Uchaguzi 2020 Polepole: Zitto Kabwe atafute kazi nyingine, 2020 hatarudi Bungeni

Uchaguzi 2020 Polepole: Zitto Kabwe atafute kazi nyingine, 2020 hatarudi Bungeni

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole amefunguka na kusema Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe mwaka 2020 atafute kazi nyingine ya kufanya kwa sababu jimbo hili litarudi kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM)

View attachment 718311

Polepole amesema hayo Machi 17, 2018 wakati akifanya ukaguzi wa mradi wa kusambaza maji mkoa wa Kigoma ambapo amesema kuwa wanataka kuhakikisha kuwa mkoa huo unapata maji safi kabla ya mwaka 2020.

"Mkandarasi ameniahidi mpaka mwezi wa tano maji yataanza kutolewa kwa karibia asilimia mia moja katika mji wote wa Kigoma Ujiji na maeneo ya pembezoni na mimi nimezungumza na viongozi wenzangu wa CCM wafike hapa mwezi mmoja kutoka leo kujiridhisha juu ya maendeleo ya kukamilisha mradi huu na kupeleka maji katika mji wetu wa Kigoma , sisi tunafanya hivi sababu tunao mkataba na wananchi na tunataka kuukamilishe mapema kabisa kabla ya 2020 ili ifikapo 2020 basi mbunge wa hapa atafaute kazi nyingine" alisisitiza Polepole

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole yupo mkoani Kigoma katika ziara ya Kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mwaka 2015 - 2020

Chanzo: EATV
Waziri Mkuu wakati huo Mizengo Pibda aliwahi kusema hivyo hivyo na bado Zitto akapera uchaguzi uliofuata. Dua la kuku halimpati mwewe.
 
Kama ni kwa nguvu ya wananchi sawa, ila kama ni kwa nguvu ya dcm, napata mashaka kidogo
 
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole amefunguka na kusema Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe mwaka 2020 atafute kazi nyingine ya kufanya kwa sababu jimbo hili litarudi kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM)

View attachment 718311

Polepole amesema hayo Machi 17, 2018 wakati akifanya ukaguzi wa mradi wa kusambaza maji mkoa wa Kigoma ambapo amesema kuwa wanataka kuhakikisha kuwa mkoa huo unapata maji safi kabla ya mwaka 2020.

"Mkandarasi ameniahidi mpaka mwezi wa tano maji yataanza kutolewa kwa karibia asilimia mia moja katika mji wote wa Kigoma Ujiji na maeneo ya pembezoni na mimi nimezungumza na viongozi wenzangu wa CCM wafike hapa mwezi mmoja kutoka leo kujiridhisha juu ya maendeleo ya kukamilisha mradi huu na kupeleka maji katika mji wetu wa Kigoma , sisi tunafanya hivi sababu tunao mkataba na wananchi na tunataka kuukamilishe mapema kabisa kabla ya 2020 ili ifikapo 2020 basi mbunge wa hapa atafaute kazi nyingine" alisisitiza Polepole

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole yupo mkoani Kigoma katika ziara ya Kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mwaka 2015 - 2020

Chanzo: EATV
Kuna muingiliano wa madaraka, na baadhi ya viongozi wa chama kujisahau na kudhani wanaongoza serikali. Polepole hastahili kabisa kukagua na kuagiza watekelezaji wa miradi ya serikali. Lakini kwa kuwa ni siasa za kuzomeana, tunawasikia wakijiaminisha serikali ni yao. Serikali ikishaundwa siyo mali ya chama.

Hata hivyo jambo moja la kushangaza ni jinsi Polepole alivyojionyesha kutoka mtu aliyedhaniwa kuwa na uwezo wa fikra hadi mtu asiyeweza kabisa kupambanua mambo. Alivyo sasa hivi ni kama ana bahatisha mambo. Au, tatizo ni vyombo vya habari vilivyomuonesha kama kijana anayeweza kumbe anakumbuka tu yale aliyo kariri shuleni. Anakatisha tamaa!!!!!
 
Mpaka 2020 kwani project yake ya kununua madiwani na wabunge imephase out?
Hii zana ya kununua ni kichaka kipya cha ufipa boys kujificha ili wapate nafuu wakati chama kinateketea.

Stop this nonsense .
 
Hii ni kweli kabisa. Nitafanya kazi ya Urais
Bw. Zitto anayoyasema Polepole, anamaanisha. Kiasi hata wewe ulikuwa mgumu wa kuenda na wakati, na ukajitenga na wenzako. Tangu Rais huyu anaaanza, wenzako walisusia hotuba yake kwa Bunge, wewe ukatofautiana na wenzako. Ukishakuwa pamoja na adui, ujue aliyeko pembeni hakutofautishi na adui yako. Itakuwa vigumu sana wana Kigoma kukutofautisha na CCM.
 
