Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Mm simkubali sana sa100 ila kwa kauli chafu alizotoa kwa rais ambaye mm namuona kama mama kwa kweli kakosea na huyo mpuuzi mange ana wadhalilisha sana watu hana adabu hivi tunataka aje amtukane nani na kumdhalilisha nani ndo tutamchukulia hatua.
 
He is just a populist. Nothing more.

Ametatua shida gani za wananchi? Nipe mfano?
Alipokuwa,mwenezi CCM,tumeshuhudia alivyokuwa kimbilio la wananchi kwenye ziara zake [mikoa tofauti],jinsi alivyokabiliana na changamoto zao kwa kuwabana viongozi/watumishi wavivu, miungu watu,mafisadi,dhulumati n.k.na baadhi yao walipatiwa suluhisho hapohapo [kitu ambacho Samia S.H.hajawahi kufanya na hawezi],alipokuwa mkuu wa mkoa Dar es salaam alidiriki kutenga siku 2 za wiki,maalum kwaajili ya kuwasikiliza wananchi[malalamiko na kero zao]ofisini kwake.
 
..mbona Uvccm wanatukana viongozi wa upinzani matusi makubwa kabisa na watu wanavumilia?

..Rais aonyeshe uvumilivu na ukomavu kama kiongozi.

..Mtu huyuhuyu alimsingizia mwenzake ugaidi na akamfunga kwa miezi minane, leo kasemwa kidogo analialia.
Hivi alisingiziwa ugaidi ama Mahakama ilimkuta na kesi ya kujibu halafu “Serikali kupitia kwa DPP ikaamua kuachana na kesi?

Kwanini alitoka gerezani na kwenda moja kwa moja Ikulu kuzungumza na Rais? Walizungumza nini?

Viongozi wa upinzani wanaotukanwa na wanavumilia ni kwamba wameamua kuvumilia kwa sababu sheria ziko wazi kwanini wasiwawajibishe watukanaji wao?
 
Kwema Wakuu!

Usijeleta u-serious wako uwapo mbele ya Watanzania. Mambo ya akili mingi watanzania hawayataki, mambo ya kweli watanzania sio Wafuasi wake.

Ndio maana kijamii sio ajabu ukawakuta Watu kama kína Mwijaku, Dotto Magari, Piere Liquid, kina Mange Kimambi, na wengineo wakiwa na influence ndani ya jamii ya Tanzania.

Watanzania wanapenda udaku, habari za uongouongo na uzushi, habari za kufarakana na kufarakanisha, umbeaumbea. Habari za connections za video za ngono ndio watanzania wanazozipenda.

Habari za usimba na Uyanga, udiamond na ualikiba. Ndio mambo yenyewe hayo.

Niliwahi andika makala fulani miaka kadhaa nyuma kuwa úkitaka kutoka na kufanikiwa hapa Tanzania, Basi wekeza kwenye mambo ya ujingaujinga.

Watanzania wengi kwenye ujinga hawahitaji Usimamizi mkubwa. Wataufanya kwa kiwango kizuri na kikubwa utakachokipenda.

Makonda na uongozi wa Tanzania unajua wananchi wa Tanzania wakoje na wanataka nini.

Asije akakudanganya mtu kuwa watanzania wanataka Katiba mpya. Nop!
Asije akakudanganya mtu watanzania wanahitaji sijui Maendeleo, nop!
Hilo sio hitaji la msingi la Watanzania.

Watanzania wengi wanahitaji furaha, na furaha ya ni kusikia habari za udaku, uongouongo, habari mbaya za Watu wengine.

Ukiwa mzuri kwenye drama hapa Tanzania wewe ni Lulu na soko lako ni kubwa mno.

1. Ukiwa mwanasiasa jifanye unakoromea wanasiasa wenzako. Wachimbe mkwara hadharani na jifanye unaweza kuwaweka ndani la wasipofuata maelekezo yako

2. Jifanye unasakwa kwa udi na uvumba ili uuawe na ushategewa mitego, mabomu, na sumu ili uuawe kwaajili ya kutetea wananchi.

3. Jifanye unasikiliza matatizo ya Watu. Watanzania wengi wanapenda danganya Toto.

4. Sema upo tayari kwa lolote ikiwezekana kufa kwajili ya wananchi.

5. Vunja sheria na katiba ya nchi kisa kutatua mgogoro unaotokana na kuvunjwa kwa hizohizo sheria.
Watanzania wengi sio Watu wa kuheshimu utaratibu, kanuni na sheria.
Ukiwa mtu wa sheria na taratibu na kujifanya unafuata kanuni upo kwenye hatari ya kuchukiwa na watanzania wengi.
Watanzania wanachojali ni kusaidiwa matatizo yao bila kujali sheria imefuatwa au laah! Hii ni kutokana na tabia ya ubinafsi.

