Uchaguzi 2020 Polepole: Upinzani wamekuwa mstari wa mbele kutumia uongo kama nyenzo ya kampeni, adai Lissu ana tatizo la 'memory'

Nimekuja mbio nikidhani anamchanachana na mapanga,kume kwa maneno ya kwenye khanga
 
Wale watu wanapenda uongo wa kupitiliza au wakujiondoa ufahamu.Lakini yote tisa baada ya uchaguzi ndio wao wa kwanza kuunga juhudi za Magufuli.
Hawana namna,wataunga juhudi tu.Huyu jamaa tuliemwachia Uhuru wa kutukana jeshi,nadhani baada ya uchaguzi atarudi alikotoka.
 
Hahahahahahhaha hivi Kwa nini mnaichukia chadema? Ndio maana mlitaka Hadi mbatia awe chama kikuu cha upinzani mkashangaa chadema inawapepeta sijui kaishia wapi mbatia
Joyce nilikuwa namjibu huyo mtu anayedhani CCM Ina hati miliki kwenye Taifa hilo
 
Vipi Kuhusu mifuko ya jamii na Mafao?

Pole pole amejibu Kuhusu FAO la kujitoa na kuchelewa Malipo?

Na ardhi eka 25000? Amejibu huyo.

Je kurudishia watu Pesa zao za vitambulisho?
Napesa za rambirambi za wahanga wa tetemeko Bukoba amezitolea ufafanuzi?

Ameonyesha sitakabadhi za ununuzi wa ndege?
 
Wakati wa kampeni huwezi kukaa kimya ukizingatia ni mtu mwenye maneno mengi yenye ujumbe unaopotosha.

Kuwaambia watu uhalisia wa jambo linalopotoshwa kisiasa ni sehemu ya kampeni.
Kwenye kampeni kila mgombea anaongopa tukianza na Magufuli Ni muongo kupindukia, mbaguzi kupindukia, mkabila kupindukia ,mbinafsi kupindukia na mengine mengi tu
 
Kwenye kampeni kila mgombea anaongopa tukianza na Magufuli Ni muongo kupindukia, mbaguzi kupindukia, mkabila kupindukia ,mbinafsi kupindukia na mengine mengi tu
Hana uongo wowote aliahidi kufufua shirika la ndege akikuta lina ndege moja mbovu na sasa zipo kumi na moja.

Hana ukabila wowote, zahanati, shule za sekondari na msingi zinajengwa nchi nzima. Upanuzi wa bandari ni wa nchi nzima.

Hana ubaguzi wowote, serikalini kuna walemavu wa ngozi na viungo wenye vyeo vikubwa tu.
 
Vip laptop kwa kila mwalimu na milioni hamsini Kila Kijiji, Bado katiba mpy zote zilikuwa ahadi zake na Nilimpigia kura kea kujua kuwa Tanzania ya viwanda itakuwa lakini ninayo yashuhudia Ni Kama haya

Sent from my TECNO B1p using JamiiForums mobile app
 
Hizo laptop ni mchakato wa muda mrefu.

Kuna zahanati kila wilaya ambazo zina lengo la kuimarisha afya za watu, Hizo zina thamani kuliko milioni 50 zinazotumika leo na kesho zikawa zimeisha.

Kuna kazi kubwa inafanyika nchi nzima na wenye akili tunasema: kazi iendelee.
 

Kigogo ni mpuuzi mmoja kama wapuuzi wengine.

Kasahau kuwa dunia ina corona mwaka huu na biashara nyingi kubwa zimeyumba.

Makampuni makubwa ya China na US yamepunguza watu wengi tu sembuse Bakhresa anayeuza ngano na juice.
 

Alichosema Ndg Humphrey Polepole ni kweli.
Tundu Lissu amekua ni Mtu wa kudanganya Umma wa Watanzania wanaoenda kumsikiliza kwenye kampuni zake.
Kadanganya kuhusu Uwanja wa Wandege wa Mpanda, Kadanga kuhusu treni, Kadanganya kuhusu vitambulisho vya wamachinga.
Amekosa mwelekeo, Anatafuta kura kwa kusema uongo.
 
Ni kweli tume itaamua imtangaze nani,
Lakini Kama kura zetu zitaheshimiwa .
Mtabaki midomo wazi.
 
mimi kuusema uwanja wa Mpanda kuwa haufai aminivuruga kwa kweli.uwanja ule una manufaa kweli.yeye mwenyewe anapanda.Nitoe wito watanzania wasidanganyike.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…