Uchaguzi 2020 Paul Makonda, hawezi kupita Kigamboni kura za Maoni

Uchaguzi 2020 Paul Makonda, hawezi kupita Kigamboni kura za Maoni

Naona mlima mrefu Makonda kuukwea kupitishwa Kigamboni..

Kauli za Rais zimemlenga moja kwa moja, leo tena kauli za katibu mkuu CCM zimemlenga moja kwa moja na ukuu wa mkoa utakuwa ushaota mbawa.

Bila shaka kauli zake za madharau akiwatukana watu kwamba ingawa labda nimesoma na nyie, mna vyeo kuliko mimi na wengine mmenizidi umri ila nimewazidi sana hata boss wenu anatambua, hao hao watu ndio anategemea wampitishe, wengi CCM hawampendi.

Wote walioachia nafasi zao walizoteuliwa wanataka kuonyesha kwamba uwezo wa kushinda wanao, na wakuu wao wanaonyesha wazi kuwa prove wrong.

Muda upo tusubiri.

Wewe mwanaccm au mmbeya tu. Acha chuki fanya kazi.
 
Ndugai na Majaliwa - mmoja wao asubiri kuugulia maumivu tu endapo dogo atashinda ubunge.

asipokatwa halafu akashinda ubunge, ataukwaa uspika au nako akifanyiwa figisu na wabaya wake chamani basi babake atampa u PM lazima.

akikatwa ubunge, babake atamteua viti maalumu na kumpa portfolio ama ya home affairs ama ya defence ama atamrejeshea u RC wake.

Bashite asingeweza kuacha u RC bila ya kwanza kuchanga karata zake vyema na babake. huyu dogo as long as babake yupo madarakani, ni bata batani kwa kwenda mbele!

Tatizo unaandika ukiamini unamjua JPM kuliko anavyojijua. Makonda aliteuliwa ukuu wa Wilaya na JK. KIKWETE.
 
Huyu hata hajui kuwa Makonda alikuwa team Membe kindakindaki.
Ndugai arudi bungeni keshatumika ametupwa, bashite ndie spika ajae na gambo ndie waziri wa Mambo ya ndani ili wawashughulikie wapinzani
 
Yule kala Pete ya Simba...hakuna wa kuthubutu kutoa jina..

Nguvu za kiza zina nguvu msisahau
Ina maana wajumbe wa kamati wataulizana "kaah huyu kapitaje?" au...
Nchi ya mauzauza...
 
Kuna mjumbe asimpigie Bashite kura kweli ?Bashite ana pesa bwana,na hajakurupuka. Akishinda kura wakamkata basi atamfuata Membe ACT.
Akishindwa atapewa ubalozi wa chaguo lake!! Huyo ni mchapa kazi na mpambe namba moja wa ofisi namba moja!! Ni maandalizi ya kuomba ofisi namba moja mwaka 2025! I may be wrong but most probably I am right!
 
Hawezi kukatwa labda itokee miujiza
Hivi watu walitegemea kuwa aseme ndiyo Kuna watu nimewatuma? Katika Hali ya kawaida, lazima mkuu ana timu anayotegemea kuanza nayo! Maandalizi ya timu hiyo ni kuhakikisha wanapata ubunge Kwanza! Mkubali msikubali japo si wengi lakini nadhani wapo waliotumwa ila ni wachache Sana!! Hata kutumwa mwenyewe ni indirectly!! Japo wengi wanaodai wametumwa ni waongo!! Aliyetumwa kiukweli hawezi kusema kuwa nimetumwa!!
 
Lazima atapita kule labda wamkate kura za maoni
Kiukweli kabisa, Makonda ana uwezo mkubwa sana na Ni mbunifu Sana, na bila shaka atapitishwa na hatimaye atapita!! Wana kigamboni Lulu hiyo inakuja! kaeni mkao wa kula!! Makonda Ni Lulu!!
 
Nyie mnanichekesha kweli...Bashite ataingia bungeni kama sebuleni kwake

Whether wakate jina nor kuiba kura yaan vyovyote hata kwa kupaa na ungo, mjengoni lazima aingie!