6. Ita viongozi wa dini jifanye ni marafiki zako.
Hii itakufanya watanzania wakuone wewe ni mtu mwema na mpenda Mungu. Jambo ambalo wewe mwenyewe unajijua sio kweli.

7. Penda kuwabughudhi wenye vipato ikiwemo wafanyabishara na hakikisha unawatolea maneno ya vitisho mbele ya kamera na wananchi.
Watanzania wengi hujisikia furaha pale wanapoona wale Watu waliowazidi wakibughudhiwa.

Kamwe ukiwa kiongozi kama unataka umaarufu na kupendwa na wananchi wa kitanzania waliowengi jiepushe kuwa karibu na wenye uwezo na vipato.

Wachezee watanzania kekundu, mchana upo nao alafu usiku wakienda kulala unaenda zako kwa wenye navyo.

8. Watanzania huamini maneno mabaya zaidi kuliko mazuri.
Ukitunga propaganda ya ubaya wa mtu hasa mwenye kipato ni rahisi kwa watanzania waliowengi kuipokea na kuiamini.

9. Usisahau, watanzania wengi yaani asilimia kubwa ni majizi na hawana shukran. Vyovyote utakavyo wasaidia elewa kuwa kama utakuwa unaishi kweli yale uyasemayo yaani Haki kwelikweli na ukawa maskini ndio watakao kuwa wakwanza kukucheka na kukubeza.

Hao wenye Akili ni wachache mno. Na hakuna tija kisiasa kuwa upande wa Watu wachache. Hivyo tumia mbinu kulingana na wingi wa wahusika katika eneo ulilopo.

Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mtoa mada umesahau kuamini waganga/kurogwa,kutoana mapepo,miujiza,maji ya upako,Imani za dini za kitapeli na kuombewa .

Watu wanategemea maendeleo yatoke kwenye hayo mambo 😂😂😂😂
 
Alipokuwa,mwenezi CCM,tumeshuhudia alivyokuwa kimbilio la wananchi kwenye ziara zake [mikoa tofauti],jinsi alivyokabiliana na changamoto zao kwa kuwabana viongozi/watumishi wavivu, miungu watu,mafisadi,dhulumati n.k.na baadhi yao walipatiwa suluhisho hapohapo [kitu ambacho Samia S.H.hajawahi kufanya na hawezi],alipokuwa mkuu wa mkoa Dar es salaam alidiriki kutenga siku 2 za wiki,maalum kwaajili ya kuwasikiliza wananchi[malalamiko na kero zao]ofisini kwake.
Acha maneno jibu swali ametatua changamoto gani???

Yale yalikuwa maigizo tu kama maigizo mengine kuwarubuni watu msio na akili kama wewe.
 
Em ngoja tuone kunakuchaje...
Huyu Makonda akisurvive next 12 hrs..

Basi hatuna Nchi.
Ni kweli mkuu ikifika Jumatatu tarehe 15/04 kama Makonda atemdelea kuwa RC Arusha basi, nchi yetu itakuwa ya HOVYO
 
Hivi alisingiziwa ugaidi ama Mahakama ilimkuta na kesi ya kujibu halafu “Serikali kupitia kwa DPP ikaamua kuachana na kesi?

Kwanini alitoka gerezani na kwenda moja kwa moja Ikulu kuzungumza na Rais? Walizungumza nini?

Viongozi wa upinzani wanaotukanwa na wanavumilia ni kwamba wameamua kuvumilia kwa sababu sheria ziko wazi kwanini wasiwawajibishe watukanaji wao?

..mimi nilifuatilia ile kesi na nimeridhika kwamba ilikuwa kesi ya uongo na hila mbaya dhidi ya Mbowe.

..Na kama kweli Mbowe ni gaidi kwanini Dpp aliondoa kesi? Vilevile kwanini Rais alimkaribisha gaidi Ikulu?

..wanaotukana wapinzani ni viongozi wa Ccm, na serikali. Wengi wao ni wateule wa Rais wa Jamhuri na Mwenyekiti wa Ccm.

..Sasa tunajiuliza, kwanini Rais anateua watu wenye lugha za matusi na udhalilishaji?

..Malalamiko kwamba Rais anatukanwa yana maana gani ikiwa yeye mwenyewe ameteuwa ktk serikali na chama watu wenye rekodi za kutukana na kudhalilisha?
 
Endelea kujifariji.

Bongo nyoso, Makonda na hao ccm wanawin akili za watu wa kipato cha chini ambao ni wengi na wengi wao ndo hao hufuata mkumbo, hawana source tukuka za habari zaidi ya hizo ambazo zinaendeshwa na hao hao.