Si hairuhusiwi Kufanya Siasa?
Huyu Mbona anazunguka daah hata sielew kwakweli..
 
Watu wa Kigoma hawadanganyiki kirahisi,Ngoja tusubiri hiyo 2020 tukiwa hai tutashuhudia
 
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole amefunguka na kusema Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe mwaka 2020 atafute kazi nyingine ya kufanya kwa sababu jimbo hili litarudi kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM)

View attachment 718311

Polepole amesema hayo Machi 17, 2018 wakati akifanya ukaguzi wa mradi wa kusambaza maji mkoa wa Kigoma ambapo amesema kuwa wanataka kuhakikisha kuwa mkoa huo unapata maji safi kabla ya mwaka 2020.

"Mkandarasi ameniahidi mpaka mwezi wa tano maji yataanza kutolewa kwa karibia asilimia mia moja katika mji wote wa Kigoma Ujiji na maeneo ya pembezoni na mimi nimezungumza na viongozi wenzangu wa CCM wafike hapa mwezi mmoja kutoka leo kujiridhisha juu ya maendeleo ya kukamilisha mradi huu na kupeleka maji katika mji wetu wa Kigoma , sisi tunafanya hivi sababu tunao mkataba na wananchi na tunataka kuukamilishe mapema kabisa kabla ya 2020 ili ifikapo 2020 basi mbunge wa hapa atafaute kazi nyingine" alisisitiza Polepole

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole yupo mkoani Kigoma katika ziara ya Kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mwaka 2015 - 2020

Chanzo: EATV
Polepole anaamini kwamba siasa ndio ajira pekee !
 
Si hairuhusiwi Kufanya Siasa?
Huyu Mbona anazunguka daah hata sielew kwakweli..
Kwa kuwa yeye ni chama tawala kilichopewa dhamana na watanzania na anawajibu wa kuihoji na kuisimamia Serikali vilivyo...!Sasa zitto anamuiga kwa kutaka kwenda kukagua miradi isiyomhusu huku akikwepa kutokea kwenye vikao vya baraza la madiwani kwenye halmashauri yake.
 
Zito ajikite kunako kilimo cha umwagiliaji maana cha kutegemea mvua na kama kufanya siasa tu.
 
Hivi hiyo miradi ni pesa za CCM au pesa za walipakodi??? Sasa kivp CCM wanaruhusiwa kukagua miradi ila zitto akienda kwenye miradi inayotekelezwa na madiwani wa kata zilizo chini ya ACT wanazuiwa???

Polepole anachofanya ni siasa ila nashangaa wapinzani wanaambiwa siasa mpala 2020!! Kujipigia kampeni kama hivyo ni siasa tosha sasa sielewi walichozuia ni kipi???

Hizo ni pesa za walipakodi hivyo mradi ni wa umma sio wa chama flani cha siasa kiasi wakitumie kama kampeni ya 2020!!!

Ajifunze kwa nape leo ngoja ajipendekeze mwisho wake utafika tu
Tulia usome kwa umakini uelewe si kukimbilia kujibu
 
Wapiga kura wamemkataa?. Afunguke zaidi maana kilichomo kwenye box hatukijui.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole amefunguka na kusema Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe mwaka 2020 atafute kazi nyingine ya kufanya kwa sababu jimbo hili litarudi kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM)

View attachment 718311

Polepole amesema hayo Machi 17, 2018 wakati akifanya ukaguzi wa mradi wa kusambaza maji mkoa wa Kigoma ambapo amesema kuwa wanataka kuhakikisha kuwa mkoa huo unapata maji safi kabla ya mwaka 2020.

"Mkandarasi ameniahidi mpaka mwezi wa tano maji yataanza kutolewa kwa karibia asilimia mia moja katika mji wote wa Kigoma Ujiji na maeneo ya pembezoni na mimi nimezungumza na viongozi wenzangu wa CCM wafike hapa mwezi mmoja kutoka leo kujiridhisha juu ya maendeleo ya kukamilisha mradi huu na kupeleka maji katika mji wetu wa Kigoma , sisi tunafanya hivi sababu tunao mkataba na wananchi na tunataka kuukamilishe mapema kabisa kabla ya 2020 ili ifikapo 2020 basi mbunge wa hapa atafaute kazi nyingine" alisisitiza Polepole

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole yupo mkoani Kigoma katika ziara ya Kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mwaka 2015 - 2020

Chanzo: EATV
 
Back
Top Bottom