Polisi "wame-underestimate impact" ya kumtuhumu Mbowe kwa makosa ya ugaidi?

Polisi "wame-underestimate impact" ya kumtuhumu Mbowe kwa makosa ya ugaidi?

Siku nzuri kwa kiongozi ni pale gaidi likitiwa nguvuni.
 
Rais, ambaye ni amiri jeshi mkuu, kasema subirini kwanza mambo ya katiba mpya, yeye anaanzisha makongamano (ni uasi huo). RC na DC wanasema ili kudhibiti corona tupunguze mikusanyiko isiyo ya lazima, ya lazima iombewe kibali, yeye anawaita wajinga. Huoni kama hizo ni chokochoko?
Siyo kweli na wala hizo siyo vurugu, unajua kuwa leo kuna mechi ya simba na yanga? Hapo corona inakuwa likizo au hilo walizungumziaje? Ok waweza weka ushahidi/clip ya Mbowe akiwaita wajinga?
 
Sehemu salama ya Gaidi ni jela, Mbowe yupo sehemu anayostahili, anapiga story na kunguni tu, hakuna mwekezaji serious anayeona Mbowe ni mtu muhimu, hizi story zenu za vijiweni zibaki huko huko kwa nyumbxxx wenzio.
Nashangaa hadi saivi Gwantanamu hawajaomba tu export mtu wao wakamuhifadhi gereza kuu la magaidi Duniani.

Hapo ndo unaona Marekani haijatambui

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Toka nchi hii ipate uhuru kuna kesi kama mbili ama tatu za Uhaini. Lakini toka tumepata kuanza mfumo wa vyama vingi vya kisiasa kumekuwepo na kamatakamata hasa kule ambapo Samia katoka Zanzibar kutokana na mfumo wao wa Siasa za chuki.

Magufuli alikuwa mhuni tu na ukatili wake wa kumalizana kikatili kisiasa kwa Wapinzani wake uongozi wake uliweza kutumia mfumo wa kueliminate Wapinzani mfano hai ni tukio la Lissu. Pamoja na mambo yake kidogo alikuwa na haya ama aibu kwa kuogopa kuonekana mbele ya jamii ya wastaarabu ukatili wake kukaundwa msemo wa watu wasiojulikana.

Huyu mama sijui anatafuta nini ama haelewi kuwa kapachikwa pasi moja mbaya sana kutokana na kusifiwa kuwa anaupiga mwingi sasa kapewa pasi mkasi kwa kumpa Kiongozi wa Chama kikuu cha Upinzania kesi ya Ugaidi. Mama ajue kabisa kajitafutie ubaya na waliokuwa wanampenda.

Hofu yake ni nini kwani angeacha haya makongamano ya kudai katiba mpya angepungukiwa na nini? Kenya wanaupinzani Mkubwa na kufikia hatua ya Mpinzani kujiapisha kuwa Rais wa watu wa Kenya hatukusikia Ugaidi wala Uhaini.

Mama nakutabiria utaongoza hii nchi kwa hofu kubwa sana. Tegua huu mtego ambao wapinzani wako ndani ya CCM hasa akina Mwigulu wanakupigia ngoma unaicheza.

Zipa masikio acha kukanyaga Katiba ruhusu watu waongee. Wewe ni mama unajisikiaje mtoto wa mwanamke mwenzio anasokomezwa kesi ngumu kuwa na huruma.
Sukuma Gang wamemset naye kajaa mzima mzima kwenye fremu yao,walio wanagongesheana glass
 
the basis of all the definitions given by scholars all over the world and. -the real issues involved in terrorism , terrorism could be defined here as an act or threat of an act of tactical violence by a group of trained individuals, having international linkage, to achieve political objective.
 
MUJINI tunasema IMEKULA KWAO sasa polisiccm wanahaha jinsi ya kumuachia mtuhumia wa ugaidi bila dhamana. Ngoja tusubiri tuone hii kasheshe inavyoendelea. Nimetokea kuipenda sana Twitter kwani kwenye sakata kama hili la Mbowe ni rahisi sana kuvitag vyombo vya habari vikubwa duniani ná pia Viongozi wakubwa duniani hasa wale wa nchi za Magharibi AKA BEBERUS,
Ukiacha kelele zinazopigwa kwa nguvu Sana hapa nchini Tanzania za kutakiwa, Freeman Mbowe aachiwe huru, kutokana na makosa yanayoonekana wazi kuwa Jeshi la Polisi nchini limeamua "kubambika" ya ugaidi, lakini vyombo mbalimbali vya dunia navyo vimeungana na wapigania haki wa hapa nchini, kama vile mashirika ya habari ya CNN na Aljazeera na BBC, yamejitokeza na kuipa "headline" hiyo taarifa ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kupata tuhuma hiyo nzito ya ugaidi.

