Picha za wakuu wa JWTZ tokea Tanzania ilipopata uhuru wake

Picha za wakuu wa JWTZ tokea Tanzania ilipopata uhuru wake

mkuu JokaKuu historia ya nchi yetu inafichwa fichwa hata bila sababu za msingi. wizara inayohusika na utamaduni amkeni basi muweke kumbukumbu hizi. ni aibu sana kwa matukio ya miaka ya 60 au 70 kutokufahamika au kurekodiwa kwa ufasaha. nchi kama Ethiopia wameweza kutunza historia ya matukio ya miaka 3000 iliyopita, inakuwaje hapa inashindikana?

..sisi hapa tumejikita kwenye siasa tu.

..kwenye nchi za wenzetu utakuta kuna minara ya kumbukumbu za mashujaa.

..pia sherehe za mashujaa, na kumbukumbu za kuanzishw kwa majeshi yao, ni matukio makubwa. utaona yanatangazwa kwenye vyombo vya habari kwa Raisi na viongozi mbalimbali kushiriki. pia huwa ni siku za mapumziko kwa wanafunzi na watumishi wa serikali.

..pia wanakuwa na vitu kama Kofia, t-shirts, beji, number za magari, vyote hivyo kuonyesha kumbukumbu, na kusherehesha ushindi wao, ktk vita mbalimbali.

..lakini zaidi ni huduma za afya wanazojitahidi kuwapatia mashujaa waliotumikia jeshini.

NB:

..lakini siyo matukio ya ushindi tu hukumbukwa. hata kule walikoshindwa wenzetu huwakumbuka wenzao "who paid the ultimate sacrifice." Kwa mfano, nimewahi kuona documentary ya Operation Eagles Claw ambapo Wamarekani walifeli ktk jaribio lao la kwenda kuwaokoa mateka waliokuwa wakishikiliwa Iran.

..Lakini kufeli kwa Operation Eagle Claw ndiyo chanzo cha wao ku-fine tune mbinu zao mpaka walipoweza kufanikisha operation ya kumuua Osama Bin Laden. Kama umetizama film ya kuuwawa Osama utaona pale helikopta moja ilipopata matatizo kuna jamaa mmoja aliyekuwa makao makuu ya CIA akifuatilia video feed toka Abottabad alisema "Operation Eagles Claw all over again!!". Hofu iliwatanda kwamba yaliyotokea Iran in 1980s yanajirudia Pakistan.

cc Echolima, Pasco, Nguruvi3, Kichuguu, Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
mkuu wa majeshi,Uhuru mpaka 1964 nani???

..mkuu wa Tanganyika Rifles alikuwa Muingereza anaitwa Brig.Patrick Sholto Douglas.

..kabla Tanganyika Rifles kulikuwa na King's African Rifles. Sijafuatilia taarifa za KAR kujua viongozi wao.

..uwepo wake, pamoja na maafisa wengine wa Kiingereza, ndiyo ulisababisha maasi ya 1964 ambapo askari Waafrika walianza kudai zoezi la Africanization litekelezwe na jeshini pia.

..Jeshi la Polisi lilikuwa linaongozwa na IGP Mzalendo, Elangwa Shaidi, kwa hiyo askari wa Tanganyika Rifles wakawa wanaona kuwa wamesahauliwa.

..Waasi wa 1964 walimpachika Ukuu wa Majeshi na kumpa cheo cha Brigadier, Luteni Elisha Matayo Kavana.

..Baada ya kuanzishwa JWTZ ndipo Raisi akamteua Captain Sam Mirisho Sarakikya kuwa Brigadier na Mkuu wa Majeshi.

NB:

..moja ya sifa za Gen.Sarakikya ni kuzingatia sana mazoezi. Sarakikya alijiwekea utaratibu wa kupanda mlima Kilimanjaro kila mwaka. Utaratibu huo amekuja kuucha hivi majuzi.

cc Ally Kombo, Echolima, Nguruvi3, VOICE OF MTWARA, Manyerere Jackton
 
attachment.php


Kuna kitu sikielewi vizuri juu ya huyu mkuu, je alipandishwa kuwa General baada ya kustaafu? ili afanane na hao wengine?
 
..sisi hapa tumejikita kwenye siasa tu.

..kwenye nchi za wenzetu utakuta kuna minara ya kumbukumbu za mashujaa.

