TANROADS afariki dunia Jijini Dodoma

Wewe endelea kujifariji nakwambia kama hutamsamehe yeyote kati ya wabaya wako hata Mungu hatakusamehe. Na ninakwambia usipende sana kushadadia mambo yasiyokuhusu bibilia inasema cheka na wanaocheka na lia na wanao lia.
ila kweli
 
Patrick Aron Nipilima Mfugale mhandisi tajwa nchini Tanzania na alikuwa mtendaji mkuu wa Mamlaka ya barabara nchini Tanzania TANROADS.

Injinia Patrick A. N. Mfugale RIP

=====

Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Injinia Mfugale amefariki Jijini Dodoma.

Mfugale jana aliondoka na ndege akiwa na Katibu Mkuu ujenzi kuelekea Dodoma kwa safari ya Kikazi

Amezidiwa leo saa tano asubuhi na kukimbizwa Hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma, Tanzania ambapo ndipo Mauti umemfika muda mchache baada ya kufikishwa.

Tutaendekea kuwapasha kinachoendelea.

Apumzike kwa Aman

Wasifu:
Alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Consalata Fathers Primary School mjini Iringa
-1975 Alimaliza elimu yake ya shule ya upili katika shule ya upili ya Moshi.
-1977-Mfugale aliajiriwa katika wizara ya ujenzi
-1983 alijipatia shahada yake ya kwanza katika chuo kikuu cha Rocky nchini India
-1991 Mfugale alisajiliwa kama muhandisi mtaalam.
-1992- Aliteuliwa kuwa mkurugenzi wa barabara za mikoa.
-1994-1995-Alipokea shahada yake ya pili katika chuo kikuu cha Loughborough, nchini Uingereza
-2003-Alipokea tuzo ya Distinguished Engineering Accomplishment.
-Aliteuliwa kuwa muhandisi mkuu wa madaraja nchini Tanzania wakati huohuo na akiwa masomoni nchini Uingereza mwaka 1995 alitafiti na kutengeneza mfumo wa madaraja nchini.
-Alitengeza mfumo wa usimamizi wa madaraja kwa jina Tanzania Bridge Management System
-2014- Alisajiliwa kuwa muhandisi mshauri na kuwa mwanachama wa chama cha wahandisi Tanzania.
-Ametumia muda wake mwingi kama mtaalamu wa madaraja .
Alibuni daraja la Malagarasi lenye mita 178 kwa shilingi za Tanzania milioni 300.
-Baadhi ya madaraja aliyoweza kusimamia yakakamilika kujengwa ni:
  • Daraja la Mkapa Rufiji
  • Daraja la Umoja linalounganisha Tanzania na Mozambique huko Ruvuma.
  • Daraja la Rusumo
  • Daraja la Kikwete huko Malagarasi.
  • Daraja la Nyerere huko Kigamboni
- Mfugale akiwa mtendaji mkuu wa Tanroads amesaidia ujenzi wa madaraja 1400 nchini Tanzania.
Amebuni na kusimamia barabara za kitaifa zenye urefu wa takriban kilomita 36,258.
  • Alikuwa Mwenyekiti wa kikosi cha ujenzi wa Reli ya kisasa SGR inayoendelea kujengwa.
  • Alikuwa mjumbe wa timu ya majadiliano ya miradi mikubwa ya umeme.
-2018 Alituzwa tuzo ya uhandisi ya Engineering Execellency

Picha: Daraja la Kikwete mto Malagarasi Daraja la Kikwete lililopo Mto Malagarasi
Mwendazake anawavuta wanawe aliokula nao ufalme wake
 
Mbona unaonekana una makasiriko sana na Mfugale? Una ugomvi nae binafsi Mkuu,tangu mwanzo unamsimanga tu,jamani tujifunze walau jinsi ya kudeal na stress zetu za maisha.Haya ameshakufa,unadhani itakupa ahueni ya maisha wewe binafsi?
[emoji21][emoji21][emoji21]Maisha sijui yanachanganya watu au roho mbaya!unakuta mtu anademkwa hata unashindwa kuelewa,kwamba daraja likiitwa mfungale sijui linamkwaza nini!




Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
 
Patrick Aron Nipilima Mfugale mhandisi tajwa nchini Tanzania na alikuwa mtendaji mkuu wa Mamlaka ya barabara nchini Tanzania TANROADS.

Injinia Patrick A. N. Mfugale RIP

=====

Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Injinia Mfugale amefariki Jijini Dodoma.

Mfugale jana aliondoka na ndege akiwa na Katibu Mkuu ujenzi kuelekea Dodoma kwa safari ya Kikazi

Amezidiwa leo saa tano asubuhi na kukimbizwa Hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma, Tanzania ambapo ndipo Mauti umemfika muda mchache baada ya kufikishwa.

Tutaendekea kuwapasha kinachoendelea.

