Polisi wa Zanzibar kuwakamata watu kisa kuwakuta wakila mchana kipindi cha Ramadhan ni uvunjifu wa sheria za Nchi


1. Ujinga kama huu ndiyo unaowapa wajinga wengine kama kina MK254 kuwa na la kusema.

2. Imani yako wewe inatuhusu vipi wengine tusiohusika?

3. Kwani hata umejua je kama hao wengine wanataka kwenda huko mbinguni kwenu?

4. Kwanini hudhani labda mbingu yenu kwingine ndiyo jehanum?
 
Mimi muislam ila hii sheria sijaikubali.
Ni mambo ya kijinga kwa mimi navyoona.
 
Kitu kingine kinachoshangaza, wanasema kuna sheria,ila raia wanajichukulia sheria mkononi. au hiyo sheria ya zanzibar imesema watu wachukue sheria mkononikuchapa wengine viboko?

Na kama sheria inakataza kuchukua sheria mkononi, mbona hao waliojirekodi wakipiga wengine hawajachukuliwa hatua zozote? mwinyi anaruhusu hili na anafurahi ikiwa hivyo. Au kwasababu sio dini ya amani wanaogopa watasababisha kuvunjika kwa amani wakiwakamata hao waliopiga wengine?

Ndio maana tunasema watu waukimbie uislam kwasababu sio dini ya amani, ni ya ukatili. ushahidi mojawapo ni kama huu.
 
hakuna sheria inaelekeza wachukue sheria mkononi kupiga wenzao fimbo, wamejirekodi wakifanya hivyo, tunatarajia mwinyi aelekeze wakamatwe ili wachukuliwe hatua za kujichukulia sheria mkononi. ama la, yeye anabariki ukatili huu.
 
ninachoshangaa, unasema kula mwezi wa ramadhani ni ushetani, bila kujua kuwa uislam wenyewe ni ushetani. au tukufafanulie zaidi huo ushetani? utakuwa tayari kupata za uso?
Nafikiri suala ambalo linabidi tulifahamu ni hekima tu. Kama inavyosemwa; Ukiwa Roma fanya kama Roma wanavyofanya.

Wao kwao Zanzibar wamefanya ni utamaduni katika nchi yao basi ni kuheshimu tu tamaduni yao.

Ni kama tunavyoheshimu tamaduni za budha, wayahudi na waislamu kuwa kwao haifai kusalimiana kwa kupoana mikono na wanawake.

Kwa namna hiyo tukiwa Zanzibar kipindi cha mfungo tusile hadharani.
 
Nakuunga mkono kaka! Umenena vyema kabisa.
 
hakuna sheria inaelekeza wachukue sheria mkononi kupiga wenzao fimbo, wamejirekodi wakifanya hivyo, tunatarajia mwinyi aelekeze wakamatwe ili wachukuliwe hatua za kujichukulia sheria mkononi. ama la, yeye anabariki ukatili huu.
Hapo kweli wamefanya kosa.
Na mimi nataraji kusikia kauli kutoka kwa viongozi wao.
 
sheria inakataza kufanya hivyo sawa, basi tuamini hivyo, hoja ni je, sheria imesema mtu akamatwe na kupelekwa vyombo vya dola au achapwe viboko na raia? yaani raia wajichukulie sheria mkononi?
Sijakuelewa.
Maana hakuna sheria katika uislam inayoruhusu kwa wanachofanya Zanzibar.
Labda sijakuelewa unaulizia sheria ipi.
Kufunga ni kwa mtu mwenyewe wengine hawahusishwi hata wawe wanakula hadharani.
Japo kibusara si vizuri kula hadharani kipindi hiki,ila hakuna sheria iliyowekwa ya kumhukumu mtu akila hadharani.
 
Sidhani kama mtume aliwatuma kushambulia watu physically kama ndio njia ya kupambana na shetani, hiyo ni aina tu ya social terrorism.

Why utandike bakora mtu mzima tena kwa issue ndogo kama kula hadharani.

Nadhani busara ni kuongea nae kwa kumuelekeza na kumuomyesha sehemu sahihi ya kula chakula chake.

Halafu jambo lingine kula hakuna uhusiano wowote na kuharibu swaumu ya mtu.

Wewe umefunga unawaza nini kichwani kwako hadi uwe distracted na mtu anayekula chakula chake na hajakulisha wala hakukuita ule?

Wewe komaa na funga yako tena fanya busara ya kukaa ndani kama ukitoka nje unaharibiwa funga yako na watu wanaokula hawajafunga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…