Pendekezo: Dr Edwin P. Mhede ateuliwe kuwa waziri wa Fedha

Pendekezo: Dr Edwin P. Mhede ateuliwe kuwa waziri wa Fedha

Unampigia debe anko,kwa iyo Kati ya Watanzania milioni 60 yeye ndo anafaa tu.
Nonsense
 
Unamfahamu vizuri Prof. Assad?

Unafahamu CV yake na uzoefu alonao?

Kwa taarifa yako jamaa yuko vizuri sana.

Kama kuna mengine useme lakini kuhusu akili jamaa ni Mzamivu na Mbobezi haswa .
Assad ni mwalimu wa book keeping hajui uchumi, na umri na haya makorona atafia ofisini tu kama wenzie
 
Aje mtu atakayeweza kutuambia kwa nini sisi tuende kuhemea Kampala?Ina maana Kampala ndiyo mjini?

Au kwa nini vitu vyovyote ukikosa Tanzania lazima uende Nairobi na unavipata?
Kwa nini Nairobi iwe ndio mjini kuliko Dar?

Aje mtu atwambie zaidi ya mazao ambayo tunauza kwa bei ya chini sana,waganda na wakenya wanakuja Tanzania kununua nini?

Wasomi wetu kwa nini haya mambo huwa hayawaumizi kichwa na kila siku ndio tunawaamini katika nafasi za uongozi?
TRA kazi yake ilikuwa kukusanya kodi sio ku formulate polices, tukimpa wizara utaona uchumi utakavyo changamka, kule UDART tayari keshaingiza magari sabini na bado kuna drawing plan kibao mezani, sio huyu jamaa anaekimbizana na vimiamala vya "nitumie nayakutolea"
 
Katika kusoma uhasibu na Uchumi huwa ni sehemu muhimu ya kozi inayosomwa.

Mtu alosoma uhasibu au fedha huwa anasoma na uchumi pia.
Ansoma kiasi kidogo sana yaani managerial economics au some issues of micro economics. Evonomists wenyenye wanasoma mpaka game theoriea ambapo huo ndo uchumi. This world is controlled or governed on game basis
 
Toka enzi za wakina Dk Yona sipendi Hawa PHD'S holders kuwa na vyeo vya kisiasa ovyo kabisa...
 
Hiki kindumbwendubwe cha mpesa kimeonyesha uwezo mdogo wa waziri wetu wa fedha. Kiukweli huyu kakayangu kapwaya kwenye viatu kwa Dr Mpango.

Nilitamani Mpango arudi lakini kwa nafasi aliyonayo itakuwa kumshusha hadhi. Mie napendekeza Dr Edwin P. Mhede ateuliwe kuwa waziri wa fedha, huyu ni "Man of absolute integrity" eti kusema alikuwa ana kusanya kodi kinguvu jamani tuache masihara hawa wabongo bila kuwakomalia kodi hupati, situnajuana.

Qatar usipolipa kodi wanakata kichwa ndio maana wanapiga hatua kubwa na hawana mafuta kama Saud Arabia.
Usitowe mfano wa qatar na Tanzania tatizo Tanzania hiyo kodi ambazo watu wanalipa hazionekani maslahi yake wanalipana wao maposho na safari za kila siku ukenda hospitali hakuna dawa mtu akiumwa atangaze kwenye mitandao TV apelekwe na wasamaria wema akatibiwe india au hata muhimbili anatakiwa alipe ili atibiwe bila ya hivyo ataachwa afe wakati wao na wanafamilia wao wanapelekwa matibabu nje kwa kodi zetu huko qatar unakosema wananchi wanatibiwa bure na wanalipwa vizuri na elimu bure na kama huna kazi unasaidiwa mafao kwa hivyo kulipa kodi c tatizo hata kidogo.
 
Back
Top Bottom