Picha adimu za TANU, Julius Nyerere na wazalendo waliosahaulika katika Historia ya kudai Uhuru

Picha adimu za TANU, Julius Nyerere na wazalendo waliosahaulika katika Historia ya kudai Uhuru

Osaka,
Huna haja kufadhaika wala kushangaa wala hakuna mwanga hapana
atakae kufukua makaburi.

Ni jambo jepesi.
Mie naandika historia ya
wazee wangu.

Imekuwa bahati mbaya sana kuwa baadhi ya watu
historia hii inawafadhaisha.
 
BigBro,
Katika kitabu changu sehemu ya mwisho nimejaribu kueleza wapi
misingi ile imara ilipovunjwa.

Kipate kitabu usome.
 
Duuh !! Mkeka ndo carpet..?!!
Aisayee Wanawake kumbe wali PLAY ROLE ya kikubwa !!!?!!
 
Unamaanisha Tanu ya Nchi nzima ama Dar es salaam Wing na maeneo yaliyokuwa na Waislam wengi?

"Tanu ya Nchi nzima" imeanzia wapi?

Tuwekee wewe TANU ya mikoani ambayo haijakuwa na waanzilishi Waislam.

Hebu soma historia ujuwe kuwa harakati za TANU za awali zilisambazwa nchi nzima kupitia Tarika za Waislam na si vinginevyo.

Kama una historia ya TANU awali kusambazwa nje ya Dar (kokote pale) vingine, tafadhali tuelimishe, hatutaki uandikie mate na wino upo.
 
Kuna Magreat thinkers humu Nguruvi3, Mag3, Jasusi, Mzee Mwanakijiji na wengineo walikuwa wanabainisha kuwa wewe unachoandika siku zote ni Histohisia na wala sio Historia, maana umeandika kitu bila kuwa na dta na utafiti wa kutosha, Huwezi kuwa unasimamia kisa cha Mshume Kiyate na ukamsahau Bwana Ally Masham, inaonekana hilo tawi lilikuwa active sana lakini wewe wala habari nalo huna, wewe ni Gerezani na Kipata tu, Ukiulizwa habari za Magomeni basi wa kwanza kutajwa ni Tambaza

Kaka Mohamed Said, unajinasibisha kuwa unaandika historia ya waliosahaulika, mbona wewe hukuweka habari za hilo tawi la Jaribu? Nalo umelisahau? Kwa hiyo na watoto wake waje na Historia yao ya waliosahaulika?

Naomba pia kuuliza kwa nini zaidi ya asilimia 90 ya picha za Tanu zinazoonekana hakuna the Skyes family members wanayeonekana? Nilitegemea kabisa picha za hilo tawi la Jaribu kumuona Abdul

Hao unaowaita "Magreat thinkers humu" ni historia ipi wameandika? au na wao ni kama wewe tu, roho zinawauma mnapoona Dah! kumbe ni Waislam waliokuwa mstari wa mbele!

Hebu tupe kisa cha babu zako kwenye historia ya Tanganyika, kama hujaleta kituko tu.
 
Safi nini toa mchango

Safi sana hizo picha za Kihistoria. Kumbe hata meza ya kwanza yenye hadhi, ya Mwenyekiti wa TANU ilitengenezwa na Muislam.

Sijuwi wamekumbuka kuiweka makumbusho ya Nyerere hii?
 
level of efforts hasa intellectually hiko vipi hapo?
 
Mimi nikiiangalia picha hizi nakumbuka tu kazi ya kwanza aliyoifanya Mwalimu baada ya uhuru kupitia iliyoitwa "operation makuti" katika kubadilisha mazingira ya mji wa Dar es Salaam. Hizo mnazoziona ndizo nyumba za wakati huo mjini Dar es Salaam toka Kariakoo, Ilala hadi Magomeni na ndio maana hata kuna sehemu ilijulikana kama Magomeni Makuti...nyumba hizo za makuti ndizo zilitamalaki.

