Pole Catherine Magige, hii iwe fundisho kwa wadada maarufu nchini

Pole Catherine Magige, hii iwe fundisho kwa wadada maarufu nchini

Mwanaume halisi na mwenye kisu hahangaiki na kuomba namba dm...yaan automatic utajikuta unapata wepesi tu kupata namba yake!yaan unaletewa tu namb! Masuala ya kuombana namba ni dalili kuu ya ww maisha kuunga unga
Dah.. mkuu umeninyong'onyeza sana. Kwahiyo kumbe sisi wanaume tusio na kisu sio wanaume halisi..?🙄
 
Seriously wabunge wenye akili kama za huyu cathy means tuna safari ndefu sana kama taifa. Nasikia ana masters ya mzumbe lakini mbona kama ana behave kama ndalandefu kutoka sakina au unga ltd.

#Vitimaalumbasisasa wanakula jasho letu bila maana yoyote. Arusha na ujanja wote ccm wanapitisha mtu huyuhuyu zaidi ya 15 yrs mbunge wa viti maalum arusha Uvccm. Akili ndogo anagombania hawala maiti hata kama ana fedha ni kujifedhehesha.
 
Huyu ndiyo yule 1st lady wa wasafi kila event yupo. Inakumbusha vicky kamata alivyotapeliwa na charles mzena baada ya kuchangisha michango ya harusi halafu mke halali wa charls akaweka pingamizi. Michango msela kaikamata halafu ndoa hakufunga.Mambo ya mjini hayo.
 
Msiba wa marehemu Kudula Madoda anayedaiwa kuwa mchumba wa mbunge wa viti maalumu Catherine Magige, umetawaliwa na vituko ya aina yake Mara baada ya Magige na kundi lake kuvunja geti ili kushiriki maziko ya marehemu baada ya kuzuiwa.

Marehemu Madoda amezikwa leo katika shamba lake eneo la Nduruma,ambapo katika mazishi hayo yaliyoratibiwa na ndugu wa marehemu Magige hakutakiwa kuingia kaburini na wapambe wake baada ya familia hiyo kueleza kwamba watakao ingia kaburini ni wachache.

Hata hivyo Mbunge Magige akiwa na kundi lake aliamua kuvamia kwa kuvunja lango la kuingilia ndani ya shamba Hilo na kufanikisha kushiriki mazishi kwa kuweka shada la maua kaburini.

Watu walipokuwa kwenye kaburi walijawa na taharuki kuona Mbunge huyo akiongoza kundi la wanawake kuingia ndani ya shamba ambako mwili wa marehemu ulizikwa.

Kabla ya mazishi hayo Magige alidai marehemu alikuwa mchumba wake lakini ndugu wa marehemu wakidai huyo alikuwa mwizi Kama wezi wengine wa wanaume na familia inamtambua mke halali wa marehemu ni Aziza Msuya.

Marehemu ameacha watoto watatu wa mke wake wa ndoa Aziza Msuya aliyefunga naye ndoa ya kikristu mwaka 2003mjini Dodoma.
Wanaume wenye mahawara wanapaswa kujua madhira wanayowasababishia watoto na wake zao baada ya kufa. Ni aibu na ujinga mtupu ukiachia mbali ubinafsi. Angekuwa anafaa si angemuoa badala ya kumweka kinyumba.
 
Back
Top Bottom