Madhara ya serikali hii kumbambikia Freeman Mbowe Makosa hayo ya ugaidi ni makubwa Sana kuliko tunavyofikiria.

Lazima ifahamike wazi kuwa wawekezaji ambao walikuwa wanafikiria kuleta mitaji yao hapa nchini, baada ya kuona mabadiliko ya uongozi wa juu, baada ya kufariki Rais Magufuli, watasita kufanya hivyo, kutokana na kuogopa kuleta mitaji yao kwenye nchi ambayo uongozi wa nchi umeutangazia dunia kuwa kiongozi mkuu wa chama cha upinzani cha Chadema, anatuhuma za ugaidi!

Lakini ukiangalia mwenendo wa viongozi wakuu wa nchi hii, wanatumia mwanya wa wanaodai Katiba yetu ya nchi, kuwabambikia viongozi wa upinzani kwa Makosa yasiyokuwa na dhamana ya ugaidi, kwa lengo tu la kuwakomoa, kutokana na kupigania haki za watanzania, ambapo wao viongozi wa serikali hawapendi watanzania waipate haki hiyo!

Kwa hiyo tutarajie wawekezaji kutoka nchi za nje kupungua Sana kuja hapa nchini kutokana na hofu hii, waliyoianzisha wao viongozi wa serikali, kuwa nchi yetu ina magaidi!
 
Kila ukipita mitaani, hata wale wwnaCCM wenye akili timamu, wanasema wazi kuwa kwenye hili huyu Bibi ameharibu, na kukitia aibu chama.
Mtaa gani Mheshimiwa?

Mtaani watu wanajishughulisha na mambo yao. Wengine hawajui hata kilichotokea huko Mwanza.

Tatizo linakuja huu ukweli hamtaki kuukubali. Bali mtatoa lugha zisizo na staha kwa anaye wasilisha hili. Nguvu ya mwanasiasa ni umma. Umma wa mitandaoni (hususani Jf na Twitter) ndiyo huu tunaoishi nao mtaani kwa sababu raia ndiyo sisi. Lakini inapokuja lililokwenye ardhi ya mtandaoni na ardhi inayokanyagwa na raia mtandaoni ni mazingira tofauti hili linapaswa kuhijiwa, niaje tena?

Ndiyo maana nahoji, "kila ukipita mtaani ni mtaa gani huo? Juma lililopita nimejichanganya kwenye mazingira tofauti ya kwenye daladala, kukaa vituoni, kwenye nyumba za ibada, makazini na mtaani pia. Lakini sijaona na kusikia hata mmoja akizungumzia lililowakuta Mwanza.

Hii ni nguvu ya kwenye mitandao, italeta athari (pengine) kimataifa lakini wengi katika raia hawajui hili! Kwa tafsiri nyengine Chadema haijawekeza vya kutosha kwa raia ambao ni Wtz wenyewe. Wao wamewekeza kwenye mitandao ambao ni makada wao (hili halikwepeki) na kwenye Jumuiya za Kimataifa. Hili ni kosa! Itatumiwa kama kete kuwa mnatumiwa na mataifa ya nje ili kuvuruga amani ya Tz.

Kingine mnachokosea mnamtuhumu rais na kumtaka Mbowe aachiwe kwa hili. Yeye anaweza kuwajibu kwa urahisi tu kuwa hakutamka Mbowe akamatwe! Ni vyombo vya dola vimefanya hivyo kwa kanuni za kazi zao. Kuwa katiba haimruhusu kuingilia mihimili mingine. Anachoweza kusema ni kuwataka uchunguze uharakishwe ili mtu apatiwe haki yake.
 
Huu ujinga upinzani utawa cost sana, Term iliyopita, madai yale yale ya mashirika ya nchi na vikwazo lkn wajue hao wanaowaita wawekezaji wako na interest ya faida sio mtu.

Halafu bora hata walalamike nchi za kiarabu au mashariki ya mbali sio hao watawala wetu wa zamani.
Mambo yamebadilika sana hata china anataka koloni kwahiyo wao wakilinga China anaona fursa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. Eti hata china anataka koloni. Yani tumeshatawaliwa mpaka tumechukulia ni kawaida
 
MUJINI tunasema IMEKULA KWAO sasa polisiccm wanahaha jinsi ya kumuachia mtuhumia wa ugaidi bila dhamana. Ngoja tusubiri tuone hii kasheshe inavyoendelea. Nimetokea kuipenda sana Twitter kwani kwenye sakata kama hili la Mbowe ni rahisi sana kuvitag vyombo vya habari vikubwa duniani ná pia Viongozi wakubwa duniani hasa wale wa nchi za Magharibi AKA BEBERUS,
Sasa Mkuu hii ni akili yenu. Vipi na wao wakitumia akili kama ya kwenu? Mtafanyaje sasa?

