Uchaguzi 2020 Please CHADEMA, mtapata mnachokitafuta

1. Kwanza inaonekana hujui maana ya sampling kwenye takwimu ni upuuzi kudhani wanaotumia social network hawapo kitaa!! Ndio maana sampling inakupa picha tu ya the remaining population ambayo kma ikipata smartphone ingetoa maoni gani. Jiuliza mange kuwa na followers 4M toka aanze kuikosoa serikali inakupa picha gani?? Kweli haireflect kitaa? Hao 4M wapo nchi gani? Hawana friends wa kuwashawishi?

2. Kuhusu siasa za kitaifa, ni mpuuzi tu atakosoa mchango wa Lissu kwenye siasa za bunge. Kama uliona mjadala wa sheria ya cybercrime/Gesi, ripoti za CAG, Mpango wa taifa wa 5 years basi una haki ya kusema hana alilofanya ila wote wanafahamu hakuna muswada wa CCM uliwahi pita bila kupitia mchujo wa hoja za Lissu. Kwa hili tumpe credit hta kma wamchukia. Na nikwambie tu Leo akienda CCM atapewa uwaziri na ww hutokua na lakufanya zaidi ya kupiga makofi tu.

3. Jimboni kwake hawamtaki?? Lissu ndio mpinzani pekee ambaye uchaguzi serikali za mitaa wa mara ya mwisho upinzani wanashiriki alipata 98% ya serikali za vijiji then unasema walimchoka?? Kwa data zipi mkuu? Nlikuwepo huko Ikungi january huyo mbunge wa CCM hana ushawishi kabisa na yye anajia tu kashika jimbo kimaguvu tu ila come october atapisha tu kwa nguvu ya sanduku.

Na ndio maana aliwapa challenge leo Maalim kma mnakubalika sana kwanini mnaogopa uchaguzi huru na haki?? Jibu ni Mnafahamu akisimama atapukutisha CCM vipande pande kwa facts!!

Turudi wakati wa kampeni utakuwa umenielewa nachosema
 
Lissu atarudi tu he has nothing to lose at the moment afungwe aachiwe, azuiliwe kugombea ama auawe!! All are expected na hivyo kwake yye hana option zaidi ya kusonga mbele maana afterall kma alipona kifo sidhani kma ataogopa kesi tena zilizo baseless!!! Eti uchochezi? Sijui utoro? Are we serious?

Lissu atarudi tu hilo lipo wazi unless CCM wazuie ila kuhusu yye, obviously hana hofu maana anajua hta akibaki huko atakuwa amewapa ushindi CCM "without shots being fired"!!

Muhimu tu chama kimtafutie usalama wa kutosha wakati wote wa kampeni maana huu utawala hauoni aibu hta kurusha grenade jukwaani!! Otherwise CCM are in for it hyo oktoba maana kampeni zitakua kali sana kma Dr Slaa wa 2010!!
 
K
Kwanza msaidie lissu kutembea sasa gwaride atakaguaje wakati anatembea kama kaa
 
Wanatangaza nia tu Mkuu,lakini watachujwa Na ushindi atapatikana si lazima sasa hivi ajulikane Nani ndie mgombea uraisi kupitia chadema (ondoa hofu Mkuu)
 
Nakufagilia kwa jinsi unavyojenga hoja kama nahodha wa chombo kinachoenda mrama.

Ndani ya nafsi yako unajua ukweli kuwa Serikali ya awamu ya tano, bila kumung'unya maneno, imewatendea wananchi haki kubwa kuliko ilivyotegemewa. Kumshindanisha Magufuli katika kunyang'anyiro cha Urais ni kama kumwaga kijiko cha chumvi kwenye mto.

Kimaendeleo, Rais Magufuli hana mfano kwa Marais wa nchi hii. Kisiasa kuna mapungufu lakini maamuzi yake yalikuwa sahihi ndiyo maana amefanikisha yote mazuri ya mfano kimaendeleo.

Jinsi upinzani ulivyotaka nchi ikabili maambukizi ya COVID-19 hakika imewaweka kwenye wakati mgumu wakati wa kampeni.

Tuhuma dhidi ya Mbowe, naamini itakuwa agenda ya vyama vingine vya upinzani, hasa NCCR Mageuzi, ili kirejee kuwa chama kikuu cha upinzani.

Iwapo CHADEMA itaungana na ACT- Mzalendo kwenye uchaguzi mkuu, kitakuwa kimepoteza mwelekeo kwa kuwa Zitto atamzidi kete Mbowe kwa kutumia tuhuma dhidi yake.
 
