Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Mtu anaambiwa huwezi kuvuka kwenye hayo maji ni mengi halafu analeta ubishi kisa tu kavuta mibangi yake ya Arusha,matokeo yake analeta maumivu kwa familia hakupoteza uhai wa malaika na watoto wasio na hatia na wasioolewa kitu wala kuwa namaamuzi wala uwezo wa kujiokoa. Baadhi ya Vijana wa Arusha wajinga sana. Bangi zinawapeleka kubaya sana.
waliokufa ni aliyetumbukiza gari au malaika wale? niambie wapi Makonda katoa hata pole? Waganga wa kienyeji hawa mtakufa mdomo wazi! mazindiko kila mahali
 
Jana nimeona kikao baina ya RC Makonda na wafanyabiashara wa hotel na TRA na tours. RC kauliza vitu vingi na kashangaa iweje mzungu atoke Ulaya aje kulala badala ya kutalii.

Napenda nitoe ushauri, wakati fulani tulisoma kozi na serikali ya China katika hizo kozi kuna kitu kinaitwa Night tourism, hapa maeneo mengi nchini China utalii unafanyika mpaka usiku. Mfano private tours at night in the city, museums.

Kuna maeneo unapata local food usiku mzima, wenzetu wana utalii wa mito sio kama sisi mito yetu yote tumekonect maji taka.

Kwa Arusha ili jiji liwe vibrant ni lazima shuguli za utalii ziwe 24hrs. Wengine wanapenda kwenda museums usiku pametulia, uliza Arusha kuna Museum inayoeleweka?

Mtalii anaweza kutaka local foods at night je zipo sehemu hizo? Usalama je? Naamini watu wa Arusha wanaelewa utamu wa hela ya mzungu kama mazingira mheshimiwa atapambana kuyaweka sawa jamaa watapiga kaz.

Nimemskia yule jamaa kichwa Chambulo anasema kalipa mil 23 kapewa risit ya mil 3. Yule ana ideas nyingi za kuhakikisha mzungu anabakiza nauli tu ya kurudi kwao. Hapo Arusha itapaa kiutalii.

TTB pale nothing creative nothing no museums hakuna tradition wataalam wamekaaa hata huko Dodoma kukimbiza madokezo ya poshoook tu.
MAKONDA AMESEMA HAITAJI USHAURI AU KUJIFUNZA YEYE ANAJUA KILA KITU HATA MGOGORO UKIWA MAHAKAMANI YEYE ANAUTATUA
 
Huenda ww sio mwanasiasa kweli , lakini hili ni jukwaa la siasa, hivyo tegemea michango iliyo kisiasa. Sina tatizo sana na asemacho Makonda, tatizo langu lipo kwenye utekelezaji. Makonda angeingia kwenye utekelezaji kuhusu hayo awazayo maana tayari mapendekezo ya hayo yapo. Hii kuita wafanyabiashara ni michezo ya siku zote isiyo na utekelezaji. Hata Magufuli aliwaita hao wafanyabiashara, lakini story zimebaki ni hizo hizo. Na kesho kutwa ataondoka Makonda, kisha atakuja RC mwingine, na story zitakuwa hizo hizo.
Mimi na wewe tumetimiza wajibu wetu ..muda ni mwamuzi.
 
Ili jipu , ila mda ni mwalim mzuri , wapo watu nchi wanayafanyia ma kubwa tz kama nchi na wametulia tuli , sasa huyu nikujifanya Kambare , ikumbukwe amewahi mkwida mzee Warioba , Mungu halali haijalishi ni nani ila mda utajibu
Upo kwenye malalamiko tu Makonda yeye anachapa kazi. Dawa ni kuachana naye ufanye mambo mengine
 
Makonda anapaswa ajue, mtalii anayekuja Afrika anakuja kwa ajili ya kufanya vitu vichache tu ambavyo kwaoo hakuna...

