Pesa nyingi ninazopata kwenye Freelancing zianaishia kuwalipa vijana wanaonisaidia kufanya kazi. Hii level inaitwa dropservicing

youngkato

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
3,319
Reaction score
3,097


Pesa nyingi ninazopata kwenye Freelancing zianaishia kuwalipa vijana wanaonisaidia kufanya kazi. Hii level inaitwa dropservicing

Nitakuelekeza mambo muhimu ya kuzingatia ili uweze kufanya dropservicing... Pia ukitaka kufanya freelancing zingatia haya

Kwanza kabisa lazima uanze kama freelancer wa kawaida. Ili ujifunze utaratibu wa Freelancing ulivyo kuanzia kwenye kutafuta clients, kufanya kazi, kupokea malipo.

Unaweza ukaanza na freelancing platforms kwa ajili ya kupata experience. Experience + portfolio

Kwanza kabisa, kufanikiwa kwenye Freelancing ili ufanye dropservicing
Jifunze kutafuta clients wengi na kazi nyingi

Kuna njia nyingi sana za kutafuta clients, (tumia zote) Ni rahisi sana kutafuta clients. Kwasababu kuna soko kubwa sana na watu ni wengi sana wa kufanyia kazi

Njia nyingine lazima ujue kutengeneza offer zenye rate kubwa. Ili kufanya dropservicing lazima ujue kuchaji pesa kubwa ili uwapatie wengine wazifanye.

Offer zinatengenezwa kwa kutuma proposal na kutengeneza project gigs. Jifunze offer creation Kitabu kinaitwa mafia offer

Ukichaji bei kidogo, utapata clients madalali wanakupa kazi nyingi ila malipo kidogo sana na mara nyingi hawapo serious

Ukichaji bei kubwa unapata clients wachache wenye bei nzuri pia wanakuwa serious na kazi zao. Ni rahisi ku outsource kazi zao ukabaki na pesa

Fanya kazi na team bora, ukimpatia kazi kijana wa chuo anakwambia umpe pesa ya bundle, atakwambia umeme umekata, atakwambia ana tes, au atakaa kimya deadline ikifika anakwa sory nilikuwa bize😅 Tafuta watu professional

Njia nyingine rahisi ni unatafuta clients wako wanaolipa vizuri. Unaingia Fiverr, unachukua freelancer wahindi, na wafilipino wa bei ndogo wanakufanyia kitu kizuri sana.

Tafuta kazi kulingana na niche yako, usikimbilie kila kazi. Mfano mimi nimewafundisha vijana wangu niche ya blockchain. Kwahiyo focus yetu ni kazi za blockchain peke yake.

Hii inatusaidia kupata kazi za pesa nzuri na kujitofautisha na wengine wanaofata mkumbo.

Degree, certificate, website, utaalamu wako hautakuletea wateja / clients hautakusaidia
Focus na marketing, sales, kutafuta wateja. Matokeo yatajionesha

Skills za muhimu ni marketing, sales, offer creation, clients retention, project management

Freelancing ni rahisi sana ukiweza hizo skills
 
Kuna kitu unataka kusema halafu ukitaka kukisema unaogopa. Au pengine huna uhakika na hadhira yako.

Muhimu: ➡️➡️➡️ Freelancing inataka uvumilivu sana na ujifunze ujuzi wa eneo lako bila kuchoka. Usiwe na papara wala tamaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…