9429573.jpg


Nakumbuka mtaa maarufu wa Idrissa Magomeni ulivyoweza kuwa na nyumba za kisasa (kwa wakati huo), barabara za lami zenye mitaro ya kisasa kupitisha maji machafu. Magomeni Makuti, Magomeni Mikumi, Magomeni Kota zote ziliweza kuunganishwa kwa barabara za lami zikipita mabasi ya DMT (Dar es Salam Motor Transport) hadi Mikumi mwisho. Sehemu kama za Gerezani zilikaliwa na walowezi wengi wakiwa Manyema, Wanubi na Wazulu.

Kwa nini hizo barabara zilizojengwa kitaalamu hazikuweza kudumu ni mjadala mzito unaohitaji mada yake peke yake. Hivyo hivyo baadaye nyumba za starehe za kisasa chini ya DDC zilizokuja kujengwa baadaye Karikaoo. Magomeni hadi Ilala na kuwekewa "fittings" za Kisasa (wakati huo) nazo hazikudumu kwa sababu ambazo hasa zilihusiana na utamaduni wa wakazi wa hizo sehemu...hawakujua matumizi rasmi ya vifaa vya kisasa vilivyowekwa.
 
Hii inaonesha kuwa Mwl Nyerere alikuwa ni mtu wa kipekee sana.

Ukiona hawa wazee wote bila kujali tofauti za kidini na hata umri wakafikia hatua ya "kumkubali" na "kumheshimu" kwa kiasi picha hizi zinavyoashiria kwa hakika alikuwa ni wa kipekee.

Yesi mwingine anaweza pia kusema, wazee hawa walikuwa ni wa kipekee sana kuweza kuwa tayari kuongozwa na kijana huyu tena mkristo!

Inatufunza sisi wa sasa kuweka maslahi ya taifa mbele kabla ya maslahi binafsi au ya dini na madhehebu yetu.
 
Mohamed Said

My guess is,
Nyerere was like a celebrity by then na watu wengi walipiga naye picha walipopata nafasi. Na si lazima kila aliyepiga picha naye alikuwa ni "mpigania uhuru".
Maeneo fulani yalikaliwa zaidi na watu wa utamaduni/dini fulani kuliko watu wa utamaduni mwingine. Hata ingekuwa leo, Nyerere apige picha Pemba, ataonekana kama amepiga na waislam watupu.
Ninaamini kuwa alipokuwa anatembelea maeneo ya wasukuma au wamasai (kama picha zitawekwa za enzi hizo), picha zitaonesha kuwa ni watanzania wa kawaida wa asili ya kisukuma au kimasai ndio walimpiga "tafu" kwenye mambo ya uhuru. Pia ninaamini kuwa zilikuwepo picha nyingi zilizopigwa wakati huo lakini hazikukidhi ule mtazamo wa mwandishi. It is therefore no coincidence, kwa tunavyokufahamu Mohamed Said, kubandika picha zilizopigwa DSM na kuziacha za sehemu nyingine ili tu kukidhi haja yako ya kuonesha kuwa watu fulani wamesahaulika.

upo sahihi kabisa,et kisa mwl amepga pics na hvyo vizee vilivyovaa bagharashia et navyo vimepigania uhuru
je km hzo samani jamaa alimuuzia mwl n wakat mwlm anakwend kuziona watu wakakusanyika hapo kw kuwa walijua mwl angeenda wakala mapics,leo hii et nao wapigania uhuru

# mohamed; utakufa kihoro km takadiri na kanxa yako ya udini
 
Last edited by a moderator:
Daa ndio uhalisia unavyohonekana hapo alikuwa nao pamoja sasa sijui sasa chuki imetokea wapi
 
BigBro,
Katika kitabu changu sehemu ya mwisho nimejaribu kueleza wapi misingi ile imara ilipovunjwa. Kipate kitabu usome.

Mohamed said tafadhari uwe unalipia haya matangazo ya vitabu vyako hapa jf au kama vipi anzisha forum yako ujitangaze zaidi na zaidi.
 