1. Kutazama vivutio vya asili ambavyo ni wanyama na mandhari...

2. Utamaduni na maisha ya wanadamu wengine ambao bado wanaenzi tamaduni za asili kama Maasai...

3. Kukwepa msimu mkali wa baridi kaskazini mwa dunia...

4. Ni utamaduni kwa wenzetu kufanya utalii au kupumzisha mwili na akili...

Ijulikane ya kwamba hakuna mtalii anayekuja Afrika kutaka kula bata la usiku, kwa sababu huko kwao ni salama zaidi kufanya hivyo zaidi kuna nchi ambazo ni maarufu kwa utalii wa usiku kuliko Afrika...

Kwenye bata la usiku ni bora mzungu aende zake Vegas, Bora bora, Dubai, Bangkok n.k mahali ambapo walau kuna usalama nyakati za usiku...

Afrika ili tuendelee tunapaswa kuacha kukumbatia UJINGA
Akili yako inaona haiwezekani tuwaache wanaoona inawezekana wafanye.
 
Naona anazunguka tu mbuyu, mtalii anapokuja Arusha anajua nini anakuja kufanya, na anaweza kwenda popote muda wowote, tatizo kubwa ni hapa;

1. USALAMA DUNI
-Matukio ya uharifu mdogo mdogo na makubwa ni mengi kupita maelezo huko mitaani.
-Maeneo mengi usiku ni giza, hakuna taa za barabarani, mitaani, maeneo ya wazi, maeneo ya umma.

2. UCHAFU KUPITILIZA
-Barabara chafu
-Mitaro imeziba na imejaa uchafu
-Masoko machafu
-Migahawa michafu
-Vyoo vya umma vichafu
-Chemba za maji taka ziko wazi na kutiririsha maji machafu na vinyeji hadi katikati ya jiji.

3. USTAARABU DUNI
-Bei za bidhaa na huduma zimejaa ubaguzi na ujanja ujanja mtupu (Kuna bei za mtanzania na kuna bei za mtalii, Why? Mnadhani kuna mtalii anapenda huo ubaguzi wa wazi?)

-Viwango vya huduma na bidhaa ni duni kupita maelezo. (Yaani mpaka leo bado watoa huduma na wauza bidhaa wanashindwa kuweka price tag, bei zinatolewa mdomoni kwa kukuangalia rangi ya ngozi yako, umevaaje, unaongea lugha gani nk)

-Mipango miji mibovu. Yaani biashara na huduma zimetandazwa chini barabarani kila mahali.

-Urasimu (ni rushwa tu) umejaa kila kona, kuanzia barabarani kwa matrafiki (yaani wanaweza kukusimamisha bila kosa, wakakuweka zaidi ya robo saa barabarani kutafuta kosa), airport nk.

4. MIUNDO MBINU MIBOVU
-Mvua kidogo tope kila mahali
-Jua kidogo vumbi kila kona
-Barabara nyingi hazina mitaro, mvua ikinyesha kidogo hazipitiki
-Mitaa haina vibao, barabara hazina vibao.

Sasa warekebishe hizo mambo halafu uone kama kuna mtalii atakwepa kuja Arusha.
 
Mtu atakae sifa huwa yupo tayari afanye lolote hata kama litaumiza watu ili akusanye sifa.
 
Kwahiyo huyo kwenye picha anayevuja damu ndio nani? Hapo anaambiwa nini?


Mtoa mada julaibibi uko sahihi, mtalii hatakiwi kulala akikanyaga ardhi ya Tanzania ni party after party mpaka siku ya kurudi kwao.

Bahati mbaya Arusha ikifika usiku machalii wa hovyo wanatake over mamlaka.
Hao machalii wapotezwe watakoma tu.

Sent from my Infinix X656 using JamiiForums mobile app
 
Ila CC TANAPA kadhalililka sana kwenye kile kikao
 
Makonda alikuwa kwenye kikao na wadau wa utalii pamoja na menejimenti ya TANAPA.
 
Back
Top Bottom