Hizi storee zingine ni changamsha genge tu
Kunywa konyagi kubwa nitalipia nusu bei
 
Rushwa inatembea kama kawaida kwa mfumo wa tigo pesa m-pesa kwa namba ambazo siyo zake

Hivi unamlinganisha na nani kati ya waluochukua fomu? Akina Mpoki? Au X MP? Kuongelea ushabiki sawa, lkn uhalisia sio huo, Wanakigamboni wanachotaka ni JEMBE LA KUTUMIA INFLUENCE NA MISIFA ALIYONAYO, KUTUKIMBIZIA MAENDELEO YA KIHAMBONI. Wanakigamboni tunamsubiri kwa hamu
 
Sio wote waccm wanamchukia, baadhi yao tu tena wanadaresalama kisa msukuma/mchapakazi na anasaidia wagonjwa, walemavu n.k

Navyojua pale kapelekwa makusudi kugombea ubunge na atapita tu ili iwe njia rahisi kupewa uwaziri, Magu anaakili nyingi, anaona mbali huyu mzee.

Makonda usibabaishwe na watu wachache,
Yaan anakili nyingi za double standard....upendeleo.Duuuh ama kweli lumumba ni kisiwa cha mazombie
 
Anaachaje sasa akati alitumbuliwaa na mzee baba.. Alafu ndugulile hajui kusifu na kuabudu kabisa. Toka atumbuliwe kimyaa sio kama kina Nape na Mwigulu au Gambo yani full kujikombaa kwa Stone ili wapate kulaa
Kwani amechukua naye form?
 
Hivi zaidi ya Mpoki nani mwingine amechukua fomu huko Kigamboni?!
Angalia hii list[emoji116]
*WALIO CHUKUA FOMU KURA ZA MAONI JIMBO LA KIGAMBONI*

1-Winifrida Shonde,
2-Frank Chalamila
3-Kassim Juma
4-Edwin Kweshijabo
5-Christian Hall
6-Daniel Sarungi
7-Ally Malima
8-Januari Kimanywa
9-Wande Kasaja
10-Kwesi Ukwaju
11-Dk. Faustine Ndungulile
12Lilian Wassira
13-Eliudi Mganga
14-Sogone Wambura
15-Mujuni Mwajauki (Mpoki)
16-Christopher Sauti
17-Daniel Madushi
18-Deogratous Kanyesa
19-Ramadhan Abdallah
20- *paul_christian_makonda*
21-Emanuel Lyimo
23-22-Rajabu Gundumu
24-Buimura Mboja
25-Winifrida Shonde
26-Denis Kalikawe
27-Thaddeus Musembi
28-Themis Rwegasira
29-Rashid Jumbe
30-Ally Msaki
31-Francis Mugisha
32-Jovin Sanga
33-Fredrick Mumba
34-Dk. Benjamin Mohamed
35-Dorit Glorious
 
Anaachaje sasa akati alitumbuliwaa na mzee baba.. Alafu ndugulile hajui kusifu na kuabudu kabisa. Toka atumbuliwe kimyaa sio kama kina Nape na Mwigulu au Gambo yani full kujikombaa kwa Stone ili wapate kulaa
Ila yupo na mtoto pendwa sijui kama atatoboa!! Mwanamme kulamba viatu ni Uboya bora alivyokaza!!
 
Ila yupo na mtoto pendwa sijui kama atatoboa!! Mwanamme kulamba viatu ni Uboya bora alivyokaza!!
Hatoboii mzeee...!! Ukitaka kujua Stone anaongeaga kinafiki tu mzee kuna yule mama wa kibaha sijui mkuu wa wilaya alimkosoa Bashite kuhusu swala la kuwaambia upinzani waliopo Dar kipindi kile jamaa wapo Qurantine kuwa wareport kwake kuwa ni Kauli ya ovyooo sana watu wakasema huyu mama kapata wapi nguvu ya kumkosoa Bashite. Dadeki juzi katumbuliwaaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Mapenzi ya baba kwa mwana hayapimikiii muulize Nape.
 
Back
Top Bottom