..pia sherehe za mashujaa, na kumbukumbu za kuanzishw kwa majeshi yao, ni matukio makubwa. utaona yanatangazwa kwenye vyombo vya habari kwa Raisi na viongozi mbalimbali kushiriki. pia huwa ni siku za mapumziko kwa wanafunzi na watumishi wa serikali.

..pia wanakuwa na vitu kama Kofia, t-shirts, beji, number za magari, vyote hivyo kuonyesha kumbukumbu, na kusherehesha ushindi wao, ktk vita mbalimbali.

..lakini zaidi ni huduma za afya wanazojitahidi kuwapatia mashujaa waliotumikia jeshini.

NB:

..lakini siyo matukio ya ushindi tu hukumbukwa. hata kule walikoshindwa wenzetu huwakumbuka wenzao "who paid the ultimate sacrifice." Kwa mfano, nimewahi kuona documentary ya Operation Eagles Claw ambapo Wamarekani walifeli ktk jaribio lao la kwenda kuwaokoa mateka waliokuwa wakishikiliwa Iran.

..Lakini kufeli kwa Operation Eagle Claw ndiyo chanzo cha wao ku-fine tune mbinu zao mpaka walipoweza kufanikisha operation ya kumuua Osama Bin Laden. Kama umetizama film ya kuuwawa Osama utaona pale helikopta moja ilipopata matatizo kuna jamaa mmoja aliyekuwa makao makuu ya CIA akifuatilia video feed toka Abottabad alisema "Operation Eagles Claw all over again!!". Hofu iliwatanda kwamba yaliyotokea Iran in 1980s yanajirudia Pakistan.

cc Echolima, Pasco, Nguruvi3, Kichuguu,
Mkuu Jokakuu
Tarehe 11nilikuwa naangalia kumbukumbu za mashujaa waliopigana katika nchi za magharibi(Remembrance day). Tukio hilo lilikuwa nchi nzima, iipofika saa 5 asubuhi( 11[SUP]TH[/SUP]hr of 11[SUP]th[/SUP] day of 11[SUP]Th[/SUP] month) radio, TV, maofisi, mashule na kila kitu kilisimama kwa dakika 3 kwa kumbu kumbu ya waliokufa wakitetea nchi zao.

Watu walikwenda makaburini wakiwa na bendera, na kila aina ya tamaduni zao zakukumbuka mashujaa.
Hata hapa Dar, wazungu wanakumbuka askari wao walifariki na kuzikwa hapo mjini.
Utashangaa kuwa askari wengi waliokufa ni waafrika lakini hatuna habari.


Jeshi nalo halionekani kujua nini cha kufanya.
Siku ya mashujaa ni siku ya kuwakumbuka walijitoa na kulipa gharama kubwa’’ultimate price’’ kwa ajili yetu.

Siyo siku ya kugawa Michele, au kufungua visima vya maji kama tulivyoona majenerali wetu wakifanya mwaka huu.

Ni siku ambayo akina Echolima walitakiwa kushukuriwa, waliopoteza roho zao kukumbukwa,na kuangalia afya na maisha ya wale waliopo. Je, wanapata japo matibabu?
Je,wanapata huduma za kuwasaidia kimaisha.


Mwezi huu niliduwaa pale mabaki ya askari wa vitakuu miaka 70 iliyopita yaliporudishwaCanada kutoka Ujerumani. Nilisoma na kuona mazishi ya kijeshi ya askari huyo. Miaka 70 bado taifa lake lilikuwa linatafuta ukweli na mwisho kuupata

Leo,tujiulize mashujaa wetu wa vita hata vya karibuni vya Kagera , nani anawajua?
Lini akina echolima watapewa nafasi ya kueleza na kujenga uzalendo kwa kizazi kipya?
 
Na Gen. Twalipo alikuwa front kwenye uwanja wa mapambano na kushika machine gani. Ilikuwa ni jambo la kushangaza manake hakutaka kubaki nyuma kusubiria ripoti za makamanda wakisonga!

Ulikuwepo kwenye vita? CDF hawezi pigana front kijana yeye alikuwa karibu na uwanja wa vita ili aweze kuongoza kwa umakini zaidi.
 
Zanzibar wapi? Hata illustrious sons of Zanzibar , military accomplished Cuba trained comrades walitengwa then? Muungano una kasoro.