Mkuu bado naamini ww ni mtu makini sana so jikite kwenye hoja umesema Lissu hana hoja za kitaifa!! Kivp? Mchango wake bungeni haupo?

Umedai hakubaliki jimboni kwake? Aliwezaje Kushinda vijiji 42? Umetumia takwimu gani?

Umedai waliopo social media ndio wanaunga mkono upinzani ila wasio na smartphone hawapo upinzani? Je hao 4 Million wanaosupport critiques wa serikali hapa nchini wanaishi nchi gani?

Naomba uya adress hayo maswali kwa huo mtiririko kabla hatujahamia kujadili Magu na Covid 19!! Kukimbia hoja hakuwezi iokoa CCM.

Nikwambie tu CCM bado haikubaliki mkuu ndio maana wanataka kutembelea mbeleko ya Magufuli ila bado wananchi hawana imani na kijani. So hta upinzani usiposhinda Urais but wataretain majimbo mengi sana trust me on this one!! Considering uchaguzi huru na haki
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100

Ni Tundu Lissu pekee anayestahili kusimama kwenye nafasi ya Urais, kati ya waliochukua fomu, tiwaombe tena Chadema, watafakari kwa makini hoja za wananchi na waepuke kikigawa chama chao, katika hili suala nyeti sana la kugombea Urais na watambue pia, namna ambavyo adui yao CCM alivyopania kuiua Chadema, kosa kidogo watakalofanya, basi wamekipeleka kaburini chama chao milele
 

Hitimisho lako hilo linaondoa uhalali wa kujadiliana bali kusubiri matokeo ya Uchaguzi Mkuu.

Hata vile, kama nilivyofafanua kwenye bandiko ulilojibu hapo juu wagombea wa upinzani, hasa CHADEMA, watakuwa na wakati mgumu kwenye kampeni. Ama watalazimika kumsafisha Mbowe kwa tuhuma dhidi yake, au kujitetea kwa nini wamekuwa wakibeza juhudi za Serikali kuwaondolea kero wananchi.

Ukumbuke pia, tayari CCM ina mtaji kwa kuwekeza kwenye "maendeleo ya vitu", na upinzani unakiri hivyo. Kama wahenga walivyonena, " mkono mtupu haulambwi"

Mkuu zitto junior, nami nahitimisha kwa kukupongeza umekuwa mwungwana kutambua mchango wa Magufuli katika maendeleo ya nchi hii, nikikunukuu: [wanataka kutembelea mbeleko ya Magufuli/I].
 
Mleta mada, hivi ni wewe pekee unayejua uwezo wa Tundu Lissu kuliko hao wenzake alionao ndani ya chama?

Kwa nini unachochea mifarakano isiyokuwepo ndani ya chama?

Umemuuliza Tundu Lissu kakulalamikia kwamba anaogopa uwezo wake alionao hautaonekana na wala hautambuliwi ndani ya chama?

Tundu Lissu anauwezo mkubwa wa kumkabiri Magufuli, na chama lazima wanajua hivyo.

Inakuwaje wewe uje hapa kuhoji kana kwamba ni jambo lililojificha?

Wewe unadhani CHADEMA kama chama, hawataki mafanikio?

Sasa tulia. Acha chama kifanye taratibu zake. Kama itathibitika kwamba chama hakijitambui, acha wafilie mbali kungali mapema, kabla hawajaingia kutuharibia nchi, zaidi ya ilivyokwishaharibika tayari.
 
Tuhuma zip? ameiba?
 
Ila kwa hiyo clip ya Lema inayozunguka kwenye mitandao, kwa kweli nimekwazika sana aisee! Sijui MATAGA wamefanya yao au ni kweli? Kama ni kweli wamenivunja moyo sana! Wapinzani wana akili gani aisee? Lema katia aibu sana!! Bora tu Jiwe liendelee kututawala hamna namna!!
 
Baba pasco kuwa muwaz tuu usiwe popo upo upande gani mzee baba??
Mpuuzi sana huyo, ameng'ang'ania hoja za kijinga jinga tu mara kesi za jinai n.k? Kesi zenyewe za jinai ni za kubuni buni tu na kutungwa na maCCM yenyewe.
 
Mkuu nataka niseme moja tu, hivi Jpm na lissu nani mwenye dharau? Siasa hizi duh
 
Tatizo LA chadema kila MTU Ni kambale, lema ahojiwe kama kweli kasema hayo maneno, isijeonekana Lumumba kafanya yao, kama kasema kakosea sana.Chama Ni kuvumiliana na vikao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…