Ninachokiona hapa hamuwakomoi bali mnarahisisha kazi yao.

Suala jengine ni kuvitag vyombo vikubwa ili kuwapa taarifa kinachoendelea nchini kuhusu haswa kinachoitwa demokrasia. Najaribu kuvuta kumbukumbu kipindi cha Magu nguvu aliyoitumia ilikuwa ni kubwa sana na hao Jumuiya za Kimataifa hawakufanya wengi waliyokuwa wakiyataraji.

Tumeona Uganda kilichotokewa kwa Bobby Wine si kizuri lakini hamna walichokifanya na sehemu nyengine tofauti tofauti. Hii inatupa nini?

Cha ziada na cha umuhimu Chadema iwekeze zaidi kwa umma wa Wtz wenyewe ili Wtz wenyewe wawaamini kama ilivyokuwa 2010. Mbali na hapo kwa hizi njia mnazozitumia mtaonekana vibaraka wa nchi za nje.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Maccm mtaji wao mkubwa ni ujinga uliokithiri nchini. Kwa Watanzania wanaojitambua wanasimama bega kwa bega na Chadema. Unadhani ni kwanini maccm YANAHOFIA Katiba mpya ná Tume huru ya uchaguzi Mkuu!?
Sasa Mkuu hii ni akili yenu. Vipi na wao wakitumia akili kama ya kwenu? Mtafanyaje sasa?

Ninachokiona hapa hamuwakomoi bali mnarahisisha kazi yao.

Suala jengine ni kuvitag vyombo vikubwa ili kuwapa taarifa kinachoendelea nchini kuhusu haswa kinachoitwa demokrasia. Najaribu kuvuta kumbukumbu kipindi cha Magu nguvu aliyoitumia ilikuwa ni kubwa sana na hao Jumuiya za Kimataifa hawakufanya wengi waliyokuwa wakiyataraji.

Tumeona Uganda kilichotokewa kwa Bobby Wine si kizuri lakini hamna walichokifanya na sehemu nyengine tofauti tofauti. Hii inatupa nini?

Cha ziada na cha umuhimu Chadema iwekeze zaidi kwa umma wa Wtz wenyewe ili Wtz wenyewe wawaamini kama ilivyokuwa 2010. Mbali na hapo kwa hizi njia mnazozitumia mtaonekana vibaraka wa nchi za nje.
 
Nchi za MAGHARIBI na UGAIDI....

Unapotaja tu ugaidi ,Magaidi ,gaidi ujue nchi za MAGHARIBI hushtuka mno......nimeshangaa eti unasema kuwa NCHI HIZO ZITAKUWA NA HURUMA na wahusika wa vitendo hivyo......

Hivi ni lini nchi hizo zimeanza kuwa na HURUMA NA KUGUSWA NA WANAOHUSIKA NA HAYO MAMBO?!!!

Kwao ukituhumiwa ugaidi basi ujue utatambulika sio gaidi mpaka pale MAHAKAMA ikithibitisha hayo......

Kutuhumiwa si KUHUKUMIWA....

Tusubiri mahakama ifanye kazi yake.....

Nasubiri mahakama ifanye kazi yake zaidi ya humu mitandaoni KUHUKUMU kuwa ANA/HANA HATIA......

#MahakamaNiMuhimiliWaNchi
#KaziIendelee
Kwa jinsi unavyochangia humu inaonekana umepata cheo hivi karibuni ambacho hukustahili kukipata na bahati mbaya sana cheo hicho ni kila kitu kwako na unaamini utaishi nacho Milele.

Ila nikukumbushe tu Mungu yupo.
 
Hataki kujifunza na kubadirika. Mwendazake alivuruga Uchumi na maisha ya kila mtu kwa kuendekeza visasi na siasa za hovyo zilizoitumbukiza Nchi shimoni
Kama hili linatambulika yeye rais akaomba apatiwe muda ili aliweke vizuri hili. Kuna miradi mikubwa ipo nje ya uwezo wa serikali imeachwa na awamu iliyopita.

