Uchaguzi 2020 Polepole: Kuna mgombea mmoja amekimbia yupo nje ya nchi, ameona maji yamemfika shingoni. CCM tunafanya kampeni za kisayansi

Uchaguzi 2020 Polepole: Kuna mgombea mmoja amekimbia yupo nje ya nchi, ameona maji yamemfika shingoni. CCM tunafanya kampeni za kisayansi

Wazo Kuu

Senior Member
Joined
Oct 21, 2018
Posts
114
Reaction score
295


Kampeni za CCM 2020 tunazifanya kisayansi, tumegawanya viongozi waandamizi wa chama kwenye maeneo tofauti. Msafara mkuu unaongozwa na Dkt. Magufuli, msafara mwingine wa Mhe. Samia Suluhu, na mwingine unaongozwa na Kassim Majaliwa, sisi hatutumii chopa." - Humphrey Polepole.

Mzee Jakaya Kikwete yupo Ukanda wa Kusini kule anavuruga, Mzee Pinda na Spika Job Ndugai nao wanaendelea. Muziki ni mzito mpaka sasa tunapozungumza kuna mgombea mmoja amekimbia yupo nje ya nchi, ameona maji yamemfika shingoni, tunafanya kampenzi za kisayansi." -Humphrey Polepole

Tangu Mhe. Magufuli aingie madarakani hakujawa na mfumuko wa bei, tumefanya kazi nzuri mno, bidhaa haiongezeki, Mhe. Magufuli amefuta kodi kwa wenye mishara midogo, hawa wanaosema ni wapotoshaji, tumelazimika kuwajibu, tunawaambia wasifanye siasa na hivyo." - Humphrey Polepole.

"Ukisema kushuka kwa Diplomasia ni uongo, Mhe Magufuli ameingia tu madarakani akapewa Uenyekiti wa EAC, ameendeleza mwendo wa kubana matumizi, miradi mikubwa imefanyika, ameacha alama, SADC amefanya mambo makubwa, MSD inapeleka dawa nchi zote za SADC." - Humphrey Polepole.

Tumefuatilia na kujiridhisha kwamba ni uongo mtupu, na TCAA imeshatoa ufafanuzi, lakini unajiuliza nini dhamira ya kusema uongo, kwamba mmezuiliwa kwenda kufanya kampeni maana yake unataka kupandikiza chuki, na hata hakukuwa na mpango wa safari"
 
Bofya hapa


Kampeni za CCM 2020 tunazifanya kisayansi, tumegawanya viongozi waandamizi wa chama kwenye maeneo tofauti. Msafara mkuu unaongozwa na Dkt. Magufuli, msafara mwingine wa Mhe. Samia Suluhu, na mwingine unaongozwa na Kassim Majaliwa, sisi hatutumii chopa." - Humphrey Polepole.

Mzee Jakaya Kikwete yupo Ukanda wa Kusini kule anavuruga, Mzee Pinda na Spika Job Ndugai nao wanaendelea. Muziki ni mzito mpaka sasa tunapozungumza kuna mgombea mmoja amekimbia yupo nje ya nchi, ameona maji yamemfika shingoni, tunafanya kampenzi za kisayansi." -Humphrey Polepole

Tangu Mhe. Magufuli aingie madarakani hakujawa na mfumuko wa bei, tumefanya kazi nzuri mno, bidhaa haiongezeki, Mhe. Magufuli amefuta kodi kwa wenye mishara midogo, hawa wanaosema ni wapotoshaji, tumelazimika kuwajibu, tunawaambia wasifanye siasa na hivyo." - Humphrey Polepole.


"Ukisema kushuka kwa Diplomasia ni uongo, Mhe Magufuli ameingia tu madarakani akapewa Uenyekiti wa EAC, ameendeleza mwendo wa kubana matumizi, miradi mikubwa imefanyika, ameacha alama, SADC amefanya mambo makubwa, MSD inapeleka dawa nchi zote za SADC." - Humphrey Polepole.

119057614_197973511683765_7178176507246786920_n.jpg
 
Tangu Mhe. Magufuli aingie madarakani hakujawa na mfumuko wa bei, tumefanya kazi nzuri mno, bidhaa haiongezeki,
Sukari ?

Unajua kama mtu anaweza kudanganya moja kwanini asidanganye mawili au matatu au yote?, tangu huyu jamaa aache kuongelea issue na kuamia kwenye mipasho na taarabu wala huwa simpi time ya kumsikiliza
 
Polepole aache kusaka pointi za mezani, huyo Membe hajawahi kuwa mshindani wa kweli wa Magufuli. Mshindani wa kweli wa Magufuli ni Lisu. Kama Membe alishindana na Magufuli, basi ni wakati akiwa ccm sio nje ya hapo. Huyo Membe hata angekuwa anapiga kampeni usiku na mchana hana lolote jipya, hivyo asijifanye eti kakimbia kwa kuwaogopa ccm.
 
Hivi kuna watu wanaweza kupoteza muda kumsikiliza Polepole?
Ndugai atafanya kampeni jimbo gani? Nani anamjua? kwa lipi? Wangekuwepo Mh. Sitta hapo sawa.
 
Back
Top Bottom