Walamchele hao hawana ujasiri wa kupigana, angalia miaka ya zamani makabila yaliyoongoza kuwa na askari jeshi wengi walikuwa ni Wakurya, Wangoni, na wahehe kwasababu wao ni wapiganaji tangu enzi za zamani kabla na baada ya ukoloni,
 
attachment.php


Kuna kitu sikielewi vizuri juu ya huyu mkuu, je alipandishwa kuwa General baada ya kustaafu? ili afanane na hao wengine?

Huenda ikawa hivyo maana mi nakumbuka alikuwa brigadier baada ya kupandishwa cheo kutoka lieutenant
 
Nguruvi3,

..mwanachama mwenzetu Wickama aliwahi kututumia link ya mtandao ambapo unaweza kutafuta majina ya askari waliofariki ktk vita ya I na ya II ya dunia. Kwenye link hiyo unaweza kukutana na majina ya Watanganyika waliopoteza maisha wakipigana upande wa himaya ya Muingereza.

cc Echolima, Kichuguu
 
Last edited by a moderator:
attachment.php


Kuna kitu sikielewi vizuri juu ya huyu mkuu, je alipandishwa kuwa General baada ya kustaafu? ili afanane na hao wengine?

Sarakikya aliondoka akiwa Brigadier; ni baada ya hiyo skendo iliyom,uondoa ndipo JWTZ ilipopangwa upya ikiwa na brigade nne au tano sikumbuki sawasawa ambapo akina Mayunga, Walden, Marwa, Yusufu Himid na wengine walipandihswa kuwa mabrigadier halafu mkuu wa majeshi Twalipo akapanda kuwa Major General, halafu baada ya vita ya kagegra zikaundwa divishen kadhaa zilzioongozwa na majoor general ndipo kuanzia hapo mkuu wa majeshi akawa General, na Chief of staff akawa Lt General.

Sarakikya, Nyirenda na wale maafisa wa kwanza wazalendo walipandishwa vyeo baadaye sana na Mkapa kuwa majenerali wakiwa tayari nje ya jeshi
 
Sarakikya aliondoka akiwa Brigadier; ni baada ya hiyo skendo iliyom,uondoa ndipo JWTZ ilipopangwa upya ikiwa na brigade nne au tano sikumbuki sawasawa ambapo akina Mayunga, Walden, Marwa, Yusufu Himid na wengine walipandihswa kuwa mabrigadier halafu mkuu wa majeshi Twalipo akapanda kuwa Major General, halafu baada ya vita ya kagegra zikaundwa divishen kadhaa zilzioongozwa na majoor general ndipo kuanzia hapo mkuu wa majeshi akawa General, na Chief of staff akawa Lt General.

Sarakikya, Nyirenda na wale maafisa wa kwanza wazalendo walipandishwa vyeo baadaye sana na Mkapa kuwa majenerali wakiwa tayari nje ya jeshi
Ahsante kwa taarifa hii, sidhani kama watu wengi wanafahamu hivyo.
 
Zanzibar wapi? Hata illustrious sons of Zanzibar , military accomplished Cuba trained comrades walitengwa then? Muungano una kasoro.

mkuu wazanzibar walikuwa na nafasi pengine kama Colonel Ally Mahfoudh angeendelea na utumishi ndani ya jeshi siku moja angepata ukuu wa majeshi au cheo kingine cha juu zaidi. kuhusishwa kwake na mauaji ya Karume kwenye jaribio la mapinduzi ndio kukamnyima nafasi
 
General Msuguri inaelekea ana undugu japo wa mbali na Idi Amini
 
It is very interesting to know this. Lakini kwa hii knowledge yangu ndogo sana yakusoma stories mbali mbali naweza kupima umakini wa mleta huu uzi. Ipo siku atapiga picha document nyeti nakuiweka JF. Pia Sidhani wakubwa wote wanapenda kuwekwa kwenye hii mitandao ya kijamii. Unajua ni kwanini!!? Unatoa nafasi yakujadili mambo mengine yasiyostahili kujadiliwa humu hasa unapogusa vyombo na individual figures za intelligence and Defence.
Hahahahaaa
 
mwamunyange anaonekana soft of them all..ogopa wateule wa jk,unaweza kukuta hakustahili.
 
Back
Top Bottom