Kweli kwa kuomba muda kwa hili limekuwa kosa mpaka Mbowe uvumilivu umshinde atumie kauli za nguvu? Ijapokuwa si hisani kwa awamu hii kuwaachilia wafungwa wa kisiasa na wengine hukumu kutoka kurudishiwa mali zao ilimbidi Mbowe atizame ni wapi walipotoka! Itasemwa ni haki, ila haki inataratibu vilevile.
 
Maccm mtaji wao mkubwa ni ujinga uliokithiri nchini. Kwa Watanzania wanaojitambua wanasimama bega kwa bega na Chadema. Unadhani ni kwanini maccm YANAHOFIA Katiba mpya ná Tume huru ya uchaguzi Mkuu!?
Niweke wazi msimamo wangu sina chama!

Hao watanzania wanaosimama bega kwa bega kwa hili siwaoni zaidi ya mitandao miwili ya Jf na Twitter. Amini ninachokuambia kuna wengine hawajui kama Mbowe kakamatwa! Hawajui kama Chadema inadai katiba mpya! Na ni watu wa hapa mjini kabisa!

Ila nilichokiona kwa wale ambao wanaolifahamu hili wanaona ni Makosa ya Mbowe kwa hili kwa sababu siyo hisani rais kutenda haki bali ni kwa mujibu wa sheria ila Mbowe na Chadema wakumbuke ni wapi walipotoka wakikusudia awamu iliyopita kwa maana uhuru unaopatikana sasa hivi tofauti na awamu iliyopita na kesi za wafungwa wa kisiasa zilikuwa zinaachiliwa ama kufutwa na Mbowe mahakama imetaka arudishiwe fedha zake.

Tutarudi tena kwa kufanywa haya si hisani bali ni sheria. Sasa ingeliwafaa wakumbuke ni wapi walipotoka. Mbali na hilo hii nchi ameipokea ikiwa na uchumi hoi. Miradi mikubwa imeachwa kuliko uwezo wa serikali, wahitimu hawana ajira, sekta binafsi zipo hoi n.k kwa hili akaomba apatiwe muda ili atengeneze mazingira yawe angalau kwa kiasi chake. Na ndicho raia wanachokilalamikia kwa sasa.

Sasa ni kipi kilichomfanya Mbowe na Chadema wakose uvumilivu? Hiki ndicho wanachokihoji kwa wale wanaojua na kwa hili wanamlaumu Mbowe mwenyewe kuwa hakuutambua wakati.
 
Wewe ungekuwa ná uvumilivu kama babaako angetandikwa risasi 16 bila kuwa ná hatia yoyote ile? Wewe ungekuwa na uvumilivu kama Ben Saanane na Azory wangekuwa ni ndugu zako Baba mmoja mama mmoja halafu wanapotea kinyemela na Serikali kugoma kufanya uchunguzi?
FYI Chadema wamekuwa wavumilivu kwa miaka 30 sasa. Nchi ina mfumo wa vyama vingi tangu 1991 lakini katiba ya nchi ni ile ta chama kimoja!? Unataka wawe wavumilivu kwa muda gani ili wewe uridhike ná uvumilivu wa Chadema? Miaka 30 mingine!? 😳😳😳😳
Niweke wazi msimamo wangu sina chama!

Hao watanzania wanaosimama bega kwa bega kwa hili siwaoni zaidi ya mitandao miwili ya Jf na Twitter. Amini ninachokuambia kuna wengine hawajui kama Mbowe kakamatwa! Hawajui kama Chadema inadai katiba mpya! Na ni watu wa hapa mjini kabisa!

Ila nilichokiona kwa wale ambao wanaolifahamu hili wanaona ni Makosa ya Mbowe kwa hili kwa sababu siyo hisani rais kutenda haki bali ni kwa mujibu wa sheria ila Mbowe na Chadema wakumbuke ni wapi walipotoka wakikusudia awamu iliyopita kwa maana uhuru unaopatikana sasa hivi tofauti na awamu iliyopita na kesi za wafungwa wa kisiasa zilikuwa zinaachiliwa ama kufutwa na Mbowe mahakama imetaka arudishiwe fedha zake.

Tutarudi tena kwa kufanywa haya si hisani bali ni sheria. Sasa ingeliwafaa wakumbuke ni wapi walipotoka. Mbali na hilo hii nchi ameipokea ikiwa na uchumi hoi. Miradi mikubwa imeachwa kuliko uwezo wa serikali, wahitimu hawana ajira, sekta binafsi zipo hoi n.k kwa hili akaomba apatiwe muda ili atengeneze mazingira yawe angalau kwa kiasi chake. Na ndicho raia wanachokilalamikia kwa sasa.

Sasa ni kipi kilichomfanya Mbowe na Chadema wakose uvumilivu?
 
Back
Top Bottom