Polisi: Magari ya abiria kuingia Tanga mwisho saa sita usiku

Polisi: Magari ya abiria kuingia Tanga mwisho saa sita usiku

Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limepiga marufuku, magari yanayosafirisha abiria kufanya safari usiku wa zaidi ya saa sita na kwamba atakaekaidi agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

RPC wa Tanga, Safia Jongo amesema: “Ukiwa unatokea Dar kama hesabu zako zitakuonesha kuwa utafika Mkata zaidi ya saa sita usiku, ujue mtaalala hapo hamtapita.

“Hatua hiyo ni kutokana na wimbi la ajali katika barabara ya Tanga - Segera, hii itahusu magari yote ya abiria.”

Chanzo: Millard Ayo
Hivi sasa tuna majimbo? Kila sehemu sheria zao.
 
Bora angetangaza kusimamisha giza lisiingie na mvua isinyeshe Tanga...😂
 
Mimi nishazoea nafanya mishe zangu mpaka saa mbili usiku nasogea hapo Kibo ubungo, nakamata kosta mpka njia panda.

Sasa haya Matamko vipi tena
 
Mimi nishazoea nafanya mishe zangu mpaka saa mbili usiku nasogea hapo Kibo ubungo, nakamata kosta mpka njia panda.

Sasa haya Matamko vipi tena
Hao polisi wanawaambia majambazi kwamba kuanzia saa 6 wao hawapo kwa hiyo ni zamu ya majambazi.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limepiga marufuku, magari yanayosafirisha abiria kufanya safari usiku wa zaidi ya saa sita na kwamba atakaekaidi agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

RPC wa Tanga, Safia Jongo amesema: “Ukiwa unatokea Dar kama hesabu zako zitakuonesha kuwa utafika Mkata zaidi ya saa sita usiku, ujue mtaalala hapo hamtapita.

“Hatua hiyo ni kutokana na wimbi la ajali katika barabara ya Tanga - Segera, hii itahusu magari yote ya abiria.”

Ajali zenyewe zinatokea mchana kweupee
 
Suluhu ya yote aya ni kupanua au kujenga barabara zetu katika ubora. Tuweke miundo mbinu stahiki kwenye barabara zetu. Mfano vitu kama taa za barabarani kwa ajili ya magari yote uzuri sasa za solar zipo. Taa za kuongoza magari. Camera zenye kupiga picha speed ya chombo na kutoa faini 24 hrs.

Camera za kurekodi matukio ya barabara kwa ajili utambuzi au kutoza faini kunapotokea uharibifu.
 
... hili linatakiwa kuwekwa clear maana magari mengi ya misiba (coasters, etc.) yanakuwa yamebeba abiria (unless by definition hao sio abiria). Kuulaza msiba barabarani tangu saa 6 hadi 12 ndipo safari ianze ina changamoto zake.
 
dah ila mambo mengine tunalaumu tu lakini uhalisia kwenye ground ni tofauti sana, hiyo barabara ya Dar - Tanga via Chalinze au via Msata ni nyembamba sana, halafu ina malori mengi sana yanayotembea usiku kucha...Gari ndogo pia nyingi sana zinasafiri 24hrs kuelekea Tanga, Moshi na Arusha + coaster za viroba vya ndugu zetu wachaga kwenda Moshi/Arusha...

Ajali za malori kutoka na miundombinu mibovu ya barabara, uzembe wa madereva ni nyingi sana, hali hii inafanya hiyo barabara kuwa hatari sana kusafiri usiku...bus tukumbuke linabena 65passengers likikutana na kicheche usiku ni hatari tupu..
 
suluhu ya kudumu kwa sasa ni kujenga barabara pana, kuweka mataa barabarani, kufunga cameras za speed na za kucontrol mienendo ya barabara... Kupunguza flow ya malori usiku baadhi ya maeneo hatarishi nk..
 
Kuna clip niliiona kuna gari za msiba zimezuiwa watu wanalalamika..
 
Tusirudishane nyuma tafadhali. Nchi gani hii mishe zopigwe mchana tu? Tusipangiane muda bhana, kila mtu atimize wajibu wake ili maisha yasonge mbele.
 
Kumbe serikali za majimbo zinatawala kimyakimya. Kesho mkoa mwingine itatoa tamko lao. "Mwisho kuendesha magari ni saa saba ya mchana ili kuepusha ajali za barabarani."
Mmeshindwa kutatua tatizo la ajali barabarani, sasa polisi wamepanick na kuanza kutoa matamko yasiyokuwa na kichwa wala miguu.
 
... hili linatakiwa kuwekwa clear maana magari mengi ya misiba (coasters, etc.) yanakuwa yamebeba abiria (unless by definition hao sio abiria). Kuulaza msiba barabarani tangu saa 6 hadi 12 ndipo safari ianze ina changamoto zake.

Magari ya msiba si huwa pamoja na jeneza mkuu?

Hata hivyo katazo hili halijakaa sawa ukichukulia barabara kuu zinazopita wilaya kadhaa za Tanga ni barabara kuelekea mikoa tofauti na Tanga Arusha, Kilimanjaro, Manyara...

Pili sheria za barabarani sio mali ya mamlaka ya mkoa fulani, bali nchi nzima...

Mamlaka ya usimamizi ya usafiri ni ya nchi nzima na sio mkoa fulani na fulani...

Wao kama mkoa namna pekee wanaweza wakadhibiti ajali labda wawe wanatoa escort, au wafunge kamera za usalama, au waongeze tochi...n.k
 
Jee, ni halali kila mji kujiwekea sheria zake? Miaka ya 80 sheria ilipitishwa kukataza usafiri wa usiku kwa nchi nzima. Hilo sawa kwa kuwa lilihusu nchi nzima. Hili la kuweka sheria zinazohusu mji mmoja mmoja lina utata. Kwa mfano gari la abiria linatoka Mbeya kwenda Tanga likaharibika kilomita 100 kutoka Tanga; wakalishughulikia likatengamaa saa sita kasoro za usiku. Ni halali hilo gari kuendelea na safari kutoka hapo lilipoharibikia mpaka ukingoni mwa Tanga halafu hapo lisiendelee kwa kuwa saa sita usiku itakuwa imegonga tayari?

Labda huu nao ni mkoa wa wenyewe kama yule ndugu
 
Back
Top Bottom