Polisi wamenitrack niliokota simu, kesho natakiwa kituoni

Polisi wamenitrack niliokota simu, kesho natakiwa kituoni

zima simu itupilie chini ya uvungu ata miaka alaf tupa line
Haitosaidia, Maana kitendo cha yeye kuchomeka tu laini ya simu, taarifa zake zote, ikiweno majina yote, namba ya NIDA, mahali alipo n.k hata akikimbia ni kazi ndogo kwa polisi kumtrace na kumkamata
 
Siku moja gari la Magereza lilipita spiidi ikadondoka kofia ya afisa magereza. Nikapeleka kituo cha polisi. Yaani pamoja na wema niliofanya niliulizwa maswali mengi sana. Moja ya maswali waliniuliza.
" Kofia kama hii kwanini umeileta polisi kwanini usiiache hapo hapo?"
Swali la kimtego nikawajibu kwamba Kofia hii ina nembo halisi ya jeshi la polisi magereza, kama mhalifu ataipata kazi yake itakuwa ndogo sana ni kujishonea mag Wanda na akikamilisha ataenda gereza lolote na kujifanya askari akafanya uhalifu wowote.
Huwezi amini niliachiwa nikarudi nyumbani. Kesho yake nilipoenda kuripoti nikaambiwa jamaa alienda kituoni kuulizia kama kuna kofia imepelekwa pale. Niliikuta elfu kumi zawadi.
Hahah na ukute akuacha 10 tu waliilamba kiasi,,siku ingine usiende peke ako pale unapoiokota kama upo na watu anagalau sindikizana nao polisi,
 
Msaada wa kisheria simu ya kuokota nakamatwa na polisi. Mama yangu aliokota simu smat phone akanipa sababu yeye Hawezi tumia nikaweka laini hapa nimepagawa,

Hii imekaaje mbaya zaidi aliepoteza simu anadai kwao ilibiwa simu, TV nch 32, jiko la ges plate mbili.

Je, machomokaje katika hili tatizo?
Mkiona kimya mjue nawasiliana na polisi maana wanasumbua balaa
Andaa tu pesa ili wakuachie,hilo kwao tayari ni dili,utaratibu ni kuwa ukiokota simu sio ya kwako unatakiwa kutoa taarifa polisi,kwahiyo kwakuwa hukutoa taarifa wewe tayari ni suspect no.1,mkwala wao wa kwanza watakuweka ndani,then watajifanya wanataka kukufungulia mashtaka ya wizi,msipoelewana kwenye kuwapa chochote hatua inayofuata ni mahamani kwa kosa wizi...
 
Dah umemkosea sana huyo jamaa.

Leo nimeconfirm kichwani ni mtupu hadi sio poa.
Ukweli ubaki kuwa ukweli

Ni heri mnichukie kwa ukweli wangu kuliko kunipenda kwa kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

Ni kondoo tu asiyelijuwa hilo.
 
Zima simu potea. Waachane na wewe.
Hata akizima Laini aliyoweka inautambulisho wa Nida hivyo watadeal na mhusika , ukishaweka laini kupitia IMEI number ya kifaa huwa kunapatikana taarifa za laini, IP address, location n.k kwahiyo hawezi toboa hata kama akizima as longer as walishanasa hizo taarifa.
 
Fanya haraka sana uende kituoni ukaeleze kwa kina kwanini unaokota simu na kukaa nayo kama yako vile badala ya kuipeleka kituo cha polisi . Tena shukuru Mungu hawajasema kuwa ilipoibiwa simu palikuwa pia na millioni kumi pamoja na kadi ya CCM iliyolipiwa Mwaka mzima pamoja na jezi ya yanga Mpya . Msipende vya kuokota okota tu. Tafuta hela ununue smartphone yako na ukiokota nyingine hakikisha unaipeleka haraka sana kituo cha polisi kilicho karibu na wewe.
 
Msaada wa kisheria simu ya kuokota nakamatwa na polisi. Mama yangu aliokota simu smat phone akanipa sababu yeye Hawezi tumia nikaweka laini hapa nimepagawa,

Hii imekaaje mbaya zaidi aliepoteza simu anadai kwao ilibiwa simu, TV nch 32, jiko la ges plate mbili.