Apumzike kwa Aman

Wasifu:
Alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Consalata Fathers Primary School mjini Iringa
-1975 Alimaliza elimu yake ya shule ya upili katika shule ya upili ya Moshi.
-1977-Mfugale aliajiriwa katika wizara ya ujenzi
-1983 alijipatia shahada yake ya kwanza katika chuo kikuu cha Rocky nchini India
-1991 Mfugale alisajiliwa kama muhandisi mtaalam.
-1992- Aliteuliwa kuwa mkurugenzi wa barabara za mikoa.
-1994-1995-Alipokea shahada yake ya pili katika chuo kikuu cha Loughborough, nchini Uingereza
-2003-Alipokea tuzo ya Distinguished Engineering Accomplishment.
-Aliteuliwa kuwa muhandisi mkuu wa madaraja nchini Tanzania wakati huohuo na akiwa masomoni nchini Uingereza mwaka 1995 alitafiti na kutengeneza mfumo wa madaraja nchini.
-Alitengeza mfumo wa usimamizi wa madaraja kwa jina Tanzania Bridge Management System
-2014- Alisajiliwa kuwa muhandisi mshauri na kuwa mwanachama wa chama cha wahandisi Tanzania.
-Ametumia muda wake mwingi kama mtaalamu wa madaraja .
Alibuni daraja la Malagarasi lenye mita 178 kwa shilingi za Tanzania milioni 300.
-Baadhi ya madaraja aliyoweza kusimamia yakakamilika kujengwa ni:
  • Daraja la Mkapa Rufiji
  • Daraja la Umoja linalounganisha Tanzania na Mozambique huko Ruvuma.
  • Daraja la Rusumo
  • Daraja la Kikwete huko Malagarasi.
  • Daraja la Nyerere huko Kigamboni
- Mfugale akiwa mtendaji mkuu wa Tanroads amesaidia ujenzi wa madaraja 1400 nchini Tanzania.
Amebuni na kusimamia barabara za kitaifa zenye urefu wa takriban kilomita 36,258.
  • Alikuwa Mwenyekiti wa kikosi cha ujenzi wa Reli ya kisasa SGR inayoendelea kujengwa.
  • Alikuwa mjumbe wa timu ya majadiliano ya miradi mikubwa ya umeme.
-2018 Alituzwa tuzo ya uhandisi ya Engineering Execellency

Picha: Daraja la Kikwete mto Malagarasi Daraja la Kikwete lililopo Mto Malagarasi
R.i.P ila huyu alikua anaonekana dhaifu kiafya nilihisi anasumbuliwa na ugonjwa usio wa kuambukiza
 
Nyerere hakupenda majina yake kutumika akiwa hai alisema ni uchuro.

Magufuli - Stendi, Daraja; Mfugale - tower, flyover; Kijazi - Daraja, Flyover.

Maneno ya Nyerere yanaweza kuwa na hoja.

Pale Dodoma napo pana soko nashauri jina kubadilishwa haraka.

Au nasema uongo ndugu zangu?
Nimechekaaa,kuna mtu hatalala leo akisoma ujumbe wako
 
Mfalme Daudi alipokuwa anaenda vitani na kuua maadui zake wengi hakua anafurahia vifo vyao?
Mtumishi ukisoma kitabu cha Samuel utajua ni kwa nini Daudi aliwaua wafilisti na mataifa mengine, Na ukumbuke ya kuwa mambo yote hayo yalifanyika ili kutimiza ahadi ya Mungu kwa wana wa Israel maana hayo yote Mungu mwenyewe aliyaruhusu yatokee kwa Muda ule laikini kwa sasa sisi tuliookolewa kwa jina la Kristo Yesu mwenyewe ni muhimu kumfata na ndo maana alisema samehe saba mara sabini na muuombee adui yako, wapendeni maadui zenu na pia alisema kisasi ki juu ya Mungu mwenyewe.
 
Nyerere hakupenda majina yake kutumika akiwa hai alisema ni uchuro.

Magufuli - Stendi, Daraja; Mfugale - tower, flyover; Kijazi - Daraja, Flyover.

Maneno ya Nyerere yanaweza kuwa na hoja.

Pale Dodoma napo pana soko nashauri jina kubadilishwa haraka.

Au nasema uongo ndugu zangu?
Majina yote ya watu yatolewe hakuna mtu aliyetoa pesa zake mfukoni kujenga hawa walifanya kazi zao walizokuwa wanalipwa. Tusipokuwa makini nchi nzima itakuwa majina ya watu. Nakubali viongozi tu wa juu kama ma Rais kuenziwa lakini sio tena leo Mfugale kesho Juma kesho kutwa Mwajabu bla bla bla... futa yote majina mengine nuksi kama Ndungai na soko limedoda kama mwenye jina.
 
Mtumishi ukisoma kitabu cha Samuel utajua ni kwa nini Daudi aliwaua wafilisti na mataifa mengine, Na ukumbuke ya kuwa mambo yote hayo yalifanyika ili kutimiza ahadi ya Mungu kwa wana wa Israel maana hayo yote Mungu mwenyewe aliyaruhusu yatokee kwa Muda ule laikini kwa sasa sisi tuliookolewa kwa jina la Kristo Yesu mwenyewe ni muhimu kumfata na ndo maana alisema samehe saba mara sabini na muuombee adui yako, wapendeni maadui zenu na pia alisema kisasi ki juu ya Mungu mwenyewe.
Kwa hiyo agano la kale kwa sasa hivi ni kitabu kisicho na maana?
 
Back
Top Bottom