Hao unaoona ni werevu ni wale ambao ni wafukunyuku, wapenda kusomasoma vitu na hawajabase kwenye source moja kupata habari.

Kuna watu Millard Ayo asipopost habari yoyote basi hawaiamini, wao mtandaoni ni Millard Ayo.
Wengine ITV , wengine TBC yaani hao hiyo source yake ilichokipost ndo hicho anakibeba na kukiamini wala hakifanyii tathmini yoyote.

Srma Makonda anawin watu wa akili ndogo. Siyo wote wenye kipato cha chini wana akili ndogo.
 
..mimi nilifuatilia ile kesi na nimeridhika kwamba ilikuwa kesi ya uongo na hila mbaya dhidi ya Mbowe.

..Na kama kweli Mbowe ni gaidi kwanini Dpp aliondoa kesi? Vilevile kwanini Rais alimkaribisha gaidi Ikulu?

..wanaotukana wapinzani ni viongozi wa Ccm, na serikali. Wengi wao ni wateule wa Rais wa Jamhuri na Mwenyekiti wa Ccm.

..Sasa tunajiuliza, kwanini Rais anateua watu wenye lugha za matusi na udhalilishaji?

..Malalamiko kwamba Rais anatukanwa yana maana gani ikiwa yeye mwenyewe ameteuwa ktk serikali na chama watu wenye rekodi za kutukana na kudhalilisha?
Wewe ukijilidhisha kwamba kaonewa hiyo inatosha kubadili msimamo na maneno ya Mahakama? Wewe ni nani?

DPP aliondoa kesi kwa niaba ya Serikali, tujiulize mimi na wewe kwanini?

Na Mimi nimekuuliza kwanini alitoka Jela na kwenda moja kwa moja Ikulu kuzungumza na Rais ambae Serikali yake kupitia Mahakama ilimkuta na kesi ya kujibu? Walizungumza nini?

Mtu kuwa mteule wa Rais na Serikali yake haina maana kwamba Tabia zake za hovyo ni wajibu wa Rais, awajibishwe huyo mtu kwa mujibu wa sheria na taratibu kinyume na hapo sympathy is for cowards.

Kwamba Rais anafanya makusudi kuteua watu ili wawatukane upinzani? Hao upinzani ni wajinga kiasi gani hawajui njia ya kufuata kuwawajibisha wakosaji wao?

Hiyo aya ya mwisho ni hoja kabisa kutoka kwako ama unatania? Kwamba Rais anapoteua anajua kabisa huko mbeleni mdomo wako utageuka choo Kwahiyo anafanya kusudi?
 
Wewe ukijilidhisha kwamba kaonewa hiyo inatosha kubadili msimamo na maneno ya Mahakama? Wewe ni nani?

DPP aliondoa kesi kwa niaba ya Serikali, tujiulize mimi na wewe kwanini?

Na Mimi nimekuuliza kwanini alitoka Jela na kwenda moja kwa moja Ikulu kuzungumza na Rais ambae Serikali yake kupitia Mahakama ilimkuta na kesi ya kujibu? Walizungumza nini?

Mtu kuwa mteule wa Rais na Serikali yake haina maana kwamba Tabia zake za hovyo ni wajibu wa Rais, awajibishwe huyo mtu kwa mujibu wa sheria na taratibu kinyume na hapo sympathy is for cowards.

Kwamba Rais anafanya makusudi kuteua watu ili wawatukane upinzani? Hao upinzani ni wajinga kiasi gani hawajui njia ya kufuata kuwawajibisha wakosaji wao?

Hiyo aya ya mwisho ni hoja kabisa kutoka kwako ama unatania? Kwamba Rais anapoteua anajua kabisa huko mbeleni mdomo wako utageuka choo Kwahiyo anafanya kusudi?

..Sawa.

..Wapinzani wanatukanwa.

..Raisi anatukanwa.

..Ngoma droo!!

..Kazi iendelee.
 
Hivi alisingiziwa ugaidi ama Mahakama ilimkuta na kesi ya kujibu halafu “Serikali kupitia kwa DPP ikaamua kuachana na kesi?

Kwanini alitoka gerezani na kwenda moja kwa moja Ikulu kuzungumza na Rais? Walizungumza nini?

Viongozi wa upinzani wanaotukanwa na wanavumilia ni kwamba wameamua kuvumilia kwa sababu sheria ziko wazi kwanini wasiwawajibishe watukanaji wao?
Kama naanza kukuelewa kwa karibu sana,Mbowe ni masta maind wa kasikazini,ni mpangaji wa matukio na sio matukioa madogo,Kama lile la kusema kapigwa kumbe alilewa akaanguka kwenye Ngazi akaumia mguu!!!!
 
Back
Top Bottom