Je, machomokaje katika hili tatizo?
Mkiona kimya mjue nawasiliana na polisi maana wanasumbua balaa
Hapo kwa kutumia DOCTRINE OF RECENT POSSESSION wewe ni mwizi na ndiye uliyeiba simu hiyo

Mara tuu, uokotapa kitu chochote ambacho sii Mali yako Moja kwa Moja nenda Kituo chochote Cha polisi kilichopo karibu yako na utaandika maelezo jinsi ulivyokiokota. Kitafunguliwa Taarifa kwenye kitabu kiitwacho LOSS AND FOUND PROPERTY REGISTER na utapewa kumbukumbu ya Taarifa hiyo kama unapopewa RB ya kesi

Pale ambapo mwenye Mali atapatikana na kutoa vielelezo vyote vya umiliki atakabidhiwa Mali yake na wewe utajulishwa

Pale ambapo kwa kipindi kirefu mwenye Mali hajaonekana ,itaandikiwa inventory na baada ya kutoka kwenye gazeti la serikali itauzwa kwa mnada.

Epuka msemo wa uongo wa kiswahili usemao CHAKUOKOTA SII CHA KUIBA.Hapa wahenga waliodanganywa umma na msemo huu upo kinyume na sheria na unahamasishi wizi utaishia jela, mbaya zaidi ukute simu hiyo kabla ya kuibiwa lilifanyika kosa la jinsi kubwa
 
Simu naitupa kabisa,natumia simu yenye imei nyingine na laini nyingine kabisa,hapo vipi mkuu?
usisahau kupitia laini uliyotupa kama ulisajili kwa jina lako kwa kitamulisho chako rasmi mfano cha NIDA basi washapata jina lako hata picha yako wanaweza hadi fika hadi baraza la mitihani NECTA au chuo ulikopata diploma au degree kama ulifika,leseni ya udereva kama unayo,pia wanaweza kusikiliza simu zote ulizopiga kwa kutumia laini uliyotupa watapata wazazi wako,mkeo au ndugu yoyote wa karibu kupitia hao watakupata.. kote huko system imehifadhi taarifa zako ndomana ushauriwa usimpe mtu kitambulisho chako asajilie namba ya simu siku akiyakoroga hilo janga lako
 
usisahau kupitia laini uliyotupa kama ulisajili kwa jina lako kwa kitamulisho chako rasmi mfano cha NIDA basi washapata jina lako hata picha yako wanaweza hadi fika hadi baraza la mitihani NECTA au chuo ulikopata diploma au degree kama ulifika,leseni ya udereva kama unayo,pia wanaweza kusikiliza simu zote ulizopiga kwa kutumia laini uliyotupa watapata wazazi wako,mkeo au ndugu yoyote wa karibu kupitia hao watakupata.. kote huko system imehifadhi taarifa zako ndomana ushauriwa usimpe mtu kitambulisho chako asajilie namba ya simu siku akiyakoroga hilo janga lako
Wakiadvance kufikia huku itakua poa sana,wahalifu watakamatwa kama kuku bandani
 
Msaada wa kisheria simu ya kuokota nakamatwa na polisi. Mama yangu aliokota simu smat phone akanipa sababu yeye Hawezi tumia nikaweka laini hapa nimepagawa,

Hii imekaaje mbaya zaidi aliepoteza simu anadai kwao ilibiwa simu, TV nch 32, jiko la ges plate mbili.

Je, machomokaje katika hili tatizo?
Mkiona kimya mjue nawasiliana na polisi maana wanasumbua balaa

Duuh, simu huwa zinaokotwa?
 
Kuna jamaa na yeye alikutana na binti anazurulazurula na nguo za shule (primary) kama km 20 nje ya mji.Kumuuliza binti haelewi.Akamlipia nauli akampeleka kituo cha polisi.Kwa kifupi jamaa alikoma sidhani kama atarudia tena.
Ilikuwaje?
 
mkuu nenda polisi hapo usijitambulishe tafuta tujiina la polisi yoyote na namba yake.....

after nenda karibu na sehemu ya pikpik weka kwenye bahasha sawa mpe mtu wapikpik bana sehemu confirm ameingia polisi a tafutr uuyo polisi amwambie khna mtu kaokota simu kantuma ili asiogope andika karatasi ndani akimpa bahashaanasoma ataelewa..... umenawa mikono
Mkuu ukifika pale kujifanya una huruma umeleta simu hawakuachii utalipa TV..condom.. kila kilichoandikwa
 
Back
Top Bottom