Ziweke wewe, unangoja nini? tafuta tu hata kwenye mtandao zimejaa picha za Nyerere, tafuta za enzi hizo za wapigania Uhuru wa maeneo mengine utuwekee. Mimi mbona nime google nikapata hiyo ya wazee wa TANU, anza.

Msisahau na za Comrade John Okelo the founder and father of Zanzibar island.
 
upo sahihi kabisa,et kisa mwl amepga pics na hvyo vizee vilivyovaa bagharashia et navyo vimepigania uhuru
je km hzo samani jamaa alimuuzia mwl n wakat mwlm anakwend kuziona watu wakakusanyika hapo kw kuwa walijua mwl angeenda wakala mapics,leo hii et nao wapigania uhuru

# mohamed; utakufa kihoro km takadiri na kanxa yako ya udini

Tarangile,
Unaandika umekasirika na kutumia lugha zisizo za kiungwana.

Kuanzia leo asubuhi pamekuwa na hamu kubwa ya watu wengi kupitia
Majlis na kusoma.

Nimefahamishwa mmoja wa akina mama waliokuwa katika ile sherehe
ya Mwalimu Nyerere kupokea samani kwa ajili ya ofisi yake ni marehemu
Bi. Khadija Said ni mama ya rafiki yangu Bwana Athman Kassanda.

Bi. Khadija Said ni huyu wa pili kushoto:

img258.jpg



Huyu mama kazikwa kiasi cha majuma matatu yaliyopita.
Nina hakika wengi watawatambua wazee wao katika hizi picha.

Haitakuwa vyema kama wewe utawatukania baba na mama zao.

Huijui historia ya Ali Msham na watu wa nyumbani kwake katika harakati
za TANU.

Nitakufahamisha kwa ufupi.

Baada ya kufungua tawi la TANU 1954 hapo nyumbani kwake Ali Msham
alitoa sehemu katika nyumba yake akaanzisha shule chini ya Tanganyika
African Parents Asociation (TAPA).

Hizi shule zilikuwa maarufu wakati wa kudai uhuru.

Baada ya kufungua shule hii alitoa sehemu ndogo ya nyumba yake akafungua
biashara ndogo ya mafuta ya taa na kumpa Mama Maria Nyerere aendeshe.

Hizi zilikuwa nyakati ngumu sana kwa TANU na wazee wanazikumubuka sana.

Abdulrahman Msham anasema kaka yake binamu Omari Likonda mtoto wa
shangazi yake Biti Mwanaisha Msham dada yake Ali Msham ndiye aliyekuwa
akimsindikiza Mama Maria nyumbani jioni na kumbebea mzigo yake hadi nyumbani
kwake Magomeni Majumba Sita.

Omari Likonda yu hai na sasa ni mtu mzima.
Watu hawa si wa kutukanwa na kufanyiwa kebehi.

Hawa wanastahili heshima zote.
Watu hawa wameacha alama katika historia ya nchi yetu.

Huyo hapo chini ni Abdulrahman Ali akiwa mbele ya nyumba ya baba yake Ali
Msham.

Hapo aliposimama ndipo lilipokuwa tawi la TANU wakati wa kupigani uhuru wa
Tanganyika.

DSCN1803.JPG
 
Msisahau na za Comrade John Okelo the founder and father of Zanzibar island.

Hakuna ukweli ambao Wazanzibari HAWAPENDI kuusikia kama huu na sijui kwa nini inakuwa hivyo!
John Okello atabaki kuwa mtumuhimu sana wa kukumbuka katika historia ya Mapinduzi ya Zanzibar milele na milele.
 
Hakuna ukweli ambao Wazanzibari HAWAPENDI kuusikia kama huu na sijui kwa nini inakuwa hivyo!
John Okello atabaki kuwa mtumuhimu sana wa kukumbuka katika historia ya Mapinduzi ya Zanzibar milele na milele.

Uzuri wa ukweli kadiri unavyozidi kufichwa ndivyo unavyozidi kustawi.
 
Back
Top Bottom