warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,218
- 18,440
AMA kweli fedha mwanaharamu ! Kama bado ulikuwa ukiamini kwamba Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu anayependelea kuitwa Madam ana mtonyo ( fedha) kumzidi aliyekuwa shosti wake, mwigizaji Kajala Masanja ' Kay ' , umekosea sana kwani upepo umegeuka.
Habari za ' ufukunyuku ' zinadai kwamba, kwa utajiri alionao kwa sasa , Kajala anaweza kudiriki kumwajiri Wema kama kisemavyo chanzo.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na wote kwa maana ya kutafuna pande zote , mwigizaji huyo ambaye enzi za ushosti wake na Wema alikuwa akionekana kama kijakazi, sasa fedha imemtembelea kiasi cha kutosha wakati mwenzake kwa bahati mbaya eti ' anatembelea ringi ' .
Chanzo kilisema kwamba Kajala kwa sasa ana maisha ya ' kitonga ' , amepanga kwenye nyumba nzuri ya ghorofa , ana kampuni yake ya filamu ( KAY Entertainment ) , magari manne, anatembea na wapambe ( walinzi) huku akaunti yake benki ikiwa imetuna.
"Kajala ameonesha jeuri ya fedha . Ametoka katika nyumba ya kawaida sasa analala angani. Kwa taarifa yenu amepanga ghorofa nzima maeneo ya Sinza -Madukani jijini Dar .
"Yupo vizuri, anamiliki ofisi kubwa ya kuzalisha sinema, magari mawili ya ofisi pamoja na magari mawili ya kutembelea ( Brevis na Harrier ) na anaishi katika nyumba anayolipa kodi kwa mwezi dola 2, 000 ( zaidi ya Sh . milioni 3.2 ) ," kilidai chanzo hicho na kudai kwamba si mbaya Kajala akamkumbuka mwenzake hata kwa kumwajiri kwenye kampuni yake . Pichani ni mjengo ambao Kajala Masanja amepanga .
KAJALA AMEHONGWA ?
Akizungumza na waandishi wetu , Kajala alisema anamshukuru Mungu kwani fedha hizo amezizalisha kupitia kazi zake pamoja na biashara mbalimbali alizokuwa akizifanya ,hajahongwa na mtu yeyote .
"Sijahongwa na mtu yeyote , kila mtu ana akili zake katika kutafuta fedha , nafanya biashara huku nikiigiza sinema zangu na Mungu amenijalia mambo yanakwenda vizuri, " alisema Kajala .
Kuhusu kumwajiri staa mwezake huyo, Kajala hakutaka kulizungumzia hilo.
WEMA HALI IPOJE ?
Utafiti umeonesha Wema ambaye alikuwa akimiliki magari kadhaa likiwemo la kufanyia kazi za sinema, kwa sasa amebakiwa na gari moja tu ambalo ni Toyota Harrier . Kama hiyo haitoshi , ilidaiwa kuwa hata akaunti benki haijanona na hata wapambe wa kutembea naye wameyeyuka.
Utafiti uliofanywa na Ijumaa Wikienda umebaini kwamba Wema aliyemlipia Kajala Sh . milioni 13 asiende jela mwaka jana,ambaye kipindi kifupi kilichopita alikuwa na kampuni ya kuzalisha sinema, wapambe,akaunti iliyonona benki , magari ya kifahari ya kutembelea na samani nyingine , nyingi zimepotea kama si kuyeyuka kabisa .
WEMA ATAFUTWA
Ili kutaka kujua anazungumziaje ' challenge 'hiyo ya kudaiwa kuporomoka kiuchumi,wanahabari wetu walimtafuta Wema kwa siku tatu mfululizo lakini hakupatikana huku simu yake ikiita muda mrefu bila kupokelewa.
Habari za ' ufukunyuku ' zinadai kwamba, kwa utajiri alionao kwa sasa , Kajala anaweza kudiriki kumwajiri Wema kama kisemavyo chanzo.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na wote kwa maana ya kutafuna pande zote , mwigizaji huyo ambaye enzi za ushosti wake na Wema alikuwa akionekana kama kijakazi, sasa fedha imemtembelea kiasi cha kutosha wakati mwenzake kwa bahati mbaya eti ' anatembelea ringi ' .
Chanzo kilisema kwamba Kajala kwa sasa ana maisha ya ' kitonga ' , amepanga kwenye nyumba nzuri ya ghorofa , ana kampuni yake ya filamu ( KAY Entertainment ) , magari manne, anatembea na wapambe ( walinzi) huku akaunti yake benki ikiwa imetuna.
"Kajala ameonesha jeuri ya fedha . Ametoka katika nyumba ya kawaida sasa analala angani. Kwa taarifa yenu amepanga ghorofa nzima maeneo ya Sinza -Madukani jijini Dar .
"Yupo vizuri, anamiliki ofisi kubwa ya kuzalisha sinema, magari mawili ya ofisi pamoja na magari mawili ya kutembelea ( Brevis na Harrier ) na anaishi katika nyumba anayolipa kodi kwa mwezi dola 2, 000 ( zaidi ya Sh . milioni 3.2 ) ," kilidai chanzo hicho na kudai kwamba si mbaya Kajala akamkumbuka mwenzake hata kwa kumwajiri kwenye kampuni yake . Pichani ni mjengo ambao Kajala Masanja amepanga .
KAJALA AMEHONGWA ?
Akizungumza na waandishi wetu , Kajala alisema anamshukuru Mungu kwani fedha hizo amezizalisha kupitia kazi zake pamoja na biashara mbalimbali alizokuwa akizifanya ,hajahongwa na mtu yeyote .
"Sijahongwa na mtu yeyote , kila mtu ana akili zake katika kutafuta fedha , nafanya biashara huku nikiigiza sinema zangu na Mungu amenijalia mambo yanakwenda vizuri, " alisema Kajala .
Kuhusu kumwajiri staa mwezake huyo, Kajala hakutaka kulizungumzia hilo.
WEMA HALI IPOJE ?
Utafiti umeonesha Wema ambaye alikuwa akimiliki magari kadhaa likiwemo la kufanyia kazi za sinema, kwa sasa amebakiwa na gari moja tu ambalo ni Toyota Harrier . Kama hiyo haitoshi , ilidaiwa kuwa hata akaunti benki haijanona na hata wapambe wa kutembea naye wameyeyuka.
Utafiti uliofanywa na Ijumaa Wikienda umebaini kwamba Wema aliyemlipia Kajala Sh . milioni 13 asiende jela mwaka jana,ambaye kipindi kifupi kilichopita alikuwa na kampuni ya kuzalisha sinema, wapambe,akaunti iliyonona benki , magari ya kifahari ya kutembelea na samani nyingine , nyingi zimepotea kama si kuyeyuka kabisa .
WEMA ATAFUTWA
Ili kutaka kujua anazungumziaje ' challenge 'hiyo ya kudaiwa kuporomoka kiuchumi,wanahabari wetu walimtafuta Wema kwa siku tatu mfululizo lakini hakupatikana huku simu yake ikiita muda mrefu bila kupokelewa.